Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Kichuguu,
Mkuu tatizo la sheria sio swala la sisi kujua alivyoupata mradi wa Tanesco ama mingineyo isipokuwa inatutaka sisi kutoa ushahidi against yeye tukisha fanya uchunguzi wa njia zilizotumika..Mkapa hana haja ya kuzitoa hizo njia unless sisi tuwe na ushahidi kwanza kuthibitisha kwamba alikiuka sheria..
Sasa kama kuna mmoja wetu anazo hizo njia haramu zilizotumika nadhani itakuwa mwanzo mzuri..
Kama ningekuwa mimi na sii mwana CCM ningesema weka ndani itajulikana baadaye! lakini Kikwete sio Dikteta anatafuta haki na kuna hatari kubwa kama hatachukua hatua za Kisheria kuna watu nyuma ya huyu jamaa na wenzake wanaweza kuzua balaa ya kwa kutumia Udini, sasa hivi tu kuna watu wanaamini swala la Yona na Mramba limesababishwa na Kisasi..
tatizo wote tunajua Yona na Mramba walitumia vibaya madaraka yao na kujilimbikiza mali lakini hatuna ushahidi tosha zaidi ya kutumia hoja ya walitumia vibaya madaraka yao!..

Yona, Mramba, Karamagi nk walichunguzwa na vyombo vya sheria ikaonekana kuwa Yona na Mramba wana kesi ya kujibu, na Karamagi hana kesi ya kujibu. Basi vyombo hivyo hivyo pia vimchunguze Mkapa na kama ikionekana hana kesi ya kujibu watuambie hivyo
 
Kichuguu,
Mkuu tunarudi kule kule kuwa katiba inamlinda Mkapa tofauti na hao kina Yona, Mramba, Karamagi na wengine...Bunge pekee ndilo linaweza kuirudisha sheria ya kuwajibisha viongozi waliotumia madaraka yao vibaya na pengine uchunguzi kufanyika zaidi ya hapo mkuu chukulia kama baba kajamba!
 
Kichuguu,
Mkuu tunarudi kule kule kuwa katiba inamlinda Mkapa tofauti na hao kina Yona, Mramba, Karamagi na wengine...Bunge pekee ndilo linaweza kuirudisha sheria ya kuwajibisha viongozi waliotumia madaraka yao vibaya na pengine uchunguzi kufanyika zaidi ya hapo mkuu chukulia kama baba kajamba!


Mkandara, katiba haimlindi Mkapa hivyo hana kinga yeyote ya kama atashitakiwa. Kama Mkapa ana kinga, sio kinga ya kikatiba.
 
Kichuguu,
Mkuu tunarudi kule kule kuwa katiba inamlinda Mkapa tofauti na hao kina Yona, Mramba, Karamagi na wengine...Bunge pekee ndilo linaweza kuirudisha sheria ya kuwajibisha viongozi waliotumia madaraka yao vibaya na pengine uchunguzi kufanyika zaidi ya hapo mkuu chukulia kama baba kajamba!

Mkandara, mimi sikubaliani na hili la katiba inamlinda Mkapa. Katiba inamlinda Mkapa kwa maamuzi aliyoyafanya kama Rais wa Tanzania na siyo maamuzi aliyoyafanya kama Mkapa. Na hata aliyoyafanya kama Rais wa Tanzania kama alipewa rushwa ili kufikia maamuzi hayo basi katiba haimlindi huyo Fisadi mfano ni ununuzi wa Rada, ndege ya Rais, magari na helicopters za jeshi ambapo Mkapa ndiye alikuwa mshiriki mkubwa katika kufanya maamuzi ya ununuzi.

Fisadi Mkapa alipoamua kufanya biashara akiwa Ikulu alijua wazi katiba haimlindi na ndiyo maana akafanya siri na kutotutangazia Watanzania kwamba yeye kama Rais wa Watanzania ameamua pia kuwa mfanyabiashara wakati huo huo akiendelea na wadhifa wake wa Rais wa muungano.

Pia alipoamua kutupora Watanzania mgodi wa Kiwira alijua fika kwamba anachofanya si halali ndiyo maana kuuzwa kwa mgodi huo haukutangazwa hadharani kwa sababu walijua fika ingekua ni kasheshe ya hali ya juu na hivyo kununua kwake mgodi huo yeye na Yona, kusaini mkataba na TANESCO wa miaka 20 kwa shilingi bilioni 340 vyote vilifanywa siri kwa makusudi kabisa na nadhani mkataba huo ulisainiwa na wale makaburu walioletwa na fisadi Mkapa wa Net Group Problems.

Hivyo Fisadi Mkapa ana haki ya kuchunguzwa na hatimaye afikishwe mahakamani kujibu tuhuma nzito dhidi yake. Katiba ya Tanzania haimlindi Rais pale anapofanya wizi au hujuma dhidi ya Wananchi waliomchagua na kuna ushahidi wa kutosha tu wa kumtia hatiani fisadi Mkapa.
 
Jamani si jk katika hili alishajibu kwamba hawezi kumshitaki kwa sababu nchi haitakalika? au mimi ndiye nimesahau nini?

Hapana Mchukia fisadi, Tanzania itakalika tu tumechoka na hawa wanaojivisha ngozi ya uongozi ili kuwafisadi Watanzania ili kukidhi uroho wao wa utajiri wa haraka haraka kupitia migongo ya Watanzania. Na Mkapa ni mmoja wa mafisadi hao ambaye inabidi sheria iachwe ifuate mkondo wake.
 
Bubu ataka Kusema,
Mkandara, mimi sikubaliani na hili la katiba inamlinda Mkapa. Katiba inamlinda Mkapa kwa maamuzi aliyoyafanya kama Rais wa Tanzania na siyo maamuzi aliyoyafanya kama Mkapa
Mkuu labda sijakuelewa.. Ni maamuzi gani alofanya Mkapa ambayo kayafanya kama Mkapa na sio rais wa Tanzania!..
Kwani access na nguvu ya yote aliyoyafanya na tunayodai kayafanya ni kwa sababu alikuwa rais wa Tanzania na hayapingani na Azimio la Zanzibar - Uporaji.

Na kuhusu rada mnatakiwa kuthibitisha kuwa alipewa rushwa, hapo ndipo katiba haiwezi kumlinda lakini yeye kama rais mstaafu hatakiwi kujieleza kwa mtu yeyote kabla ya mashtaka!.. Ni jukumu letu sisi kuwa na ushahidi kwanza hata kama tunajua kajamba yeye!
 
Bubu ataka Kusema,

Mkuu labda sijakuelewa.. Ni maamuzi gani alofanya Mkapa ambayo kayafanya kama Mkapa na sio rais wa Tanzania!..
Kwani access na nguvu ya yote aliyoyafanya na tunayodai kayafanya ni kwa sababu alikuwa rais wa Tanzania na hayapingani na Azimio la Zanzibar - Uporaji.

Na kuhusu rada mnatakiwa kuthibitisha kuwa alipewa rushwa, hapo ndipo katiba haiwezi kumlinda lakini yeye kama rais mstaafu hatakiwi kujieleza kwa mtu yeyote kabla ya mashtaka!.. Ni jukumu letu sisi kuwa na ushahidi kwanza hata kama tunajua kajamba yeye!

Alipoamua kufanya biashara akiwa Ikulu uamuzi ule haukuwahusu Watanzania. Pia alipoamua kutupora mgodi wa Kiwira na kuwashinikiza wakuu wa TANESCO wakati ule kusaini mkataba na 'kampuni' alifanya maamuzi yale kama Mkapa na siyo kama Rais wa Tanzania.

Huwezi kufungua mashtaka dhidi ya mtu yeyote yule bila ya kuwa na ushahidi wa tuhuma dhidi ya mshtakiwa. Hivyo inabidi Mkapa achunguzwe maamuzi yake mbali mbali aliyoyafanya yakiwamo ya rada, ndege ya Rais, mikataba ya uchimbaji n.k. ili kukusanya ushahidi mbali mbali ambao unaweza kumtia hatiani.
 
Bubu ataka kusema,
Alipoamua kufanya biashara akiwa Ikulu uamuzi ule haukuwahusu Watanzania. Pia alipoamua kutupora mgodi wa Kiwira na kuwashinikiza wakuu wa TANESCO wakati ule kusaini mkataba na 'kampuni' alifanya maamuzi yale kama Mkapa na siyo kama Rais wa Tanzania.
Mkuu bado sijakuelewa naomba ufafanuzi wa yeye kufanya maamuzi hayo kama Mkapa..

1. Azimio la Zanzibar lilimruhusu kufanya biashara haikueleza kama Ikulu hapafai wala haparuhusiwi, ndio Ofisi na makazi yake kama rais na sio Mkapa..
2. Uwezo wa kupora Kiwira mtu kama Mkapa bila kuwa rais aliwezaje... na mashrti gani yalikuwepo ambayo hakuyafuata!..
 
Bubu ataka Kusema,

Mkuu labda sijakuelewa.. Ni maamuzi gani alofanya Mkapa ambayo kayafanya kama Mkapa na sio rais wa Tanzania!..
Kwani access na nguvu ya yote aliyoyafanya na tunayodai kayafanya ni kwa sababu alikuwa rais wa Tanzania na hayapingani na Azimio la Zanzibar - Uporaji.

Na kuhusu rada mnatakiwa kuthibitisha kuwa alipewa rushwa, hapo ndipo katiba haiwezi kumlinda lakini yeye kama rais mstaafu hatakiwi kujieleza kwa mtu yeyote kabla ya mashtaka!.. Ni jukumu letu sisi kuwa na ushahidi kwanza hata kama tunajua kajamba yeye!

Kaka Mkandara,

Nadhani wewe unaloshindwa kutofautisha ni kuwa rais ni binadamu kama wewe na mimi.
 
Bubu ataka kusema,

Mkuu bado sijakuelewa naomba ufafanuzi wa yeye kufanya maamuzi hayo kama Mkapa..

1. Azimio la Zanzibar lilimruhusu kufanya biashara haikueleza kama Ikulu hapafai wala haparuhusiwi, ndio Ofisi na makazi yake kama rais na sio Mkapa..
2. Uwezo wa kupora Kiwira mtu kama Mkapa bila kuwa rais aliwezaje... na mashrti gani yalikuwepo ambayo hakuyafuata!..

Hayo yote ndiyo yatajulikana baada ya huo uchunguzi. Je, alivyoamua kufanya biasha akiwa Ikulu Azimio la Zenj lilimruhusu? Je, alipoamua kutupora Kiwira alitumia madaraka yake kama Rais wa Tanzania ili kujinufaisha? Je, Alivunja sheria zozote ili kujimilikisha mgodi huo na hatimaye kusaini mkataba wa miaka 20 na TANESCO wenye thamani ya shilingi bilioni 340? Je alipoamua kufanya mikataba ya uchimbaji dhahabu siri alivunja sheria zozote? Je alinufaika katika ununuzi wa ndege ya Rais, Rada, magari na helicopters za jeshi ambapo kote huko kumegubikwa na harufu ya rushwa na ufisadi?

Kama kuna ushahidi wa kutosha dhidi yake basi ni wa kufikishwa mahakamani na sheria iachwe ifuate mkondo wake. Katiba ya Tanzania kamwe hamlindi Rais ambaye ni mwizi na fisadi aliyewahujumu wale waliomweka madarakani.
 
I think one important thing JamiiForum is missing is the concrete plan of action. We increasingly debate without moving forward. It's time now to put our debate, analysis, perspectives, etc. into action. The constitution allows us to sue Mkapa. In the process we will be able to debate whether this man has immunity or not for the dirty he commited while in Ikulu. Kikwete could not initiate every move. We need to push him. The president needs our support now more than ever.

NGOS, MEDIA, LAYERS ASSOCIATION, OPPOSTION PARTIES, BLOGERS......LET US DO SOMETHING NOW. LET US SUE MKAPA RIGHT AWAY! YES WE CAN!
 
I think one important thing JamiiForum is missing is the concrete plan of action. We increasingly debate without moving forward. It's time now to put our debate, analysis, perspectives, etc. into action. The constitution allows us to sue Mkapa. In the process we we be able to debate whether this man has immunity or not for the dirty he commited while in Ikulu. Kikwete could not initiate every move. We need to push him. The president needs our support now more than ever.

NGOS, MEDIA, LAYERS ASSOCIATION, OPPOSTION PARTIES, BLOGERS......LET US DO SOMETHING NOW. LET US SUE MKAPA RIGHT AWAY! YES WE CAN!

- Cool, I am down!
 
Kichuguu,
Mkuu nakueleweni nyote isipokuwa nasimama upande wa pili kuona kama sisi tunao ushahidi tosha wa kumsimamisha Mkapa mahakamani. Chukulia tu kwamba mimi ni mwajiriwa upande wa utetezi kumwakilisha Mkapa ktk hoja za hapa lakini haina maana namuunga mkono ama siamini kwamba hakuhusika na hujuma za uchumi wa nchi yetu.

Mkuu nachokiona hapa kulingana na hoja zilizotangulia ni matokeo ya kile tulichokiona Mkapa kisha simamisha. Sawa na muuza unga aliyejenga nyumba lakini hata siku moja hajakamatwa na unga.. Hiyo nyumba sio ushahidi wa kuuza unga na hata kama tukifanya uchunguzi biashara yake ya kuuza nguo za India au Pakistan inaweza kuvunja tuhuma zote halali..Kinachotakiwa ni ushahidi zaidi, uchunguzi zaidi na pengine Kikwete anayafanya haya bila wananchi kufahamu.. unajua tena FBI..
Pamoja nayote haya, hakuna hata mmoja wetu anayefahamu mali za Mkapa zilipatikana kwa njia gani zaidi ya kusema haramu.. je alifanya nini kinyume cha sheria hadi tuite haramu....No one knows!
Pili, discussion yote hii ni ktk kutafuta njia za kumshitaki Mkapa kama rais mstaafu na sio Mkapa.. Huo ndio msisitizo wangu na ndio sababu sote tumetazama katiba kama inamlinda, laa sivyo sioni sababu ya kutazama katiba ikiwa yeye ni Mkapa na binadamu kama sisi...Ndani ya katiba kuna kipengele hicho kinachomhusu rais peke yake tofauti na sheria nyingine zinazowahusu watu wote...Mimi na wewe hatuwezi kuwa impeached isipokuwa kiongozi wa nchi na sio Mkapa..sheria ipo kwa WHO is he/she hilo jina imetokea tu kuwa jina lake linaitwa Mkapa.

Viongozi wa Kiafrika ni Miungu na sheria zilizowekwa zimeambatana na Azimio linalomruhusu wala sio yeye pekee yake.. Viongozi wote wa chama wamenufaika na madaraka tuliyowakabidhi. waziri wa Utalii walifungua ofisi za Utalii, Kilimo walinunua mashamba, Afya wakafungua mahospital, Elimu wkafungua mashule lakini wote wametumia ujanja ujanja kuweza kuficha madhambi yao na kisheria inakuwa kazi sana kuwabana wote kwa sababu kwanza hilo Azimio la Zanzibar ambalo liliruhusu Conflict of interest..na haikuwa dhambi kama ilivyokuwa Takrima ktk uchaguzi uliopita..
Sasa ikiwa leo hii tukiondoa takrima na kuiharamisha Je, tunaweza kutumia sheria hiyo mpya kuwahukumu viongozi waliopita ktk uchaguzi wa 2005..kisheria sidhani!
Ndio maana msisitizo wangu ni kujaribu kuwaonyesha nyote kwamba kuhusiana na Mkapa tumesha liwa wakuu zangu. hakuna mtu humu JF ambaye atafurahi sana kuona Mjomba katinga Kisutu ama mahakama yoyote zaidi yangu... nina usongo na mtu yule isipokuwa nikitazama possibility kisheria sioni ndani kabisa zaidi ya kuwepo Mageuzi/Mapinduzi ya utawala...
Kikatiba, he is above the law wajomba!
 
Kichuguu,
Mkuu nakueleweni nyote isipokuwa nasimama upande wa pili kuona kama sisi tunao ushahidi tosha wa kumsimamisha Mkapa mahakamani. Chukulia tu kwamba mimi ni mwajiriwa upande wa utetezi kumwakilisha Mkapa ktk hoja za hapa lakini haina maana namuunga mkono ama siamini kwamba hakuhusika na hujuma za uchumi wa nchi yetu.

Mkuu nachokiona hapa kulingana na hoja zilizotangulia ni matokeo ya kile tulichokiona Mkapa kisha simamisha. Sawa na muuza unga aliyejenga nyumba lakini hata siku moja hajakamatwa na unga.. Hiyo nyumba sio ushahidi wa kuuza unga na hata kama tukifanya uchunguzi biashara yake ya kuuza nguo za India au Pakistan inaweza kuvunja tuhuma zote halali..Kinachotakiwa ni ushahidi zaidi, uchunguzi zaidi na pengine Kikwete anayafanya haya bila wananchi kufahamu.. unajua tena FBI..
Pamoja nayote haya, hakuna hata mmoja wetu anayefahamu mali za Mkapa zilipatikana kwa njia gani zaidi ya kusema haramu.. je alifanya nini kinyume cha sheria hadi tuite haramu....No one knows!
Pili, discussion yote hii ni ktk kutafuta njia za kumshitaki Mkapa kama rais mstaafu na sio Mkapa.. Huo ndio msisitizo wangu na ndio sababu sote tumetazama katiba kama inamlinda, laa sivyo sioni sababu ya kutazama katiba ikiwa yeye ni Mkapa na binadamu kama sisi...Ndani ya katiba kuna kipengele hicho kinachomhusu rais peke yake tofauti na sheria nyingine zinazowahusu watu wote...Mimi na wewe hatuwezi kuwa impeached isipokuwa kiongozi wa nchi na sio Mkapa..sheria ipo kwa WHO is he/she hilo jina imetokea tu kuwa jina lake linaitwa Mkapa.

Viongozi wa Kiafrika ni Miungu na sheria zilizowekwa zimeambatana na Azimio linalomruhusu wala sio yeye pekee yake.. Viongozi wote wa chama wamenufaika na madaraka tuliyowakabidhi. waziri wa Utalii walifungua ofisi za Utalii, Kilimo walinunua mashamba, Afya wakafungua mahospital, Elimu wkafungua mashule lakini wote wametumia ujanja ujanja kuweza kuficha madhambi yao na kisheria inakuwa kazi sana kuwabana wote kwa sababu kwanza hilo Azimio la Zanzibar ambalo liliruhusu Conflict of interest..na haikuwa dhambi kama ilivyokuwa Takrima ktk uchaguzi uliopita..
Sasa ikiwa leo hii tukiondoa takrima na kuiharamisha Je, tunaweza kutumia sheria hiyo mpya kuwahukumu viongozi waliopita ktk uchaguzi wa 2005..kisheria sidhani!
Ndio maana msisitizo wangu ni kujaribu kuwaonyesha nyote kwamba kuhusiana na Mkapa tumesha liwa wakuu zangu. hakuna mtu humu JF ambaye atafurahi sana kuona Mjomba katinga Kisutu ama mahakama yoyote zaidi yangu... nina usongo na mtu yule isipokuwa nikitazama possibility kisheria sioni ndani kabisa zaidi ya kuwepo Mageuzi/Mapinduzi ya utawala...
Kikatiba, he is above the law wajomba!

Kamwe katiba ya Tanzania haipo pale ili kumlinda Rais mwizi, fisadi na anayewahujumu wananchi waliomchagua. Na ushahidi wa kumfikisha mahakamani fisadi Mkapa hauwezi kupatikana hewani inabidi uchunguzi ufanyike na kama inabidi kuhojiwa basi ahojiwe na kama kuna ushadi wa kutosha ashtakiwe kwa tuhuma dhidi yake. Haiwezekani kabisa hao walioandika katiba hiyo kuandika katiba kwa kukusudia katiba hiyo imlinde Rais mwizi, fisadi na mhujumu uchumi wa nchi.
 
Hata USA wakati wa skendo ya ngono ya Bill Clinton sio vyombo vya serikali vilivyom-bana. Ni mwendesha mashtaka binafsi. Nadhani imefika wakati sasa hata sisi hapa TZ tuchukue hatua kwa vitendo. Mtikila alifanikiwa sana kwenye suala hili la kutumia mahakama (naona amepunguza kasi na yeye siku hizi). Tukiwa na dhamira ya dhati na kuwa tayari kufanya kazi kwa kushirikiana makundi mbalimbali na wanasheria wetu, huyu bwana Mkapa hatafika mbali, tutamnasa tu!

Mnakumbuka Legal and Human Rights walilipeleka suala la Takrima mahakamani na wapenda haki wote tukashinda? Let's surge forward folks!
 
Hapana Mchukia fisadi, Tanzania itakalika tu tumechoka na hawa wanaojivisha ngozi ya uongozi ili kuwafisadi Watanzania ili kukidhi uroho wao wa utajiri wa haraka haraka kupitia migongo ya Watanzania. Na Mkapa ni mmoja wa mafisadi hao ambaye inabidi sheria iachwe ifuate mkondo wake.

Sawa BAK lakini nakumbuka alisema tumuache mzee apumzike? maana yake na yeye anakubaliana na wizi wa kiongozi mwenzake.
Ole wao!
 
Bubu Aataka Kusema,
Mkuu kweli kabisa katiba haimruhusu rais mwizi...Je, unaweza kunambia aliiba vipi? navyofahamu mimi mwizi wa chungwa sokoni mkamate akiiba, au ana chungwa liloibwa, ama kuna shahidi aliyemwona akiiba...lakini wakati huo huo ubishi wangu unakuja pale napomwoina huyu mtu anayeitwa mwizi alichuma machungwa shambani wakati ambao kuchuma chungwa shambani haikuitwa wizi..Mwenye shamba aliingia hasara kweli lakini unapokwenda shtaki ktk korti ya kijijini utawaambia vipi wazee wa baraza wakuelewe!..
Nachoogopa mimi ni kwamba leo hii Mkapa ambaye sio rais tena ila mstaafu anaweza shtakiwa kwa kosa la leo kama Mkapa...Tunaporudi nyuma wakati akiwa rais ni lazima sheria za mwaka huo zitumike na hapo ndipo tunapokuta Azimio la Zanzibar ambalo limewa nguvu ya kuchukua mali za serikali kwa mtaji mbuzi..Na bado wanaendelea kulitumia wakuchukua nyumba za serikali worth billions kwa asilimia 10 tu..

Unless kama alivyo suggest Nurujamii iundwe commission ya uchunguzi kuhusiana na machafu ya viongozi waliotumia madaraka yao vibaya kisha iundwe special tribunal...(nani ataunda hilo sijui)bila kuonyesha kuwa Mkapa ndiye target kwani haki haiwezi kuchagua mtu mmoja ktk kundi la viongozi wachafu wote.. Nina hakika hii itawavuta wengi sana toka utawala wa Mwinyi kwani nako waliyafanya kama alofanya Mkapa kwa gharama kubwa..
Tusitegemee kabisa kuwa Kikwete anaweza kufanya hivyo!..Inawezekana kabisa kuwa hayaoni hata mabaya ya Utawala wa Mkapa kwa sababu alikuwa general ktk Utawala wa Hitler..Ni vigumu sana kufikiria kwamba general wa Hitler anaweza kufikiria leo mabaya ya Hitler wakati yeye mwenyewe alikuwa mhusika hata kama alipewa amri ama ilikuwa moja ya kazi yake kuongoza mauaji..
 
Samahani, tunapolizungumzia Azimio la Zanzibar tunazungumzia kama Azimio lililobadilisha sheria au ni azimio ambalo watawala walikaa wakaamua kuwa hili na hili lifanyike maana sijaona popote hata katika Sheria yao ya maadili walikosema kuwa sheria zinazotawala maadili ya viongozi zinabadilika na kwa sasa viongozi wafuate matakwa ya azimio la Zanzibar

samahanini kama nimeenda nje ya topic ila naomba ufafanuzi
 
Kwa kweli mimi binafsi nasikitishwa sana jinsi watu makini sana hapa JF tunavyotumia muda mwingi sana hapa kumshupalia mzee Mkapa kwa makosa aliyoyafanya akiwa ikulu! hili swala la kuzungumzia kumpeleka Mkapa mahakamani halina maana kabisa, ni wendawazimu tu! hizi ni fikra hafifu kabisa ambazo ni hatari sana kwa demokrasia ya nchi, kama mkapa amefanya kosa akiwa rais, basi ni wajibu wa rais anayefuata kutengua hayo maamuzi 'mabaya' ya rais aliyetangulia na nhi ikaendelea mbele, mfano tu tunamsikia Obama akiainisha maamuzi ya rais Bush ambayo yeye atabalisha mara atakapoingia ikulu...hatumsikii Obama akisema atampeleka rais Bush mahakamani kwa maamuzi yake mabaya sana yaliyoigharimu Marekani na dunia kwa ujumla! lakini katika nchi yetu maskini kabisa, watu makini kabisa tumejisahau kabisa na kuongelea hili kama vile ndilo jambo muhimu kabisa na kusahau kwamba wananchi wetu wanazidi kuteseka na serikali yetu kwa kweli inahitaji msaada wa kifikra ya jinsi ya kumnasua mtanzania kwenye umaskini uliokithiri. whether we take Mkapa to court or not does not have effect on the livelyhood ya mtu mtu wa kawaida, lakini kama the sitting president can reverse his decisions, hiyo inaweza kusaidia jamii.
Nimesema hapo juu kwamba swala la kukimbilia kuondoa immunity ya rais mstaafu na kumpeleka ni hatari sana kwa demokrasia kwa sababu inaweza kuanzisha madikteta kwa sababu rais ataona kwamba akistaafu atashitakiwa na kusumbuliwa hivyo ni vyema apiganea abakie madarakani. Mimi nafikiri tuige wenzetu wa nchi za magharibi hususan marekani wanavyofanya, rais anayeingia madarakani aweze kutengua maamuzi ya rais aliyetangulia na kumwacha mstaafu aendelee kuishi bila bughudha. narudia tena kusema hili la kumsakama Mkapa aondolewe kinga ni sawa na 'kuuza dume kwa ajili ya kesi ya kuku'... Watanzania tuna matatizo mengi mazito kabisa yanayohitaji uchambuzi mzuri wa wana JF.
 
Kwa kweli mimi binafsi nasikitishwa sana jinsi watu makini sana hapa JF tunavyotumia muda mwingi sana hapa kumshupalia mzee Mkapa kwa makosa aliyoyafanya akiwa ikulu! hili swala la kuzungumzia kumpeleka Mkapa mahakamani halina maana kabisa, ni wendawazimu tu! hizi ni fikra hafifu kabisa ambazo ni hatari sana kwa demokrasia ya nchi, kama mkapa amefanya kosa akiwa rais, basi ni wajibu wa rais anayefuata kutengua hayo maamuzi 'mabaya' ya rais aliyetangulia na nhi ikaendelea mbele, mfano tu tunamsikia Obama akiainisha maamuzi ya rais Bush ambayo yeye atabalisha mara atakapoingia ikulu...hatumsikii Obama akisema atampeleka rais Bush mahakamani kwa maamuzi yake mabaya sana yaliyoigharimu Marekani na dunia kwa ujumla! lakini katika nchi yetu maskini kabisa, watu makini kabisa tumejisahau kabisa na kuongelea hili kama vile ndilo jambo muhimu kabisa na kusahau kwamba wananchi wetu wanazidi kuteseka na serikali yetu kwa kweli inahitaji msaada wa kifikra ya jinsi ya kumnasua mtanzania kwenye umaskini uliokithiri. whether we take Mkapa to court or not does not have effect on the livelyhood ya mtu mtu wa kawaida, lakini kama the sitting president can reverse his decisions, hiyo inaweza kusaidia jamii.
Nimesema hapo juu kwamba swala la kukimbilia kuondoa immunity ya rais mstaafu na kumpeleka ni hatari sana kwa demokrasia kwa sababu inaweza kuanzisha madikteta kwa sababu rais ataona kwamba akistaafu atashitakiwa na kusumbuliwa hivyo ni vyema apiganea abakie madarakani. Mimi nafikiri tuige wenzetu wa nchi za magharibi hususan marekani wanavyofanya, rais anayeingia madarakani aweze kutengua maamuzi ya rais aliyetangulia na kumwacha mstaafu aendelee kuishi bila bughudha. narudia tena kusema hili la kumsakama Mkapa aondolewe kinga ni sawa na 'kuuza dume kwa ajili ya kesi ya kuku'... Watanzania tuna matatizo mengi mazito kabisa yanayohitaji uchambuzi mzuri wa wana JF.
Tunaotaka rais Mkapa ashitakiwe tunataka haki ifanyike kwa wizi wa mali ya umma alioufanya akiwa Ikulu. Na si kwa sababu za maamuzi aliyoyafanya akiwa rais. Ukilielewa hilo utatuelewa.
 
Back
Top Bottom