Mishahara ya SUMATRA kufuru

Mishahara ya SUMATRA kufuru

Millioni 1.35 ni mshahara wa kufuru? Kweli tunatofautiana.watu wanalipwa dola 25000 ambayo ni kama millioni 40 kwa mwezi endelea kulalamika na vyeti vyako

Shangaa na wewe... Kuna CEO wa Kampuni moja analipwa 50m.. Tena analipiwa expenses zote bila kukatwa mshahara!!!!
 
bila shaka huyu jamaa anafanya kwa wahindi wa kariakoo...anashangaa 1.53......!! akiona wanaolipwa mishahara minono atazimia...
 
Nchi zote ziko hivyo hakuna nchi ambayo mishahara iko sawa kwa idara zote kulingana na elimu ila ni unyeti wa idara au idara za kukusanya mapato hupewa kipaumbele. Ila kwa Tz bado kuna makundi yalitakiwa kulipwa zaidi kama walimu lakini idadi yao ukilinganisha na uwezo inakuwa ngumu hii imechangiwa na mapato madogo ya serikali na utumiaji mbaya wa fedha za umma. Zaidi punguza kulalamika kuwa chachu ya mabadiliko kwako na kwa wengine siku na wewe ukiwa gvt decision maker ukumbuke hayo usijesahau ukiwa kivulini
wakuu, hii mamlaka ya serikali inayoendeshwa kwa kodi za wavuja jasho ina unyeti sana kiasi cha watumishi wake kuenjoy pepo duniani? Cjajua Taasisi zingine kama TRA mishahara yao ikoje ila nimeijua mishahara ya SUMATRA hadi nimeshangaa. Huenda sijafahamu unyeti wa mamlaka hii ila wanaoijua watatueleza. Rafiki yangu amemaliza pale IFM akichukua Accouting, amepata ajira mwanzoni mwa mwaka huu katka mamlaka ya SUMATRA na kwa macho yangu amenionyesha Salary Slip yake daah, ni Milioni 1.53 kwa mwezi. Wakuu hii mishahara inapangwa na ofisi ya utumishi au wanajipangia wafanyakazi wenyewe wa Mamlaka?
 
Millioni 1.35 ni mshahara wa kufuru? Kweli tunatofautiana.watu wanalipwa dola 25000 ambayo ni kama millioni 40 kwa mwezi endelea kulalamika na vyeti vyako

Mwambie huyo ndo katoka shule.
 
Unashangaa nini sasa hapo? Huo si mshahara bali masikhara tu. Uliza watu huko kwingine wanaanzia kiasi gani? Sasa unataka ashushiwe mshahara wake? Badala ya kuomba na kumshinikiza mwajiri wako nawe uongezewe unaanza kuwangalia wenzio kwa kijicho na husda. Kwanza ujue katika nchi hii miongoni mwa watu ambao wanalipwa maskhara ni pamoja na hao wanaoitwa wahasibu.



mara nyingi watanzania hawajui ku - negotiate mshahara unajipinda kumbana muajri unapoingia huko ndani unjikuta unalipwa karibia mara tatu ya hao walioko humo halafu badala watafute stategy binafsi za kuongezwa mshahara wanaanza kukuchukia na kukufanyia visa ili uonekane hau - perfome ili nao wa -legitimize kulipwa kama wewe au zaidi na kumfanya muajiri aone kwamba anakulipa mshahara mkubwa kimakosa usivyo stahili. ukimpa mtu kazi ya kukufanyia anazingua na kutafuta visingizio, ukienda sehemu unanyimwa usafiri yaani ili mradi kuharibu kazi, kila unachogtaka kutoka kwa wenzako unakipata sio kwa kupenda ni kwa nguvu na kuvutana sana
 
Hii thread ni nzuri sana,,,,


wanaochangia kwa lugha yamatusi nakudharau huo mshahara,,,wanaonekana wamezaliwa na kulelewa na wazazi ambao wanafanya biashara yakusafirisha sembe,,,,,wamelelewa na fedha chafu

wanashidwa kujiuliza swali dogo tu,,,je ni asilimia ngapi yawatanzania wanaolipwa huo mshahara au zaidi na je wanamda gani kazini???

Baaadhi yawachangiaje wanabaki kusema maneno ya hovyo hovyo,,,,,,,,,,,,
 
mamabo ya kishamba sana haya kwanza kwa huyo kukuonyesha salary slip yake ili iweje,,,,???? kwa akili yake kaona kajipatia ujiko na ulivyotolea mimacho kwa ushamba wako ndugu we ulisikia wapi mshahara kama huo ukawa wa kufuru kwa taarifa yako hata walimu wanapata mshahara huo na ni kawaida tu na kwa ushamba wako huenda umeona gross salary wewe ukakurupuka mshahara mkubwa na kwa ushamba wako zaidi ukaleta huu uzi humu. wajanja huwa hawashangai na hawaonyeshi mishahara wewe na mwenzio woooteee na wenye tabia kama hizi ni USHAMBA.

Hebu tulia kwanza! Vuta pumzi kwa nguvu! Acha mwili wako urelax, eeh si unaona, haya tulia hivo hivo!! Huna haja ya kutoa mapovu jingi hivo.
Si unaona, povu lote limeisha.
Ok, now unaweza kuanza upya.
 
hapo bold sasa umeanza matusi,
una uhakika gani kwamba mtoa mada ni mwanamke??
je wewe mama yako alikuwa baba?? na dada yako ni kaka??
mwanao wa kike ni mvulana na mkeo ni mume??

Bongo watu wengi hatuna discipline katika mambo kama kauli.

NIshamsikia Pius Msekwa, noted legislature scholar, erudite lawmaker, ruling party cadre, speaker of parliament, akaenda kusema neno hilo, publicly.

Sasa nilipoona kina baba viongozi wenyewe ndo hawa kina Msekwa, nikajua huku kwingine itakuwa balaa tu na wala sishangai sana.

Ndio haya tunayoyaona sasa.
 
Bongo watu wengi hatuna discipline katika mambo kama kauli.

NIshamsikia Pius Msekwa, noted legislature scholar, erudite lawmaker, ruling party cadre, speaker of parliament, akaenda kusema neno hilo, publicly.

Sasa nilipoona kina baba viongozi wenyewe ndo hawa kina Msekwa, nikajua huku kwingine itakuwa balaa tu na wala sishangai sana.

Ndio haya tunayoyaona sasa.

hahahahahah! umenichekesha sana na kunifanya nikumbuke maneno niliyokuwa nawaambia wanangu juzi kishindo jana.

niliwaambia hivi duniani ukitaka ufaulu uwe na nidham katika kila eneo la maisha, sasa naona na wewe umesema nidham katika maongezi.kimsingi watu wanapaaswa kuwa na nidham sana kwenye kila jambo mtu alitendalo.

hivi usipokuwa na nidham katika kauli yako, ndio utakuwa na nidham kwenye jambo gumu kama muda??

kanishangaza huyu aliyetoa hii kauli.
 
Millioni 1.35 ni mshahara wa kufuru? Kweli tunatofautiana.watu wanalipwa dola 25000 ambayo ni kama millioni 40 kwa mwezi endelea kulalamika na vyeti vyako

Unalinganisha na wapi. Kwa hapa Tz ni mkubwa compared to majority of workers be it in private or government employment particularly for a fresh from university employee. Ni wangapi wanapata hiyo 40 mil Tz!
 
Kijana ni mgeni kabisa anauliza mibaba mizima mnamzodoa!jf imeanza poteza radha
 
Mie nachukua 700.000 after tax na maisha yangu Alhamdulilah! Kila mbuzi atakula kwa urefu wa kamba yake

Haaahaaaa umenivunja mbavu mkuu, nachukua 650,000/= mara 1/1 namm naingia mliman cty nabeba mazaga na mrembo wangu!
 
Mdau Gsana na wengine! Umeeleza vema sana na kwa hoja zenye mashiko. Lipo tatizo kwa baadhi yetu wengi, hatusoma na kuielewa hoja na tunabaki kujivimbisha mabega na vifua kuwa tunajua watu wanaolipwa zaidi ya alichoshangaa mtoa mada.
Mtu anakuja na rejea ya serikalini na kioja rejea kinakuja na mishahara ya mashirika binafsi, huku ni kutoupa kazi ubongo na kusukumwa na mihemuko ya ndoto-jua.
Tunatambua misharaha ya serikali na hasa kwa wanaoanza kazi bila kujali kada imesimama kuanzia laki tano+. Zipo taasisi na mamlaka za serikali Sumatra ikihusika inalipa kutokana na kanuni walizojiwekea kama mamlaka huru.
Ndiyo, lazima nishangae na ni kweli kulinganisha 1.5m kwa 0.5m.
Tujifunze kutafuta maarifa na si kujifanya kuyajua yote

Wewe angalau unaweza kuwa Great Thinker kati ya wengi waliojaribu kujitutumua huku na mishahara yao bila kujaribu kumwelewa mleta mada.
Wengi walivyo shalo na wameishia kusema Tshs 1.35M badala ya Tshs 1.53M aliyoitaja mleta mada.
Watu wanashindwa kusoma btn the line, mleta mada anasema anayepata amount hiyo ni fresh from school, na hiyo ni salary ya kuanzia, sasa mtu najiita great thinker analinganisha mshahara wake wa TZS 10m na wa novices. Hapo utakuwa great thinker kweli? Mtu anazungumzia mtumishi wa uma na si wa mashirika ya kimataifa. Kama wewe unafanya huko UN utajilinganishaje na mtumishi wa uma wa TZ anayeanza kazi? Mwenyewe ni mtumishi wa uma wa hayo mnayofikiria yanalipa sijui TANESCO, TRA, TPA na kwa taarifa tu wanaoanza kazi kwingine wanaishia kupata gross za hizo laki nane na tisa so acheni mleta mada alete hoja yake kwa SUMATRA kulipa TZS1.53 kwa anyeanza kazi.
Kwa kumuelimisha tu ni kuwa nijuavyo mimi na kama mambo hayajabadilika huko SUMMATRA, tofauti na agency na authority nyingina , SUMMATRA ajira zao ni za mikataba ya miaka 2-3 ambapo wengine ni permanent na pensionable. Hiyo yaweza kuwa moja ya sababu ya mshahara kuwa mkubwa relative to others.
Tuache kubeza watu na kutishiana na vimishahara vyenu na badala yake jibu hoja au kaa kimya
 
Back
Top Bottom