Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Tumechoka na maneno yenu.Mambo mangapi mazuri Mkapa ameifanyia Tanzania?Ila kwa vile mmeumbwa kuona mabaya tu hamtaki kuyakumbuka mazuri.Waulizeni awamu ya nne ile jeuri ya kuunda baraza la utitiri wa mawaziri waliipata wapi?
Halafu kwa nini mumuone Mkapa tu?Mbona hamzungumzii ufisadi alioufanya Mwinyi na mama siti awamu ya pili?Mbona hampigi kelele na wao wafikishwe kwenye mkono wa sheria?
Au bado mna wivu wa kike kwavile aliwaambia ni wavivu wa kufikiri?

Tuchukulie kuwa unayosema ni kweli, kuna mambo mazuri aliyofanya Mkapa ambayo hatuyaongelei.

Je, umewahi kuona mwanamke aliyelea mimba ya mtoto pamoja na usumbufu wake mpaka akamzaa mtoto na akamlea mtoto yule vizuri hadi alipofikia umri wa kuanza shule ndipo mama yule akamvunja mtoto mikono yote na kumtupa porini? Je unadhani mama huyu atakushukuriwa kwa kumlea mtoto hadi umri ule au atakumbukuwa kwa madhara aliyomwachia mtoto yule maisha yake yote.
 
Rais Kikwete, nakuomba usicheze nalenale, ushamfikisha Mramba, Yona na Mgonja, tunamtaka Lowassa, Rostam na zaidi ya yote, tunamtaka Mramba.

Mkuu Rev heshima mbele nakupa 100%, Ila hapo kidogo nafikiri ulitereza badala ya MKAPA ukaandika MRAMBA, sijui lakini ila nimekupata. TUNAMTAKA MKAPA
 
Tumechoka na maneno yenu. Mambo mangapi mazuri Mkapa ameifanyia Tanzania? Ila kwa vile mmeumbwa kuona mabaya tu hamtaki kuyakumbuka mazuri. Waulizeni awamu ya nne ile jeuri ya kuunda baraza la utitiri wa mawaziri waliipata wapi?

Halafu kwa nini mumuone Mkapa tu? Mbona hamzungumzii ufisadi alioufanya Mwinyi na mama siti awamu ya pili? Mbona hampigi kelele na wao wafikishwe kwenye mkono wa sheria?
Au bado mna wivu wa kike kwavile aliwaambia ni wavivu wa kufikiri?


Kwa nini usianzishe thread yako ukawajadili Mwinyi na Mama Sitti? au ukaanzisha thread kusifu aliyofanya Mkapa? kwa nini utulazimishe kuongea unalotaka na usilianzishie hoja?
 
Mkuu Rev heshima mbele nakupa 100%, Ila hapo kidogo nafikiri ulitereza badala ya MKAPA ukaandika MRAMBA, sijui lakini ila nimekupata. TUNAMTAKA MKAPA

Oh my! That's who I want and I want him bad. Gotdamnit! If I could only get my hands on him...if I only could.
 
Jinsi kila kitu kinavyosambaratika na kuangamia, uharamia, uzembe, ukosefu uadilifu, kukosa uungwana na utu, hujuma, wizi, ufisadi na dhuluma zikiongezeka, vifole vyote vinabidi vimnyokee mtu mmoja, Benjamin William Mkapa, Rais wa Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
.

Ahsante kwa chachu nzuri Mchungaji,
Hapa tupo pamoja kabisa, bila yeye kina Mramba hawana vichwa, vile ni viwiliwili tu. Inabidi kichwa kiwepo ili mwili uweze kukamilika!
 
You have beaten right on the bush. Mimi nakumbuka Mkapa alikuwa anasema kuwa utawala wake ulikuwa ni utawala wa ukweli na uwazi, kupambana na ufisadi(lakini ajabu ni kuwa) alisema rushwa ndogondogo ndiyo inayoumiza sana wananchi na alitaka kupambana na hiyo, no wonder why aliwacha kina EPA na kuikalia kimya grand corruption. Kuikalia kimya Grand corruption kunaendana kinyume na nyote aliyokuwa akiyatangaza hadharani.
Lakini ni vizuri akipewa nafasi aseme yapi ni ya kwake na yapi si ya kwake. Inabidi akubali kwanza la mauaji ya Zanzibar na kusema alilea mafisadi. Aqt least hayo tunayafahamu akisema na mengine na kutuambia ni yepi ambayo si yake, then atakuwa mzalendo wa kweli
 
Kwa nini usianzishe thread yako ukawajadili Mwinyi na Mama Sitti? au ukaanzisha thread kusifu aliyofanya Mkapa? kwa nini utulazimishe kuongea unalotaka na usilianzishie hoja?

Hayo ndiyo majibu ya wana JF wengi wakishakosolewa.ohh Anzisha thread yako!
Siku nyingine ukianzisha thread weka onyo kabisa kuwa watu wenye mtizamo tofauti na wako wasichangie!
 
Tuchukulie kuwa unayosema ni kweli, kuna mambo mazuri aliyofanya Mkapa ambayo hatuyaongelei.

Je, umewahi kuona mwanamke aliyelea mimba ya mtoto pamoja na usumbufu wake mpaka akamzaa mtoto na akamlea mtoto yule vizuri hadi alipofikia umri wa kuanza shule ndipo mama yule akamvunja mtoto mikono yote na kumtupa porini? Je unadhani mama huyu atakushukuriwa kwa kumlea mtoto hadi umri ule au atakumbukuwa kwa madhara aliyomwachia mtoto yule maisha yake yote.

Mbona unatoa mfano wa mama pekee kama mlezi wa mtoto?Kama baba alishaanza kumvunja miguu huyo mtoto kwanini lawama abebeshwe mama peke yake?Na mbona hutoi sababu zilizomfanya mama kumvunja mikono yule mtoto?Umejuaje,labda mtoto alipata hitilafu ya mikono angali tumboni(congenital) na ilibidi kwa vyovyote mikono ile ivunjike whether spontaneously or by induction?
 
Hayo ndiyo majibu ya wana JF wengi wakishakosolewa.ohh Anzisha thread yako!
Siku nyingine ukianzisha thread weka onyo kabisa kuwa watu wenye mtizamo tofauti na wako wasichangie!

Sikiza wewe,hii ni forum moja.Kokote utakoweka thread itafikiwa na kusomwa na kuchangiwa if it is wirth it.Kwanini ung'ang'ane kubanana hapahapa kwenye thread hii tu?Ushauri uliopewa ni mwafaka kabisa.Anzisha thread nyingine ili huo upande mwingine wa Ben ujadiliwe kwa kina na mapana stahiki.

Pili,unamtaka mwinyi na siti wake:fine.Hakuna akuzuiaye kuwataka hao kortini,weka thread nyingine.Jenga hoja.

Kinachokutia woga kufanya hivyo ni nini?Au hujiamnini?Unadhani members hawatapita huko?Is that why unadandia dandia thread maalum kwa malengo kinyume na ya mwanzisha thread?Wewe vipi wewe?Ala!
 
Sikiza wewe,hii ni forum moja.Kokote utakoweka thread itafikiwa na kusomwa na kuchangiwa if it is wirth it.Kwanini ung'ang'ane kubanana hapahapa kwenye thread hii tu?Ushauri uliopewa ni mwafaka kabisa.Anzisha thread nyingine ili huo upande mwingine wa Ben ujadiliwe kwa kina na mapana stahiki.

Pili,unamtaka mwinyi na siti wake:fine.Hakuna akuzuiaye kuwataka hao kortini,weka thread nyingine.Jenga hoja.

Kinachokutia woga kufanya hivyo ni nini?Au hujiamnini?Unadhani members hawatapita huko?Is that why unadandia dandia thread maalum kwa malengo kinyume na ya mwanzisha thread?Wewe vipi wewe?Ala!

Kwahiyo unachotaka kusema ni kuwa mtu akianzisha thread basi wote tuchangie kama anavyotaka yeye na si vinginevyo?
 
Mbona unatoa mfano wa mama pekee kama mlezi wa mtoto?Kama baba alishaanza kumvunja miguu huyo mtoto kwanini lawama abebeshwe mama peke yake?Na mbona hutoi sababu zilizomfanya mama kumvunja mikono yule mtoto?Umejuaje,labda mtoto alipata hitilafu ya mikono angali tumboni(congenital) na ilibidi kwa vyovyote mikono ile ivunjike whether spontaneously or by induction?

Mwanzoni nilichukulia critique yako kama ni constructive lakini sasa naona unataka kuleta ubishi usio kuwa na maana yoyote. Hebu tufahamishe sababu za maana unazoona kuwa ndizo zilizomfanya Mkapa aanze kujenga utawala wenye kuendekeza rushwa na jinsi hatua hiyo ilivyosaidia kutuondolea tatizo tulilozaliwa nalo la umaskini. Ni rushwa hiyo ndiyo iliyosababisha mikataba yote iliyoandikwa wakati wa utawala wake kuwa haina manufaa yoyote kwa nchi kwa vile iliandikwa ikiwa inaangalia rushwa zaidi.
 
Mbona unatoa mfano wa mama pekee kama mlezi wa mtoto?Kama baba alishaanza kumvunja miguu huyo mtoto kwanini lawama abebeshwe mama peke yake?Na mbona hutoi sababu zilizomfanya mama kumvunja mikono yule mtoto?Umejuaje,labda mtoto alipata hitilafu ya mikono angali tumboni(congenital) na ilibidi kwa vyovyote mikono ile ivunjike whether spontaneously or by induction?
Wewe umetumwa nini, ndio maana kuna mtu alikuandikia kwamba basi Mkapa asingekula kiapo wakati anataka kuiongoza Tanzania, ingawa sijui kwenye kiapo unatumia maneno gani lakini najua hayo maneno aliyokuwa akiapa pale kaenda kinyume chake, maana najua kimoja ilikuwa ni kulinda wananchi wa Tanzania na hakufanya hivyo Mwembechai na Pemba, na kingine ilikuwa ni kulinda mali za nchi na kakiuka hicho, kauza na kujiuzia na kufanya uzembe kazini. Hizi kama wewe umeiba kazini kwanini usifungwe? Ukiiba uraiani na ukiiba ukiwa Raisi wote ni uwizi tuu, nadhani ukiwa kazini unasaini mahali ambapo hutakiwwi kuiba. NAOMBA WATU WENYE KIAPO CHA RAISI WATUWEKEE HAPA ILI TUONE KAMA MKAPA AKIWA RAISI HAKUKIUKA KIAPO CHAKE.
 
Kwahiyo unachotaka kusema ni kuwa mtu akianzisha thread basi wote tuchangie kama anavyotaka yeye na si vinginevyo?

Hoja yangu ni hii:unga mkono au pinga kwa hoja sio kuleta mada tofauti kabisa ndani ya mada nyingine.We need coherence and consistency in exhausting a given point.Ya mwinyi na sitti yametoka wapi palee?
 
Mwanzoni nilichukulia critique yako kama ni constructive lakini sasa naona unataka kuleta ubishi usio kuwa na maana yoyote. Hebu tufahamishe sababu za maana unazoona kuwa ndizo zilizomfanya Mkapa aanze kujenga utawala wenye kuendekeza rushwa na jinsi hatua hiyo ilivyosaidia kutuondolea tatizo tulilozaliwa nalo la umaskini. Ni rushwa hiyo ndiyo iliyosababisha mikataba yote iliyoandikwa wakati wa utawala wake kuwa haina manufaa yoyote kwa nchi kwa vile iliandikwa ikiwa inaangalia rushwa zaidi.

Mwinyi naye akamatwe afikishwe kwenye vyombo vya sheria
1.Mkewe alikamatwa na magendo live uwanja wa ndege.
2.Alikuwa anafanya mapenzi na mtoto mwanafunzi wa jangwani kinyume cha sheria
 
Tumechoka na maneno yenu. Mambo mangapi mazuri Mkapa ameifanyia Tanzania? Ila kwa vile mmeumbwa kuona mabaya tu hamtaki kuyakumbuka mazuri. Waulizeni awamu ya nne ile jeuri ya kuunda baraza la utitiri wa mawaziri waliipata wapi?

Halafu kwa nini mumuone Mkapa tu? Mbona hamzungumzii ufisadi alioufanya Mwinyi na mama siti awamu ya pili? Mbona hampigi kelele na wao wafikishwe kwenye mkono wa sheria?
Au bado mna wivu wa kike kwavile aliwaambia ni wavivu wa kufikiri?

Mzee uzalendo unakushinda.
 
Mwanzoni nilichukulia critique yako kama ni constructive lakini sasa naona unataka kuleta ubishi usio kuwa na maana yoyote. Hebu tufahamishe sababu za maana unazoona kuwa ndizo zilizomfanya Mkapa aanze kujenga utawala wenye kuendekeza rushwa na jinsi hatua hiyo ilivyosaidia kutuondolea tatizo tulilozaliwa nalo la umaskini. Ni rushwa hiyo ndiyo iliyosababisha mikataba yote iliyoandikwa wakati wa utawala wake kuwa haina manufaa yoyote kwa nchi kwa vile iliandikwa ikiwa inaangalia rushwa zaidi.

Hivi kama unazungumzia rushwa katika tawala za Tanzania ni awamu ipi haikuwa na rushwa?Ni awamu ipi ilikuwa na rushwa iliyokithiri na hata kutishia mustakabali wa taifa?Hivi unaikumbuka rushwa ya utawala wa Mwinyi ilivyokuwa?Unakumbuka kiasi cha kodi kilichokuwa kinakusanywa na serikali ya Mwinyi kwa mwezi?Sasa kwanini rushwa muione wakati wa Mkapa tu?Je utawala wa Mwinyi haukuingia mkataba wowote ule,haukufanya magendo?Sasa kwa nini kila siku haya hamyaoni na badala yake ni Mkapa,Mkapa tu?
Tuache unafiki wabongo.
 
Hoja yangu ni hii:unga mkono au pinga kwa hoja sio kuleta mada tofauti kabisa ndani ya mada nyingine.We need coherence and consistency in exhausting a given point.Ya mwinyi na sitti yametoka wapi palee?

Hakuna mada tofauti.Mada ni moja katika ujumla wake,yaani rushwa,matumizi mabaya ya pesa ya uma na utawala mbovu tanzania.
 
Wewe umetumwa nini, ndio maana kuna mtu alikuandikia kwamba basi Mkapa asingekula kiapo wakati anataka kuiongoza Tanzania, ingawa sijui kwenye kiapo unatumia maneno gani lakini najua hayo maneno aliyokuwa akiapa pale kaenda kinyume chake, maana najua kimoja ilikuwa ni kulinda wananchi wa Tanzania na hakufanya hivyo Mwembechai na Pemba, na kingine ilikuwa ni kulinda mali za nchi na kakiuka hicho, kauza na kujiuzia na kufanya uzembe kazini. Hizi kama wewe umeiba kazini kwanini usifungwe? Ukiiba uraiani na ukiiba ukiwa Raisi wote ni uwizi tuu, nadhani ukiwa kazini unasaini mahali ambapo hutakiwwi kuiba. NAOMBA WATU WENYE KIAPO CHA RAISI WATUWEKEE HAPA ILI TUONE KAMA MKAPA AKIWA RAISI HAKUKIUKA KIAPO CHAKE.

Hayo yote uliyoyaandika hayakufanyika katika utawala wa Mwinyi?Hayakuwa zaidi katika awamu ya pili?
Kama tunataka kweli haki itendeke hakyanani hatobaki kiongozi yeyote Tanzania!
 
Back
Top Bottom