Kwanini mume wangu hawapendi NDUGU ZANGU?

Kwanini mume wangu hawapendi NDUGU ZANGU?

H r n

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2019
Posts
1,014
Reaction score
1,900
Hili limekuwa likinikishangaza sana 😢 majibu sipati,alisema suzy nimeolewa na mume wangu kwa miaka 5 na tuna watoto 2, na tumejenga nyumba yetu nzuri na tuna usafiri wetu, kwa kifupi maisha yetu si haba. Kinachashangaza kuhusu mume wangu hapendi kuona ndugu zangu kuja kwetu tulipo, either kwa kukaa au kusalimia, sijawahi hata muelewa ni kwanini.

Kuna siku nilimpa taarifa mdogo wangu wa kike na wakiume wanakuja nashangaa SURA yake ilibadilika ,na si mara moja ila kwa upande wa kwao huwa wanakuja bila hata taarifa nikitoka kibaruani huwa nawakuta tu yaani nabaki nashangaa kwa nini iwe hivyo je ? Sipaswi mimi kutembelewa na ndugu zangu! Au nakosea wapi mimi?, wenzangu ipoje kwenu huko ? Aliuza suzy
 
Hili limekuwa likinikishangaza sana 😢 majibu sipati,alisema suzy nimeolewa na mume wangu kwa miaka 5 na tuna watoto 2, na tumejenga nyumba yetu nzuri,na tuna usafiri wetu ,kwa kifupi maisha yetu si haba .cha kushangaza kuhusu mume wangu hapendi,kuona ndugu zangu kuja kwetu tulipo,either kwa kukaa au kusalimia,sijawahi hata muelewa ni kwa nini ,kuna siku nilimpa taarifa mdogo wangu wa kike na wakiume wanakuja nashangaa SURA yake ilibadilika ,na si mara moja ila kwa upande wa kwao huwa wanakuja bila hata taarifa nikitoka kibaruani huwa nawakuta tu yaani nabaki nashangaa kwa nini iwe hivyo je ? Sipaswi mimi kutembelewa na ndugu zangu ! Au nakosea wapi mimi wenzagu ipoje kwenu huko ? Aliuza suzy
Pole sana, lakini tambua kuwa ndoa ni ya wawili wa tatu ni kikaragosi.

Ningependa pia nimsikie Mme wako anasemaje kabla sijatoa hukumu.
 
Huenda
1. huko nyuma uliqah mdanganya mtu fulani ni ndugu yako halafu akaja akajua anakumega

2. Kuna kitu aliwahi kukukataza ila kwenu walivyo kushauri ukakifanya, kumaanisha ukadharau katazo lake ukatii la wa kwenu (lazima awamaindi)

3. Huenda wakati hamjajipata (mkiwa hamjapata fedha) kwenu/ndugu zako walimuonesha dharau kwa vile hakuwa na kitu

4. Huenda uliwahi wewe mwenyewe au kupitia ndugu yako wa karibu iba fedha au chochote ukapeleka kwenu na baadae akaja kujua.

5. Huenda kuna siku katika mahusiano yenu mlikosana na ndugu zako waliingilia huo ugomvi eidha kwa simu au sms au uso kwa uso, na katika hilo walionesha kuegemea kwa mwanamke na kumuonesha mwanaume mkosefu na kwamba wanaweza kukuchukua na kukurudisha kwenu wakihitaji.

6. Uliwah tamka neno baya kwa ndugu zake wa mwanaume au aliwah said8a mtu nyumbani kwao hasa mama na ukahoji (epuka kuingilia mipango ya mwanume dhidi na kwao hasa wazazi wake). Tunajua wazazi wetu na ndugu zetu walivyotufichia viporo tukitoka shule tule tupozee na maji ya kumywa ya kisimani. Halafu ukubwani unakutana na mtu hana hata bikra anaanza kusema hili na lile linalohusu kwenu usifanye au usicanyie wazazi wako, hapo unayatimba kimia kimia
 
Hili limekuwa likinikishangaza sana 😢 majibu sipati,alisema suzy nimeolewa na mume wangu kwa miaka 5 na tuna watoto 2, na tumejenga nyumba yetu nzuri,na tuna usafiri wetu ,kwa kifupi maisha yetu si haba .cha kushangaza kuhusu mume wangu hapendi,kuona ndugu zangu kuja kwetu tulipo,either kwa kukaa au kusalimia,sijawahi hata muelewa ni kwa nini ,kuna siku nilimpa taarifa mdogo wangu wa kike na wakiume wanakuja nashangaa SURA yake ilibadilika ,na si mara moja ila kwa upande wa kwao huwa wanakuja bila hata taarifa nikitoka kibaruani huwa nawakuta tu yaani nabaki nashangaa kwa nini iwe hivyo je ? Sipaswi mimi kutembelewa na ndugu zangu ! Au nakosea wapi mimi wenzagu ipoje kwenu huko ? Aliuza suzy
Inashangaza sana hii hali kutokea kwa mwanaume mara nyingi wanawake ndo huwa na tabia hizo. Kiasili wanaume ni wakarimu sana na pia huwa hatujali kuishi na watu kwenye familia zetu
 
Back
Top Bottom