Mengi Vs Masha tuhuma, vitisho na matokeo!

Mengi Vs Masha tuhuma, vitisho na matokeo!

Status
Not open for further replies.
Naona kwako kaka kila kitu ni kujiudhulu,sijui watajiudhulu wangapi?Ata kama wanataka mheshimiwa atoe uthibitisho wa Waziri anayemtuhumu!Lakini kuna kitu lazima tujiulize mimi nadhani huyu Mengi naye ana matatizo kila wakati amekuwa akigombana na watu kwa visingizio tofauti.Mara nyingi amekuwa akifikiri kutokana na jina lake watu watampa kila kitu bure.Aligombana na Masilingi kisa hotel,amekosana na Manji kisa magodauni na sasa ameyaanza mengine.Kiboko yake Mkapa alilia lia hakumsikiliza kabisa!

Tusifikirie kila wakati kuwa huyu mzee anakuwa sahihi lakini yeye ana interest yake kubwa ambayo ni biashara na tusije kufikiri kuwa atakuwa anamtetea Mtanzania wa kawaida la hasha anatafuta maslahi tu huyu.

Wanasema "doing well by doing good". Kama lengo lake kuu ni biashara na on the way akajikuata anawasaidia watanzania wa kawaida kuna ubaya gani? Kama alianzisha Kulikoni na This Day kwa lengo la biashara tu halafu on the way yakatusaidia kupata ukweli ambao kwa kawaida tusingeupata kuna ubaya gani? Au kwako hiyo haina tofauti na yule anayenunua chombo cha habari akiwa hana lengo la biashara yake, bali kuuficha ukweli wa aina hiyo usimfikie mtanzania wa kawaida?

Give credit where credit is due bwana. M-blast kwa ya hovyo, mazuri mpongeze... huo ndio uungwana.

Kama ni kugombana na watu, hata akigombana na watu miamoja hiyo sio sababu tosha ya kuhitimisha kwamba lazima yeye ndiye ana matatizo. Unachotakiwa kufanya ni at least kutuonyesha katika mara hizo mia, mara nyingi eventually yeye ndio anakuwa na makosa.
 
On serious note: Anyone knows wot happened to Zeutamu blog?

Zeutamu is the height of idiocracy, if that is your serious note I don't know what your light touch will be, some mollusc-brain level of engagement?
 
- Sio tabia yangu kutetea ujinga, na pia sio tabia yangu kufuata bendera, na pia sio tabia yangu kujikomba kwa watu flani ili nilindwe, na sio tabia yangu kuingia kwa ID nyingi, maana unahitaji kujikomba ili wakulinde kwa sababu ya tabia zinazofanana, kama ninavyoona siku hizi sina hizo tabia period!

Ashindwaye kwa hoja huanza viroja. Kumbe kuna wengine nao hutuhumiwa kwa ID nyingi - nilifikiri ni mimi peke yangu. Some guys are so predictable.
 
Zeutamu is the height of idiocracy, if that is your serious note I don't know what your light touch will be, some mollusc-brain level of engagement?

Just to let u know our beloved blog is back with a bang! if thats usefull 2 u....
 
1.
Sasa kwa nini Masha karukia issue bila kuangalia chain of command ikoje? Hivi akitaka kufuatilia issue kama hii kuna issue ngapi za kufuatilia? Atapata muda wa kufuatilia? Kwa nini asiwaachie polisi na wapelelezi wamdai Mengi uthibitisho?

- Mkuu wa objectivity kwa nini usionyeshe sheria inayosema kuwa waziri wa ndani hahusiki wanaohuiska ni polisi na wapelelezi? Kama hahusiki ikienda kwenye sheria basi Mengi atakua na upenyo mkubwa sana wa kushinda maana anahaitaji tu ku-raise hilo kwamba kwa nini waziri amehusika wakati sheria haimruhusu!

2.
Hiki kimbelembele cha Masha kuivalia njuga hii issue, pamoja na suspicion kwamba issue inamhusu, ndivyo vitu vinavyotufanya kufikiri kwamba Masha ana a personal stake in this issue, na kutokana na hilo, anaweza kutokuwa fair na kutumia Uwaziri wake isivyotakiwa.

- Unajua ndio maana mimi sina objectivity, maana look wewe una objectivity lakini unaona hapa mwenye kimbele mbele ni waziri na sio Mengi aliyeanza, Malima alipomshitaki Mengi, aliwahi kufanya kazi kama Director katika kampuni za Manji, na bado Mengi alishinda kesi, sasa kwa nini this time kuna wasi wasi kama itakwua ni yeye? Mbona Malima hakutumia uwaziri wake isivyotakiwa? So much for being objectivity's champion!

3.
Kwa nini amerukia hili wakati kuna watu kibao huko kuanzia ma inspector wa polisi mpaka wapelelezi wangeweza kumkaba Mengi atoe majina? tena kimya kimya bila hata ma headline yanayozidi ku complicate na ku sensationalize hii issue?

- Waziri wa ndani analinda wananchi wa ndani ya Tanzania, Mengi included, where is a complication? kinachotakiwa hapa ni Mengi kufuata sheria tu, maana ninaamini kwamba Masha anafuata sheria na kama hafuati basi Mengi si anao wanasheria, au?
 
Ashindwaye kwa hoja huanza viroja. Kumbe kuna wengine nao hutuhumiwa kwa ID nyingi - nilifikiri ni mimi peke yangu. Some guys are so predictable.

- Semo semo, hopefully tutaona jipya soon maana so far ni yale yale tu kweli kuna wasiochoka, kila siku michosho tu na never ending rants, wote ni lazima tufuate bendera tu!

JF sometimes kwa vichekesho bwana!
 
Just to let u know our beloved blog is back with a bang! if thats usefull 2 u....

It is what they call a "guilty pleasure", do you playa. My austere almost hypocritically puritanical self would forbid me to even dream of thinking of hinting about the prospect of engaging in the unfathomably and grotesquely tacky venture of frolicking in that temple of abomination and debauchery.Not to mention the fact that my wannabe gallant soul could never stomach women being so callously and unwarrantedly wrongfully exposed.

But it can be seductively educative and self-gratifying to see human beings steep so low, so if you see me there for some psychological studies on the functionings of the subconscious annals of the cognitive chambers of an idiocratic netizen's medulla oblongata, do not be surprised at all. Even nuns were known to watch Madonna's "Truth or Dare"

If I sound self contradictory it is because the truth of nature and nature of truth is self contradictory, that is why there is such a thing as "wave particle duality". After all it was that Norwegian sage Niels Bohr who so aptly and intuitively said "the opposite of a profound truth may very well be another profound truth".

Now don't derail some good old Masha/ Mengi lynching with some base fleshy innuendos.
 
Last edited:
Mengi jino kwa jino na Masha

Habari Zinazoshabihiana
• Polisi avunjwa jino kwa chupa ya bia 03.08.2007 [Soma]
• Shekhe jino kwa jino na Mchungaji kuhusu Dito 22.03.2007 [Soma]
• Kupanda kwa bei za mafuta:Masha asema Serikali inafanyia kazi mapendekezo 27.05.2006 [Soma]

*Serikali yampa siku saba ajieleze kuhusu kutishwa
*Yeye asema nyingi, amtaka Waziri ampeleke kortini


Na Waandishi Wetu

SERIKALI imempa siku saba Mwenyekiti wa Kampuni za IPP, Bw. Reginald Mengi, kuthibitisha madai yake kwamba kuna waziri kijana katika Serikali ya Rais Jakaya Kikwete amemtishia na kwamba kuna mikakati ya kufilisi biashara zake.

Akizungumza na Kituo cha Televisheni ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC1) na kurushwa jana asubuhi Waziri wa Mambo ya Ndani, Bw. Laurence Masha, alisema madai yaliyotolewa na Bw. Mengi yanaonesha kwamba Serikali haiwalindi vyema raia wake.

Waziri Masha alisema Mwenyekiti huyo anapaswa katika muda huo awe amethibitisha madai hayo, ili Serikali iweze kuangalia taratibu za kuyashughulikia.

Alisema jana angemwandikia rasmi barua ya kumtaka kuthibitisha madai yake ambayo aliyatoa juzi mbele ya vyombo vya habari, Dar es Salaam.

Kabla ya kutolewa agizo hilo jana, Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, lilisema lilikuwa halijapokea taarifa yoyote kutoka kwa Bw. Mengi kuhusu kutishiwa na Waziri na hivyo lisingeweza kuliingilia suala hilo.

Akizungumza na Majira, Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Bw. Evarist Mangala, alisema hadi juzi Desemba 3 hawakuwa na taarifa yoyote ambayo iliripotiwa kuhusu kutishiwa maisha kwa Bw. Mengi na badala yake walizisoma taarifa hizo kwenye vyombo vya habari.

Kuhusu siku saba alizopewa na Bw. Masha kuwasilisha ushahidi wake, Bw. Mengi alisema siku hizo ni nyingi na kumtaka Waziri kumpeleka Mahakamani haraka iwezekanavyo.

"Vitisho ni vingi sana, lakini si kila kitu ninaweza kupeleka taarifa Polisi, hivyo ninaangalia kikubwa ni kipi kinachotisha zaidi ndipo ninatoa taarifa Polisi, lakini iwapo itagundulika kuwa niliudanganya umma kuwa nilitoa taarifa katika kituo cha Polisi wakati sijatoa, niko tayari kwenda jela,

"Lakini pia iwapo itagundulika kuwa Waziri pia ameudanganya umma kuwa sikutoa taarifa Polisi wakati nilitoa, je yuko tayari kujiuzulu wadhifa wake?" alihoji Bw. Mengi.

Kuhusu suala la kumtaja Waziri kijana na msomi aliye katika Wizara nyeti, Bw. Mengi alisema kwa kawaida Mwenyezi Mungu ana nguvu kubwa na za kipekee, hivyo zinaweza kumfanya mtu huyo kujitaja mwenyewe.

"Kwa kawaida Mungu ana nguvu kubwa na za pekee sana, hivyo katika mazingira ya sasa, nguvu hizo zinaweza kumfanya mhusika kujitaja mwenyewe," alisema.

Bw. Mengi alisema ameshindwa kuelewa majukumu ya Waziri Masha katika jambo hili alilosema kupitia TBC1, kwani hajawahi kusikia kama yeye ni Msemaji Mkuu wa Serikali au wa Wizara.

"Kitu nisichokielewa ni majukumu ya Waziri Masha katika suala hili, alikuwa akitoa tamko hilo kama Msemaji Mkuu wa Wizara au Serikali, alikuwa akizungumza kama nani, nauliza hivyo kwani sijui taratibu za Serikali kama yeye ni msemaji wa sehemu hizo.

"Nilizungumzia Waziri kijana wa wizara nyeti, mawaziri vijana wako wengi, yuko Ngeleja (William, 41), Kamala (Deodorus, 40) na yeye Masha (38) hivyo umri wao unashabihiana, sijui atakuwa amezungumza kwa niaba ya vijana wengine ama vipi?," alisisitiza Bw. Mengi.

Bw. Mengi alihoji kuwa iwapo suala la kuripoti Polisi linalomhusu yeye katika Wizara yake ameshindwa kukubaliana nalo, je kuwapo kwa suala la kumfilisi ambalo haliko katika wizara yake, atakuwa tayari kulikubali?

Waziri Masha alipoulizwa na waandishi wa habari kuhusu suala la kumpeleka Bw. Mengi mahakamani haraka iwezekanavyo na kumpelekea barua ikimtaka kutoa ushahidi ndani ya siku saba, alisema suala la kumpa siku saba Bw. Mengi si sababu, hivyo angeweza kupeleka ushahidi huo hata jana.

Bw. Masha alisema alishindwa kupeleka barua hiyo jana asubuhi, kutokana na kuwa mkutanoni, hivyo aliahidi mara baada ya kutoka mkutanoni angeipeleka barua hiyo mara moja.

Hata hivyo, hakuweza kutoa ufafanuzi kuhusu suala hilo, kutokana na kuwa mkutanoni na Waziri mwenzake wa Burundi.

Awali vyombo vya habari viliripoti kuwa Bw. Mengi anadai kutishiwa kifo na mtu aliyemtaja kuwa ni Waziri kijana katika Serikali ya Rais Kikwete akihusisha vitisho hivyo na msimamo wake wa kukemea ufisadi.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari ambao ulifanyika juzi, Mengi alidai kuwa amekuwa akitumiwa ujumbe ambao unavituhumu vyombo vyake vya habari kuwa vimekuwa mstari wa mbele katika kukemea ufisadi jambo ambalo 'waziri kijana' kuwa si jambo zuri kwa sababu linawanyanyasa baadhi ya watu.
 
Mengi jino kwa jino na Masha

Habari Zinazoshabihiana
• Polisi avunjwa jino kwa chupa ya bia 03.08.2007 [Soma]
• Shekhe jino kwa jino na Mchungaji kuhusu Dito 22.03.2007 [Soma]
• Kupanda kwa bei za mafuta:Masha asema Serikali inafanyia kazi mapendekezo 27.05.2006 [Soma]

*Serikali yampa siku saba ajieleze kuhusu kutishwa
*Yeye asema nyingi, amtaka Waziri ampeleke kortini


Na Waandishi Wetu

SERIKALI imempa siku saba Mwenyekiti wa Kampuni za IPP, Bw. Reginald Mengi, kuthibitisha madai yake kwamba kuna waziri kijana katika Serikali ya Rais Jakaya Kikwete amemtishia na kwamba kuna mikakati ya kufilisi biashara zake.

Akizungumza na Kituo cha Televisheni ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC1) na kurushwa jana asubuhi Waziri wa Mambo ya Ndani, Bw. Laurence Masha, alisema madai yaliyotolewa na Bw. Mengi yanaonesha kwamba Serikali haiwalindi vyema raia wake.

Waziri Masha alisema Mwenyekiti huyo anapaswa katika muda huo awe amethibitisha madai hayo, ili Serikali iweze kuangalia taratibu za kuyashughulikia.

Alisema jana angemwandikia rasmi barua ya kumtaka kuthibitisha madai yake ambayo aliyatoa juzi mbele ya vyombo vya habari, Dar es Salaam.

Kabla ya kutolewa agizo hilo jana, Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, lilisema lilikuwa halijapokea taarifa yoyote kutoka kwa Bw. Mengi kuhusu kutishiwa na Waziri na hivyo lisingeweza kuliingilia suala hilo.

Akizungumza na Majira, Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Bw. Evarist Mangala, alisema hadi juzi Desemba 3 hawakuwa na taarifa yoyote ambayo iliripotiwa kuhusu kutishiwa maisha kwa Bw. Mengi na badala yake walizisoma taarifa hizo kwenye vyombo vya habari.

Kuhusu siku saba alizopewa na Bw. Masha kuwasilisha ushahidi wake, Bw. Mengi alisema siku hizo ni nyingi na kumtaka Waziri kumpeleka Mahakamani haraka iwezekanavyo.

"Vitisho ni vingi sana, lakini si kila kitu ninaweza kupeleka taarifa Polisi, hivyo ninaangalia kikubwa ni kipi kinachotisha zaidi ndipo ninatoa taarifa Polisi, lakini iwapo itagundulika kuwa niliudanganya umma kuwa nilitoa taarifa katika kituo cha Polisi wakati sijatoa, niko tayari kwenda jela,

"Lakini pia iwapo itagundulika kuwa Waziri pia ameudanganya umma kuwa sikutoa taarifa Polisi wakati nilitoa, je yuko tayari kujiuzulu wadhifa wake?" alihoji Bw. Mengi.

Kuhusu suala la kumtaja Waziri kijana na msomi aliye katika Wizara nyeti, Bw. Mengi alisema kwa kawaida Mwenyezi Mungu ana nguvu kubwa na za kipekee, hivyo zinaweza kumfanya mtu huyo kujitaja mwenyewe.

"Kwa kawaida Mungu ana nguvu kubwa na za pekee sana, hivyo katika mazingira ya sasa, nguvu hizo zinaweza kumfanya mhusika kujitaja mwenyewe," alisema.

Bw. Mengi alisema ameshindwa kuelewa majukumu ya Waziri Masha katika jambo hili alilosema kupitia TBC1, kwani hajawahi kusikia kama yeye ni Msemaji Mkuu wa Serikali au wa Wizara.

"Kitu nisichokielewa ni majukumu ya Waziri Masha katika suala hili, alikuwa akitoa tamko hilo kama Msemaji Mkuu wa Wizara au Serikali, alikuwa akizungumza kama nani, nauliza hivyo kwani sijui taratibu za Serikali kama yeye ni msemaji wa sehemu hizo.

"Nilizungumzia Waziri kijana wa wizara nyeti, mawaziri vijana wako wengi, yuko Ngeleja (William, 41), Kamala (Deodorus, 40) na yeye Masha (38) hivyo umri wao unashabihiana, sijui atakuwa amezungumza kwa niaba ya vijana wengine ama vipi?," alisisitiza Bw. Mengi.

Bw. Mengi alihoji kuwa iwapo suala la kuripoti Polisi linalomhusu yeye katika Wizara yake ameshindwa kukubaliana nalo, je kuwapo kwa suala la kumfilisi ambalo haliko katika wizara yake, atakuwa tayari kulikubali?

Waziri Masha alipoulizwa na waandishi wa habari kuhusu suala la kumpeleka Bw. Mengi mahakamani haraka iwezekanavyo na kumpelekea barua ikimtaka kutoa ushahidi ndani ya siku saba, alisema suala la kumpa siku saba Bw. Mengi si sababu, hivyo angeweza kupeleka ushahidi huo hata jana.

Bw. Masha alisema alishindwa kupeleka barua hiyo jana asubuhi, kutokana na kuwa mkutanoni, hivyo aliahidi mara baada ya kutoka mkutanoni angeipeleka barua hiyo mara moja.

Hata hivyo, hakuweza kutoa ufafanuzi kuhusu suala hilo, kutokana na kuwa mkutanoni na Waziri mwenzake wa Burundi.

Awali vyombo vya habari viliripoti kuwa Bw. Mengi anadai kutishiwa kifo na mtu aliyemtaja kuwa ni Waziri kijana katika Serikali ya Rais Kikwete akihusisha vitisho hivyo na msimamo wake wa kukemea ufisadi.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari ambao ulifanyika juzi, Mengi alidai kuwa amekuwa akitumiwa ujumbe ambao unavituhumu vyombo vyake vya habari kuwa vimekuwa mstari wa mbele katika kukemea ufisadi jambo ambalo 'waziri kijana' kuwa si jambo zuri kwa sababu linawanyanyasa baadhi ya watu.
 
- Sio tabia yangu kutetea ujinga, na pia sio tabia yangu kufuata bendera, na pia sio tabia yangu kujikomba kwa watu flani ili nilindwe, na sio tabia yangu kuingia kwa ID nyingi, maana unahitaji kujikomba ili wakulinde kwa sababu ya tabia zinazofanana, kama ninavyoona siku hizi sina hizo tabia period!.
Ni vizuri kabisa kuona una nia njema na msimamo thabiti. Watu wa aina hiyo ni endangered species kwenye jamii zetu.

Ila tu nikukumbushe kwamba kuwa na msimamo thabiti tu pengine haitoshi; kujitahidi kuwa na msimamo thabiti na sahihi ndio ishara ya hekima. Na hii inakuwa rahisi unapoweza kuwa mpole, msikivu, na kukubali kusahihishwa pale ambapo makosa madogo madogo yapo wazi; sisi sio miungu, twakosea.


- Masha kama waziri akikosa nitakua wa kwanza kusema, kwa mfano alipoliongelea shirika la IMMA akiwa waziri wa jamhuri, sikumtetea kabisa on that maana he was out of the line, IMMA wana wasemaji wao.

My objectivity, katika ishu za taifa hapa JF sio lazima iwe approved na member mwingine, na sio lazima nifuate mkumbo ili just ku-fit in the crowd, msimamo wangu on this ishu uko vile vile kwamba Mengi this time anahitaji kutihibitiwa kisheria maana now he is going out of the line na sheria za jamhuri, na sio lazima niwe na mawazo kama yako kuwa objective. Masha kama waziri anatimiza tu wajibu wake kama sheria inavyotaka.
Kuwa objective haimaanishi kuweza kuswitch side mbili zinazokinzana from time to time.

Kuwa objective nadhani ni kuangalia facts zilizopo nu ku-draw logical conclusion kwa usahihi. Na kikwazo hapo mara nyingi ni hisia kumtawala mtu kupitiliza. La sivyo inakuwa si majadiliano ila ushabiki.

Kitu ambacho ninakimiss sanau humu ndani ni watu kutofautisha imani na mambo ya kweli. Kila mtu anauhuru wa kuamini anachotaka kuamini, tatizo ni pale mtua anapoichukulia imani yake kwamba ndio ukweli na kutaka wengine nao waichukulie kama ndio ukweli, la sivyo ni vita.

Kwa mfano, kusema kwamba "kwamba Mengi this time anahitaji kutihibitiwa kisheria maana now he is going out of the line na sheria za jamhuri" unaonyesha wewe unaamini nini kwenye hili. Ambayo its ok, na unajua mwenyewe sababu zilizokufanya uamini hivyo, na una haki kabisa ya kuamini unachoamini. Ila unapoiweka kwenye public domain, wengine watapenda kujua umefikiaje hitimisho hilo ili wachague kuamini unachoamini ama la. Sasa usiwe mkali wanapokuuliza maswali kama "anaenda out of line na sheria ipi ya jamuhuri?", au "hivi hakuna uwezekano kwamba kuna ka plan kama hako?", "hivi hakuna insidence za wafanyabiashara wanabambikiwa kodi nchi hiii?".

Ukiwa na msimamo na ukauweka kwenye public domain, jua kwamba watu wata-uchallenge. Sasa badala ya kuwa mkali, busara ni kuonyesha mantiki katika kufikia kuamini unachoamini. Kama huwezi, waambie hiyo ni imani yangu tu na naomba msinibugudhi. Na mtu akisema hivyo muheshimu, kaa mbali. Lakini ukisema huo ndio ukweli, kila mtu ana haki ya kuku-challenge. Ukishindwa kuitetea hoja yako, kuwa mpole sema nimechemka.

Tatizo linakuwa pale sasa mtu anapotaka imani yake ndio ichukuliwe kama kweli na kila mtu bila hata sababu za msingi. Tatizo kubwa zaidi ni pale walio kwenye mjadala wana imani na hypothesis tofauti na kila mmoja anataka yake ndio ichukuliwe kama ukweli bila kuhojiwa.


Sio lazima tukubaliane mawazo, na huwi press secretary wa Mengi kwa kuwa na mawazo tofauti na mimi kwenye hii ishu, hizi name calling ni dalili za kutokua na hoja, ukiisoma sana hii thread utaona wenye hoja huwa hawana time za name calling ni wale tu wasiokuwa nazo ndio utawaona wanahangaika.

Sadakta.

Ukweli ni ukweli ila imani zetu ndio zinatofautiana. Lengo la mazungumzo kama haya nikujaribu kuangalia imani ipi inakaribiana na ukweli, na pengine tunaweza kuufikia ukweli.

Namecalling inakuja pale mtu anapokuwa na hasira pindi wengine wanapokuwa wagumu kuichukulia imani yake kama ndio ukweli. Na inawezekana ni kwamba tu ameshindwa kuwaonyesha yeye amefikiaje hitimisho fulani, lakini yeye anaichukulia personal.

Mimi nilidhani pia kumtuhumu mtu kwamba anatamani kuwa secretary wa Mengi ndio maana anajaribu kuwa na mawazo tofauti na wewe ni name calling pia. Samahani kama nimekosea. 🙂
 
Mimi nilidhani pia kumtuhumu mtu kwamba anatamani kuwa secretary wa Mengi ndio maana anajaribu kuwa na mawazo tofauti na wewe ni name calling pia. Samahani kama nimekosea. 🙂

You know,

Unabonda, unabonda, halafu unarudia kile kile ulichobonda!

Unapoteza moral authority yote uliyojenga katika kubonda.

Zaidi ya hapo, ili kumuonyesha mtu aliyefanya "name calling" kuwa ni mtu frivolous, dispute name calling kwa kuonyesha ilipo wrong. Unasema mimi ni Press Secy wa Masha siyo, ona hapa nilimsema hivi, hapa nilimhold responsible hivi, hivyo siwezi kulinganishwa na Press Secy.

Otherwise kukuita Press Secy kunaweza kuwa a bit below the belt, but will actually encompass a shorthand and concise reflection of what a politically correct description could take a whole paragraph or two.
 
Ni vizuri kabisa kuona una nia njema na msimamo thabiti. Watu wa aina hiyo ni endangered species kwenye jamii zetu.

Ila tu nikukumbushe kwamba kuwa na msimamo thabiti tu pengine haitoshi; kujitahidi kuwa na msimamo thabiti na sahihi ndio ishara ya hekima. Na hii inakuwa rahisi unapoweza kuwa mpole, msikivu, na kukubali kusahihishwa pale ambapo makosa madogo madogo yapo wazi; sisi sio miungu, twakosea.

- Unajua siku hizi nimegundua kua kuwa mpole na kuwa msikivu kwa maana ya kwako hapa JF ni kufuata bendera ya mtu mmoja humu, I am not ready for that ninakuja hapa kukata ishus sio kujikomba kwa mtu, never!

- Sasa be who you are na mimi niache niendelee kuwa nilivyo lakini tukate ishus za taifa wka kutii sheria za JF, maana mimi I do not care kama wewe ni msikvu au hapana, maana tabia zako it is none of my business!. Halafu please can we talk kuhusu Mengi na Masha kuliko mimi zaidi maana unaweza kufungua thread kuhusu mimi if you want!

Thanxs na nitarudi later!
 

wakati mwingine hwua naanza kuhisi kama wewe ni mchaga bai haujadiliki.Sioni mantiki ya watu kumtete a Mtu kama Mengi.Mtu ambaye anadaiwa na wafanyaki wake pesa ya fidia.

Iko wapi maana ya kutoa million 100 wakati unadaiwa?


Kwani tunaongelea madai ya Mengi ama Mengi mwenyewe.

Tunapinga na kusupport mtu binafsi au kauli madai yao katika swala hili la vitisho kwa Mengi kama raia na Masha kama Waziri.

Kudaiwa na wafanyakazi wake kunamnyima utetezi wa kisheria kuhusu vitisho vyake .
Kama utakuwa tunajadili issues hatutasita kumtetea Mengi anahitaji utetezi kama raia mwezetu na hatuta sita kumlaumu pale anapokosea kama vile unavyodai anadaiwa na wafanyakazi wake(kama kweli)
 
Ni aibu sana na inatisha sana pale ambapo viongozi wetu wanatumia fedha zetu kutuhujumu sisi na wapendwa wetu.

Mara nyingi nimezoea kwenye vita ambayo mfanyabiashara mzalendo anajikuta akigongana vichwa na wafanyabiashara waasia au wazungu, basi mara moja viongozi wetu wanapambana kinyume na huyu mzalendo.

Sijui hii ni dalili ya utumwa uliokomaa sana au ni ubinafsi au ni kujiona duni kwa viongozi wetu au ni nini haswa?

Nitakuja na hoja ya kuchambua jambo hili la Uafrika (Weusi), Uasia na Uzungu muda si mrefu.
 
Binafsi natatizwa mno na kauli ya Masha. Napata picha kuwa hakuwa makini na alikurupuka. Pengine dhamira inamsuta kuwa ndiye aliyepeleka vitisho hivyo na sasa anajihami kutumia madaraka yake au ni ulevi wa madaraka unaopumbuza uwezo wa kufikiri. Natatizwa na kauli yake kwasababu:
(1) Amekurupuka kutangaza hadharani kabla hajampelekea mhusika barua, na hata hiyo barua ilikuwa haijaandikwa wakati anatangaza. Je kulikuwa na haraka gani? Tangazo lenyewe litadumu kwa siku 7!
(2). Akipata hivyo vielelezo na kama vinamuhusu yeye binafsi kama Masha, atafanya nini? Maana naye yumo katika hiyo probability (1/3).
(3). Ni kwanini adai vielelezo vipelekwe wizarani wakati utaratibu wa kawaida unafahamika kuwa hayo ni masuala ya polisi na mahakama? Yeye kama waziri, si ingetosha kumshauri Bwana Mengi, tena si lazima kupitia TBC, kufungua kesi ya kutishiwa kuuawa na kupeleka vielelezo vyake mahakamani ili mhusika wa vitisho awajibishwe kwa mujibu wa sheria.
(4). Kama anafikiri maelezo ya Bwana Mengi yameiumbua serikali, basi serikali haiwezi kuwa hakimu wa kesi yake mwenyewe kwa kudai vielelezo kutoka kwa mtuhumiwa wake - Bwana Mengi. Serikali ilipaswa kufungua kesi dhidi ya Mengi ili Mengi alioshe jina la serikali mahakamani.

Napata wasiwasi kuwa kwa mtindo wa kufikiri wa Masha, serikali haina kiongozi katika wizara hii. Namshauri kwa dhati kabisa Bwana Mengi asipeleke vielelezo vyake wizarani. HAKUNA MANTIKI yeyote ya kufanya hivyo. Hata akiletewa barua (kichekesho: barua inafuata tangazo!!!!), aijibu barua hiyo kwa kumwambia waziri apeleke suala hili mahakamani na yeye (Mengi) atoe vielelezo vyake mahakamani kama mshtakiwa.

Binafsi, nalichukulia tangazo la Masha kama la kitoto. Halipaswi kutolewa na waziri kwa namna alivyoitoa. Masha anaiaibisha serikali, wizara na taaluma yake ya sheria.
 
Binafsi natatizwa mno na kauli ya Masha. Napata picha kuwa hakuwa makini na alikurupuka. Pengine dhamira inamsuta kuwa ndiye aliyepeleka vitisho hivyo na sasa anajihami kutumia madaraka yake au ni ulevi wa madaraka unaopumbuza uwezo wa kufikiri. Natatizwa na kauli yake kwasababu:
(1) Amekurupuka kutangaza hadharani kabla hajampelekea mhusika barua, na hata hiyo barua ilikuwa haijaandikwa wakati anatangaza. Je kulikuwa na haraka gani? Tangazo lenyewe litadumu kwa siku 7!
(2). Akipata hivyo vielelezo na kama vinamuhusu yeye binafsi kama Masha, atafanya nini? Maana naye yumo katika hiyo probability (1/3).
(3). Ni kwanini adai vielelezo vipelekwe wizarani wakati utaratibu wa kawaida unafahamika kuwa hayo ni masuala ya polisi na mahakama? Yeye kama waziri, si ingetosha kumshauri Bwana Mengi, tena si lazima kupitia TBC, kufungua kesi ya kutishiwa kuuawa na kupeleka vielelezo vyake mahakamani ili mhusika wa vitisho awajibishwe kwa mujibu wa sheria.
(4). Kama anafikiri maelezo ya Bwana Mengi yameiumbua serikali, basi serikali haiwezi kuwa hakimu wa kesi yake mwenyewe kwa kudai vielelezo kutoka kwa mtuhumiwa wake - Bwana Mengi. Serikali ilipaswa kufungua kesi dhidi ya Mengi ili Mengi alioshe jina la serikali mahakamani.

Napata wasiwasi kuwa kwa mtindo wa kufikiri wa Masha, serikali haina kiongozi katika wizara hii. Namshauri kwa dhati kabisa Bwana Mengi asipeleke vielelezo vyake wizarani. HAKUNA MANTIKI yeyote ya kufanya hivyo. Hata akiletewa barua (kichekesho: barua inafuata tangazo!!!!), aijibu barua hiyo kwa kumwambia waziri apeleke suala hili mahakamani na yeye (Mengi) atoe vielelezo vyake mahakamani kama mshtakiwa.

Binafsi, nalichukulia tangazo la Masha kama la kitoto. Halipaswi kutolewa na waziri kwa namna alivyoitoa. Masha anaiaibisha serikali, wizara na taaluma yake ya sheria.
 
Ni vizuri kabisa kuona una nia njema na msimamo thabiti. Watu wa aina hiyo ni endangered species kwenye jamii zetu.

Ila tu nikukumbushe kwamba kuwa na msimamo thabiti tu pengine haitoshi; kujitahidi kuwa na msimamo thabiti na sahihi ndio ishara ya hekima. Na hii inakuwa rahisi unapoweza kuwa mpole, msikivu, na kukubali kusahihishwa pale ambapo makosa madogo madogo yapo wazi; sisi sio miungu, twakosea.


Kuwa objective haimaanishi kuweza kuswitch side mbili zinazokinzana from time to time.

Kuwa objective nadhani ni kuangalia facts zilizopo nu ku-draw logical conclusion kwa usahihi. Na kikwazo hapo mara nyingi ni hisia kumtawala mtu kupitiliza. La sivyo inakuwa si majadiliano ila ushabiki.

Kitu ambacho ninakimiss sanau humu ndani ni watu kutofautisha imani na mambo ya kweli. Kila mtu anauhuru wa kuamini anachotaka kuamini, tatizo ni pale mtua anapoichukulia imani yake kwamba ndio ukweli na kutaka wengine nao waichukulie kama ndio ukweli, la sivyo ni vita.

Kwa mfano, kusema kwamba "kwamba Mengi this time anahitaji kutihibitiwa kisheria maana now he is going out of the line na sheria za jamhuri" unaonyesha wewe unaamini nini kwenye hili. Ambayo its ok, na unajua mwenyewe sababu zilizokufanya uamini hivyo, na una haki kabisa ya kuamini unachoamini. Ila unapoiweka kwenye public domain, wengine watapenda kujua umefikiaje hitimisho hilo ili wachague kuamini unachoamini ama la. Sasa usiwe mkali wanapokuuliza maswali kama "anaenda out of line na sheria ipi ya jamuhuri?", au "hivi hakuna uwezekano kwamba kuna ka plan kama hako?", "hivi hakuna insidence za wafanyabiashara wanabambikiwa kodi nchi hiii?".

Ukiwa na msimamo na ukauweka kwenye public domain, jua kwamba watu wata-uchallenge. Sasa badala ya kuwa mkali, busara ni kuonyesha mantiki katika kufikia kuamini unachoamini. Kama huwezi, waambie hiyo ni imani yangu tu na naomba msinibugudhi. Na mtu akisema hivyo muheshimu, kaa mbali. Lakini ukisema huo ndio ukweli, kila mtu ana haki ya kuku-challenge. Ukishindwa kuitetea hoja yako, kuwa mpole sema nimechemka.

Tatizo linakuwa pale sasa mtu anapotaka imani yake ndio ichukuliwe kama kweli na kila mtu bila hata sababu za msingi. Tatizo kubwa zaidi ni pale walio kwenye mjadala wana imani na hypothesis tofauti na kila mmoja anataka yake ndio ichukuliwe kama ukweli bila kuhojiwa.



Sadakta.

Ukweli ni ukweli ila imani zetu ndio zinatofautiana. Lengo la mazungumzo kama haya nikujaribu kuangalia imani ipi inakaribiana na ukweli, na pengine tunaweza kuufikia ukweli.

Namecalling inakuja pale mtu anapokuwa na hasira pindi wengine wanapokuwa wagumu kuichukulia imani yake kama ndio ukweli. Na inawezekana ni kwamba tu ameshindwa kuwaonyesha yeye amefikiaje hitimisho fulani, lakini yeye anaichukulia personal.

Mimi nilidhani pia kumtuhumu mtu kwamba anatamani kuwa secretary wa Mengi ndio maana anajaribu kuwa na mawazo tofauti na wewe ni name calling pia. Samahani kama nimekosea. 🙂

You couldn't be clearer! Amen!
 
Mengi jino kwa jino na Masha

Habari Zinazoshabihiana
• Polisi avunjwa jino kwa chupa ya bia 03.08.2007 [Soma]
• Shekhe jino kwa jino na Mchungaji kuhusu Dito 22.03.2007 [Soma]
• Kupanda kwa bei za mafuta:Masha asema Serikali inafanyia kazi mapendekezo 27.05.2006 [Soma]

*Serikali yampa siku saba ajieleze kuhusu kutishwa
*Yeye asema nyingi, amtaka Waziri ampeleke kortini


Na Waandishi Wetu

SERIKALI imempa siku saba Mwenyekiti wa Kampuni za IPP, Bw. Reginald Mengi, kuthibitisha madai yake kwamba kuna waziri kijana katika Serikali ya Rais Jakaya Kikwete amemtishia na kwamba kuna mikakati ya kufilisi biashara zake.

Akizungumza na Kituo cha Televisheni ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC1) na kurushwa jana asubuhi Waziri wa Mambo ya Ndani, Bw. Laurence Masha, alisema madai yaliyotolewa na Bw. Mengi yanaonesha kwamba Serikali haiwalindi vyema raia wake.

Waziri Masha alisema Mwenyekiti huyo anapaswa katika muda huo awe amethibitisha madai hayo, ili Serikali iweze kuangalia taratibu za kuyashughulikia.

Alisema jana angemwandikia rasmi barua ya kumtaka kuthibitisha madai yake ambayo aliyatoa juzi mbele ya vyombo vya habari, Dar es Salaam.

Kabla ya kutolewa agizo hilo jana, Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, lilisema lilikuwa halijapokea taarifa yoyote kutoka kwa Bw. Mengi kuhusu kutishiwa na Waziri na hivyo lisingeweza kuliingilia suala hilo.

Akizungumza na Majira, Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Bw. Evarist Mangala, alisema hadi juzi Desemba 3 hawakuwa na taarifa yoyote ambayo iliripotiwa kuhusu kutishiwa maisha kwa Bw. Mengi na badala yake walizisoma taarifa hizo kwenye vyombo vya habari.

Kuhusu siku saba alizopewa na Bw. Masha kuwasilisha ushahidi wake, Bw. Mengi alisema siku hizo ni nyingi na kumtaka Waziri kumpeleka Mahakamani haraka iwezekanavyo.

"Vitisho ni vingi sana, lakini si kila kitu ninaweza kupeleka taarifa Polisi, hivyo ninaangalia kikubwa ni kipi kinachotisha zaidi ndipo ninatoa taarifa Polisi, lakini iwapo itagundulika kuwa niliudanganya umma kuwa nilitoa taarifa katika kituo cha Polisi wakati sijatoa, niko tayari kwenda jela,

"Lakini pia iwapo itagundulika kuwa Waziri pia ameudanganya umma kuwa sikutoa taarifa Polisi wakati nilitoa, je yuko tayari kujiuzulu wadhifa wake?" alihoji Bw. Mengi.

Kuhusu suala la kumtaja Waziri kijana na msomi aliye katika Wizara nyeti, Bw. Mengi alisema kwa kawaida Mwenyezi Mungu ana nguvu kubwa na za kipekee, hivyo zinaweza kumfanya mtu huyo kujitaja mwenyewe.

"Kwa kawaida Mungu ana nguvu kubwa na za pekee sana, hivyo katika mazingira ya sasa, nguvu hizo zinaweza kumfanya mhusika kujitaja mwenyewe," alisema.

Bw. Mengi alisema ameshindwa kuelewa majukumu ya Waziri Masha katika jambo hili alilosema kupitia TBC1, kwani hajawahi kusikia kama yeye ni Msemaji Mkuu wa Serikali au wa Wizara.

"Kitu nisichokielewa ni majukumu ya Waziri Masha katika suala hili, alikuwa akitoa tamko hilo kama Msemaji Mkuu wa Wizara au Serikali, alikuwa akizungumza kama nani, nauliza hivyo kwani sijui taratibu za Serikali kama yeye ni msemaji wa sehemu hizo.

"Nilizungumzia Waziri kijana wa wizara nyeti, mawaziri vijana wako wengi, yuko Ngeleja (William, 41), Kamala (Deodorus, 40) na yeye Masha (38) hivyo umri wao unashabihiana, sijui atakuwa amezungumza kwa niaba ya vijana wengine ama vipi?," alisisitiza Bw. Mengi.

Bw. Mengi alihoji kuwa iwapo suala la kuripoti Polisi linalomhusu yeye katika Wizara yake ameshindwa kukubaliana nalo, je kuwapo kwa suala la kumfilisi ambalo haliko katika wizara yake, atakuwa tayari kulikubali? Waziri Masha alipoulizwa na waandishi wa habari kuhusu suala la kumpeleka Bw. Mengi mahakamani haraka iwezekanavyo na kumpelekea barua ikimtaka kutoa ushahidi ndani ya siku saba, alisema suala la kumpa siku saba Bw. Mengi si sababu, hivyo angeweza kupeleka ushahidi huo hata jana.

Bw. Masha alisema alishindwa kupeleka barua hiyo jana asubuhi, kutokana na kuwa mkutanoni, hivyo aliahidi mara baada ya kutoka mkutanoni angeipeleka barua hiyo mara moja.

Hata hivyo, hakuweza kutoa ufafanuzi kuhusu suala hilo, kutokana na kuwa mkutanoni na Waziri mwenzake wa Burundi.

Awali vyombo vya habari viliripoti kuwa Bw. Mengi anadai kutishiwa kifo na mtu aliyemtaja kuwa ni Waziri kijana katika Serikali ya Rais Kikwete akihusisha vitisho hivyo na msimamo wake wa kukemea ufisadi.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari ambao ulifanyika juzi, Mengi alidai kuwa amekuwa akitumiwa ujumbe ambao unavituhumu vyombo vyake vya habari kuwa vimekuwa mstari wa mbele katika kukemea ufisadi jambo ambalo 'waziri kijana' kuwa si jambo zuri kwa sababu linawanyanyasa baadhi ya watu.


Na pale pa blue ndio point of interest kwa mimi.............kwingine kwekundu ni ni changamoto katika sakata hili
 
1.
Kuwa objective haimaanishi kuweza kuswitch side mbili zinazokinzana from time to time.

- Kwangu ni black and white, kwenye ishu yoyote ninachagua either black or white, na kuwa objective kunaweza kwua na maana nyingi sana kama unavyosema sio lazima iwe moja tu ya kuto-switch sides.

2.
Kuwa objective nadhani ni kuangalia facts zilizopo nu ku-draw logical conclusion kwa usahihi. Na kikwazo hapo mara nyingi ni hisia kumtawala mtu kupitiliza. La sivyo inakuwa si majadiliano ila ushabiki.

- By who's standards? au usahihi wa nani?

3.
Kitu ambacho ninakimiss sanau humu ndani ni watu kutofautisha imani na mambo ya kweli. Kila mtu anauhuru wa kuamini anachotaka kuamini, tatizo ni pale mtua anapoichukulia imani yake kwamba ndio ukweli na kutaka wengine nao waichukulie kama ndio ukweli, la sivyo ni vita.

- Tatizo hapa sio imani maana sidhani kama kuna dini hapa, ila ni kuchagua side na kujenga hoja, halazimishwi mtu kukubali asiyotaka, lakini na wewe huwezi lazimisha anybody hapa kuwa wako tu ndio ukweli kila hoja huchambuliwa hapa.

4.
Kwa mfano, kusema kwamba "kwamba Mengi this time anahitaji kutihibitiwa kisheria maana now he is going out of the line na sheria za jamhuri" unaonyesha wewe unaamini nini kwenye hili. Ambayo its ok, na unajua mwenyewe sababu zilizokufanya uamini hivyo, na una haki kabisa ya kuamini unachoamini. Ila unapoiweka kwenye public domain, wengine watapenda kujua umefikiaje hitimisho hilo ili wachague kuamini unachoamini ama la.

- Nimetoa sababu zote ni kwa nini ninafikiri kwamba Mengi this time yuko out of the line, ukienda kule utayaona unless kama ueamua kuwa hutaki kuyaona siwezi kukusaidia kwenye hilo.

5.
Sasa usiwe mkali wanapokuuliza maswali kama "anaenda out of line na sheria ipi ya jamuhuri?", au "hivi hakuna uwezekano kwamba kuna ka plan kama hako?", "hivi hakuna insidence za wafanyabiashara wanabambikiwa kodi nchi hiii?".

- Nafikiri ukisoma post zako na zangu ukweli uko wazi nani mwenye hasira na nani asiyekwua nayo, mimi I am having a lot of fun kwa sababu this is me, hasira ni zako na maneno mengi ya kujificha as sasa umebadilika hapana rangi ni ile ile nenda nyuma ukasome tena psot zangu nimeweka kila kitu wazi kwa on my conclusion.

6.
Ukiwa na msimamo na ukauweka kwenye public domain, jua kwamba watu wata-uchallenge. Sasa badala ya kuwa mkali, busara ni kuonyesha mantiki katika kufikia kuamini unachoamini. Kama huwezi, waambie hiyo ni imani yangu tu na naomba msinibugudhi. Na mtu akisema hivyo muheshimu, kaa mbali. Lakini ukisema huo ndio ukweli, kila mtu ana haki ya kuku-challenge. Ukishindwa kuitetea hoja yako, kuwa mpole sema nimechemka.

- Nonesense!, Mengi amesema na Waziri amesema nimechagua side ya waziri na sababu nimesema, hayo ya kuchemka na the rest of the story ni pure nonesense kwangu kwa sababu either uko upande wa Mengi au wa Waziri, weka hoja hapa tuchambue I am not interested na sykologia maana ni waste of people's time hapa!

7.
Tatizo linakuwa pale sasa mtu anapotaka imani yake ndio ichukuliwe kama kweli na kila mtu bila hata sababu za msingi. Tatizo kubwa zaidi ni pale walio kwenye mjadala wana imani na hypothesis tofauti na kila mmoja anataka yake ndio ichukuliwe kama ukweli bila kuhojiwa.

- Hapana tatizo hapa ni wewe ambaye huna hoja ya msingi badala yake unaleta sykologia, tunachotaka hapa ni hoja zako na msimamo wako kuhusu the ishu ya Mengi na Waziri, hayo mengine ni waste of time, na hakuna unayeweza kumdanganya na haya maneno yako mengi, mimi simo kabisaaa!

7.
Sadakta.Ukweli ni ukweli ila imani zetu ndio zinatofautiana. Lengo la mazungumzo kama haya nikujaribu kuangalia imani ipi inakaribiana na ukweli, na pengine tunaweza kuufikia ukweli.

- Again hakuna ishu ya imani hapa kuna hoja za kuhusu the ishu, the ishu sio ukweli wala uongo, the ishu unasimamia upande upi na hoja ziko wapi! ya ukweli na imani hayapo!

8.
Namecalling inakuja pale mtu anapokuwa na hasira pindi wengine wanapokuwa wagumu kuichukulia imani yake kama ndio ukweli. Na inawezekana ni kwamba tu ameshindwa kuwaonyesha yeye amefikiaje hitimisho fulani, lakini yeye anaichukulia personal.

- Name calling ni dalili za kushindwa hoja period!

9.
Mimi nilidhani pia kumtuhumu mtu kwamba anatamani kuwa secretary wa Mengi ndio maana anajaribu kuwa na mawazo tofauti na wewe ni name calling pia. Samahani kama nimekosea. 🙂

- Great manipulations lakini hukubadili anything, jamaa ameniita secretary kwa msimamo wangu asioutaka na mimi nimemrudishia, end of the story,

Now back to the ishu, can we talk the ishu now yaani Mengi Vs Waziri!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom