Mume wangu amempa mimba mdogo wangu

Mume wangu amempa mimba mdogo wangu

Give them an inch they take yard, Give them the yard they take mile... Aint no use Leah2, total distruction is the only solution. Achana naye move on na mishe nyingine.
 
Kama hutakuwa na mpango wa kuolewa tena achana naye. Iwapo utamwacha na kuolewa, waweza kupatwa na magumu zaidi. Kama unampenda mumeo msamehe.
 
Maana ukisema umsamehe mmeo muendelee kuishi pamoja harafu mdogo wako arudi Nyumbani bado naona amani haitakuwepo,mdogo wako atahitaji matumizi kwa ajili ya ujauzito pia mtoto atakayezaliwa hivyo lazima wawe Na mawasiliano.
Bado wataendelea kukucheat tu kwa Siri aise ndo ninapouona ugumu Wa Jambo hili tena ndugu yako Wa damu mweeh Mungu akukumbuke jamani ktk kipindi hiki kigumu.
Baada ya wazazi kuja waliomba msamaha? Pia toka wameondoka hapo kwako mmeo ameshakupigia simu walau hata kukujulia hali? Hata kuendelea kujutia kosa alilolifanya kwa ajili ya kuomba msamaha?
 
Pole sana Leah2 nimejarib kuvaa viatu vyako kwa kwel ni ngum sana!! Ni bora angefanya huo uchaf huko mitaani!! Lakin underone roof??? Tena kwa mdgo wko??? Hapana kwa kwel.. Hapo hakuna ndoa kabisa!! Kuanza upya c ujinga huyo mwanaume hakufai hata kidgo..Maamuz yko yapo sahihi kabisa!! Hongera nimegundua ww ni mvumiliv sn!! Na ni mama bora! Una hekima ya kutosha hasa kwa jins ulivyo handle hyo situation... Mungu atakupa mume bora.kwanza mshukur Mungu huyo Bazazi Ibilisi hajakuachia hata mbegu(mtoto) tena ni mipango ya Mungu...endelea na maisha yko!!!
 
How old are you?
Partly kabla ya kuanza kumlaumu mumeo nitakulaumu na wewe.
  1. Kutokuufwatilia kwa karibu uhusiano kati ya mdogo wako na shemeji yake. Mbali na kuwa ni ndugu yako wa damu,utakuwa unajua tabia zake na ni mwanamke kama wanawake wengine.
  2. Hilo la kuchelewa kumzalia mumeo mtoto. Inaweza kuwa lilikuwa jambo lako tuu na namna alivyokubali inaweza kuwa kutokana na sababu zako ila je? mliridhiana pasipo shaka kwamba atakubali wewe umalize kusoma ndio umzalie mtoto?
Wanaume ni wadhaifu being a man I know this, na wanahitaji kufuatiliwa kwa ukaribu sana hasa kwenye mambo kama haya yanayohusisha hisia. Ki mtazamo sijui namna mambo unavyoyaendesha nyumbani kwako ni maoni yangu kuwa unaipa sana kazi yako na masomo as priority kuliko mume wako (sisemi usithamini kazi) to me, family comes first. Na hiyo weakness shetani ndio akapitia hapo hapo.

Bottom line: Fuata ushauri wa wazazi, dogo arudi kijijini ajifungue mtoto, mtoto akiwa mkubwa, aje hapo nyumbani, kaeni kikao cha kifamilia mdogo wako na mumeo waombe msamaha kwa jambo lililotokea na mzungumzie utaratibu wa matunzo ya mtoto. Life goes on. Ukishindwa hilo. File for a divorce ukaolewe na mtu atakayekusubiria umalize shule (tena Masters, unga na PHd kabisa) ndio ukubali kumzalia mtoto.
Huu ushauri ni rahisi sana kuutoa kama Jambo halijakufika eti Yule mtoto aje Hapo seriously? Wanaume bana.
 
Leah2

Tambua kuwa hapo hakuna ndoa tena. Mme wako ameshavunja misingi ya ndoa kwa:
(1) Kufanya uasherati
(2) Kuzaa mtoto nje ya ndoa.

Ingelikuwa tayari nyie mna watoto, ungelisema ngoja tuendelee kuishi pamoja kwa ajili ya kulea familia/watoto.

Watoto hamna, je unachotaka kukivumilia ni kipi?
Huu ushauri mzuri aisee nimekupenda ulivyomshauri.
 
Muachie dogo kwanza ana mimba yake, we kasome na PHD kabisa. Ki ufupi apo shule ilikuponza. Alaf elim haina mwisho sista, Kwa nini usingesema uzae ndo ukaendelee na shule!!?, na hakika hata mdogo ako angeona mna mtt ange chukulia uzito hiyo kitu, next time ujue ku prioritize mambo ya muhim
 
Mmh mmeo nae nlisoma maelezo yake japo hakueleza kirefu kama wew...poleni sana
 
Imeandikwa samehe saba mara sabini, sisi wanaume ni mbwa.
Umnaweza kuachana kwa kosa la uzinzi Ila kama anakifua asamehe Ila hii ndoa imeingiwa Na mdudu sio rahisi.
 
Inategemea wewe ni mwenyeji wa wapi. Kule kwetu ni ufahari. Wala hakuna issue hapo. Sanasana unachoweza kufanya ni kumwambia mdogo wako akupishe maana hapo ni kwako. Watakuwa wanakutana hukohuko anakoenda.
Sikushauri kabisa kuachika.
 
Umeshasema huoni sababu ya kuendelea kuwa naye.. Hii inamaanisha maamuzi uliyochukua ndio sahihi na hukukosea kuhusu hilo lakini tambua maamuzi hayafanywi wakati ukiwa na hasira na kule kuwaondoa hapo kwako ndio umewapa uhuru wa kuendeleza penzi lao
 
Pole dada,
Ulimwengu umeoza huu, hakuna hiyana wala utu kama zamani. Ukweli kuishi na huyo mume ni kuishi kinyume na matarajio yako! Afadhali hata angekuwa mtu baki....

Lakini tafadhali hembu jaribu kuongea tena na moyo wako usifate maamuzi ya ubongo ya ghafla...acha jazba.
Nikupe mfano kidogo, hii ilitokea kwa watoto wa mjomba wa marehemu mama yangu!

Dada aliolewa mjini, baadae akaona amchukue dogo wake aje kumsaidia kazi ya kuuza duka.. mdogo kaja na biashara ikakuwa vyema, miaka miwili mbele mdogo kapata mimba kuulizwa ya nani hasemi!
Kwa huruma ikaamliwa akae na kuzaa pale, haya kamaliza kunyonyesha kabeba tena na tena.!

Dada kaamua amtafutie pake aishi, wanabe wakaanza yao chini chini kuwa watoto ni wa shemeji kula..,lakini dada kapuuza na hakuwahi kuhisi jambo. Sasa siku moja ikaja kesi ,mume wa dada kajeruhi mtu vibaya ,kisa kamfuma ndani na shemejie! Hapo ndo ikaliki..mana ikibidi wabanwe na polisi kutokana na mazingira ya kesi yalivyo..

Majirani na mwenye nyumba kule alikopanga mdogo mtu walikuwa wakimjua yule shemeji ndo mumewe, na siku nyengine akilala vuzuri tu.

Mwisho walikubali kuwa ni wapenzi na washa zaa watoto watatu tena wanamfanana baba yao,dada mtu alilia kilio cha mbwa! Akajuta majuto ya farao..na akaachana na mume kwa miaka mingi.
Lakini hivi naandika dada alisha msamehe mumewe na wanaishi kama kawa,mdogo karudi kijijini anapelekewa matumizi.

Ukimuuliza dada sababu anajibu ,alijaribu kuishi na watu tofauti lakini hakuna aliyefikia sifa za mumewe wa mwanzo.!
Sasa nawe sikiliza nafsi yako...sema na moyo wako mama !
Upate kilicho bora kwako...
 
Mpaka ulipofika nakushukuru kwa hekima yako. Inaonyesha kabisa unamoyo wa suluhu. Sio jambo rahisi hekima kubwa sana inahitajika.

Hapo nikuokoa mstakabili wa watu watatu , wewe, mdogo wako na mtoto. Zaweza kuwepo njia tatu. Ya kwanza wewe kuondoka na mdogo wako kubaki. Pili wewe kubaki na dogo kuondoka. Tatu wote kuondoa.

Vikwazo wewe ni mwandoa, mwenyewe mimba ni mdogo wako, mtoto atakayezaliwa ni mtoto wako pia cause ni wa mdogo wako. Kuna uwezekano wa kujenga chuki ya milele baina yako na dogo.

Ukimsamehe dogo ukamchukia mume hakuna upendo wa kweli. Ukimuachia mdogo wako mji wako utafedheheka kwa muda mrefu na hiyo kitu.

Nakuomba kama ulivyowaomba wakupishe na wakakubali. Mumeo amekupa heshima kiasi omba hekima ya Mungu ikuokoe.

Kwa mtazamo wangu mpe mmeo nafasi ya Pili. Dogo arudi home wasamehe wote 3 yaan pamoja na mtoto. Ili apate kibali machoni pako Kwa sababu kuna wakati atakaa kwako.

Anglia pia msimamo wako wa kutozaa mpaka umalize shule kama unaweza kuwa sababu. Pima kama wewe ndiye ulikuwa unavuta zaidi hilo litokee. Iombe nafsi yako msamaha ili uwe radhi.

Wewe ni mkubwa mfichie mdogo wako aibu, watu wote watamsema kuwa amekutoa kwa mume wako. Mhifadhi ata pata shida muda mrefu sana ukitoka kwenye hiyoo ndoa
 
Muachie dogo kwanza ana mimba yake, we kasome na PHD kabisa. Ki ufupi apo shule ilikuponza. Alaf elim haina mwisho sista, Kwa nini usingesema uzae ndo ukaendelee na shule!!?, na hakika hata mdogo ako angeona mna mtt ange chukulia uzito hiyo kitu, next time ujue ku prioritize mambo ya muhim

Thank you!!!!

Hapa ndipo kwenye msingi wa tatizo, halafu watu wanaanza kuliangalia tatizo karibu na lilipotokea wakati kiini kiko mbali sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom