Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Hatukubali Mkapa adhalilishwe -Pinda


*Asema wataalamu wetu ni butu kujadili mikataba
*Azungumzia mapokezi ya vigogo waliowajibishwa

Na Mwandishi Wetu

SERIKALI imesema haipo tayari kuona Rais mstaafu Bw. Benjamini Mkapa anadhalilishwa kwa kuzomewa hadharani na haitasita kuchukua hatua kali kwa yeyote atayebainika kufanya hivyo kwani kufanya hivyo ni ukiukaji wa utawala wa sheria.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda alipokutana na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari katika mkutano wa kufahamiana na kubadilishana mawazo ambapo pia walipata fursa ya kumuuliza maswali.

Akijibu swali kuhusu taarifa za madai ya kukamatwa kwa baadhi ya watu wanaotuhumiwa kumwita Rais huyo fisadi hivi karibuni, Bw. Pinda hakuthibitisha wala kukanusha jambo hilo lakini alisema kamwe hafurahii kuona Rais Mkapa anazomewa anapopita mitaani.

Bw. Pinda alisema yapo mambo yanaweza kufanywa lakini si sahihi hata kidogo kumzomea kiongozi huyo na kwamba vitendo vya kumdhalilisha kamwe havitaruhusiwa katika nchi inayofuata misingi ya utawala wa sheria.

" Hatuwezi kuwa watu wasiojiheshimu, kwa lengo hilo hapana ! waliomwita mhujumu uchumi huenda tabia yao haikuwa ya Kitanzania. Siwezi kufurahia kuona Mkapa anapita anazomewa hata kidogo ! Yapo mambo yanaweza kufanywa, kumshtaki mtu si tatizo lakini sio sahihi kumhukumu mtu bila taratibu kufikiwa," alisema na kusisitiza;

Vitendo vya kumdhalilisha kama Taifa tuseme hapana ! katika nchi inayoongozwa chini ya utawala wa sheria tusichukue sheria mikononi. Siafiki Rais Mkapa kuzomewa, ana heshima yake ni binadamu anastahili heshima, zipo taratibu zinazotakiwa," alionya

Akijibu swali lililohoji usafi wa mawaziri waliobaki madarakani baada ya Rais Jakaya Kikwete kupangua baraza hilo, Bw. Pinda alisema hawezi kuwathibitisha kwa hilo kwani waliomo serikalini ni binadamu kama watu wengine na kufafanua kuwa jukumu lake kama Waziri Mkuu ni kuhakikisha timu hiyo inafanya kazi kwa maadili yanayokubalika na umma.

Alisema Rais Kikwete anajitahidi kutambua na kuteua viongozi wazuri bali matatizo yanayojitokeza ni wahusika wenyewe wanapoingia kwenye dhamana hizo na kusisitiza kwamba suala la uadilifu vita dhidi ya rushwa ni vita endelevu.

"Rais amejitahidi kutambua watu wazuri lakini wanapoingia wanaanza kuhangaika kuangalia huku na huko. Yapo yaliyotokea siku za nyuma lakini hawa tuliona tutazidi kusisitiza suala la uadilifu. Hii ni vita endelevu. Hakuna rushwa inayotoka mbinguni zote zinatoka humu humu," alisema.

Richomond
Kuhusu swali la nani anaendelea kupokea pesa zinazodaiwa kulipwa kampuni hiyo kila siku na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),Bw. Pinda, alisema kampuni hiyo sasa haipo na majukumu yake yalichukuliwa na Dowans ndiyo inapaswa kuhusishwa kwa hilo.
Hata hivyo, alisema uchunguzi kuhusu mapendekezo yaliyotolewa na Tume teule ya Bunge iliyochunguza mchakato wa zabuni ya Richmond bungeni yanaendelea kufanyiwa kazi na tayari kwenye maeneo mengine utekelezaji unaendelea.

Sambamba na hilo alizungumzia mkataba Kampuni ya Kupakua na Kupakia Mizigo Bandarini ya (TICTS) na kueleza kuwa pamoja na uhalali wake umeonekana kuwa na dosari nyingi.

