Mishahara ya SUMATRA kufuru

Mishahara ya SUMATRA kufuru

hapo bold sasa umeanza matusi,
una uhakika gani kwamba mtoa mada ni mwanamke??
je wewe mama yako alikuwa baba?? na dada yako ni kaka??
mwanao wa kike ni mvulana na mkeo ni mume??
ukali huu nao ukizidi waweza kuwa matusi, punguza munkari.
 
Hahahahahhaha
kuna mameneja tu ambao wanapewa housing allowance dola 2000(milioni 3.2) kwa mwezi huo sio mshahara ni allowance ya nyumba,


Huyu bwana siyo kosa lake, walishakubaliana katika vikao vyao kuwa lolote linalofanywa na Serikali wanapaswa kulaani. Sasa wenzake wanapochanganya akili zao na zile za kuambiwa yeye anatoka mzima mzima, teh teh teh.
 
Nadhani kikubwa anachokizungumzia mleta hoja ni kutkowepo na uwiano wa mishahara baina ya watumishi wa umaa, huyu anayelipwa hayo mahela anafanya nini cha zaidi kumshinda mwalimu anafundisha kule kwetu Ilongero kusikokuwa na nyumba ya mwalimu, barabara mbaya hakuna usafiri wa uhakika wala hata maji ya kunywa ni shida?!!!
 
hiyo pesa uwa nawatunza waimbaji wa band kwa usiku mmoja nikiwa tanzania
 
Daah wahenga walisema kuwa uyaone sasa wewe unaita mshahara wa 1.35 million kufuru....wakati mm take home yangu ni 2million na bado naona mshahara wa kawaida 2......aiseee kweli kijana una safari ndefu hapa duniani
 
ME NADHAN BASIC SALARY KWENYE SLIP YA MLETA MADA INASOMA 432,000.kwa hyo sio kosa lake,ila hajawah kuona salary slip nyingne zaid ya za watumish wenzie wa kada yake na ya huyo jamaa yake.
 
hapo bold sasa umeanza matusi,
una uhakika gani kwamba mtoa mada ni mwanamke??
je wewe mama yako alikuwa baba?? na dada yako ni kaka??
mwanao wa kike ni mvulana na mkeo ni mume??
Mwalimu si unajua toka mheshimiwa mkaa-hapa atumie haka kasemo kamekuwa maarufu sana.......ni matumaini yangu mkuu MSHINO atakuwa amekuelewa .....
 
Last edited by a moderator:
Millioni 1.35 ni mshahara wa kufuru? Kweli tunatofautiana.watu wanalipwa dola 25000 ambayo ni kama millioni 40 kwa mwezi endelea kulalamika na vyeti vyako

Mi mwenyewe nimemshangaa mleta hoja sasa huo si mshahara wa kawaida kabisa
 
Huenda hata vyeti hana. Kama naona ananyonywa si akatafute kazi kwingine. Kuna Kilimo kwanza na Gesi vinalipa vizuri.


Gesi ? Inalimwa wapi kaka na nichukue KOBOTA yangu ya Kichina nikakwatue na kutifua huko kwenye kilimo cha Gesi Kimbunga
 
Last edited by a moderator:
Kweli wabongo hatujui thamani yetu,nyie ndo wale ukienda interview ukiulizwa mshahara unasema 'wowote tu"
huo mshahara wa kawaida sana,,jitambue thamani yako hapo hamna kufuru.Maisha yamebadilika thaman ya hela nayo inashuka.elfu kumi ukichenchi hapo kwishney
 
Dada punguza pafu!
Wivu wa kike haina maana kwamba mtoa hoja ni mwanamke!
Ila wivu wa aina hiyo, ni tabia za kike, kwamba mwanamke mwenzangu kapendeza zaidi, katengeneza nywele zaidi yangu, na mengine mengi, ambayo ni wivu wa kijinga. Hizo ndio Tabia za Kike

hapo bold sasa umeanza matusi,
una uhakika gani kwamba mtoa mada ni mwanamke??
je wewe mama yako alikuwa baba?? na dada yako ni kaka??
mwanao wa kike ni mvulana na mkeo ni mume??
 
Baada ya makato anabakia na 954,000. Je huo unauona ni mshahara wa kufuru.
Huyu inabidi apande basi ili aweze kusave hela nyingi.

Huu ni mshahara wa kawaida sana


Ni ahueni mara mia ukilinganisha na wa mwalimu mwenye bachelor!
 
Lakini bado ni mshahara mdogo sana ukilinganisha na mahitaji (social needs)
 
Nadhani kikubwa anachokizungumzia mleta hoja ni kutkowepo na uwiano wa mishahara baina ya watumishi wa umaa, huyu anayelipwa hayo mahela anafanya nini cha zaidi kumshinda mwalimu anafundisha kule kwetu Ilongero kusikokuwa na nyumba ya mwalimu, barabara mbaya hakuna usafiri wa uhakika wala hata maji ya kunywa ni shida?!!!

Ni kweli kabisa mkuu,hoja ya mleta hii threads ilikuwa ni hii,ila ameshindwakuiwasilisha vyema..Kiukweli kabisa moja ya vitu vinavyonifanya niichukue serikali hii ni tofauti kubwa ya mishahara miongoni mwa wafanyakazi wa serikali na taasisi zake,imu hata miongoni mwa wahitimu waliosoma chuo na kozi moja,Hii imepelekea kila mtu now anataka kuwa mbunge,kufanya kazi BOT,Bandari,TRA,Mkurabita(Idara ndani ya Wizara ya Fedha),TANESCO,EPZD,Mifuko ya hifadhi ya jamii mengineyo inafanana na hii..HII SI SAWA!
 
wakuu, hii mamlaka ya serikali inayoendeshwa kwa kodi za wavuja jasho ina unyeti sana kiasi cha watumishi wake kuenjoy pepo duniani? Cjajua Taasisi zingine kama TRA mishahara yao ikoje ila nimeijua mishahara ya SUMATRA hadi nimeshangaa. Huenda sijafahamu unyeti wa mamlaka hii ila wanaoijua watatueleza. Rafiki yangu amemaliza pale IFM akichukua Accouting, amepata ajira mwanzoni mwa mwaka huu katka mamlaka ya SUMATRA na kwa macho yangu amenionyesha Salary Slip yake daah, ni Milioni 1.53 kwa mwezi. Wakuu hii mishahara inapangwa na ofisi ya utumishi au wanajipangia wafanyakazi wenyewe wa Mamlaka?


Una point ingawa watu wanashindwa kumuona.

Kama wote wanalipwa kwa kodi ya wananchi inakuwaje wa SUMATRA achukue 1.5 halafu mwalimu alipwe laki mbili? Kwa private company sawa lakini siyo wale wanaolipwa kutoka katika chungu kimoja (kodi yetu ya hazina)!!
 
Unajua mnaweza kumlaumu mtu kumbe yeye hajawahi ona huo mshahara wa mamilion ya fedha, so mnachotakiwa ni kumuelimisha kuwa kuna walio zidi huo na wamo humu humu Tanzania, inawezekana yeye mshahara wake kwa mwezi ni 366,666/= kwa mwezi na hapo hajakatwa kodi, so akiona huo wa milion 1.35, anaona kama ni kumkufuru Mungu.Unajua humu Tanzania kuna wengine wanaishi kama peponi wengine wanajiuliza watapata wapi mlo mmoja kwa siku.
 
Mleta mada amekariri kuwa humu kila kitu ni kupingana na Serikali. AIBU iliyoje hii jamani ndo ma-great Thinkers tunaojivunia humu. Mimi nimekariri ID yake hii ili nianze kufuatilia michango yake kwa kwaribu labda nitajiridhisha kama anastahili kuendelea kuwemo humu au tumhamishie gumzo la jiji.
Mimi naamini wengi wa wanaoshambulia mleta mada ni mafisadi kwa sababu zifuatazo
-Mleta mada ameonekana hajui mishahara ya sekta nyingine ndo maana amesema hajui mishahara ya TRA na wengine
pia anaweza akawa hajui vizuri maana ya neno kufuru tulitakiwa kumuelimisha kiungwana na si kuporomosha matusi;tunaposema ni mshahara wa kawaida tunalinganisha na mshahara wa nani? Prof.wa chuo kikuu? mwl.wa sekondari mwenye degree,mwalimu wa shule ya msingi au unalinganisha na upi?
Mh.chenge aliziita shilingi 1.5 bilion ''vijichenji''Ni nani mtumishi wa kawaida wa serikali anayeenda kununua vitu binafsi akarudishiwa chenji kiasi cha bilioni moja?
- Kwa kawaida mwizi hawezi kufurahia kuona watu wanapewa taarifa zitakazoshtua wengi na kuanza kufuatilia mambo akafurahi
naamini wenye vipato halali hata kama wanalipwa milioni 100 hawawezi kutokwa povu kwa sababu ya uzi huu,kwa sababu wanalipwa ki-halali,kama ni mshahara wa kimagumashi watatokwa povu kwa sababu wanaona wafanyakazi wengine wa serikali hiyo hiyo wanalipwa mishahara ya aibu.
- Ni vema kusoma na kuelewa kinachozungumziwa kabla ya kuchangia uzi,hata kama umeapa kulinda mtandao wa uovu ni vema kuangalia maslahi ya waliowengi kwanza. Miongoni mwa majanga ya kitaifa ni mishahara ya wafanya kazi hapa nchini so, sioni sababu ya kumshambulia mtu anayeongelea suala la mshahara bali tuelimishane.
 
Back
Top Bottom