Venus Star

JF-Expert Member
Dec 6, 2018
19,674
59,774
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa mamlaka aliyopewa, alitoa maagizo kwa Msajili wa Vyama vya Siasa kuhusu kuandaa mkutano maalum wa Baraza la Vyama vya Siasa.

Lengo la maagizo hayo lilikuwa kutoa fursa kwa wadau wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa kutathmini utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa na Kikosi Kazi kilichojikita katika kufanyia kazi masuala yanayohusiana na demokrasia ya vyama vingi vya siasa Nchini Tanzania.


View: https://www.youtube.com/live/gZteo95nx84?si=80sJfbMUI52t-UHX

1704271277706.png


1704271294503.png


OTHMAN MASOUD SHARIF, MAKAMU WA KWANZA WA RAIS-ZANZIBAR
Mkutano wa majadiliano hasa wa utajiri wa mawazo ya Washiriki na sio Mkutano wa mapambio na kutimiza tu utaratibu tunaoanza kuuzoea wa kusema “WADAU WALISHIRIKISHWA” japokuwa kiuhalisia HAWAKUSIKILIZWA.

Kwa maneno mengine sote kwa pamoja tuepuke kuugeuza Mkutano huu kuwa MUHURI wa kuhalalisha mawazo ya watu wachache au MSIMAMO wa kitaasisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti na Waheshimiwa Viongozi, sote wakati tunaelekea katika Mjadala huu ni vyema tujikumbushe tulikotoka hadi kufikia hapa. Historia itatukumbusha Dhamira ya Miswada tutayoijadili na muelekeo tunaopaswa kuchukua ili kuakisi Dhamira yetu kama Taifa.

Tukumbuke kwamba Disemba 2021 Baraza la Vyama lilifanya Mkutano kule Dodoma uliopelekea kuundwa kwa Kikosi Kazi cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutazama hali yetu ya Demokrasia.

Aprili 2022 Kituo cha Demokrasia Tanzania kikafanya Mkutano wake Dodoma na kutoa mapendekezo mahususi kwa Kikosi Kazi kuhusu Sheria zetu za Uchaguzi na za Vyama. Septemba 2022 Kikosi Kazi kikakabidhi rasmi tarifa kwa Mheshimiwa Rais na Januari 2023 Mheshimiwa Rais akaondoa zuio dhidi ya Mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa na Tarehe 10 Novemba 2023, Mswada wa Sheria ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mswada wa Sheria ya Uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wabunge na Madiwani na Mswada wa Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa Sura ya 258 na Sheria ya Gharama za Uchaguzi Sura ya 278, ilisomwa kwa mara ya kwanza Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti na Waheshimiwa Wajumbe, Historia hiyo inatuonyesha kwamba Mchakato wa kutayarisha Miswada tunayotaka kuijadili haukuwa wa Serikali peke yake wala wa Chama kimoja peke yake.

Ni Mchakato uliokuwa shirikishi, uliosheheni mawazo na baraka za wadau wengi. Hivyo, katika mjadala wetu jambo hili la kuwa huu ni Mchakato shirikishi lazima tulipe kipaombele sana"
 
Wanabodi,
Niko ndani ya ukumbi wa JNICC kwenye Mkutano huu muhimu Mkutano Maalum wa Baraza la Vyama vya Siasa tarehe 3 na 4 Januari, 2024 View attachment 2855370
MKUTANO MAALUM WA BARAZA LA VYAMA VYA SIASA

Kauli Mbiu;
" TOA MAONI YAKO KUIMARISHA DEMOKRASIA "

MGENI RASMI;
Mhe. Othman Masoud Othman
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar

🗓️ Tarehe 3 na 4 Januari, 2024
📍Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City - Dar es salaam

#ImarishaDemokrasia
#TunzaAmani
Mkuu Venus Star , asante sana kwa taarifa, hii sio ya kukosa!,

Ila to be honest, nilikuwa nina wasiwasi na baadhi promo za Mkutano huu, kama baadhi ya washiriki hawa
View attachment 2855372View attachment 2855373View attachment 2855374
View attachment 2855375 japo sijabaatika kumuona yeyote kati ya hao, ila Chadema wamewakilishwa na Makamo Mwenyekiti wa Chadema na na NKM wa Chadema, Kamanda Salum Mwalimu, ambaye yuko in full regalia ya combat.

Mkutano umeanza, fuatilia live Mubashara kupitia Wasafi
View: https://www.youtube.com/live/WMNZqOQv-jo?si=gbOqXz5I22MQuyka

Kwa Tanzania Bara, ukisema upinzani unamaanisha Chadema!, huu ni mkutano wa 3 wa Baraza la Vyama vya Siasa, mikutano miwili iliyotangulia, Chadema walisusa. Mkutano wa kwanza pale Dodoma, mimi niliwaomba wasisuse Chadema, P'se, Msisusie Mkutano wa Vyama, Wasilisheni Hoja Zenu Mezani, Zitamfikia Samia, Ana Nia Njema na Nchi Hii, Mpeni Ushirikiano!.
Chadema waligomea wito wangu ila hapa walikuwa na justified reason ya kususa, Mwenyekiti wao alikuwa korokoroni akikabiliwa na kesi ya ugaidi.

Kesi ya Mbowe ikafutwa, Mbowe akaachiwa, CCM wakafanya mazungumzo ya maridhiano na Chadema, wakafikia makubaliano ya kugawana nusu mkate. Lakini mkutano wa pili wa Baraza la Vyama vya Siasa, bado Chadema walisusa!.

Hivyo mkutano huu wa 3 ulipoitishwa, nikaandika tena kuwasihi Chadema wasisuse Baada ya maridhiano kuna haja kuendele kususa na kuzira? Njooni mezani, tukae pamoja, tuwe wamoja, twende pamoja!

This time ombi hili limezaa matunda, Chadema wameshiriki kikamilifu, hivyo ni faraja kubwa kwa wapenda demokrasia.

Karibuni.

Paskali
 
Wanabodi,
Niko ndani ya ukumbi wa JNICC kwenye Mkutano huu muhimu Mkutano Maalum wa Baraza la Vyama vya Siasa tarehe 3 na 4 Januari, 2024 View attachment 2855370

Mkuu Venus Star , asante sana kwa taarifa, hii sio ya kukosa!,

Ila to be honest, nina wasiwasi na baadhi promo za Mkutano huu, kama baadhi ya washiriki hawa
View attachment 2855372View attachment 2855373View attachment 2855374
View attachment 2855375

Mkutano umeanza, nitawadondolea kile kinachojiri hapa

Karibuni.

Paskali
Si lolote na wala si chochote.
Just a wastage of time and other valuable resources.
KATIBA MPYA SIYO MALI YA WANASIASA PEKE YAO.

TUNATAKA KATIBA MPYA SASA.
Hatutaki blah blah za kisiasa za kutucheleweshea zaidi Upatikanaji wa Katiba Mpya.
 
Wajumbe wa Baraza la vyama vya Siasa wamekuja kwa wingi wao. Namuona Zitto yupo hapa anafuatilia kwa umakini sana.
 
Back
Top Bottom