Bw. Pinda alisema kinacholiumiza Taifa sasa na uwezo hafifu wa wataalam kupitia na kukubaliana juu ya mikataba mbalimbali. Alisema kutokana tatizo hilo serikali itaangalia uwezekano wa kushirikisha kamati huru za wataalam wa masuala ya sheria kupitia na kutoa mapendekezo ya mikataba mbalimbali kabla haijasainiwa, ili kupunguza dosari hizo.

Aliko Balali
"Ukiniuliza yuko wapi sijui" alisema Bw. Pinda alipoombwa kutoa taarifa za uhakika kuhusu aliko gavana huyo wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania
( BoT) . Alisema Bw. Balali anahitajika kutokana na masuala ya BoT na kurudia kauli ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Bw. Salva Rweyemamu kwamba gavana huyo akihitajika si jambo kubwa, atapatikana.

Mapokezi vigogo

Akijibu swali lililohoji kuwa anajisikia viongozi waliowajibishwa kwa tuhuma za ufisadi kupokelewa kwa makeke majimboni mwao, alisema huo ni mtazamo wa wananchi wao majimboni na kwamba tuhuma hizo haziwaondolei upendo wao. Alisema serikali haina uwezo kuwahukumu kabla ya kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Bw. Pinda aliwataka watendaji wote wakiwemo mawaziri kuwa wazi kwa vyombo vya habari na kushirikiana kutoa taarifa, binafsi alisema amejipangia utaratibu wa kukutana na wahariri kila baada ya miezi mitatu kujadili na kujibu hoja mbalimbali kwa manufaa ya jamii.


Alivipongeza vyombo hivyo na kueleza kuwa sasa vimeifikisha serikali pagumu kutoka na umakini wa kufuatilia masuala mbalimbali jambo ambalo alisema kuna mambo mengi yanayofanyika sasa ambayo kama vyombo hivyo vingelala yasingefanyika.

" Vyombo vya habari vimetufikisha pagumu tuliomo serikalini, tunafanya kazi mmesukuma mambo, kama 'press' ingelala yasingefanyika " alisema na kuahidi kuwa serikali itajitahidi kuhakikisha uhuru zaidi kwa vyombo vya habari unakuwepo.


Mkuu Mushi,
Nakubaliana na wewe kabisaa, muda wao umeshapita. Kama hata mwanasheria Pinda naye haelewi uhuru wa kukosoa, uhuru wa hotuba (hata kama ni kwa kuzomea) na uwajibishwaji wa viongozi na wananchi. Kiongozi (kwa kuzomewa au otherwise) ni wajibu wao. Kuwakamata wanaotumia uhuru wao na sauti zao ni uonevu na kuwanyima raia rukhsa ya kukosoa hadharani hata kama ni kwa kuzomea ni lazima usitishwe mara moja. Shame on you Pinda.
 
Hapa Solution Ni Kuamua Ccm Basi
Hiyo Ndio Solution Iliobakia...nani Anaanza ....hapo Ndipo Pagumu..inabidi Uingie Vijijini Ukaabadilishe Wale Wanaoujua Raisi Bado Nyerere Chama Ccm Peke Yeke....mungu Ibariki Tanzania

kwi kwi kwi kwi koh koh duh yaani mpaka nimepaliwa so inamaana vijijini ndo kuna vipofu?
 
Pinda anajidhalilisha sana, alivyochaguliwa watu kidogo walidhani kuwa angefanya maajabu lkn ni walewale, hivi jamani tutaongea hivi mpaka lini wakati kila aingiae anaongea uozo tuu
HIVI ULITAKA PINDA ASEME NINI KWA BOSS WAKE WA SIKU NYINGI PALE IKULU,MY FRIEND THIS PEOPLE ALWAYS THEY NEED PEOPLE LIKE PINDA TO PINDA PINDA MAMBO YAO NAYE ATAKATIWA PANDE KIMYA KIGUMU CHAMA CHA MAPINDUZI .
 
Pinda anajidhalilisha sana, alivyochaguliwa watu kidogo walidhani kuwa angefanya maajabu lkn ni walewale, hivi jamani tutaongea hivi mpaka lini wakati kila aingiae anaongea uozo tuu

ndugu yangu kama ulitegemea maajabu kwa pinda pole sana.
kama ni maajabu tungeyaona alipokuwa waziri wa tamisemi.
kwa kifupi tu nchi hii tokea ilipopewa uhuru hakujapata kutokea waziri mkuu kama edward moringe sokoine.
 
