- Kama nilivyosema jana, kwenye hili Mengi ameenda nje ya mstari hawezi kuanzisha serikali yake ndani ya serikali ya jamhuri, ameanzisha mwenyewe wakati kuna njia nchungu nzima angeweza kuzitumia kutatuta tatizo lake, mara mashehe mara waziri kesho itakua rais, it has to be stopped tena now.
- Taifa tunaongozwa na sheria, sio uhuni uhuni wa kukusanya habari za walevi mitaani na kuzigeuza dhana za kutishia walevi, mimi sinyiwi pombe na nina marafiki 75% wanaolewa kila siku, sasa nikijali maneno yao ya ulevi sitakua na rafiki hata mmoja. Kwenye kesi yake against Manji nilikuwa mmoja wa waliomtetea sana Mengi kwa wahusika wa uamuaji ile kesi kuwa anaonewa lakini not this time, kwa sababu this one yuko nje ya mstari tena out na ninaunga mkono kwa 100% any response kwa wale wote aliohusika na kuwarecord au kuwapiga video na picha wakiwa kwenye ulevi, kama ndio sababu ya claims zake against viongozi wa serikali.
- Priviledge ya kumiliki media au kuwa na uwezo wa kuandika kwenye vyombo vya habari ikiwa ni pamoja na magazeti na mitandao haiwezi kuwa sababu ya wale wenye hizo access kuchafua majina ya wengine kuwa ni mafisadi na the rest of the story bila sababu wala ushahidi, hapa ndipo tunapomheshimu sana Dr. Slaaa, kwa kuweka mambo yote ya ufisadi kwa kalamu na ushahidi usiopingika.
- Masha hana sababu ya kujiuzulu kwa kusimamia kiapo chake kwa jamhuri, yaani kulilinda taifa kwa njia zote zilizopo chini ya uwezo wake kisheria, ni wajibu wa waziri wa ndani kuhakikisha kua wananchi hawabughudhiwi na viongozi au wananchi wengine, na wale wanaobughudhiwa ni wajibu wao kufikisha matatizo yao kwenye vyombo vya dola kwa ufumbuzi wa kisheria iwapo wanao ushahidi wa kisheria, kama sheria yetu inavyosema. Sasa anapotokea mwananchi yoyote mwenye kuamua kwenda kinyume na sheria zetu, regardless ya who he is serikali ni lazima isiamie sheria tena kwa nguvu zote ilizonazo.
- Ninarudia tena kwamba ni wajibu wa waziri wa ndani kusimamia mambo ya ndani bila ya kujali ni waziri gani anayetajwa au asiyetajwa, Mengi ni lazima afikishwe kwenye sheria na atoe ushahidi wake uliopatikana kisheria ili kuiridhisha sheria ya jamhuri, ambayo waziri wa sasa wa ndani amekula kiapo kuilinda kwa nguvu zake zote na uwezo wake wote. Tunaishi kwa kuongozwa na sheria sio uhuni uhuni wa kukurupuka kwenye public na tuhuma nzito kwa viongozi wetu wa juu kwenye media, ni kujaribu kuwatisha ili wasifanye kazi zao walizopewa na na sisi wananchi kwa mujibu wa sheria. Hata US sheria iko wazi kuwa ukilia moto kwenye sehemu kama ya cinema wakati moto hakuna, unachukuliwa hatua za kisheria tena kali sana, sasa hapa ni wajibu wa serikali yetu ya jamhuri ikiongozwa na waziri wa ndani ambaye ndiye kisheria mhusika mkuu kuhakikisha kuwa Mengi anapewa haki yake so is waziri aliyetajwa pia akipewa haki yake na pia kutulinda sisi wananchi wengine wa kawaida na viongozi in the future na this kind of Mengi's accusations, hakuna anayekataa haki za Mengi kulindwa na sheria, lakini ni lazima huheshimu sheria za jamhuri na utaratibu wetu wa kisheria.
- Ninamuunga mkono kwa 100% kitendo cha waziri wa ndani kumpa Mengi muda wa kutoa ushahidi wake kwa serikali, na pia kumpa waziri anayehusishwa nafasi ya kusema pia mbele ya sheria, na sheria iamue nani mwenye makosa kisheria na nani hana, lakini the important ishu ni kuhakikisha kua next time Mengi anakwenda kwenye vyombo vya sheria bdala ya media, hawezi kusema kua haviamini kwani vimewahi kumpa nafasi ya kujitetea na akashinda kesi, tena against waziri wa jamhuri, ni lazima Mengi ajifunze kupeleka malalamiko yake kwenye sheria, kama sheria inavyotaka.
- Wote sisi ni wananchi wa Tanzania, na hili taifa ni letu sasa tusitishane na hizi tabia mpya za kujifanya wanamapinduzi, kwa kutaka kulazimisha kwa nguvu hoja za kuwaita walioko kwenye power tuliowachagua kisheria kuwa ni mafisadi just because hatuwataki au tuna chuki zetu za binafsi, dawa ni kudai tu kwa nguvu kuwa ni mafisadi kwa sababu ni wimbo unaokubalika kirahisi na wananchi bila hata ushahidi ulio wazi, hili sio taifa la walevi au wajinga wajinga, tunazo sheria na ni lazima zitekelezwe kwa nguvu zote.
Hatuwapendi mafisadi, lakini ni lazima kuwa na ukweli juu ya uifisadi wao, na ni wajibu wa waziri wa jamhuri kulinda sheria, bila kujali kama ni Mengi au anybody.
Mungu Aibariki Tanzania.