Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Wewe uliona wapi sheria au kanuni zinazomruhusu rais kufanya biashara kwa nchi za kiafrika?? mkapa anavuna alichopanda ulafi wake ndio umemponza wa kutaka kuwa na mali bila kutumia taratibuna sheria zinazokubalika na hatutakubali tutamtoa kafara kama wengine wanavyotolewa. yaliyomkuta chiluba na kwake yanakuja hata kama kikwete atamkwepesha lakini ipo siku.

Mkapa sio fisadi, kama una shahidi mbona huendi mahakamani kumshitaki? Acheni kumchafua mzee wetu, kumbukeni mema yote aliyofanya kuijenga nchi yetu.
 
2008-06-13 09:28:35
Na Godfrey Monyo


Mtoto wa Rais mstaafu, Bw. Benjamin Mkapa, Steven Mkapa, amevishutumu
vyombo vya habari kwa kumwandika vibaya baba yake kuwa ni fisadi.

Alisema kuwa kinachofanywa sasa na vyombo hivyo ni kumshushia baba yake
heshima na utu alionao katika jamii.

Mtoto huyo ambaye alijigamba kuwa kinachotafutwa na waandishi wa habari
katu hakiwezi kupatikana kwa kuwa uelewa wao ni mdogo.

Aidha, Bw. Steven, aliwashangaa waandishi hao pamoja na watu wengine
wanavyopoteza muda wao kukaa na kumjadili baba yake badala ya kutekeleza
majukumu yao ya kila siku.

Aliyasema hayo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na Nipashe
wakati wa hafla fupi iliyoandaliwa na kampuni inayojishughulisha na
utengenezaji na usambazaji wa vifaa vya maji ya ERV East Africa.

Bw. Mkapa, anadaiwa kufanya biashara akiwa Ikulu ambapo mwaka 1999
ilianzisha kampuni iliyoitwa ANBEM.

Aidha, anadaiwa kuchukua mkopo wa dola za Marekani 500,000 katika Benki ya
Biashara (NBC) bila ya kuweka dhamana yoyote.

Pia Bw. Mkapa maarufu kama ``Mr.Clean`` anadaiwa kununua mgodi wa Kiwira
Coal and Power Limited kwa bei ya ``kutupa`` ya Sh. milioni 70 wakati
mgodi huo unathamani ya Shilingi bilioni nne.

Aidha, anadaiwa kumiliki baadhi ya majumba ya kifahari sehemu mbalimbali
hapa nchini sambamba na kumiliki ekari 600 ya miwa huko Mtibwa mkoani
Morogoro.

Aidha, kiongozi huyo hajawahi kukanusha taarifa za kuwa yeye ni mshiriki
wa Benk M.

Bw. Steven alionekana wazi kuwa na ghadabu na waandishi wa habari kutokana
na kile alichodai kuwa wanatumiwa na watu wachache kumchafua baba yake.

Alisema kuwa waandishi hao wamekuwa wakipewa fedha kidogo na kutumia muda
mwigi kuhangaika na baba yake, jambo ambalo alisema katu hawataweza kupata
kitu.

``Najua na wewe ni miongoni mwao kati ya wale wanaotumiwa kumchafua baba
lakini hamtaweza kitu hizi ni namba zingine,`` alisema Bw. Steve.

Mtoto huyo wa Mkapa ambaye anajulikana zaidi kwa jina la ``Merinyo``
alisisitiza kuwa maneno yake yanatoka moyoni na anazungumza kwa kujiamini
bila ya kuogopa kitu na hivyo wahusika wapatiwe taarifa ili watafute kazi
zingine za kufanya.

``Wewe unakuja kunichora hapa maswali mengi ... Nikikuuliza mimi unanijibu
kwa kuniuliza swali maana yake nini? kama umekuja kunijulia hali mzee
anaingia vipi kwenye mazungumzo yetu?`` Alihoji Merinyo.

Merinyo ambaye pia alionekana kukerwa sana na madai kwamba baba yake ni
mimiliki wa mgodi wa Kiwira alihoji kwa nini habari za Kiwira haziishi
katika vyombo vya habari.

Hata hivyo, alipolulizwa kwa sasa anajishulisha na kazi gani ambayo
inampatia kipato alisema kwa hasira kuwa anafanya kazi katika mgodi wa
Kiwira.

``Najua unataka niseme nini... Nenda kaseme, nafanya kazi Kiwira... Kwa
sababu nadhani nyiye bila Kiwira na Mkapa hamna cha kuandika,`` alisema
Merinyo huku akinyanyua glasi yake tayari kwa kunywa.

Awali akizungumza katika hafla hiyo, Jaji Mark Bomani, ambaye alikuwa
mgeni rasmi aliishauri serikali kuwa wepesi kukubali ushauri unaotolewa na
watalamu.

Jaji huyo ambaye pia ni mwenyekiti wa kiwanda cha bia cha Serengeti ambayo
ndio ilikuwa moja ya wadhamini wa hafla hiyo, alisema yapo mambo mengi
ambayo kama serikali ikikubali ushauri yataweza kuiletea faida kubwa nchi
na hivyo kuongeza pato la taifa.

Baadhi ya mambo hayo ni pamoja na kutumia vifaa vinavyopendekezwa katika
kutoa huduma za maji kama vile vipuri vya kusambazia maji.

``Yapo maji mengi yanapotea njiani lakini kama kungekuwa na vifaa imara
vinavyotumika yasingepotea kiholela,`` alisema Jaji Bomani.

Naye, Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ERV East Africa Bw. Phillemon Ntahilaja,
alisema kuwa wanakusudia kuwapatia mafunzo zaidi wataalamu wao.

Alisema lengo la kufanya hivyo ni kuweza kuboresha zaidi huduma zao na kwa
watanzania kwa ujumla.

SOURCE: Nipashe
 
Kabla ya kukurupuka na kuja na mabandiko pitia vizuri forums yote... Hii mada ipo muda mrefu sasa kulikuwa na haja gani ya kuifungua tena?
 
Mimi namshangaa kwanza katokea kona ipi kumtete baba yake ambaye mpaka sasa ni bubu hataki kujibu mapigo??????? Nafikiri ki ustaarabu angekaa kimya...
 
Mimi namshangaa kwanza katokea kona ipi kumtete baba yake ambaye mpaka sasa ni bubu hataki kujibu mapigo??????? Nafikiri ki ustaarabu angekaa kimya...

Nadhani huyu mtoto wa Mkapa amefanya la maana sana kuwakata kilimilimi wenye magazeti kwa kuandika habari zisizo na uthibitisho. Mkapa sio fisadi na kila mtu anajua hilo.

chuki tu na wivu wa wapinzani.

Kidumu chama cha mapinduzi, adumu mkapa na familia yake
 
Nyie mdanganyeni tu Kimaro, watu kama yeye wanaopiga makelele na kuaibisha wazee wastaafu hawatakiwi ccm. Sasa kibao kimegeuka na itabidi tu aachie jimbo kwa wanaccm wenye kujenga nchi na sio wapiga makelele tu bungeni.
MASAKA, FUNUA SHUKA UAMKE KUMEKUCHA NA WEWE BADO UMELALA! HAO WENYE MAWAZO KAMA YAKO HUKO VUNJO NI WENZIO USINGIZINI.
KIMARO KAFANYA ALICHOPASWA KUFANYA KAMA TULIVYOMTUMA AKAFANYE BUNGENI.
 
Kuna Diwani Kijana Kule Arusha Aitwae Mawazo nae kalazimishwa kujiuzulu kwa kuomba msaada wa kusaidia kata yake isiyokuwa na hata kadispensary ndani ya mji wa Arusha.

La kimaro sio mchezo ,nae ni jiwe la mtoni . Mkapa athubuthu kumpelekea majeshi aone.
 
Mbona Mkapa na familia yake wanakwepa hoja? Nilidhani huyu mwana atajikita kutoa ufafanuzi wa tuhuma zilizvyo na si kutoa majibu ya kumajumla kama baba yake. Kweli kama baba kama mwana!
 
Mkapa hana mtetezi CCM Moshi mjini wala vijijini. Na hiyo gear ya 'ushemeji' haingii kabisa kwa hawa jamaa.

Toka mwaka 1995 Mkapa binafsi amejaribu kumsaidia shemeji yake haswai Mama Elizabeth (Maro) Minde (dada wa kuzaliwa na Mama Anna) kugombea nafasi kadhaa za chama mkoani Kilimanjaro ikiwemo ubunge viti maalum na wa majimbo, na kila mara Mkapa na Mama Minde wamepigwa chini.

Hayo mapenzi ya CCM Moshi kwa Mkapa na 'ushemeji wa jimbo la Vunjo' yameanza lini?

Kimaro anaweza kuwa na matatizo yake na wapiga kura wake wa Vunjo, lakini kamwe si kwa ajili ya Mkapa na Kiwira.
 
Nyiye waandishi, mwacheni babangu
2008-06-13 09:28:35
Na Godfrey Monyo


Mtoto wa Rais mstaafu, Bw. Benjamin Mkapa, Steven Mkapa, amevishutumu vyombo vya habari kwa kumwandika vibaya baba yake kuwa ni fisadi.

Alisema kuwa kinachofanywa sasa na vyombo hivyo ni kumshushia baba yake heshima na utu alionao katika jamii.

Mtoto huyo ambaye alijigamba kuwa kinachotafutwa na waandishi wa habari katu hakiwezi kupatikana kwa kuwa uelewa wao ni mdogo.

Aidha, Bw. Steven, aliwashangaa waandishi hao pamoja na watu wengine wanavyopoteza muda wao kukaa na kumjadili baba yake badala ya kutekeleza majukumu yao ya kila siku.

Aliyasema hayo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na Nipashe wakati wa hafla fupi iliyoandaliwa na kampuni inayojishughulisha na utengenezaji na usambazaji wa vifaa vya maji ya ERV East Africa.

Bw. Mkapa, anadaiwa kufanya biashara akiwa Ikulu ambapo mwaka 1999 ilianzisha kampuni iliyoitwa ANBEM.

Aidha, anadaiwa kuchukua mkopo wa dola za Marekani 500,000 katika Benki ya Biashara (NBC) bila ya kuweka dhamana yoyote.

Pia Bw. Mkapa maarufu kama ``Mr.Clean`` anadaiwa kununua mgodi wa Kiwira Coal and Power Limited kwa bei ya ``kutupa`` ya Sh. milioni 70 wakati mgodi huo unathamani ya Shilingi bilioni nne.

Aidha, anadaiwa kumiliki baadhi ya majumba ya kifahari sehemu mbalimbali hapa nchini sambamba na kumiliki ekari 600 ya miwa huko Mtibwa mkoani Morogoro.

Aidha, kiongozi huyo hajawahi kukanusha taarifa za kuwa yeye ni mshiriki wa Benk M.

Bw. Steven alionekana wazi kuwa na ghadabu na waandishi wa habari kutokana na kile alichodai kuwa wanatumiwa na watu wachache kumchafua baba yake.

Alisema kuwa waandishi hao wamekuwa wakipewa fedha kidogo na kutumia muda mwigi kuhangaika na baba yake, jambo ambalo alisema katu hawataweza kupata kitu.

``Najua na wewe ni miongoni mwao kati ya wale wanaotumiwa kumchafua baba lakini hamtaweza kitu hizi ni namba zingine,`` alisema Bw. Steve.

Mtoto huyo wa Mkapa ambaye anajulikana zaidi kwa jina la ``Merinyo`` alisisitiza kuwa maneno yake yanatoka moyoni na anazungumza kwa kujiamini bila ya kuogopa kitu na hivyo wahusika wapatiwe taarifa ili watafute kazi zingine za kufanya.

``Wewe unakuja kunichora hapa maswali mengi ... Nikikuuliza mimi unanijibu kwa kuniuliza swali maana yake nini? kama umekuja kunijulia hali mzee anaingia vipi kwenye mazungumzo yetu?`` Alihoji Merinyo.

Merinyo ambaye pia alionekana kukerwa sana na madai kwamba baba yake ni mimiliki wa mgodi wa Kiwira alihoji kwa nini habari za Kiwira haziishi katika vyombo vya habari.

Hata hivyo, alipolulizwa kwa sasa anajishulisha na kazi gani ambayo inampatia kipato alisema kwa hasira kuwa anafanya kazi katika mgodi wa Kiwira.