Kusema kweli hata ingekuwa wewe ndo Waziri Mkuu usingejibu vinginevyo. Ila tu nisememe nguvu ya umma hakuna anayeweza kuishinda, si Pinda wala polisi. Iko siku moto utawaka na watz watajulikana si wapole na wa kuburuzwa. i am very optimistic!!!!
 
Pinda hana haja ya kupoteza muda mwingi kumtetea Mkapa. Mkapa ni Mtu Mzima anajua kuongea, suala linalomkabili analifahamu fika siyo geni.

Ni juzi juzi tu waziri mkuu mstahafu wa UK aliulizwa maswali BBC kuhusu mahamuzi aliyofanya akiwa kiongozi serikalini. Alijibu kulingana na alivyoweza watu wakamuelewa pale ilipowezekana.

Leo hii Mtu anatuhuma hata kuongea hata kidogo hataki ananyamaza. Kwani wakati anafanya alikuwa hajui sheria za nchi zinasemaje? Watu wengine bwana.

Eti alisema ni zama za uwazi, sasa mbona anaumbuka akiwa bado duniani. Haya yote yatajulikana ulimwengu mzima, sasa adhabu huwa wanasema mbinguni Naona Mkapa ataungua hapa duniani.

Ataishia kuishi milimani kama Mnyama. Viongozi na watendaji wote wa serikali jifunzeni kutoka kwa Mkapa. Hapa hakuna cha huruma atoke ajisemee mwenyewe.

Kwa nini hata asiite mwandishi mmoja akamueleza msimamo wake?
 
Huyu Pinda ni kituko nilimchoka mwanzoni tu alipokuja na kauli kosa si kutenda kosa bali ni kurudia kosa, Tanzania ni nchi ya amani na utulivu, nchi haina raisi wala waziri mkuu na hatupigani wala nini, tunapeana usanii tuu...
 
Kusema kweli hata ingekuwa wewe ndo Waziri Mkuu usingejibu vinginevyo. Ila tu nisememe nguvu ya umma hakuna anayeweza kuishinda, si Pinda wala polisi. Iko siku moto utawaka na watz watajulikana si wapole na wa kuburuzwa. i am very optimistic!!!!

ingekuwa vizuri zaidi kama angalau angesema " siwezi kuongelea swala hilo kwa sasa maana uchunguzi bado unaendelea" (kama alivyokwisha tuambia kuwa Mkapa anachunguzwa na kiwira yake)anasahau hata aliyo yasema

THis man is talking too much, mi liwahi kusema hapa kuwa huyu bwana anaongea sana, na ukiongea sana unakosa nafasi ya kufikiri kwanza unaishia kuongea PUMBA TUU
 
Jamani ni lazima tuelewe kwamba katika ccm ya leo watu wa namana kama hiyo ndio wanao wafaa kwani katika kuidhinisha wezi na kutetea majambazi na kudhalilisha raia kwahyo zuri kutoka hapo halipo, asizomewe mkapa lakini pemba anaye dai kujitenga kwa karatasi tu amesha kuwa hafai katika jamii na ndio wa kwanza kuswekwa lupango....
 
Nina maoni tofauti kidogo... Wengine katika mkutano huo huo, wanasema Pinda kasema Mkapa hawezi kukwepa kuchunguzwa na kama kuna jinai hatakwepa kushitakiwa,,.... sasa suala la kuzomewa nilimsikia akisema, "katika kuzingatia utawala wa sheria, hatuwezi kama serikali kuruhusu watu wamzomee rais mstaafu ama yeyote yule, kama kuna makosa yatashughulikiwa kwa taratibu zinazostahili na kwa hili la Mkapa linashughulikiwa".

Kwa maneno hayo sioni kosa la Pinda, nadhani kosa kubwa ni la Gazeti la Majira ambalo jana lilikuwa na story ya kumtetea Mkapa na leo wameendeleza tena bila kuandika chochote kuhusu Pinda kusema sheria itachukua mkondo wake... Kuna ajenda ya siri MAJIRA, tuangalie kwa upande huo na kwa makini zaidi
 
Kumdhalilisha fisadi Mkapa ni kuidhalilisha CCM ambayo fisadi Mkapa alikuwa mwenyekiti wake kwa kipindi cha miaka 10 ambacho alikuwa busy kuifisadi Tanzania na Watanzania.

By the way kuna fisadi yeyote ambaye CCM iko tayari kuona anadhalilishwa? Si ndiyo sababu mafisadi wote kuanzia wa EPA, Richmond, Rada, Ndege ya Rais, magari na helicopters za jeshi, mikataba hewa ya dhahabu, Tangold, Meremeta bado wanapeta bila wasi wasi wowote?

Kwa mara nyingine tena Maslahi ya Chama Cha Mafisadi yamepewa kipaumbele kuliko yale ya Tanzania na Watanzania!
 
Mkapa alishajidhalilisha mwenyewe kwa kuamua kufanya biashara Ikulu. Wananchi wakisema ukweli na kumzomea fisadi si madhalilisho. Ni haki yao kisheria---freeedom of expression. Mwalimu alipoondoka Ikulu Watanzania wengi walibubujikwa machozi kwa sababu walifahamu Mwalimu alikuwa pale kwa ajili yao. Kwa hiyo Mheshimiwa Pinda kubali mwaliko wa babikyu lakini mafisadi ni lazima tuwape heshima wanazostahili---kuzomewa!!!!
 
Eti Pinda ni Mwanasheria? Unajua kuna kitu watu wanachanganya, Mkapa hakufanya biashara Ikulu, bali ameiba hela zetu wananchi na mali za taifa letu,

Now this is not kufanya biashara Ikulu, what he did ni wizi period!
 
Nina maoni tofauti kidogo... Wengine katika mkutano huo huo, wanasema Pinda kasema Mkapa hawezi kukwepa kuchunguzwa na kama kuna jinai hatakwepa kushitakiwa,,.... sasa suala la kuzomewa nilimsikia akisema, "katika kuzingatia utawala wa sheria, hatuwezi kama serikali kuruhusu watu wamzomee rais mstaafu ama yeyote yule, kama kuna makosa yatashughulikiwa kwa taratibu zinazostahili na kwa hili la Mkapa linashughulikiwa".

Kwa maneno hayo sioni kosa la Pinda, nadhani kosa kubwa ni la Gazeti la Majira ambalo jana lilikuwa na story ya kumtetea Mkapa na leo wameendeleza tena bila kuandika chochote kuhusu Pinda kusema sheria itachukua mkondo wake... Kuna ajenda ya siri MAJIRA, tuangalie kwa upande huo na kwa makini zaidi

Halisi
Owner wa gazeti la Majira ana close ties na Mkapa na ni Mbunge wa CCM .NI magazeti haya haya yalimfanya aupate Ubunge na sasa lazima atetee uozo.Majira hawana tofauti na magazeti ya Rostam .
 
Kwa sasa swali langu ni moja tu kwa Mh. Pinda:

Serikali imefanya nini kukomesha udhalilishaji wa wananchi kutokana na vitendo vya kiuhujumu vya baadhi ya viongozi vinavyofanya maisha ya Watanzania walio wengi yawe kama ya ombaomba?!!!


Mkuki kwa nguruwe...

Umeme, maji safi, mabarabara, madawa n.k. ambavyo ni mahitaji ya msingi kwa wananchi hayapatikani kwa urahisi hata baada ya miaka 46 ya uhuru....... ahadi zao zisizotimizwa za kutupatia mahahitaji haya msingi kila baada ya chaguzi ni kudhalilisha wananchi.



SteveD.
 
Pinda hakusema kwamba BWM ni msafi, ila alisema asizomewe wakati bado hajashitakiwa. Hivyo anatuchagiza kwamba tuendelee kushinikiza BMW apate haki yake...mahakamni.
Kumbekeni pia BMW alikua Bosi wa MPP kwa muda mrefu....
Ila Mhe. MPP anasahau kitu kimoja....kwamba kuzomewa kwa BWM ni matokeo ya hasira za watu dhidi yake...amekataa mwenyewe kukana (au kukubali?) tuhumu zote dhidi yake.
Mapambano yaendelee.....
 
Nina maoni tofauti kidogo... Wengine katika mkutano huo huo, wanasema Pinda kasema Mkapa hawezi kukwepa kuchunguzwa na kama kuna jinai hatakwepa kushitakiwa,,.... sasa suala la kuzomewa nilimsikia akisema, "katika kuzingatia utawala wa sheria, hatuwezi kama serikali kuruhusu watu wamzomee rais mstaafu ama yeyote yule, kama kuna makosa yatashughulikiwa kwa taratibu zinazostahili na kwa hili la Mkapa linashughulikiwa".

Kwa maneno hayo sioni kosa la Pinda, nadhani kosa kubwa ni la Gazeti la Majira ambalo jana lilikuwa na story ya kumtetea Mkapa na leo wameendeleza tena bila kuandika chochote kuhusu Pinda kusema sheria itachukua mkondo wake... Kuna ajenda ya siri MAJIRA, tuangalie kwa upande huo na kwa makini zaidi

I support Pind if this is what he said. Lakini kitu ambacho inaelekea Pinda na wenzake hawaelewi ni sababu hasa za Mkapa kuzomewa. Utawala wa sheria hauwezi kushamiri wala watu hawawezi kuheshimu sheria kama hizo sheria (a) hazitekelezwi na (b) zinatekelezwa selectively. Sasa watu kibao sasa wametuhumiwa na ufisadi lakini so far hakuna hata moja hakuna hata moja aliyefikishwa mahakama. Sasa hii ndio sababu inawapekekea wananchi wachukue sheria mikononi mwao.
 
Kitila, hata mauaji ya watuhumiwa wa wizi/ujambazi ni kutokana na vyombo vya dola/mahakama kushindwa kuchukua hatua ama kuchelewa kuchukua hatua na watu wanazidi kuuwawa ama kuporwa mali zao na ndipo wanapoamua kujichukulia sheria mkononi, na kwa hili la Mkapa ni yale yale, serikali inasuasua kuchukua hatua na inatoa kauli za kutatanisha. Viongozi wetu wamekua waoga na dhaifu kiasi cha kushindwa kuchukua hatua. Wanasubiri upepo uwakumbe watuhumiwa ndio wafuate upepo. Richmond, JK aliijua hata kabla ya Mwakyembe, hakuchukua hatua, Chenge na vijisenti JK alijua mapema, hakuchukua hatua na badala yake alimpa ulaji zaidi, na ya Mkapa JK aliyajua tokea akiwa Waziri wa Mambo ya Nje, lakini hadi sasa, wanasema, "tutachunguza kujua kama kuna jinai", hayo ji danganya toto lakini wasitegemee kupigiwa vigelegele, bali kuzomewa, kutukanwa na baadaye kupigwa mawe na itafika wakati magari na nyumba kuchomwa moto (Mungu aepushe mbali).. Nasisitiza kinachotokea sasa ni kama LAANA kwa CCM na viongozi wake na nimewahi kusema hii ni sawa na 'ALBADIRI YA MBAYANA' inawaumbua, kwani kwa wanaoamini hayo wanasema kama CCM/viongozi wa CCM/Watawala walidhulumu, basi sasa albadiri inaanza kufanya kazi, kila wanalofanya ni kujipaka kinyesi na si kujisafisha na BADO tutaona mengi hadi ifikapo 2010, na kama wapinzani hawajajiandaa kushika usukani basi ataongoza hata "MTIKILA" maana watu wakichoka watapiga kura ya CHUKI na hiyo ni HATARI
 
Sasa kama mtu anadhalilishwa kwa maslai ya umma kuna tatizo!
Unajua mtu mpaka anafikia kumzomea raisi mstaafu ni kuwa serikali imelala kuwaadabisha hawa watu hatiame wanazagaa mtaani ingali iliwabidi wawe ata segerea wanavuna walichopanda.
Mtu ameiliza nchi na bado anatamba mtaani na msafara juu,si dharau hii jamani/
Na huu ni mwanzo am sure siku zinavyozidi kwenda yatajitokeza mengine kibao.
Unajua twaweza fikia ata hatua ya kujitoa mhanga kuhakikisha mafisadi wapunguze jeuri na kibri walio nayo
 
Back
Top Bottom