- Kama nilivyosema jana, kwenye hili Mengi ameenda nje ya mstari hawezi kuanzisha serikali yake ndani ya serikali ya jamhuri, ameanzisha mwenyewe wakati kuna njia nchungu nzima angeweza kuzitumia kutatuta tatizo lake, mara mashehe mara waziri kesho itakua rais, it has to be stopped tena now.
- Taifa tunaongozwa na sheria, sio uhuni uhuni wa kukusanya habari za walevi mitaani na kuzigeuza dhana za kutishia walevi, mimi sinyiwi pombe na nina marafiki 75% wanaolewa kila siku, sasa nikijali maneno yao ya ulevi sitakua na rafiki hata mmoja. Kwenye kesi yake against Manji nilikuwa mmoja wa waliomtetea sana Mengi kwa wahusika wa uamuaji ile kesi kuwa anaonewa lakini not this time, kwa sababu this one yuko nje ya mstari tena out na ninaunga mkono kwa 100% any response kwa wale wote aliohusika na kuwarecord au kuwapiga video na picha wakiwa kwenye ulevi, kama ndio sababu ya claims zake against viongozi wa serikali.
Sasa na wewe ukiambiwa uthibitishe kwamba huyu mzee hana ushahidi itakuwaje? au ukiambiwa useme walevi gani ndio walimpelekea hiyo taarifa, si utapata hasira tu zaidi?
- Priviledge ya kumiliki media au kuwa na uwezo wa kuandika kwenye vyombo vya habari ikiwa ni pamoja na magazeti na mitandao haiwezi kuwa sababu ya wale wenye hizo access kuchafua majina ya wengine kuwa ni mafisadi na the rest of the story bila sababu wala ushahidi, hapa ndipo tunapomheshimu sana Dr. Slaaa, kwa kuweka mambo yote ya ufisadi kwa kalamu na ushahidi usiopingika.
Ukiambiwa uthibitishe? Wanaoshutumiwa hawaongei, maana kama wangekuwa wanajua kwamba hakuna ushahidi wangeviwajibisha hivyo vyombo faster fatser yani.
- Masha hana sababu ya kujiuzulu kwa kusimamia kiapo chake kwa jamhuri, yaani kulilinda taifa kwa njia zote zilizopo chini ya uwezo wake kisheria, ni wajibu wa waziri wa ndani kuhakikisha kua wananchi hawabughudhiwi na viongozi au wananchi wengine, na wale wanaobughudhiwa ni wajibu wao kufikisha matatizo yao kwenye vyombo vya dola kwa ufumbuzi wa kisheria iwapo wanao ushahidi wa kisheria, kama sheria yetu inavyosema. Sasa anapotokea mwananchi yoyote mwenye kuamua kwenda kinyume na sheria zetu, regardless ya who he is serikali ni lazima isiamie sheria tena kwa nguvu zote ilizonazo.
Ooho! Sasa mchezo ndio umeanza wewe ushakuwa jaji. Kama unataarifa za ziada, ungesaidia kutuelimisha. Lakini nadhani mchezo ndio umeanza, na kwa information zilizopo hatujui kwa hakika kama analinda taifa au anajilinda yeye mwenyewe.
Kwani angekaa kimya tu, hiyo taarifa ya Mengi ingekuwa na hatari gani kwa taifa kiasi kwamba lihitaji kulindwa (namaanisha taifa sio serkali, tafadhali)? Maana tunavyojua ni kwamba anasema amemsamehe, na maana yake ni kwamba kwa upande wake yamekwisha.
- Ninamuunga mkono kwa 100% kitendo cha waziri wa ndani kumpa Mengi muda wa kutoa ushahidi wake kwa serikali, na pia kumpa waziri anayehusishwa nafasi ya kusema pia mbele ya sheria, na sheria iamue nani mwenye makosa kisheria na nani hana,
Plus Plus, very objective,
lakini the important ishu ni kuhakikisha kua next time Mengi anakwenda kwenye vyombo vya sheria bdala ya media, hawezi kusema kua haviamini kwani vimewahi kumpa nafasi ya kujitetea na akashinda kesi, tena against waziri wa jamhuri, ni lazima Mengi ajifunze kupeleka malalamiko yake kwenye sheria, kama sheria inavyotaka.
Oohoo ... objectivity ni chachuu ya kutafuta ukweli ...
Lakini anahaki ya kuamua kama anaenda kwenye vyombo vya sheria ama la. Mbona wewe huwa unaleta malalamiko yako huku badala ya kupeleka kwenye vyombo vya sheria? Mbona husemi kwamba Masha angeenda mahakamni badala ya kutoa siku saba kwenye TV?
Sina tatizo na opinion zako baba, bias yako inakuwa wazi mno.
- Wote sisi ni wananchi wa Tanzania, na hili taifa ni letu sasa tusitishane na hizi tabia mpya za kujifanya wanamapinduzi, kwa kutaka kulazimisha kwa nguvu hoja za kuwaita walioko kwenye power tuliowachagua kisheria kuwa ni mafisadi just because hatuwataki au tuna chuki zetu za binafsi, dawa ni kudai tu kwa nguvu kuwa ni mafisadi kwa sababu ni wimbo unaokubalika kirahisi na wananchi bila hata ushahidi ulio wazi, hili sio taifa la walevi au wajinga wajinga, tunazo sheria na ni lazima zitekelezwe kwa nguvu zote.
Mzee nadhani wapo wanaowaita viongozi waliopo madarakani ni mafisadi, na data wanzo, na wameshare na sisi. Sasa ungesaidia katika harakati za kuwaprove wrong ungekuwa unafanya la maana zaidi.
Ukiambiwa uthibitishe kwamba sababu inakuwa ni chuki binafsi tu, utaweza? au utapata hasira zaidi tu?
Hatuwapendi mafisadi, lakini ni lazima kuwa na ukweli juu ya uifisadi wao, na ni wajibu wa waziri wa jamhuri kulinda sheria, bila kujali kama ni Mengi au anybody.
Mungu Aibariki Tanzania.
Hapo umenena vizuri, kwamba ni vizuri kuwa na ukweli. Sasa ingekuwa vizuri badala ya kulalama kwamba watu wanawasingizia wengine, ungejaribu kuonyesha kwamba either hawana uthibitisho au uthibitisho uliotoka haujitoshelezi.
Kwa swala hili, Kama una information ambazo wengine hatuna, labda hutusaidie. Lakini nadhani wengi wetu tunachokijua ni kile tunachokisikia kutoka kwa hawa mabwana. Hatujui kama hilo tishio lilitokea kweli ama la. Na kama lilitokea, hatujua kama mzee ana uthibitisho ama la. Hatujui kama waziri anatumia njia zozote kulinda taifa, ama kujilinda mwenyewe. Sasa kutumia bias yako na kuwa hakimu na ku-draw conclusion nadhani ni missues ya bytes za site; only my opinion.
Hii ni vita kati ya watu wawili, na ukweli ni kwamba kila mmoja atajaribu kutumia resourse zote zinazoweza kutmika kushinda vita. Huyu atatumia media zake, huyu atatumia wadhifa wake. Hapa labda tungejaribu kuwa objective kidogo na kutafakari yaliyo mbele yetu. Kutuonyesha side yako kwa hasira hivyo is ok, kwa sababu ya free speech and all.
Lakini na wewe pengine kutumia right yako ya free speech hapa kufanya yale yale unayowashutumu wengine kufanya, nadhani ni aina flani ya unafiki. Jinsi ambavyo unasema mzee anatumia media zake kwenye hili, na jinsi ambavyo wengine wanasema waziri anatumia madaraka yake kwenye hili, ni aina ya kitu ulichokifanya kwenye sehemu kubwa ya post yako ...
Heshima mbele