Mengi Vs Masha tuhuma, vitisho na matokeo!

Mengi Vs Masha tuhuma, vitisho na matokeo!

Status
Not open for further replies.
Mkuu hapa unamanisha kwamba Masha (the learned friend) 'kakurupuka' kuitetea serikali na ni ishara kwamba anajitetea mwenyewe?

absolutely:

a. Aliyetuhumiwa kutoa vitisho ni "Waziri"

b. Anayetoa siku saba kutolewa ushahidi ni "Waziri"

c. Sasa itakuwaje kama "Waziri" aliyetuhumiwa ndiyo "Waziri" aliyetoa siku saba?

d. Kwa yeye kutoa siku saba amejitangaza kuwa yeye siyo "Waziri" aliyetuhumiwa kwani mzee Mengi ataweza tena kusema kuwa "Waziri" aliyemnua ni Masha bila kuonekana analipiza kisasi?

e. Msemaji wa haki ambaye alitakiwa kutoa wito kwa Mengi ni adha Mwanasheria Mkuu, IGP, au DPP au hata RPC

f. Masha ametoa maelekezo ya wapi Mengi aende kutoa taarifa kwenye kituo gani cha Polisi

g. Masha ndiye WAziri mwenye dhamana ya Jeshi la Polisi na asikuambie mtu ana madaraka makubwa sana ya uendeshaji wa jeshi hilo hata kutoa maagizo kwa niaba ya Rais.

h. Mengi akienda kutoa taarifa kwenye hicho kitua na Masha akiwa Waziri akaagiza kuwa "Taarifa hizo nataka nipatiwe mara moja ili tumshughulikie Waziri huyo au niweze kumpatia taarifa Rais" itakuwaje?

I. Kwa kujitokeza hadharani na kudai ushahidi wa kutaka "Waziri" atajwe, Masha ameingilia kati kupatikana kwa haki na haiwezekani kamwe Mengi kutendewa haki.

Ndio maana nimeandika mojawapo ya tahariri kali nilizowahi kuandika, hawa watu wasichezee madaraka wakifikiri wao ni miungu watu!
 
ukweli ni kuwa, kauli kama hiyo ilipaswa kutolewa na IGP, DCI na pengine Kamanda kova!
 
-- whistling -- kitu cha kwanza Masha ajiuzulu Uwaziri kwanza just to make it a fair game.


Ajiuzuru ili iweje?

Ajiuzuru kwa kosa gani?

Tukiendeleza mambo ya nama hii basi tunaweza fika mahali nchi ikawa naongozwa kwa uoga ,mtu anaogopa kufanya jambo sababu tu linaweza kumfanya ashurutishwe kujiuzuru!

 
It's a big mistake for Mr Masha to come up illogically that early! This has no any other interpretation than FOOLISH SHOWDOWN! Hakuna busara yoyote iliyoonyeshwa na Masha ukilinganisha elimu yake na wadhifa wake. His emotional posture ilikuwa inamsuta machoni pake wakati anaelezea mambo ya Mengi TBC1 leo asbh. He was unnecessarilly too emotional when explaining his stance on the said issue.

Kuhusu elimu yake, natilia shaka uelewa wake wa philosophy of law (Jurisprudence). Kama alifaulu, in which case najua alifaulu kidogo lakini ni kuwa alikariri tu. Kamwe hutamuona mwanafalsafa yeyote akikurupuka kama alivyo jihusisha na kujibu tuhuma za Mengi.

By implication (other things being equal) hii inaonyesha kuwa yeye ndiye aliyetuhumiwa na Mengi. SHAME ON HIM. He is not the state. Hata kesho asubuhi anaweza kuwa derailed na wizara ikaendelea tu!

Na hii ndio psychology of money and power kwa WATOTO! Wakipata vijisenti kiasi fulani na wakijua BABA nawapenda huwa inakuwa taabu kwelikweli! Hata shuleni hapakaliki.

By the way, ni kwanini aende TBC1 mapema kiasi hicho kutoa vitisho, HANA SUBIRA HATA CHEMBE. Na hii inaonyesha jinsi hafai kuwa kiongozi.

NATABIRI, Masha will be derailed soon!
 
...hivi kuna sababu gani Waziri mzima kukurupuka na kuanza kutoa siku saba,hajapelekewa barua yeyote au malalamiko rasmi ni kaskia tuu kama sisi humu JF,kama mengi ana issue legit kuna utaratibu wa kufanya na alichofanya ni kama street talk tuu ambacho waziri hana sababu hata ya kujibu...Masha intergrity ni sifuri kazidi umalaya tuu na kutafuta ujiko kwa machangudoa,wizara yake ni kero kubwa kwa wananchi kuanzia uhamiaji mpaka polisi wa barabarani na kashindwa hata kuwalinda Albino...disgraceful masha must go na utatoka tuu!
 
Mengi naye si angetaja ilo jina la huyo waziri au ndio mambo ya kuviziana kama kwenye chess?
 
Ajiuzuru ili iweje?

Ajiuzuru kwa kosa gani?

Tukiendeleza mambo ya nama hii basi tunaweza fika mahali nchi ikawa naongozwa kwa uoga ,mtu anaogopa kufanya jambo sababu tu linaweza kumfanya ashurutishwe kujiuzuru!


soma tahariri yangu. Kama nchi itaongozwa kwa watu kujiuzulu na iwe hivyo, kwani sasa inaongozwa kwa kufuru! kila mwenye madaraka anataka kuwa muamuru uzima na uhai! Ajiuzulu ili iwe na haki.
 
