Mengi Vs Masha tuhuma, vitisho na matokeo!

Mengi Vs Masha tuhuma, vitisho na matokeo!

Status
Not open for further replies.
Mhe. Masha kaongea kama Waziri mwenye dhamana na Jeshi la Polisi.Mengi awezi kutoa Tuhuma kama hizo na akaachwa hivi hivi

Ile haki ya kikatiba ya kuongea ii wapi?
 
Ile haki ya kikatiba ya kuongea ii wapi?

Haki ya kikatiba ya kuongea ni ya Masha mwananchi, si Masha Waziri.

Akiongea kama Masha Waziri si tu anaongea kwa haki ya kikatiba, bali pia kwa mamlaka ya uwaziri ambayo yameenda mbali na juu zaidi ya haki ya kuongea ya kikatiba ambayo kila mwanakifulenge wa kitanzania anayo.

Kwa watu wanaojua concept ya conflict of interest, Masha hata kama angekuwa yuko katika line ya watu wa kumuuliza Mengi (ambayo hayumo by the way) ingebidi kwa kuwa yumo kwenye kundi la kutiliwa shaka kwamba amehusishwa na tuhuma hizi, ingebidi akae pembeni na kumuachia mtu mwingine ambaye hana doa la kuhusishwa na beef hili e.g msaidizi wake, aendeleze kesi. Tanzania hatuwezi hii, labda Botswana huko ambako Attorney General the official alisue the person of the Attorney General.

Ndiyo maana kuna mahakimu wengine hunawa kesi kwa kuangalia concept ya "conflict of interest"

Masha hawezi kuwa impartial katika issue ambayo ina harufu ya tuhuma dhidi ya Masha.
 
Nyani

Ile post ya kwanza kabisa iliyofungua thread ilisema kuwa Masha alitoa ultimatum hiyo akiwa kama Waziri wa Mambo ya Ndani, siyo kama mzushiwa. Halafu niliposoma taarifa zote zilizotolewa huko nyuma, Mengi alisema waziri kijana msomi anayeongoza wizara nyeti; baraza la Kikwete lina vijana wengi wasomi, na wizara zote za serikali ni nyeti, kwa hiyo malalamiko hayo ya Mengi hayakuwa yameelekezwa directly kwa Masha unless kama kuna taarifa zaidi.

Kama kweli unamini principle, basi utakubaliana nami kuwa Masha kakurupuka, kwa vile yeye katika position yake hakutakiwa kutoa ultimatum ya kuletewa ushahidi; aufanyie nini, kwani yeye ndiye mpelelezi wa makosa ya jinai.

Masha kajihisi, no doubt. Mengi naye kachemka kwa kuwa vague. Huna jina kaa kimya. Unalo na unaogopa kulitaja, kaa kimya, hakuna haja ya press release zilizo vague. Unalo lakini huna uhakika kaa kimya. Unalo lakini ushahidi ni mdogo, kaa kimya, tafuta ushahidi zaidi, then nenda mahakamani au toa press release. That's the bottom line, period, end of it!
 
Masha kajihisi, no doubt. Mengi naye kachemka kwa kuwa vague. Huna jina kaa kimya. Unalo na unaogopa kulitaja, kaa kimya, hakuna haja ya press release zilizo vague. Unalo lakini huna uhakika kaa kimya. Unalo lakini ushahidi ni mdogo, kaa kimya, tafuta ushahidi zaidi, then nenda mahakamani au toa press release. That's the bottom line, period, end of it!

Case closed?! Watakubali?
 
Hapa JF Mengi, CHADEMA, na kikundi kingine ni UNTOUCHABLES, ukiwasema tu POST YAKO HAIPITI.

INAKERA.

Solution?Kulalama bila kutoa angalau suggestion ya utatuzi wa tatizo ni sawa na kuongeza tatizo,if not useless.Had I been you mwenye mtazamo huo ningewatafuta wenzangu ambao hawataki kuona Mengi,CHADEMA na kikundi kingine (nadhani hapa ilimaanisha kikundi cha wanaopambana na ufisadi) wanakuwa UNTOUCHABLE.

Mbona post yako ya malalamiko dhidi ya JF imepita?How come then ikiwa ya Mengi,Chadema,nk isipite?
 
Kusema Mengi ni untouchable ni unfair, mbona katika thread hii hii tunamlima Mengi pamoja na Masha ?

Mbona tushaeleza maovu mengi ya Mengi, mpaka alivyoruka ukuta kutoka kwa bibi yake wa Kinyarwanda wakati mkewe alivyomfuata na bastola mkononi pale kwenye luxury apartments Upanga Mindu St next to Silver Oak?

Mbona, kwa mfano, GT anam-deconstruct Mbowe pamoja na CHADEMA yake kila kukicha?

Huyu anayesema Mengi ni untouchable ni mnazi tu. Another manifestation of looking at this issue with a one dimensional vison, kama Mengi ana beef na Masha lazima mmoja atakuwa na kosa na mwingine yuko right.

Wote wanacheza tu, that is the tragedy.
 
Mkuu hapo juu, kwa mujibu wa sheria za nchi wakati ule ilikuwa ni lazima kijana yoyote akimaliza kidato cha sita ama chuo apite kwanza JKT kwa mwaka mmoja kabla hajaingia UD ama kuajiriwa. Ilikuwa haina mjadala.
 
Kusema Mengi ni untouchable ni unfair, mbona katika thread hii hii tunamlima Mengi pamoja na Masha ?

Mbona tushaeleza maovu mengi ya Mengi, mpaka alivyoruka ukuta kutoka kwa bibi yake wa Kinyarwanda wakati mkewe alivyomfuata na bastola mkononi pale kwenye luxury apartments Upanga Mindu St next to Silver Oak?

Mbona, kwa mfano, GT anam-deconstruct Mbowe pamoja na CHADEMA yake kila kukicha?

Huyu anayesema Mengi ni untouchable ni mnazi tu. Another manifestation of looking at this issue with a one dimensional vison, kama Mengi ana beef na Masha lazima mmoja atakuwa na kosa na mwingine yuko right.

Wote wanacheza tu, that is the tragedy.

Politics za bongo michoso tupu!! mie naona ni kama Ze Comedy in real life.....mijitu mizima, akili za kuazima!! Hooooooooooooooovyo....
 
Kusema Mengi ni untouchable ni unfair, mbona katika thread hii hii tunamlima Mengi pamoja na Masha ?

Mbona tushaeleza maovu mengi ya Mengi, mpaka alivyoruka ukuta kutoka kwa bibi yake wa Kinyarwanda wakati mkewe alivyomfuata na bastola mkononi pale kwenye luxury apartments Upanga Mindu St next to Silver Oak?

Mbona, kwa mfano, GT anam-deconstruct Mbowe pamoja na CHADEMA yake kila kukicha?

Huyu anayesema Mengi ni untouchable ni mnazi tu. Another manifestation of looking at this issue with a one dimensional vison, kama Mengi ana beef na Masha lazima mmoja atakuwa na kosa na mwingine yuko right.

Wote wanacheza tu, that is the tragedy.

That's what I've been trying to say. Wote wana act kama mitoto (big babies)
 
Kwenye mgongano kati ya watu wenye madaraka na wale wenye pesa mara nyingi (kama siyo zote) wale wenye madaraka hushinda, kwa kadiri ya kwamba bado wana madaraka yale. Wakati huo huo hakuna watu ambao hawawaamini watawala kama watu wenye pesa. Hata hivyo ni wenye pesa kutokana na kutowaamini wenye madaraka hujikuta wakijiweka karibu na wenye madaraka ili angalau kuwa katika mazingira ya "kujua" nini wenye madaraka wanapanga dhidi ya wenye pesa.

Hata hivyo wenye madaraka mara zote wana hofu na wenye fedha kwa sababu wanajua kabisa kama wenye fedha wakitaka madaraka wanaweza zaidi kuliko wao (watawala) kutaka kuwa wenye fedha. Kutokana na mkinzano huo basi wenye madaraka mara zote wanawaangalia wenye fedha kwa shuku na wale wenye fedha wanawaangalia wenye madaraka kwa shuku.

Mgongano unatokea siku watawala wanapoamua kufanya kitu kinachowatishia wenye fedha au wenye fedha kufanya kitu kinachowatishia watawala; pande hizo mbili zinajiandaa kugongana na mgongano huo hauepukiki; ni mgongano wa lazima. Mgongano huu ni wa lazima ili kuweza hatimaye kuamua ni nani kati ya pande hizi mbili ndiyo mwenye nguvu zaidi (the most powerful).

