Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

ndio maana tunataka wagombea binafsi ili wasiogope kuongea bungeni
 
1.
Mtoto wa Rais mstaafu, Bw. Benjamin Mkapa, Steven Mkapa, amevishutumu vyombo vya habari kwa kumwandika vibaya baba yake kuwa ni fisadi. Alisema kuwa kinachofanywa sasa na vyombo hivyo ni kumshushia baba yake heshima na utu alionao katika jamii. Mtoto huyo ambaye alijigamba kuwa kinachotafutwa na waandishi wa habari katu hakiwezi kupatikana kwa kuwa uelewa wao ni mdogo.

Sasa naomba kuuliza, eti Tanzania tuna sheria ya waandishi wa habari kuwa ni lazima wawaaandike vizuri viongozi wa sasa na wa zamani? Sasa baba yake na huyu mtoto kumbe wanaelewa maana ya hadhi na utu? Toka lini? Kama walijua hilo sasa ikawaje tena wakaanza kufanya biashara wakiwa Ikulu? Mbona baba yake alipompa urais muungwana, alikasirika na kutukana sana kuwa baba yake hafai, sasa amegeuka tena kuwa baba yake ana utu na heshima katika jaamii? Jamii ipi hiyo? Kwani waandishi wanatafuta nini ambacho hakipo tayari? Hapa uelewa mdogo ni wa nani, kati ya baba yake aliyeiba kwa siri na sisi wananchi tuliogundua siri zake za uizi? Mbona Mwinyi hashushiwi utu na heshima katika jaamii?

2.
Aidha, Bw. Steven, aliwashangaa waandishi hao pamoja na watu wengine wanavyopoteza muda wao kukaa na kumjadili baba yake badala ya kutekeleza majukumu yao ya kila siku.

Hivi kazi ya waandishi wa habari ni nini hasa kwa uelewa wa huyu kijana? Walipokuwa wanapalilia baba yake kupewa urais 1995, mbona hakusema kuwa waandishi wanapoteza muda na wana uelewa mdogo? Majukumu ya waandishi wa habari ya kila siku ni yapi hasa kwa uelewa mkubwa wa huyu kijana?

Wakuu the pressure is working, wallahi mkuu ameshikwa pabaya tayari! lazima tuendelee kurusha mawe!
 
still a boy!! poor boy,
Waandishi bwana, kwanini mnamprovoke mtoto? itakuja kuwa kama yale ya spika?
 
Mi nadhani hao wananchi wa vunjo wanataka kuturisha mwaka 47 hivi kimaro kweli wanaona amekosa adabu kweli wakati mambo yaliyofanywa na huyo bwana BM ni machafu na nilitegemea baada ya kimaro kulianzisha alitakiwa kupata support kutoka kila upande.

Hivi wajameni hizi rangi za kijani na njano zina kitu gani cha ziada nadhani kuna watu wakiziona wanachanganyikiwa na kusahau kuwa nchi inapelekwa porini......

Ama kweli asiyejua maana usimwambie maana na ndio hao hao pembeni wanalalamika kuwa nchi inaliwa na mafisadi hivi kuna chama kilichojaza mafisadi kama CCM???? MUNGU TUSAIDIE SIJUI LINI WATU WETU WATAAMKA KUTOKA KWENYE HUU USINGIZI MZITO!!!

Jamani..tusiwahukumu bila ushahidi beyong any shadow od doubt.... ni utafiti upi umeonyesha kuwa " wananchi wa vunjo" wamememuona Kimaro kuwa kakosa adabu? Pili... kama vikao vya CCM ndo vimekaa vikamhukumu hivyo... does it mean all vunjo people are ccm members?
lets avoid generalisations..
 
hahahaha...
walijua naye ni kama RK, wamepata walichotaka.. Big up Steve. Kama wamemshindwa Steve watamuweza BWM? Ni kweli kabisa kama wanataka kutafutia ufumbuzi wa swala la Kiwira let us move at least one step up kutoka kwenye media kwenda kwenye vyombo vinavyohusika. Na tumeambiwa humu eti kuna wabunge wengine wanataka libaki hapa hapa lilipo ili kujitafutia ujiko kwa wananchi eti wanatekea taifa. Well, that is the good thing kutetea taifa lakini isiwe kutoma mdomoni tu kama Obama.
 
Aliyasema hayo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na Nipashe wakati wa hafla fupi iliyoandaliwa na kampuni inayojishughulisha na utengenezaji na usambazaji wa vifaa vya maji ya ERV East Africa.

SOURCE: Nipashe

Wabongo wakisogezewa mic, hawajui kusema "siwezi kujibu."

Inaonekana Steve hakuja hapo kikazi, ndio maana wakamuuliza anafanya kazi wapi. Sasa aliongea na nipashe kama nani katika mkutano huu?

Kama alisema msiniulize ulize maswali ina maana mazungumzo na Nipashe hayakuwa rasmi. Walimwona amejichanganya wakaanza kumrushia maswali kipaparazi paparazi. Na yeye akaanza kuingia mkenge kuyajibu. Wakati sio lazima ujibu kila unachoulizwa na Mwandishi. Japo kuna wengine wataita huo ni uwazi na haki ya kusema unachotaka, kuna busara ya kuamua wakati gani kufungua mdomo. Vinginevyo unaishia kuharibu kama hivi.
 
nani atakuja hapa, hana kazi huyo, ccm kuna mapesa na kila kitu. huyo mnyika atajiunga tu ccm kwani njaa zitamzidi huko chadema. sasa hivi ni maandalizi tu ya kuwachafua viongozi wote wa upinzani na wanachadema hapa hadi mambo yageuke.

Sio kila mtu katika hili taifa anaingia katika siasa kwa sababu ya njaa, wengine wapo kwenye siasa kwa sababu wana imani wanaweza kufanya mabadiliko kwa njia moja au nyingine. Mabadiliko hayo yanaweza yasiwe makubwa lakini yakawagusa watu na maisha yao yakabadilika.

labda katika ccm mnaweza msiwe na fikra kama hizi au hata labda Chadema, lakini kinachoshangaza sana ni mtu ambaye naweza kumuweka katika kundi la watu walioona mwanga wa shule unaweza ukatoka hadharani na kusema mwanachama wa chama kingine akizidiwa na njaa ndio anahamia CCM what kind of crap is this. kwa hiyo ccm kazi yake ni kununua wanachama wa vyama vingine walio na njaa?!!

Kwa upande wangu mimi kuwa affiliated na chama chochote cha siasa ni mapenzi yangu mimi mwenyewe na sio kwa sababu nimepewa hela. na labda wewe ni mmoja wa waliokuwa na njaa ukapatiwa hela na CCM ndio maana unaweza hata kupinga vitu ambavyo ni crystal clear.

Sio kosa kuwa mwanachama wa ccm kuna wanachama wa ccm ambao ni safi na wana mapenzi mema kwa hili taifa, lakini wengi wa wana ccm are rotten to the core na sio jambo la kuficha na wengi wao are after money.

Nina imani iko siku na siku hiyo sio mbali atatokea mzalendo wa kweli na hapo ndipo wale waliozoea kupokelewa kama wafalme baada ya kukwapua mafedha ya nchi hii watatamani wahamie pluto kwa sababu mars kutakuwa karibu sana.
 
Steve amesha waambia mtaishia kupiga kelele, hizo ni chuki binafsi tu kama mnauhakika basi jamani toeni huo ushahidi mpelekeni mahakamani, ili tuone kwamba kweli maneno yenu sio porojo. Enzi ya utawala wake maisha yalikuwa safi. Ile kodi iliyokuwa inafanya mgambo wanaluka na kukanyagana kukimbiza watu na kuwapiga hovyo si iliondolewa enzi za Mkapa na mengine mengi tu. Mkapa safi saaaaaaaaana!! Fagilia mkapa wawaaaaaaaaaaaaa.....
 
CCM si chama pekee ambacho kinaweza kumpeleka mtu bungeni. Kama watamuadhibu kwa kusema ukweli basi hicho chama hakifai kabisa. Wanapokuwa wanaimba ohh "Nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko" kumbe huwa ni kuwafurahisha wasikilizaji kwa ka-wimbo hako. Hawa wabunge sasa waanze kuangalia ile HOJA ya Mgombea Huru (Binafsi).
 
Kama mbunge anafanya kazi yake sawasawa hana haja ya kuwa na wasiwasi. Akiondolewa kwa fitina, rekodi za utendaji kazi wake hazifutwi. Wananchi wameshafumbuka macho, wanapata shida kwa sababu ya UFISADI. Kama kweli huko Vunjo hawalioni hilo eti kwa sababu FISADI kawaolea mwanao hiyo ni balaa. Huenda huko Vunjo kuna neema tele, itabidi watu wa sehemu zingine zenye matatizo luluki waangalie suala la kuhamia huko Vunjo.
 
Hao CCM wengine wamo humu wanajidanganya kwa kampeni zao za ajabu ajabu (naogopa kusema za kijinga) hawajui hali ya nchi imebadilika na Watanzania wamechangamka sana sasa, tena huko UCHAGANI ndio musisema walichangamka tokea zamani. Kimaro endelea wananchi wako pamoja nawe na hao CCM si "Baba zako"... hawana ubavu wa kukuondoa. Si wewe, hata Mwakyembe, Selelii, Ruth MSafiri, Stella Manyanya, na kadhalika wamewekewa watu kwenda kugombea na wanagharamiwa fedha kibao lakini kwa taarifa hawatafanikiwa na wakithubutu CCM itaangushwa hata katika nafasi ya URAIS maana karata ya CCM sasa ni kuwashughulikia wenzao wanaotuhumiwa ili kupata kura za wananchi wa SASA
 
Mzee Kimaro.. usiwe na wasiwasi kaza uzi ule ule mapambano ndio yameanza tu...
 