Naona wengine wanakuwa wastaarbu sana hivyo wanajizuia kukurupuka; ngoja mimi nikurupuke kuwa Masha kakurupuka.
 
Mengi naye si angetaja ilo jina la huyo waziri au ndio mambo ya kuviziana kama kwenye chess?

Mwanakijiji si alishamtaja Masha ..?Naona Masha kaamua kujibu sasa!

I love this Game
 
Lawrence Kego Masha



Partner
Admitted to the Bar, 1996.

Practice Areas:

Natural Resource Law; Banking & Finance; Privatization; Corporate Restructuring; Securities; Conveyancing.

Brief biography:

Born in Sengerema , Tanzania , March 11, 1970.

Education:

University of Dar es Salaam (LL.B., Hons., 1991);
Georgetown University (LL.M., 1993).


Work experience:

State Attorney, 1991;
Company Secretary and Managing Director, Tanzania Oxygen Limited, 1996-1997;
Council Member, Dar Es Salaam Stock Exchange.

Member:

Tanganyika Law Society
East African Law Society

Languages:

English and Swahili.

Email: masha@immma.co.tz

(NB: Mr. Masha is currently on sabbatical leave following his appointment as Deputy Minister in Tanzania’s Fourth Phase Government. Mr. Masha, who was initially appointed Deputy Minister of Energy and Minerals, is currently the Deputy Minister of Home Affairs in the Government of the United Republic of Tanzania

Masha kazaliwa 1970 na kamaliza LLB (UD) 1991...ina maana aliingia UD akiwa 17 yrs old?
 
Behind every irresponsible act, there is an illogical push from either within or without driven by a sense of desperation. Behind the scene, Et tu Brutus ?
 
Mi nadhani, kwa sababu Mengi alimtuhumu waziri (kwa kutaja cheo cha uwaziri wa Serikali ya Tz) basi anakuwa ameituhumu serikali. Kwa hiyo Masha hapa anafanya kazi ya kuitetea Serikali hata kama aliyetuhumiwa si yeye......japo pia naona kwa upande wa pili aliyepaswa kuliongolea ni hili ni yule waziri aliyesuswa na media.
Sidhani kwa kutaja kuwa waziri kijana kamwandikia ujumbe wa vitisho ni kuituhumu serikali nzima. Hayo ni mambo ya huyo waziri binafsi maana katika majukumu yake ya kazi hakuna kipengele kinachomtaka kuandika ujumbe wa vitisho kwa Mwananchi yeyote. Ndio maana tunasema kama Masha kafanya hivyo ajitoe kabisa katika madaraka aliyopewa maana yamemzidi kimo.
 
Amejua baada ya wewe kusema hapa jana.

sasa katika umakini wake timamu akaamua kwenda kusema Mengi amtaje Waziri huyo wakati akijua ni yeye mwenyewe au kwamba yeye ametajwa kwenye JF kuwa ndiye aliyekusudiwa? Inanifanya nihoji kama ningeenda shule ningekuwa na faida ya aina fulani..
 
Hebu msome kwa kutulizana, ama sivyo nyie ndio mnakuwa (as you like to put it) "wakurupukaji"

Mleta habari hapo juu amesema, "Nimesikia TBC leo asubuhi kwamba Mh. Masha kama Waziri wa Mambo ya Ndani amempa siku saba Mr Mengi athibitishe kauli alizo toa . Kazi imeanza."

Keyword, kama waziri wa mambo ya ndani....Hivyo, kutokana na habari hapo juu, Masha hajasema kuwa Mengi athibitishe maneno yale yametoka kwake.

Ama la, labda habari haijakuwa quoted kama ilivyokuwa reported. Slow your roles!

Nadhani hakuna mtu mwenye mamlaka ya kumlazimisha mtu kuthibitisha au kutoa mashitaka mahali popote (hasa kama yeye mwenyewe hajaamua kufanya hivyo). Kama niko sahihi, sioni ni kwanini Mheshimiwa Waziri ampe Mfanyabiashara, Mtanzania huru, siku zozote za kuthibitisha chochote. Ila nadhani kuna uvujaji ambao haukutegemewa uliojitokeza kuhusu suala hili, na anaetafutwa ni alievujisha. Niko tayari kusahihishwa.
 
Inanikumbusha sakata la Mengi na waziri Masilingi miaka ya awamu ya III kuhusu uuzwaji wa Kilimanjaro Hotel, sijui iliishaje.

Nadhani JK ana kazi kubwa sana kwa baraza hili la Mawaziri, wengi naamini hawana uwezo na busara katika maamuzi yao naona kama wanakurupukaga tu. Namhurumia JK, Mungu amsaidie.
 
si unaona mtu alivyofanywa check mate!? Masha amejuaje kuwa yeye siyo huyoo "Waziri"?

Ila hapa patamu...akimtaja huyo "Waziri" kuwa ni Masha, naye[Masha] anaweza kuspin na kusema analipiza kisasi kwa sababu alimpa siku saba.

Haya yetu macho.
 
Mwanakijiji si alishamtaja Masha ..?Naona Masha kaamua kujibu sasa!

I love this Game

sasa ananijibu mimi kwa kumtaka Mengi atoe ushahidi? Namba yangu si ipo wazi angenipigia kuniuliza.. but now too late!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom