Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

wajinga ni hao walioshindwa kumsweka ndani baada ya kutukana kituo kizima cha polisi, akaishia kushindikizwa nyumbani.

nchi ya ajabu kazi ni kujikomba hata kwa wavuta bangi

ETI WANAMWOGOPA MTOTO WA RAIS!!!
 
Kibano cha Watanzania dhidi ya ufisadi mkubwa uliofanywa na familia yao kinaanza kuwakosesha raha na kuhaha huku na kule kutafuta wapi wajifiche, lakini na Watanzania tumesema tutawakaromea mpaka kieleweke na mrudishe mali zetu
 
Ama kweli watu hubadilika... Yaani Steve navyomfahamu mimi alikuwa kijana mpole mkimya mwenye staha wakati akiwa US na baada ya kurudi Bongo...
Nashangaa sana navyosikia habari hizi maanake nashindwa kumchora kabisa!..
Hivi kweli dharau hizi kazianza baada ya baba yake kuwa rais ama ndio tabia yake ilikuwa toka zamani?..
Kama hawa waandishi walikuwa uchwara yaya nini kapoteza muda wake kujielezea na hata kumsafisha baba yake kwa hao hao uchwara! au naye anataka sifa za kuonekana ktk magazeti ya Bongo - Bongo Celebrity!.
 
Nadhani huyu mtoto wa Mkapa amefanya la maana sana kuwakata kilimilimi wenye magazeti kwa kuandika habari zisizo na uthibitisho. Mkapa sio fisadi na kila mtu anajua hilo.

chuki tu na wivu wa wapinzani.

Kidumu chama cha mapinduzi, adumu mkapa na familia yake

Unajua zamani wazee/ babu zetu kijana au binti alipofika umri wa kuoa au kuolewa, wazee walizunguka sana kuangalia ni ukoo gani wenye akili timamu, afya nzuri, nguvu za kufanya kazi, hawana utindio wa ubongo kama huyu jamaa Masaka. Kweli ilisaidia sana, sasa hivi hayo mambo hayapo tena mkikutana shule/vyuo/disko/ vilabu vya pombe twende tukawowane, kwa misingi hiyo ndo maana sasa hivi watu wanazaa matahila watoto wenye utindio wa ubongo mfano huyu Masaka na kuwalisha watoto mbuluga (vyakula vya nguluwe, ng'ombe, kuku) toka Marekani. Hata kama angeambiwa na kushuhudia mwenyewe hawezi kubali kamwe. hivyo ni bora kumwacha alivyo. Hii yote ni kwa sababu ya viongozi wetu kuwa omba omba sana yavyakula toka nje.
 
Hawashindi kihivo bana CCM wezi wa kura kila mtu anajua

Haya ndio maongezi ya kwenye vilabu vya mataputapu.Mtu mwenye akili zilizokaa sawa huwezi kuja na jumuisho la jumla kama hili eti "CCM ni wezi wa kura kila mtu anajua" nani kasema?Wewe ndie unayejua sio wote tunajua.
Sababu za vyama vya upinzani kushindwa kila chaguzi ziko wazi kabisa.Na hata wapinzani makini wanazielewa.Ni bahati mbaya kwamba wapinzani wanashindwa kukaa pamoja kuzifanyia kazi dosari hizo.Haiingii akilini hata kidogo kwa yeyote mwenye akili timamu kwamba kura milioni 10 walizopata CCM kwa nafasi ya urais mwaka 2005 kwamba zote waliiba.Pia kwamba wabunge wote zaidi ya 200 walishinda waliiba kura.Mtakalia kulalama kura zinaibwa ili hali mnaacha kuyashughulikia mapungufu ya msingi yanayopelekea kushindwa kila changuzi.
 
Ajibu tuhuma kwa waandishi wa habari, kwani wao wamekuwa mahakama? Kwa nini hiyo serikali ya CCM haitaki kumfikisha mahakamani?

Mkumbo njia pakee ya kubana mafisadi ni kuandika mpaka wajichanganye nawapa waandishi kumi. hata nchi zilizoendelea ili serikali kuingilia kati lazima waandike sana wakati mwingine hasa pale inapohusu watu wazito. angalia marekani kufuzwa kwa attoney general alberto au Libby au kesi ya Palm. waandishi hawakuhoka kuandika tena juuya wahusika binafsi

Hata mimi ningekuwa mtoto wake Mkapa ningekuwa na ghadhabu kubwa kabisa na waandishi wa habari kwa sababu wao wamebaki kulia na Mkapa badala ya kuibana serikali imfikishe mahakamani. Kama ni tuhuma, waandishi wa habari wameshaziweka wazi, sioni kilichobaki tena cha kuzungumza kuhusu Mkapa. Kama hatuwezi kuibana serikali imfikishe mahakamani waandishi na sisi tukae kimya waendelea kutesa mtaani na mapesa yao.

Hawatakiwi kuhamisha attention, kwa mkapa. Halafu kujichanganya huju kwa wanafamilia wao ndio bomba. Hata kama huyu mtoto ni mvuta bangi lakini ana info. hapa palikuwa pazuri kumchanganya aanze sema yeye anajua nini. waandishi wangekuwa makini kidogo ilikuwa ni move bomba ile ya kinoma.

Mkapa na serikali na kitu kimoja walie naye mpaka mwisho. madhara ya mafisadi ndio haya hata mbwa sasa wanatudharau na kututukana. huyu steve hajui kwamba wanaishi kwa kodi zetu??? dawa ni kuchoma mali zao na kuwafuata kuharibu vyote walivyovipata kwa wiozi. jino kwa jino itasidia sana.

Utawala wa katiba na sheria ulikufa siku nyingi. utawala uliopo tanzania ni wanani mwenye nguvu hivyo tukiunganisha nguv tutawashinda tuiharibu mali zao zote.
 
Nadhani huyu mtoto wa Mkapa amefanya la maana sana kuwakata kilimilimi wenye magazeti kwa kuandika habari zisizo na uthibitisho. Mkapa sio fisadi na kila mtu anajua hilo.

chuki tu na wivu wa wapinzani.

Kidumu chama cha mapinduzi, adumu mkapa na familia yake

Ukisikia mtu ana mawazo mufilisi basi ndiyo kama wewe! Labda mwenzetu ulinufaika au bado unanufaika kwa namna moja au nyingine na ufisadi wa Mkapa ndio maana unabwabwaja kama kasuku asiyejua anaongea nini. Unataka kutetea ufisadi ambao fisadi Mkapa mwenyewe anakwepa kuutetea kwa sababu hana utetezi anakwenda kuongea kijijini ambako asilimia kubwa ya wanaoishi huko hata redio hawana! hivyo hawajui lolote kuhusu ufisadi wake.

Tamaa ya fisi imemponza sasa anajuta! kwa ufisadi alioufanya. Mshahara na marupurupu aliokuwa analipwa na Watanzania wakati akiwa Rais na baada ya kustaafu vingemtosha kabisa kuishi maisha ya raha na starehe yeye na familia yake, lakini kwa tamaa aliyokuwa nayo bado akatufisadi Watanzania. Nasi tutamfuatilia mpaka afunguliwe mashtaka, afilisiwe, mali alizoiba zirudishwe chini ya miliki ya Watanzania na yeye akacheze lupango. Hii itasaidia watu kuugopa ufisadi kama ukoma.
 
Kama mbunge anafanya kazi yake sawasawa hana haja ya kuwa na wasiwasi. Akiondolewa kwa fitina, rekodi za utendaji kazi wake hazifutwi. Wananchi wameshafumbuka macho, wanapata shida kwa sababu ya UFISADI. Kama kweli huko Vunjo hawalioni hilo eti kwa sababu FISADI kawaolea mwanao hiyo ni balaa. Huenda huko Vunjo kuna neema tele, itabidi watu wa sehemu zingine zenye matatizo luluki waangalie suala la kuhamia huko Vunjo.


...ile hoja ya mbunge kimaro haikuwa na tatizo ,ilikuwa safi ..nilisikitika tu kwenye kuhitimisha ile hoja LILE AZIMIO LA BUNGE WAS SO SHALLOW......

...TATIZO LA MBUNGE NA PERCEPTION YA WAPIGA KURA WAKE HALIKUANZA LEO...WENGI WANAONA KUWA KUACHA HIYO HOJA BINAFSI...KIMARO HAJAWAHI KUONGEA LOLOTE TANGU APEWE UBUNGE HUKO BUNGENI...HATA WATU WALIKUWA WAKIJIULIZA KAMA YUPO....HUKO JIMBONI PIA HAKUNA LA MAANA ALILOFANYA....WANANCHI WANAJIONA LOSERS ZAIDI KWA KUWA WANAONA SASA KIMARO NAYE ANAKUWA ANOTHER JESSE MAKUNDI AMBAYE DID NOTHING....AU JAMES MBATIA.......AGAINST MBUNGE KAMA MREMA AMBAYE HAS UNDISPUTED RECORD KWAO....

KWA HIYO CHOKO CHOKO ZA KUMTOSA HUYU KIMARO ZILIANZA KIPINDI...TENA WENGI WANAOMJUA TANGUA ANAPANDISHA WATU MLIMA WALISHANGAA KUWA HATA MTU KAMA KIMARO ANAWEZA KUWA MBUNGE NA KUMUACHA YULE ALIYEKUWA MCHUMI WA WORLD BANK...MR MOSHA[DIRECTOR - NICO]....KATIKA HALI YA KAWAIDA BAADA YA ILE HOJA KIMARO ALITAKIWA APOKEWE KWA MBWEMBWE KAMA KINA MWAKYEMBE.....LAKINI KWA KUWA WANACHI WA MOSHI WANAMDHARAU TANGU MWANZO .....HATA HAWAKUONA UZITO WAKE PAMOJA NA HOJA YAKE KUWA NZITO.......
 
NA KUMUACHA YULE ALIYEKUWA MCHUMI WA WORLD BANK...MR MOSHA[DIRECTOR - NICO]....

Mkuu wangu heshima mbele, naomba kuweka marekebisho kidogo huyu jamaa hajawahi kuwa Director wa Uchumi wa World Bank hata siku moja, ingawa anaweza kuwa amekupandisha mkenge hata wewe mtu mzima, alikuwa na capacity ya u-director hivi kule UN, ninamjua sana ni mazishi na magirini sana,

tatizo lake sio wananchi huko jimboni, isipokuwa ni wakulu ndani ya CCM, kwa sababu Mtei alipoanizhsa Chadema, huyu mkulu alidhani kuwa huenda akashinda urais, akajiweka swa naye, na baadaye alipooona Mrema ana dalili za kuwa rais, tena mkulu akajipanga naye sawa, wakati wote huu alikuwa anaishi NY, baadaye alipooona hakuna dalili akajiingiza kwa karibu na Mwalimu(RIP) ili apate njia ya kuingia ubunge kwa tiketi ya CCM, all this time CCM walikuwa wanam-monitor bila ya yeye kujua, ndio maana mpaka leo yuko beach na wakulu huwa hawataki hata kumsikia, lakini masikini ya mungu huwa hajui na huenda kujichanganya sana nao, I wish watu wengi wangezielewa siasa za bongo as I do, wasingekuwa wananaswa kwenye mitego ya hawa viongozi wetu uchwara,kwa sababu ninajua for a fact kuwa huyu mkulu amepoteza hela zake binafsi nyingi sana kujaribu kufukuza hewa ya kupata ubunge huko!

Ahsante mkuu!
 
Huyu Mheshimiwa amechemsha, Wapigakura wa Jimbo la Vunjo (CCM) watamfutilia mbali.
 
Ccm wilaya ya moshi mjini hususani jimbo la vunjo lina mpasuko mkubwa sana wa kisiasa kwamakundi makubwa mawili ambapo kundi moja dogo na lisilo na ushawishi likijaribu kumtetea Mh Aloyce Kimaro dhidi ya kauli yake tata kuwa Ben Mkapa ashtakiwe,na kundi jingine kubwa na linaloungwa mkono na madiwani na wananchi likisema ni ukosefu wa adabu kwa chama na kwa shemeji yao Mkapa,hivyo wanadai mipango ya kumuondoa Kimaro ianze mapema.
Wafanyabiashara wakubwa wameungana na madiwani wote kwa ajili ya kumuondoa huyu bwana ambaye ni mlopokaji mkubwa,kuonyesha hali ilivyo mbaya ilifika mahali wiki aliopita kuliitishwa mkutano wa chama ambapo bwana Kimaro aliomba amani iwepo kwa muda ili aweze kutekeleza ilani japo kwa muda na kuomba msamaha wale aliowakwaza kwa namna moja au nyangine.
Baada yaujio wa katibu mpya wa mkoa mama mauldine Castico imebidi kuchukua hatua za haraka kwa kuwahamisha kituo cha kazi Katibu wa Chama wa wilaya Mama Mpambalyoto na msaidizi wake Ndg Chale,jambo ambalo kwa uchunguzi wa harakaharaka haliwezi kumsaidia Kimaro kupata adhabu ya wapiga kura wake.


Hiyo ndiyo zawadi itolewayo na CCM kwa mtu yeyote yule ateteaye maslahi ya nchi. Sijui kwa nini huyu mheshimiwa hakujifunza kutokana na yaliyomkuta mwenzie Zitto.
 
Hiyo ndiyo zawadi itolewayo na CCM kwa mtu yeyote yule ateteaye maslahi ya nchi. Sijui kwa nini huyu mheshimiwa hakujifunza kutokana na yaliyomkuta mwenzie Zitto.


Mkuu Wamgu Kichuguu,
Ulikua umepotea sana Mkuu,afadhali umerudi jamvini.

Btw: Yaani CCM wanataka hata kumsulubisha mwenzao kwa sababu ya kulitetea taifa? Wananchi nao wanalishwa hii sumu wanaikubali.Tuna kazi kweli kweli.

Halafu mkuu,ile NGO ulikua umrdokeza umefikia wapi? Taasisi kama hizo zitasaidia sana.
 
huyu anaezungumza kuhusu wananchi kumkataa kimaro kwa kumdhalilisha mkapa wanaota alinacha.
umaarufu wa mkapa unaishia pale old moshi kidia alikooa na kufunga harusi pale kanisa kuu la kristu mfalme moshi kama vile kule masasi hakuna makanisa.

ukitaka kujua msimamo wa wananchi wa moshi kawaulize akina mramba walivyopigwa mielelka 1995!
hawana mchezo wale

Mkuu,

Hata Mramba 2010 inabidi aweke manyanga chini.Pale Rombo nadhani opposition wakiweka campaign ya nyumba kwa nyumba Mramba hataona ndani
 
Tumtafute Kimaro aseme kwa kinywa chake ni mtu mzima yule he might have planned na huwezin kujua kwa ushujaa gani akaamua kumwaga maharage njiani .So tukiwa tunaona upande huu tujaribu na upande wa pili pia .Tabia ya CCM ni kama wahindi ama wazungu .They want you when they need you ukisha malizika wao wanakuacha beach na wao wana anza zao .
 
Mkapa ni FISADI au sio? Hilo ndilo swali

Nyerere ni Mjamaa au Sio?

Kikwete ni Kiongozi bora au sio? Je yeye ni msafi au sio?

Haya ni maswali ya kawaida na kama kuna vigezo vya kuuliza kama nyaraka zipo kama za kuwa na private company ukiwa Rais - hayo ni maswali haki kabisa na kama mbunge wa Chama Tawala huyu Bwana ni Jasiri mkubwa and principled in his action to ask. We need more of them

Yanayotakiwa ni majibu sio cover ups
 
Mkuu wangu heshima mbele, naomba kuweka marekebisho kidogo huyu jamaa hajawahi kuwa Director wa Uchumi wa World Bank hata siku moja, ingawa anaweza kuwa amekupandisha mkenge hata wewe mtu mzima, alikuwa na capacity ya u-director hivi kule UN, ninamjua sana ni mazishi na magirini sana,

tatizo lake sio wananchi huko jimboni, isipokuwa ni wakulu ndani ya CCM, kwa sababu Mtei alipoanizhsa Chadema, huyu mkulu alidhani kuwa huenda akashinda urais, akajiweka swa naye, na baadaye alipooona Mrema ana dalili za kuwa rais, tena mkulu akajipanga naye sawa, wakati wote huu alikuwa anaishi NY, baadaye alipooona hakuna dalili akajiingiza kwa karibu na Mwalimu(RIP) ili apate njia ya kuingia ubunge kwa tiketi ya CCM, all this time CCM walikuwa wanam-monitor bila ya yeye kujua, ndio maana mpaka leo yuko beach na wakulu huwa hawataki hata kumsikia, lakini masikini ya mungu huwa hajui na huenda kujichanganya sana nao, I wish watu wengi wangezielewa siasa za bongo as I do, wasingekuwa wananaswa kwenye mitego ya hawa viongozi wetu uchwara,kwa sababu ninajua for a fact kuwa huyu mkulu amepoteza hela zake binafsi nyingi sana kujaribu kufukuza hewa ya kupata ubunge huko!

Ahsante mkuu!

heshma kulia MKUU...UKWELI MTUPU!!!!

...BEN JIMBO LA ROMBO SHAKULA ILE....MRAMBA HAGOMBEI TENA 2010...KAMA UNAMFAHAMU MTU MWENYE MENO..MWAMBIE ANOE KISU..AGOMBEE PALE!!!!
 
Mkuu wangu heshima mbele, naomba kuweka marekebisho kidogo huyu jamaa hajawahi kuwa Director wa Uchumi wa World Bank hata siku moja, ingawa anaweza kuwa amekupandisha mkenge hata wewe mtu mzima......

Phil Hajasema Mosha alikuwa director wa World Bank, kasema alikuwa mchumi wa world bank. Kamtaja pia kama director wa NICO, ambayo najua ni sahihi pia.

Hizi siasa za Kimaro (kule ana jina la utani "Simba wa Yuda") na washindani wake wa huko Moshi ni za muda mrefu. Hata kama asingemgusa Mkapa bado hao wanaompinga wangeendelea na mipango yao, na kwa bahati mbaya crusade yake dhidi ya Mkapa haionekani kumwongezea nguvu katika ngazi ya jimbo. Hata kama ataanguka kweli uchaguzi ujao, si kwa sababu ya Mkapa.

Huko Moshi wamewahi kuwepo wanasiasa wa kushangaza. Alikuwepo mmoja akiitwa Thomas Ngawaiya, yeye alikuwa akipinga wananchi kuchangia shughuli za maendeleo, ati ni wajibu wa serikali, wasichange! Na huko bungeni akawasilisha hoja useless kabisa ya kudai "Mahakama ya Kadhi"! Watu wa Moshi wakamwahidi kuwa hapati tena kura yao, kwani kaacha vipaumbele vyao na kwenda kungangania hoja za "Mahakama ya Kadhi" ili kujitafutia umaarufu, wakati mahakama hiyo haikuwa na maslahi yoyote kwa watu wa Moshi vijijini, si tatizo lao na wala si kipaumbele chao. Muda ulipotimia akaona anatemwa kweli, akakimbilia CCM ambako hadi leo wanamtumia kama "dekio" yeye pamoja na Tambwe Hiza.

Kimaro anayo hoja nzuri kuhusu Mkapa na mafisadi, na wengi tunatamani apate nafasi ya kuendelea kutoa mchango wake katika kutokomeza ufisadi. Lakini ni wajibu wake pia kutimiza malengo ya jimboni kwake na wapiga kura wake. Namshauri tu atumie muda huu pia kujiweka sawa na wapigakura wake, asijisahau sana. Akumbuke kuwa hata akipendwa nchi nzima, si nchi nzima itakayompigia kura kwa ubunge wa Vunjo, bali ni watu wa Vunjo, ashikamane nao vizuri huku akiendeleza mapambano yote dhidi ya mafisadi, na pia kwa ajili ya maendeleo ya jimbo lake. Maji ukiyavulia nguo huna budi kuyaoga.
 

heshma kulia MKUU...UKWELI MTUPU!!!!

...BEN JIMBO LA ROMBO SHAKULA ILE....MRAMBA HAGOMBEI TENA 2010...KAMA UNAMFAHAMU MTU MWENYE MENO..MWAMBIE ANOE KISU..AGOMBEE PALE!!!!




MKUU WANGU,NITASIMAMA PEKE YANGU SASA HUKO MAANAKE NILIKUA NAJIAANDAA KWENDA KUMPA CHANGAMOTO NDANI YA CCM KWANZA KWANI 2005 HUYU MTU ALIPITA NDANI YA CHAMA BILA KUPINGWA.NILITAKA NIRUDI NIPAMBANE NAE NDANI YA CHAMA HALAFU WAKILETA MIZENGWE NAHAMA NA KUNDI LANGU NA NINGEHAKIKISHA NIMEIGAWA CCM 50/50
 
Back
Top Bottom