TATIZO HAO WANANCHI NDIO HAWAMTAKI NA WANASEMA WAZIWAZI.NJOO HUKU VUNJO UAMBIWE HAYO MAMBO.MPAKA MAKANISANI HAWATAKI KUMSIKIA..ALIOANDIKA DIKTETA NI YA KWELI.LABDA MPENI JAMBO DAR.

Umefanya survey inayowakilisha Makanisa, achilia mbali Vunjo, yote?

Wamesema kwa nini hawamtaki Kimaro?

Aliyoandika dikteta hatuyapingi, lakini yeye hajasema lolote hukusu wananchi wa Vunjo:

Ccm wilaya ya moshi mjini hususani jimbo la vunjo lina mpasuko mkubwa sana wa kisiasa kwamakundi makubwa mawili...

...Wafanyabiashara wakubwa wameungana na madiwani wote kwa ajili ya kumuondoa huyu bwana
 
Mzee Kimaro.. usiwe na wasiwasi kaza uzi ule ule mapambano ndio yameanza tu...

Nyie mdanganyeni tu Kimaro, watu kama yeye wanaopiga makelele na kuaibisha wazee wastaafu hawatakiwi ccm. Sasa kibao kimegeuka na itabidi tu aachie jimbo kwa wanaccm wenye kujenga nchi na sio wapiga makelele tu bungeni.
 
Hivi Jambazi Benjamin Fisadi Mkapa na Mkewe watafikishwa lini mahakamani ili wahukumiwe na wakanyeee debe kule Segerea.
 
Sio kila mtu katika hili taifa anaingia katika siasa kwa sababu ya njaa, wengine wapo kwenye siasa kwa sababu wana imani wanaweza kufanya mabadiliko kwa njia moja au nyingine. Mabadiliko hayo yanaweza yasiwe makubwa lakini yakawagusa watu na maisha yao yakabadilika.

labda katika ccm mnaweza msiwe na fikra kama hizi au hata labda Chadema, lakini kinachoshangaza sana ni mtu ambaye naweza kumuweka katika kundi la watu walioona mwanga wa shule unaweza ukatoka hadharani na kusema mwanachama wa chama kingine akizidiwa na njaa ndio anahamia CCM what kind of crap is this. kwa hiyo ccm kazi yake ni kununua wanachama wa vyama vingine walio na njaa?!!

Kwa upande wangu mimi kuwa affiliated na chama chochote cha siasa ni mapenzi yangu mimi mwenyewe na sio kwa sababu nimepewa hela. na labda wewe ni mmoja wa waliokuwa na njaa ukapatiwa hela na CCM ndio maana unaweza hata kupinga vitu ambavyo ni crystal clear.

Sio kosa kuwa mwanachama wa ccm kuna wanachama wa ccm ambao ni safi na wana mapenzi mema kwa hili taifa, lakini wengi wa wana ccm are rotten to the core na sio jambo la kuficha na wengi wao are after money.

Nina imani iko siku na siku hiyo sio mbali atatokea mzalendo wa kweli na hapo ndipo wale waliozoea kupokelewa kama wafalme baada ya kukwapua mafedha ya nchi hii watatamani wahamie pluto kwa sababu mars kutakuwa karibu sana.

Fuatilia uone kuwa wanasiasa hata wasomi machachari wote wamerudi ccm. Sumaye aliwaambia kuwa kama mnataka biashara na mambo yenu yafanikiwe basi muingie ccm mkabisha haya sasa unaona yanayowapata kina Mbowe, pesa zote ziko ccm na afadhali urudi mapema kabla hujachelewa na kuacha wanao wakafa kwa njaa.
 
Nyie mdanganyeni tu Kimaro, watu kama yeye wanaopiga makelele na kuaibisha wazee wastaafu hawatakiwi ccm. Sasa kibao kimegeuka na itabidi tu aachie jimbo kwa wanaccm wenye kujenga nchi na sio wapiga makelele tu bungeni.

Mkapa ni Jambazi tu hana wadhifa wowote wa maana labda tumuite Fisadi Rais Mstaafu.
 
Wewe uliona wapi sheria au kanuni zinazomruhusu rais kufanya biashara kwa nchi za kiafrika?? mkapa anavuna alichopanda ulafi wake ndio umemponza wa kutaka kuwa na mali bila kutumia taratibuna sheria zinazokubalika na hatutakubali tutamtoa kafara kama wengine wanavyotolewa. yaliyomkuta chiluba na kwake yanakuja hata kama kikwete atamkwepesha lakini ipo siku.
 
Back
Top Bottom