``Najua unataka niseme nini... Nenda kaseme, nafanya kazi Kiwira... Kwa sababu nadhani nyiye bila Kiwira na Mkapa hamna cha kuandika,`` alisema Merinyo huku akinyanyua glasi yake tayari kwa kunywa.

Awali akizungumza katika hafla hiyo, Jaji Mark Bomani, ambaye alikuwa mgeni rasmi aliishauri serikali kuwa wepesi kukubali ushauri unaotolewa na watalamu.

Jaji huyo ambaye pia ni mwenyekiti wa kiwanda cha bia cha Serengeti ambayo ndio ilikuwa moja ya wadhamini wa hafla hiyo, alisema yapo mambo mengi ambayo kama serikali ikikubali ushauri yataweza kuiletea faida kubwa nchi na hivyo kuongeza pato la taifa.

Baadhi ya mambo hayo ni pamoja na kutumia vifaa vinavyopendekezwa katika kutoa huduma za maji kama vile vipuri vya kusambazia maji.

``Yapo maji mengi yanapotea njiani lakini kama kungekuwa na vifaa imara vinavyotumika yasingepotea kiholela,`` alisema Jaji Bomani.

Naye, Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ERV East Africa Bw. Phillemon Ntahilaja, alisema kuwa wanakusudia kuwapatia mafunzo zaidi wataalamu wao.

Alisema lengo la kufanya hivyo ni kuweza kuboresha zaidi huduma zao na kwa watanzania kwa ujumla.

SOURCE: Nipashe

Huyu Mtoto wa Mkapa kwa Mama Gani? Au ndio wale wa dada zake aliokuwa akiwalea. Hata hivyo yeye sio mhusika sasa akae kimya hayamuhusu maana sidhani kama alikuwa akimsaidia BABA yake kwenye maamuzi wakati yupo Ikulu. SHUT UP!
 
Inaonekana kuna watu ambao mpaka leo hawaelewi kuwa hapa Mkuu ameshikwa pabaya tena sana, kwa sababu kwanza alisema kuwa yeye amestaafu, na kwamba hataki kuongelea anything,

Baada ya wananchi kuzidisha mawe, finally mkuu huyo huyo akaongea huko kwao, baadaye waziri wa muungwana akamuongelea, sasa mtoto naye amejibu, kwa siasa maana yake ni moja kuwa the political pressure is working, hata waseme nini ukweli ni kwamba huko Lushoto hakulaliki, na ndio hasa tulichotaka yaani wananchi, kujidai kwamba eti ushahidi hakuna hilo hata Ferguson aliyeua watu kwenye treni moja ya kwenda Long Island, alipokutana na aliowapiga risasi na wakapona mahakamani aliwauliza kama kweli wana uhakika kuwa aliyewapiga ni yeye? Mlowezi Smith, aliwahi kusema kuwa Rhodesia yaani Zimbabwe, haitakuja kupata uhuru hata siku moja, na makaburu walisema hivyo hivyo kuwa SA haitakuja kuwa huru,

Matatizo ya Mkapa ni ya kisheria zaidi kuliko kisiasa, sijui kama analijua hilo, documents zipo tena nyingi sana, sasa ni kweli kuwa labda system ya sasa inaweza kujaribu kumlinda, lakini anapaswa kujua kuwa ni temporary tu na sio permanent na sisi wananchi tuko nyuma yake tu mpaka kieleweke, sasa tunasubiri siku moja naye mama ajibu, lakini ukweli ni kuwa mahakamani hakukwepeki hata afanye nini, waendelee kujidanganya lakini ukweli uko clear ndio maana wanapojibu hawagusi ishus specifically, lakini wana ruka ruka tu kama sungura, kila chenye mwanzo ni lazima kiwe na mwisho!

Kwa kawaida debe tupu kama kina Mkapas, huwa lina kelele sana walijaribu kujifanya limejaaa lakini ukweli umeanza kujitokeza kuwa ni debe tupu hilo, tunaojua kusoma betweeen the lines tumeshaliona tena kwa karibu, kuwa mfa maji huwa haishi kutapa tapa! Ukiwauliza wanasiasa wote wakubwa watakuambia kuwa haikuwa rahisi kumfanya Mkapa aongeelee shutuma mradi ameongea basi tuko kwenye the right track!
 
Huyu mjinga alipanda counter ya polisi Salender Bridge na kuwafanyia fujo kituo kizima, kisa eti wamemfanyia fujo California Dreamer, hawajui kuwa yeye ni mtoto wa Mkapa.

Mkuu wa kituo akawaambia polisi wamsindikize nyumbani!
 
Huyu mjinga alipanda counter ya polisi Salender Bridge na kuwafanyia fujo kituo kizima, kisa eti wamemfanyia fujo California Dreamer, hawajui kuwa yeye ni mtoto wa Mkapa.

Mkuu wa kituo akawaambia polisi wamsindikize nyumbani!

Umenikumbusha mshkaji... huyu jamaa skuhiyo alitukana sana mapolisi waliokuwa zamu siku ile.... wote walimshindwa mpaka alipokuja mkuu wakituo na kumbembeleza na kumrudisha home... kwa ulevi huo ataacha kuropoka kama hivo??
 
1.
Mkapa ni Jambazi tu hana wadhifa wowote wa maana labda tumuite Fisadi Rais Mstaafu.

Saafi sana Mazee ya Geeeque, always on the point with no nonesense! ubarikiwe tu mkuu!

2.
Hao CCM wengine wamo humu wanajidanganya kwa kampeni zao za ajabu ajabu (naogopa kusema za kijinga) hawajui hali ya nchi imebadilika na Watanzania wamechangamka sana sasa, tena huko UCHAGANI ndio musisema walichangamka tokea zamani. Kimaro endelea wananchi wako pamoja nawe na hao CCM si "Baba zako"... hawana ubavu wa kukuondoa.

Mkuu Halisi,

Do not waste your time, hapa kuna watu fulani wanaamini kuwa kwa kufanya hivi wanamkomoa mtu, lakini ukweli ni kwamba ni uwezo tu mdogo wa kuelewa kinachoendelea, kwa sababu Kimaro alipowaka bungeni, alikuwa anawawakilisha wabunge wengi sana waliomuomba asimame kwa niaba yao, na kwa nia ya kumtumia ujumbe mzito mama anna, ni baada tu ya hii message ya Kimaro ndio tumeona Mkapa anajitokeza kujibu kwa mara ya kwanza,

Kimaro hana tatizo lolote bungeni wala jimboni, tuliambiwa kuwa Mwandosya hawezi kumshinda Tom kwenye NEC, lakini wabunge walienda kule na kumfanyia kazi kubwa Mwandosya mpaka akashinda tena under very diffuclt environment, sasa Mkapa mwenyewe ameshindwa mara kibao kumpitisha Mama Mende huko jimboni, tena akiwa rais sasa eti leo wananchi wa huko wamegeuka na kumpenda sana Mkapa, mpaka kumuondoa mbunge aliyemrushia mawe akiwa mstaafu?

Ndio maana mimi naaamini kuwa wengine sio raia wenzetu, maana haiwezekani kuwa hawajui kinachoendelea nchini kwetu kiasi hiki, mpaka ku-speculate hizi nyepesi nyepesi!
 
Sikujua kama huyu Mkapa ana watoto wajinga kiasi hiki. Mtoto mwenye akili alipaswa kunyamaza pale Babaye anaposutwa kwa kufanya jambo lililo kinyume na matarajio ya waungwana.
Kinyume cha hapo ni kuyafanya makosa ya Baba yake yaonekane ni makosa ya ukoo mzima jambo ambalo si kweli. Kama Ben aliiba, basi ni Ben mwizi. Ajitetee mwenyewe sio Vijitu vingine vimsemee, kwani wao nao walikuwa na ubia katika Uraisi?

aaaaaaaaa... mkuu kama baba mjinga mtoto atatoa wapi akili, kiongozi kama yule anaweza kujitetea na tuhuma nzito kwa kusema uongo.... uongo.... uongo... uongo... uongo.....lzm uquest uwezo wake kichwani
 
aaaaaaaaa... mkuu kama baba mjinga mtoto atatoa wapi akili, kiongozi kama yule anaweza kujitetea na tuhuma nzito kwa kusema uongo.... uongo.... uongo... uongo... uongo.....lzm uquest uwezo wake kichwani

The folly of arrogance, wantonly deceit
The thrill of victory, agony defeat
 
Back
Top Bottom