Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 34,103
- 43,350
- Thread starter
- #2,541
Aende tu huko mahakamani.. ile sheria ya maadili ya 1995 itatumika hata kama ina mapungufu..
mazingaombwe ni sanaa ya kuwafanya watu waamini kitu ambacho kilikuwepo hakipo! - M. M. Mwanakijiji Original
Mkuu Halisi,
Hao kina Mbuna walishindana na nani kwenye zabuni ya kuununua huo mgodi ?
Walishindana wenyewe ndo sababu WALISHINDA.
JAMANI kumbukeni kuwa JOSEPH MBUNA ni mkwewe Mkapa!!! inakuwaje wanasema huo mgodi hauna uhisiano na familia ya Mkapa? zaidi tunajua mbuna hapo kabebwa tu kufunika jina la mzee
Walishindana wenyewe ndo sababu WALISHINDA.
hii nchi ni mwendo wa sinema kwa kwenda mbele
Iweje akae kimya siku zote hizo then now ndo anakuja na haya??
alikuwa anapika vitu huyu sasa vimeiva ndo anataka kutenga
But magazeti nayo yakae tayari
Mkuu habari hii imetoka ndani kwa BWM?Rais (mstaafu) wa Tanzania Benjamin William Mkapa yuko katika mchakato wa mwisho kuyashtaki magazeti ambayo yamekuwa yakimwandama kwamba ni fisadi.
Habari kutoka ndani ya familia yake zinaeleza kuwa taratibu za kuyashitaki magazeti hayo zimekamilika na kilichokuwa kikisubiriwa ni kutolewa kwa taarifa za awali kwamba yeye na mkewe, mjasiriamali Anna Mkapa hawana hisa katika mgodi wa Kiwira.
Zaidi ya hapo inaelezwa kuwa magazeti yatakayoshikiwa bango ni Kulikoni, Thisday, Mwanahalisi, Mwananchi, Tanzania Daima, Majira na Mtanzania.
Mtoa habari huyo aliyeona makabrasha ya mashtaka hayo ameeleza kuwa kila gazeti litadaiwa bilioni mbili; akieleza kuwa anadai kiasi hicho kwa kuwa angalau kinalinganalingana na hadhi yake ndani na nje ya nchi.
Hivi majuzi kampuni ambayo ilinunua mgodi wa Kiwira wa kuzalisha makaa ya mawe iliibuka na kueleza kuwa Mkapa na mkewe hawana hisa eti kwamba walijitoa muda mfupi baada ya kugundua kuwa ilikuwa ikijiandaa kununua mgodi huo kwa bei ya kutupwa ya sh. milioni 700 (zililipwa 70 kwanza za kukopa kutoka Benki) wakati mgodi wenyewe ukiwa na gharama kubwa ya bilioni 4.
Mawakili sita wamejipanga kwa kazi hiyo, huku mmoja akiwa kutoka Afrika Kusini ambaye anaeleza kuwa mzoefu katika kesi zinazohusu kashfa kwenye vyombo vya habari.
baada ya balai kufa sio? je, JOSEPH MBUNA si mkwe wake mkapa? na hapa atakataa nini?
na MBUNA hapo alibebwa tu'. hiyo ni dili ya mzee mkapa mwenyewe asitake kututisha hapa