KakaJambazi
JF-Expert Member
- Jun 5, 2009
- 18,830
- 12,314
Dah! nimeamini education can ruin your life, mfano ni huu, una masters lakini upo tayari kushauriwa na form IIB.
dah pole sana mwaya..hawa wanaume sijui sometimes akili wanaweka wapi..yaani of all wanawake outside there ndio atue kwa mdogo wako..mxiuu
huo ni ushauri wa KIJINGA kabisa! unashauri KUUA kiumbe asokuwa na hatia? Mungu akusamehe bure.!
!
Nimeishea hii habari na mke wangu. Kwa maoni yake ni kwamba hiyo mimba kwanza itolewe mengine yatafuataga huko mbele kwa mbele.
mkuu acha kupotosha UMMA. kutokuzaa kwake kwa sababu YOYOTE ile, hakuhalishi mume wake KUZAA na MDOGO WAKE WA DAMU. umeelewa? acha dhihake zisizokuwa na tija kwa mkuu Leah 2.Muachie dogo kwanza ana mimba yake, we kasome na PHD kabisa. Ki ufupi apo shule ilikuponza. Alaf elim haina mwisho sista, Kwa nini usingesema uzae ndo ukaendelee na shule!!?, na hakika hata mdogo ako angeona mna mtt ange chukulia uzito hiyo kitu, next time ujue ku prioritize mambo ya muhim
Chezea mtoto mbichi tena dot com wewe chuchu saa 6.
Dah! nimeamini education can ruin your life, mfano ni huu, una masters lakini upo tayari kushauriwa na form IIB.
Wakati nimeamua kuingia kwenye ndoa nilijua naolewa na mwanaume mwenye level gani kielimu na pia kiuchumi, nilifanya maamuzi nikiwa najua ntawajibika kwake kama mke bila kujali tofauti ya elimu na uchumi pia..na ndivyo nilivyofanya ktk kila jambo tulishauriana na kuamua pamoja wala hakuna jambo nililoamua peke yangu.. Isipokuwa hili la kumpa kutembea na kumpa mimba mdogo wangu ndo sikuhusika.Kuna mzee mmoja aliniambiaga kitu lakini pamajo na hii scandar ya huyu dada ndo nimeona. Alisema kwamba levo za maisha zipo na zitaendelea kuwepo. Kwamba kama mtu anakuzidi tambua hilo. Akanambia hivi: "mwanangu sikujui hunijui; ila mwanamke anaekuzidi elimu; anaekuzidi kipato na hela; anaekuzidi urefu, sahau usidhani hiyo ndoa itadumu"! Sasa nayaona kwa wenzangu.
Af pili; kwenye tatizo kila mtu hujitetea. Dada sikujui hunijui lakini kama tungekuwa tunaweza ona ndani ya nafsi yako; kwa hela zako na elimu yako umechangia 70% ya haya mambo kutokea. Maana wewe ndoto zako ziko mbali saaaana. Ndo maana jama akaona bora huyo wanaenda sawa
Asante heaven sent umeugusa moyo wangu mpaka nimejikuta nalia, to be honest siwezi endelea na hii ndoa, sioni future serious na huyu mtu.Some men are selfish jamani khaaaa. Hivi ukiolewa ndo huruhusiwi kwenda shule, kwamba ndoa ndo mwisho wa ndoto zako? Mbona wanandoa wengine wanaamua kukaa kwa muda bila kupata mtoto? What if huyu mdada kwa mapenzi tu ya Mungu angechelewa kupata mtoto mumewe angeenda kuzaa nje? Angekuwa anamnyima mumewe haki yake ya ndoa at least tungesema mume alizidiwa (though hakuna justification ya cheating). Afu mbona huyo mume kama alikuwa na shida sana ya kuitwa baba, alimwambia huyo mdogo mtu atoe mimba, shida yake si mtoto au na alikosa wa kuzaa naye hadi mdogo wa mke wake? Shameless man.
Wamekubaliana wasizae kwanza dada amalize shule, kosa liko wapi? Mwanaume hatakiwi kusupport ndoto za mkewe? Kila familia ina maamuzi yake na jinsi wanavyoendesha maisha yao, tusilazimishe watu waishi kama sisi. No wonder wanawake wengi wenye mafanikio ni either
1. Hawajaolewa
2. Waliolewa wakaachika
3. Wamefanikiwa kabla ya kuolewa. (I'll get married though hihihi, Amen)
Bana wewe leah2, cheating is a deal breaker. Ukiweza kusamehe samehe tu kwa moyo mmoja. Ukishindwa pia no one is gonna blame you. Watu wanasema tu humu easy "eti huyo mtoto akikua arudi tu nyumbani umleee" eishhhhhh. Mtu unamkuta tu mwanaume ana mtoto before, but still kumlea kuna kaugumu fulani sembuse huyo wa kuletewa ndani ya Ndoa!!!! BTW are you a nanny or what kwamba mtu akaspread tu his seeds afu wewe unaletewa tu kulea mtcheew. Afu worse enough mumeo haonyeshi kuregret at all na wakati ana makosa kabisa. Haya wewe ndo ukamuombe msamaha umrudishe ndani ya nyumba au? Cha mwisho kama una dream za kusoma tena hapo baadaye kasome tu na PHD my dear na ndoa isiwe mwisho wa ndoto zake.
Hao wa kusema eti ukimuacha huyo unaweza kukosa mume mwingine, then let it be, God knows what's the best for you. Kama ndoa haikupi amani ya moyo just quit it kabla hujapata na depression kabisa au hujadondoka kwa presha. Huna haja ya kuishi na maumivu for the sake of a purposeless union. Kuna mtu kafa mapema kwa sababu hajaolewa/ kaachika ? Mungu akutie nguvu katika kipindi hiki kigumu. It shall be well with you
Inategemea wewe ni mwenyeji wa wapi. Kule kwetu ni ufahari. Wala hakuna issue hapo. Sanasana unachoweza kufanya ni kumwambia mdogo wako akupishe maana hapo ni kwako. Watakuwa wanakutana hukohuko anakoenda.
Sikushauri kabisa kuachika.
Goodluck Mshana nimekuelewa lkn to be honest hilo ni suala gumu sana, emu niambie nafuata nini kwake? Speak frankly hapa.Dada yangu leah2 ningependa ufwatwe ushauri wa mwisho wa Don Mangi na sifi leo... Wamesema na kuchambua vyema sana. Nami nasema USIVUNJE NDOA YAKO. No body is perfect under the sun. Unaweza kimbilia mume mwengine na huyo akaja kuzaa na Dada yako mkubwa (Kama yupo) ama akafanya kituko zaidi ya mumeo wasasa. Uvumilivu ndio ndoa. Hata sisi tupo kwenye hii taasisi. Ni ngumu sana. Mungu ndio hututangulia. Hakuna fundi wa ndoa leah2
Hongera kwa busara zako za kutafuta ukweli wa mambo. Heshimu mawazo na ushauri wa wazazi. Mwisho, hata Kama una mali kiasi gani, umekorofishana na mume kiasi gani, usiweke mipakano ya umiliki. Kwamba nyumba yangu hivyo toka! Gari langu usipande, bafuni peleka maji mwenyewe n.k. Hapana!
Busara ukiuongoze na uone kila kilichopo ndani ni chenu nyote, regardless. Usifukuze mume. Ni indication ya mwanamke jeuri na mwenye majivuno. Kwa maana ya kwamba siku ukimaliza PhD ukarudi home baba kachelewa basi kuna hatari ya yeye kulala nje au sitting room. Ni mbaya sana. Samehe. Piga moyo konde maisha yaendelee.
Goodluck Mshana
Leah 2 ningekuwa wewe hata nisingekuja hapa kuuliza ushauri, ndoa hakuna hapo tena. Jikusanye upya Mungu atakuletea mume mwingine. The bottom line is men are men, no comparison.
Natamani monicca ausome huu uziHaya mambo haya yapo sana ila watu hawajifunzi.
Duuh!pole sana!hii dunia imearibika total.. Yesu arudi tuuh Hamna namna nyingine..!ndoa ya kanisani pia inavunja kienyeji hivyo?!
Mungu gani anataka wanawake wapange ratiba za lini anatka kuzaa na lini hataki?? tatizo la wanawake wengi huku kusoma kwenu kunawapotosha sana, yaani wewe uolewe alafu hapohapo upange ratiba ya kuzaa, na sio wewe tu ni wengi wanagongewa wadogo zao au beki tatu na humu pia wamo ila hizo mimba hazijaingia ndio maana wako vifua mbele kukutetea.
Hilo umelitaka mwenyewe kwa kupanga ratiba za mechi na lini uzae, ndoa changa kabisa na makalenda kibaoooooooooooo. ulitakiwa ukae na ndoa yako kwanza kisha upate kamtoto kakumliwaza mzee ndio sasa ukasome hayo madudu yako. sasa masters ukae 2 years bila kuzaa, then PhD ukae 5 years bila kugegedwa we utakuwa unawazimu sio bure.
Mliobaki sasa hili ni somo kwenu, ukiolewa angalia ndoa kwanza kiasi cha 5 years, sio leo kesho unaanza minyodo ya masters. Ukija kuona jamaa ameparamia muhudumu wa tigo pesa anaweza kuoa kabisa na wewe ukabaki na makabrasha yako ya masters.