Katika kuamua hili aidha mwenye madaraka anajitahidi ili na yeye awe na fedha nyingi au yule mwenye fedha nyingi naye apate madaraka. Ukimkuta mtu mwenye fedha pia ndiye mwenye madaraka basi utaiona nchi ambayo hakuna kinachofanyika zaidi ya kurushiana vijembe, migongano, chuki n.k lakini pia utaiona nchi ambayo watawala wake wanatawala kiimla zaidi na jamii inakuwa kama kiunga chao cha mpunga ambapo wanaweza kuamua kuvuna wapendapo au kuacha ndege wajilie.

Katika sakata tunalolishuhudia Masha ataweza kushinda tu endapo ataendelea kuwa na madaraka na Mengi ataendelea kuwa tishio kwa kadiri ya kwamba yeye ni tajiri. So one of them has to give in; mmoja asiwe na madaraka au mwingine asiwe tajiri! Kwa vile vyote viwili vina mvuto tofauti, ni rahisi kwa tajiri kuwa maskini (kwani anaweza kuanza upya kutengeneza biashara yake) kuliko kwa mwenye madaraka kuachia (kwani ni vigumu kuyapata tena).

Kwa vile mwenye madaraka anauwezo mkubwa wa kushiinda katika sakata hili, lakini kwenye kushinda mioyo ya wananchi, ushindi utakuwa kwa Mengi (yawezekana ndicho alichochezea kamari?), kwani at the end, watu watalign up na mtu mwenye fedha kuliko mtu mwenye madaraka! Don't ask me why!
 
Hivi nani mmliki wa CNN au Aljazeera?Sijawaona wala kuwasikia! Lakini mengi kila siku anajitangaza kwenye vyombo vyake vya habari na kisha anazua mambo ya kuwachafua wengine mbele ya jamii.Huyu Mengi ana agenda gani?

Labda huwa hawatishiwi ... mimi sijui ... Halafu ujue kwenye nchi zao kukuta mawaziri wenye hulka za mawaziri wetu pengine ni ngumu kidogo ... kwa hiyo hapo ni sawa na ku-compare apples na oranges, au monkies na aeroplanes.
 
FMES,

Sio kazi ya waziri wa mambo ya ndani kuchunguza tuhuma, hiyo ni kazi ya polisi.

Masha kumpa Mengi siku saba ina maana mbili, moja, anampa siku saba kabla ya yeye kama Masha kumburuza mahakamani. Kama sio kwa nia hiyo basi maana ya pili ni kuingilia madaraka ya polisi, kitu ambacho naamini ni makosa. Awaachie polisi wafanye uchunguzi wao.

Kazi za waziri wa mambo ya ndani sio kuchunguza tuhuma.

- Sasa ilikuwaje wachawi waliouliwa Shinyanga wakasababisha waziri wa ndani Mwinyi, Dar akajiuzulu iwapo sio wajibu wake? Mengi amelikoroga sasa alinywe, kwenye hili hata yeye anajua kua he is on his own, tunapigana na mafisadi kisayansi sio kwa kuwapa risasi namna hii,

- Usalama wa ndani ya nchi na wananchi wake ni kazi ya waziri wa ndani, polisi kikiwa ni kitengo chake, nilifkiri utaridhika kwamba sasa hili litaamuliwa kwenye sheria ili Mengi naye apewe hakli yake kisheria, sasa hutaki sheria? Mnataka wananchi waamuke tu an kudai waziri anataka kuniua?

Let sheria ichukue mkondo wake na Mengi apewe haki yake kisheria iwapo waziri atakutwa na makosa.
 
Hehehehehe....kama nilivyotabiri hapo awali leo, thread tayari imeshaanza kupungua mvuto....Lol
 
Threads zinazoongelea familia au marafiki wa karibu ni vigumu sana watu kuwa objective. Kuna watu fulani, kama FMES, wako so predictable when it comes to mtu kama Masha.

Inabaki kidogo tu wakavaa cheo cha "Press Secretary" wake.

Masha kachemsha, Mengi kachemsha, some JF heads stand alone in objectivity.

Mwinyi kujiuzulu uwaziri inatokana na kuelewa kwamba katika chain of command, the buck stopped with him before passing on to the president. Mwinyi alikuwa anafanya kazi kama walii, na hakuchukua hatua ilipobidi, lakini ukweli ni kuwa kuna watu kibao waliokuwa responsible kabla yake ukianzia na ma RPC kushuka chini.

Vivyo vivyo, hata Masha naye, ingawa Wizara yake inahusika katika kesi hii, na yeye ultimately yuko responsible kwenye mambo yote ya law and order Tanzania, lakini at this point kuna watendaji wengi sana wako chini yake, ambao wangeweza kulishughulikia hili, sasa kwa nini anakuwa kimbelembele? Au kuna maneno yamemuuma kwa sababu issue inamhusu? Na kama ni kweli, anataka kutumia madaraka yake ya kiwaziri kushughulikia issue inayomhusu yeye mwenyewe, hapa kuna bonge la conflict of interest, hii hata si kesi ya nyani kumpelekea ngedere, hii kesi ya nyani unampa nyani mwenyewe, unategemea nini?

Kwa nini Masha katika ma beef yooote ya Mengi alikuwa hajasikika? Mpaka hili? Hili lina umuhimu gani wa pekee kwa Masha?

Asitake kujifanya ana uchungu sana wa ku keep law and order Tanzania (kuna ma albino wanakufa hatujamsikia kufanya chochote cha maana) tunajua anavalia hili njuga kwa kuwa ego yake imekuwa punctured na kadiri kila siku inavyopita watu wanavyozidi kuuona utupu wake.
 
1.
Sasa na wewe ukiambiwa uthibitishe kwamba huyu mzee hana ushahidi itakuwaje? au ukiambiwa useme walevi gani ndio walimpelekea hiyo taarifa, si utapata hasira tu zaidi?

- Mimi sihusiki na kesi hii labda umekosea mkuu, kesi itaenda kwenye sheria, utafiti wangu nimegundua kwua huenda mzee ana habari alizozirecord kwa siri, jana nimeongea na wengi sana wanaojua vizuri hii kesi, ila samahani mimi sihusiki.

2. [
B]Ukiambiwa uthibitishe? Wanaoshutumiwa hawaongei, maana kama wangekuwa wanajua kwamba hakuna ushahidi wangeviwajibisha hivyo vyombo faster fatser yani.[/B]

- ?????????????????

3.
Ooho! Sasa mchezo ndio umeanza wewe ushakuwa jaji. Kama unataarifa za ziada, ungesaidia kutuelimisha. Lakini nadhani mchezo ndio umeanza, na kwa information zilizopo hatujui kwa hakika kama analinda taifa au anajilinda yeye mwenyewe.[/B
]

- Ndio maana ninasema hivi acha sasa mchezo uende kwenye sheria, ndio ukweli utajisema wazi.

4.
Kwani angekaa kimya tu, hiyo taarifa ya Mengi ingekuwa na hatari gani kwa taifa kiasi kwamba lihitaji kulindwa (namaanisha taifa sio serkali, tafadhali)? Maana tunavyojua ni kwamba anasema amemsamehe, na maana yake ni kwamba kwa upande wake yamekwisha.

- Kwa upande wake yameisha sasa inakuja upande wa sheria, yaani jamhuri ndio kwanza yameanza.

5.
Oohoo ... objectivity ni chachuu ya kutafuta ukweli ...
Lakini anahaki ya kuamua kama anaenda kwenye vyombo vya sheria ama la. Mbona wewe huwa unaleta malalamiko yako huku badala ya kupeleka kwenye vyombo vya sheria? Mbona husemi kwamba Masha angeenda mahakamni badala ya kutoa siku saba kwenye TV? Sina tatizo na opinion zako baba, bias yako inakuwa wazi mno.

- Mimi kama member wa JF nina haki ya kutoa maoni yangu hapa kwa kutumia ukweli na sio chuki za binafsi na wivu, naomba kukumbusha tena kua I have nothing to do na hii kesi naona hili hulielewi, na pia ni haki yangu ku-take sides, kama vile kwenye kesi yake Mengi na Manji nilichukua side ya Mengi, this time nimechukua side ya serikali against Mengi, na ninasema wazi maana ni haki yangu kisheria, au?

6.
Mzee nadhani wapo wanaowaita viongozi waliopo madarakani ni mafisadi, na data wanzo, na wameshare na sisi. Sasa ungesaidia katika harakati za kuwaprove wrong ungekuwa unafanya la maana zaidi. Ukiambiwa uthibitishe kwamba sababu inakuwa ni chuki binafsi tu, utaweza? au utapata hasira zaidi tu?

- Ndio maana nimesema Dr. Slaa anastaili pongezi kwani alitoa tuhuma na ushahidi mzito usiopingika, kudai waziri ajiuzulu bila ukweli wa tuhuma ni tatizo linalotumaliza sana taifa hili, kama na wewe una ukweli wa mafisadi uweke hapa!

7.
Hapo umenena vizuri, kwamba ni vizuri kuwa na ukweli. Sasa ingekuwa vizuri badala ya kulalama kwamba watu wanawasingizia wengine, ungejaribu kuonyesha kwamba either hawana uthibitisho au uthibitisho uliotoka haujitoshelezi. Kwa swala hili, Kama una information ambazo wengine hatuna, labda hutusaidie. Lakini nadhani wengi wetu tunachokijua ni kile tunachokisikia kutoka kwa hawa mabwana. Hatujui kama hilo tishio lilitokea kweli ama la. Na kama lilitokea, hatujua kama mzee ana uthibitisho ama la. Hatujui kama waziri anatumia njia zozote kulinda taifa, ama kujilinda mwenyewe. Sasa kutumia bias yako na kuwa hakimu na ku-draw conclusion nadhani ni missues ya bytes za site; only my opinion.Hii ni vita kati ya watu wawili, na ukweli ni kwamba kila mmoja atajaribu kutumia resourse zote zinazoweza kutmika kushinda vita. Huyu atatumia media zake, huyu atatumia wadhifa wake. Hapa labda tungejaribu kuwa objective kidogo na kutafakari yaliyo mbele yetu. Kutuonyesha side yako kwa hasira hivyo is ok, kwa sababu ya free speech and all. Lakini na wewe pengine kutumia right yako ya free speech hapa kufanya yale yale unayowashutumu wengine kufanya, nadhani ni aina flani ya unafiki. Jinsi ambavyo unasema mzee anatumia media zake kwenye hili, na jinsi ambavyo wengine wanasema waziri anatumia madaraka yake kwenye hili, ni aina ya kitu ulichokifanya kwenye sehemu kubwa ya post yako ...

Heshima mbele

- Mkuu ishu inakwedna kwenye sheria kwa hiyo majibu yote yatapatikana huko na kila mhusika atapewa haki.

Heshima Mbele Mkuu!
 
- Sio tabia yangu kutetea ujinga, na pia sio tabia yangu kufuata bendera, na pia sio tabia yangu kujikomba kwa watu flani ili nilindwe, na sio tabia yangu kuingia kwa ID nyingi, maana unahitaji kujikomba ili wakulinde kwa sababu ya tabia zinazofanana, kama ninavyoona siku hizi sina hizo tabia period!.

- Masha kama waziri akikosa nitakua wa kwanza kusema, kwa mfano alipoliongelea shirika la IMMA akiwa waziri wa jamhuri, sikumtetea kabisa on that maana he was out of the line, IMMA wana wasemaji wao.

My objectivity, katika ishu za taifa hapa JF sio lazima iwe approved na member mwingine, na sio lazima nifuate mkumbo ili just ku-fit in the crowd, msimamo wangu on this ishu uko vile vile kwamba Mengi this time anahitaji kutihibitiwa kisheria maana now he is going out of the line na sheria za jamhuri, na sio lazima niwe na mawazo kama yako kuwa objective. Masha kama waziri anatimiza tu wajibu wake kama sheria inavyotaka.

Sio lazima tukubaliane mawazo, na huwi press secretary wa Mengi kwa kuwa na mawazo tofauti na mimi kwenye hii ishu, hizi name calling ni dalili za kutokua na hoja, ukiisoma sana hii thread utaona wenye hoja huwa hawana time za name calling ni wale tu wasiokuwa nazo ndio utawaona wanahangaika.
 
Sasa kwa nini Masha karukia issue bila kuangalia chain of command ikoje? Hivi akitaka kufuatilia issue kama hii kuna issue ngapi za kufuatilia? Atapata muda wa kufuatilia? Kwa nini asiwaachie polisi na wapelelezi wamdai Mengi uthibitisho?

Hiki kimbelembele cha Masha kuivalia njuga hii issue, pamoja na suspicion kwamba issue inamhusu, ndivyo vitu vinavyotufanya kufikiri kwamba Masha ana a personal stake in this issue, na kutokana na hilo, anaweza kutokuwa fair na kutumia Uwaziri wake isivyotakiwa.

Kwa nini amerukia hili wakati kuna watu kibao huko kuanzia ma inspector wa polisi mpaka wapelelezi wangeweza kumkaba Mengi atoe majina? tena kimya kimya bila hata ma headline yanayozidi ku complicate na ku sensationalize hii issue?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom