Mengi Vs Masha tuhuma, vitisho na matokeo!

Mengi Vs Masha tuhuma, vitisho na matokeo!

Status
Not open for further replies.
Hebu msome kwa kutulizana, ama sivyo nyie ndio mnakuwa (as you like to put it) "wakurupukaji"

Mleta habari hapo juu amesema, "Nimesikia TBC leo asubuhi kwamba Mh. Masha kama Waziri wa Mambo ya Ndani amempa siku saba Mr Mengi athibitishe kauli alizo toa . Kazi imeanza."

Keyword, kama waziri wa mambo ya ndani....Hivyo, kutokana na habari hapo juu, Masha hajasema kuwa Mengi athibitishe maneno yale yametoka kwake.

Ama la, labda habari haijakuwa quoted kama ilivyokuwa reported. Slow your roles!
 
Mhe. Masha kaongea kama Waziri mwenye dhamana na Jeshi la Polisi.Mengi awezi kutoa Tuhuma kama hizo na akaachwa hivi hivi
 
Anajishuku jamani....ila mchezo mzito sana hapo Power....Proffesinalism....Popularity ....and Mass support.......
 
-- whistling -- kitu cha kwanza Masha ajiuzulu Uwaziri kwanza just to make it a fair game.
 
Mtuhumiwa yeyote duniani akiona polisi ama wanausalama akili huhangaika, na wapelelezi makini wanaojua saikolojia za wahalifu huwa ni rahisi kwao kuwatambua wahalifu. Huwezi tulia ukitenda kosa haswa uliemtenda akianza kuongea nini ulifanya.....................
 
Haya ni matokeo ya uteuzi wa shukrani. Mr. M ameajiri mtoto wangu na binti wa mkuu wa nyumba ya SMZ ni lazima awe waziri hata kama hana sifa. Matokeo yake kusema ovyo; leo mauaji ya albino ni jambo dogo, kesho Mengi apewa siku saba!!! Mengi yanakuja.
 
Waziri wa mambo ya ndani siyo polisi wala mwendesha mashitaka au hakimu. Hawezi kusimamia uchunguzi wa uharifu, kukamata waharifu au kushitaki waharifu; kwa hiyo hawezi kusema Mengi athibitishe madai yake katika siku saba. Hiyo ni kazi ambayo inafanywa na polisi kutokana na ripoti zilizotolewa na raia (Mengi, in this case) . Kwa vile Mengi alishatoa taarifa zake huko polisi basi Masha awaache wataishughulikia na wala sijiingize kwa vile polis wana kesi nyingi za kushughulikia nchi nzima.

Sielewi hiyo ultimatum yake ya siku saba ni ya nini. Je Mengi akishindwa kuthibitisha katika siku hizo saba ndiyo iweje, malalamiko yake yatupiliwe mbali. Nilisikia kuwa jamaa huyu ni mwanasheria msomi aliyefanikiwa sana katika biashara ya sheria nikadhani ana busara lakini kumbe ni bomu kabisa. Anatoa vitisho vya kitoto kama vinavyotolewa na KCC aliyelewa madaraka.
 
Mi nadhani, kwa sababu Mengi alimtuhumu waziri (kwa kutaja cheo cha uwaziri wa Serikali ya Tz) basi anakuwa ameituhumu serikali.
Kwa hiyo Masha hapa anafanya kazi ya kuitetea Serikali hata kama aliyetuhumiwa si yeye......japo pia naona kwa upande wa pili aliyepaswa kuliongolea ni hili ni yule waziri aliyesuswa na media.
 
Mengi angekuwa muungwana naye si angetaja jina la huyo waziri mambo ya kutufumbia mafumbo tena ya nini?
 
nimemsikiliza waziri masha kwenye tbc asubuhi na ninaona wengi wa wachangiaji hapa wameongea na hawakuisikia sakata lenyewe na jinsi masha alivyoji.

kwanza cha kushangaza ni pale ambapo polisi wamesema hawana taarifa zozote kama mengi karipoti kuwa katishiwa wakati masha mwenyewe kataja mpaka kituo cha polisi ambacho mengi karipoti sakata hili.

kuna mambo mawili ambayo yanaenda sambamba kwanza ni swala la mengi kutumiwa msm ya vitisho vya kuuliwa na pili kutumia vyombo vyake vya habari kuituhusu serekali kwa ujumla kupitia waziri wake kijana wa wizara muhimu kuwa amependekeza yeye aflisiwe kwa kupewa kodi kubwa anmbayo hataweza kuilipa.

hili la kwanza ambalo ni kutishiwa kuuwawa kwa kutumiwa sms ndilo ambalo mengi kaliripoti polisi kufwatana na masha kuwa hata sms itabidi azitoe iliwaweze kuzifanyia uchunguzi hapa masha si kama polisi lakini ni bosi wa polisi

hili la pili la kuituhumu serekali kwa kupitia waziri wake ndilo masha alilolitolea tamko kwa kumpa Mengi siku saba awe amethibitisha kauli yake na hapa ameongea kwa niaba ya sereka kwani wizara yake ndio yenye jukumu hili au mlitaka liongelewe na wizara ya mambo ya ndani tujitahidi kuwa fair na si kwasasababu tuklishajanza fikra kuwa ni masha basi na asitoe tamko hapa amemtaka mengi kuthibitisha na kumtaja huyo waziri live na atoe ushahidi wa madai yake na amemtaka pia kupeleka madai yake kwenye kituo hicho hicho alichoripoti kutishiwa kuuwawa au kupeleka kwame masha mwenyewe kama waziri wa mambo ya ndani.

katika kauli za masha pia kulikuwa na kukurupuka kwa hali ya juu kwani naye hapa alimshutumu mengi kuwa kwasababbu anamiliki vyombo vya habari basi ametumia nafasi hiyo kutangazia watanzania kuwa kuna waziri anamuhujumu na hapa tunamuona masha naye akitumia nafasi yake kwa kutumia chombo cha umma tbc1 kuutangazia umma wa watanzania kuwa mengi athibitishe na kuwa akitoka hapo tbc1 angekwenda kumwandikia mengi barua hivyo hapo bado haikuwa rasmi mapaka hapo mengi ambapo atapokea barua hiyo na masha amesema kuwa kwa mengi kushindwa kufanya hivyo basi seria itachuklua mkondo wake hapa naona sheria ni kuvimwanahalisi vyovyo vya mengi na hichi pengine kwa mtazamo wangu ndicho haswa kilichokuwa kinatafutwa na watakipata kwa njia rahisi sana ikiwa mengi alikurupuka kuongelea swala hili.

au pengine wataitwa bungeni kwenda kupataniswa tena ????

yetu macho na masikio
 
kama ndio hivyo basi masha alituma hiyo msg kwa mengi na kamA HAKUTUMA KWA NINI ATOE SIKU SABA? KWA HIYO MENGI ANA HAKI YA KUMSHITAKI MASHA KWA KUMSINGIZIA KUWA YEYE MENGI KATUMIWA MSG NA MASHA ==================HAPA KAZI IPO

Masha ameongea kama waziri, tamko hilo limetolewa na Polisi, besides Masha alikaribishwa kwenye kipindi cha jambo Tanzania.

Mimi nimeipenda hiyo, sio kila mtu awe nakaurupuka na kujisemea semea hivyo
 
Mi nadhani, kwa sababu Mengi alimtuhumu waziri (kwa kutaja cheo cha uwaziri wa Serikali ya Tz) basi anakuwa ameituhumu serikali.
Kwa hiyo Masha hapa anafanya kazi ya kuitetea Serikali hata kama aliyetuhumiwa si yeye......japo pia naona kwa upande wa pili aliyepaswa kuliongolea ni hili ni yule waziri aliyesuswa na media.

Ndiyo maana kuna Mwanasheria Mkuu au DPP!
 
mengi yanatokea siku hizi. wanasiasa wengine bado wanaishi miaka 20 iliyopita.
watanzania walioongozwa miaka 20 iliyopita sio wa leo. leo wana ujasiri wa kuhoji na kutafiti na kufuatilia mambo yanayowahusu.
Ndio maana bei/gharama ya urafiki katika wanasiasa imepanda. hivyo kama rafiki amekuwa moto mno kisiasa inabidi umteme uwaachie wa "sanda karawe, amina! mwenye kupata apate mwenye kukosa akose"
 
Hii kazi ya kutaka Mengi athibitishe tuhuma zake ilitakiwa ifanywe na polisi. Masha kama waziri hawezi kumpa ultimatum Mengi na hapa ndio inaonyesha wazi calibre ya mawaziri wa Jakaya; wengi hawana intergrity wala foresight!!Mengi kamtegea huyu fisadi na kweli kaingia mwenyewe kichwa kichwa na sasa ataipata fresh!!
 
............................................My eyes
 
Nimesikia TBC leo asubuhi kwamba Mh. Masha kama Waziri wa Mambo ya Ndani amempa siku saba Mr Mengi athibitishe kauli alizo toa . Kazi imeanza.
Mi nadhani ni utovu wa nidhamu kijana kama Masha kumpa baba yake siku saba za kujieleza. Kijana ameanza kulewa madaraka, aha ananikumbusha enzi za mzee Tino Lyat.. Mre..Tofauti ni kwamba jamaa alikuwa anatoa siku saba majambazi wasalimishe silaha, mtu awajibike n.k. Hii ya kamanda kuleta beef na wazee wake imekaa vibaya.
 
mengi alisema amemsamehe huyu waziri, sasa asipothibitisha Masha atamlazimisha???
Tuhuma alizopewa mengi Zinaanza kuwa ni ukweli na watammwanahalisi.
Ikumbukwe Masha naye ni miongoni mwa mafisadi na ni baadhi ya mafisadi waliobaki na kuendelea kupumua japo kwa shida sasa kazi ipo....

masha tueleze ni jinsi gani IMMA ilihusika na deep green then ......
 
Ndiyo maana kuna Mwanasheria Mkuu au DPP!

Hayawezi kufika kwa hao kabla POLISI hawajafanya kazi yao. Baadhi tulidhani kauli hii ya MASHA angeitoa KOVA, MSIKA,DCI au IGP. Vinginevyo wanamwongezea umaarufu mzee wetu Mengi bila sababu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom