Mbowe na tafakuri zake...

Mbowe na tafakuri zake...

Mzee Mwanakijiji

I quite don't understand why a member of JF should have to go through your radio to respond to his fellow members.

that is a very narrow way of looking at things! Mbowe akizungumza nami siyo kwa vile ni mwanaJF bali kiongozi wa kisiasa. Hata bila ya maswali ya watu humu I'd still talk to him about other political issues zinazohusu Tanzania na chama chake cha CHADEMA. Kuzungumza kwangu na Mbowe hakutegemi uanachama wake JF.
 
that is a very narrow way of looking at things! Mbowe akizungumza nami siyo kwa vile ni mwanaJF bali kiongozi wa kisiasa. Hata bila ya maswali ya watu humu I'd still talk to him about other political issues zinazohusu Tanzania na chama chake cha CHADEMA. Kuzungumza kwangu na Mbowe hakutegemi uanachama wake JF.
Ninavyofikiri mimi kuna Mwanachama humu anaitwa Lunyungu Alimuomba mwanakiji kama kuna uwezekano wa kumpata Mbowe Ili ajibu Baadhi ya Maswali watu wengi wamekuwa wakijiuliza humu Lakini Huyu Mheshimiwa hakuweza kurudi,Nafikiri kwa kuliona hili MKJJ amekubali ombi na akaenda zaidi ya hapo kwa kuomba wenye maswali wapeleke..............................Sasa nini tena kimejiri baada ya hapo Sina uhakika!
 
Nakuunga mkono Lunyungu na Mnyika kwamba wengi humu watu wa domo hata kusimama watetee kitu hawawezi wanalia na wapinzani tu kwamba mbona hwafanyi hili ama lile . Kwani Nchi ni ya wapinzani pekee ?Nini nafasi yako wewe Mtanzanai wa JF unayepiga makelele na kutaka kutanguliza wenzio?Neno moja kuwa hapa tuingie kwenye siasa moja kwa moja tushiriki kuleta mabadiliko . CCM hawakosi usingizi kwa JF kwa kuwe wengi mko Ulaya mnaongea huko mnaangalia maisha yenu.Wao wanajua watu we madhara zaidi ambao wanaweza kuwamaliza ni wale washinda hoi wa Tunduru walio uza shahada kwa vitisho na 5000 baadaye wamerudishiwa kadi baada ya kupaya Mbunge wao .Hata karatasi za kujiandikisha hapa wengi wenu wana JF hamna lakini mnachonga sana wakati mnaishia kulala kwenye majumba ya wazungu na mnaogopa hata kurudi hapa Kariakoo tupambane . Wacheni zenu na Chadema acheni kupoteza muda hapa nendeni vijijini mkajenge chama hawa ni domo tu hawana lolote .Stress za mikazi ya wazungu zinawapa shida sana na chuki mbele .
 
Hata karatasi za kujiandikisha hapa wengi wenu wana JF hamna lakini mnachonga sana wakati mnaishia kulala kwenye majumba ya wazungu na mnaogopa hata kurudi hapa Kariakoo tupambane . Wacheni zenu na Chadema acheni kupoteza muda hapa nendeni vijijini mkajenge chama hawa ni domo tu hawana lolote .Stress za mikazi ya wazungu zinawapa shida sana na chuki mbele .

Murangira...
You can't be serious.
 
Revol I echo Murangira and I am serious kwamba leo tukianza kujua nani yuko wapi ama tupewe uhuru wa kumtaja kila mmoja kw ajina na aliko mimi nawajua watu 18 hapa JF wote wako US na Ulaya lakini wanachonga sana .Wacheche wako kona zingine za Dunia .Ni kweli hawana karatasi za kupigia kura ama kadi zile za kupata access na kura .

Mimi ndiye niliomba Mzee MKJJ amhoji Mbowe ili kuondoa utata . Mbowe siamini kama anaweza kukataa .Kuandika ingalikuwa yale yale maana leo mnasema ni Ansbert anamwandikia Course work sijui huwa mpo ama ni assumption zenu watu wa mawazo mafupi na wachunguza maisha ya watu .

Mzee MKJJ kama unaweza tafadhali tuletee mahojiano na mjenga sera Mbowe .Upinzani wote una nguvu na sera zale ndizo JK kachukua sasa anazitumia maana sera halisi za CCM ni jiwe hazibebeki hata Mkapa alisha sema .
 
Mzee ES umeuliza maswali matatu ya msingi sana. Japokuwa wewe mwenzangu wewe ni kada wa CCM, naamini umeuliza maswali haya kwa nia ya kutaka ufafanuzi kufuatana na majibu yangu niliyotoa huku nyuma kwa nia njema. Nami ninajibu kwa nia hiyohiyo bila kutia spinning!

1) Umeuliza kuwa kwa kuwa wafadhili wakubwa wa CHADEMA yaani Freeman Mbowe, Edwin Mtei na Ndesamburo wote wanatoka kabila moja, wachaga, sioni kwamba hii inathibitisha hisia kwamba hiki ni chama cha kabila moja?

Jibu langu: Huwezi kuzuia watu kufikiria wanavyotaka kufikiria. Lakini sioni kama ni sahihi kufikia uamuzi kwamba hiki ni chama cha ukabila kwa kuwa tu wafadhili mojawapo wanatoka kabila moja! Mantiki ya kawaida haiendi hivi. Lakini labda tuache mambo ya hisia. Tujadili mambo ambayo yameletekeza hizi hisia. Hisia za ukanilia kwa CHADEMA zipo hata kabla ya wewe kujua kuwa hao jamaa watatu hapo juu ni baadhi ya wafadhili wa CHADEMA. Hizi hisia zimetokana na ukweli kwamba CHADEMA ilipoanza ilikuwa na ufuasi mkubwa zaidi kaskazini na hasa katika mkoa wa Kilimanjaro. Ni ukweli pia kwamba CHADEMA ilipoanza wengi wa viongozi wake walitoka katika mkoa wa Kilimanjaro kuliko mikoa mingine. Naamini hali sasa hivi ni tofauti. CHADEMA sasa ina uwakilishi katika sehemu mbalimbali za nchi yetu.

Labda ni muhimu kueleza ni kwa nini hali ilikuwa kama ilivyokuwa. Kwanza, nafikri wote tunakubaliana kuwa kuanzisha chama cha siasa ni hiari ya mtu. Kujiunga na chama pia ni hairi ya mtu kwa sababu zake zake mwenyewe, zenye maslahi ya kijamii au yake binafsi. CHADEMA ilianzishwa na Mzee Mtei ambaye ni mchaga kwa hiari yake. Walioamua kuwa wanachama wa CHADEMA wa mwanzo waliamua hivyo kwa hiari yao wenyewe. Ni bahati nzuri kwamba Mzee Mtei alianza kukubalika kwao, kwa hivyo wengi wa wananchi wa mwanzo waliojiunga na CHADEMA walitoka katika mkoa wa Kilimanjaro, tena wachaga wakiwemo akina Ndesamburo na Freeman Mbowe. Lakini ni ukweli pia kwamba walikuwepo wananchi wengine kutoka mikoa mingine kama akina Bob Makani na Zitto Kabwe. Ni bahati nzuri pia kuwa wanachama waliojitolea kuichangia CHADEMA walikuwa ni baadhi ya marafiki zake Mtei wakiwemo hao uliowataja. Sasa swala la kuchangia chama ni la hiari. Duniani nzima ingemshangaa Mtei kukataa ufadhili wa akina Ndesamburo eti kwa sababu tu hawa ni wachaga wenzake, ebo!

Katika uhai wa miaka yake 15, chadema sasa imesambaa katika mikoa mbalimbali Tanzania. Ndio hivyo sasa nasi unatuona tunaotokea katika kona ingine kabisa ya Tanzania. Kwa hivyo hisia kuwa chadema ni chama cha ukabila zinabaki kuwa hisia. Nakubali kuwa viongozi wa CHADEMA na sisi wanachama wa kawaida tunawajibu wa kuthibitisha kuwa haya madai sio ya kweli, ni hisia tu!

2) Swali: Umeuliza kama uamuzi wa kutumia helikopta ulikuwa ni maamuzi ya Kamati Kuu: Kwa kadri nijuavyo, jibu ni ndio. Kwa jinsi ninavyoijua Kamati Kuu ya CHADEMA yenye wajumbe kama Profesa Baregu, anagefanya maamuzi yake mwenyewe, Mbowe angekuwa katika wakati mgumu, na pengine historia ya CHADEMA sasa ingekuwa tofauti.
Kuhusu malalamiko ya wagombea ubunge, lazima tukumbuke kuwa ni jambo la kawaida kwa maamuzi mazito katika siasa kuzua malalamiko kutoka kwa baadhi ya wanachama. Sasa uamuzi wa kutumia helikopta ilikuwa ni uamuzi mzito kuwahi kuchukuliwa na CHADEMA na ilitarajiwa ungezua malalamiko kutoka ndani na nje ya CHADEMA kama tulivyoshuhudia. Lakini haina maana kuwa maamuzi yanayolalamikiwa sio mazuri. Na hili halijaanza katika CHADEMA. Hapa nilipo nashuhudia kila jinsi ambavyo Tony Blair na Labour wanafanya maamuzi yanayozua malalamiko hata ndani ya baraza lake la mawaziri. Lakini ndio matunda ya demokrasia. Pengine tofauti ya CHADEMA na CCM katika hili ni kuwa nyie katika CCM mmefundishwa kulalamika ndani kwa ndani, yaani kufa kibudu kwa kisingizio cha msimamo wa chama. Ndio maana wabunge wenu walishindwa hata kuhoji mambo mazito kama Richmond, rada, lakini inajulikana jinsi walivyokuwa wakitukana kule kwenye kuchoma nyama pale kwenye mnada wa Dodoma! Msimamo wa chama! Sisi katika CHADEMA tunataka watu watoe dukuduku lao waziwazi bila kitisho chochote. Ndio katika wale waliolalamika hakuna hata moja aliyeitwa kuhojiwa wala kufukuzwa uanachama au uongozi.

3) Umeuliza ni mafundisho gani CHADEMA imejifunza, kuanzia na positives na pia negatives.

Jibu: Hili ni swali pana, kwa hivyo linahitaji jibu pana. Panapo majaliwa nitatoa maoni yangu. Lakini kwa haraka tu niseme kuwa, mimi binafsi nimejifunza yafuatayo:

i) Kwa siasa za Tanzania, ili chama cha upinzani kikubalike ni swala la image zaidi kuliko subastance and style ya chama na mgombea. Kwa hiyo tuna kazi ya kutengeneza image ya vyama vyetu sana
ii) Watanzania wameshatambua umuhimu wa vyama vingi. Lakini bado ni woga wa mabadiliko ya kisiasa (poiltical change-phobic society). Wanajiuliza maisha yatakuwaje bila CCM? Tunawajibika kuwathibitishia kuwa maisha yatakuwa bora zaidi bila CCM katika serikali na kwamba mabadiliko ya kisiasa ni jambo jema kwao binafsi na kwa nchi.
iii) Tuna uhaba wa wasomi na wanasiasa majasiri Tanzania: Ukiangalia jinsi watu wanavyoikosoa na wasivyopenda yale mambo yanayofanywa na CCM, lakini bado watu walewale hawataki kujiunga na gurudumu la mabadiliko na hawataki kutoka katika hicho chama, lazima ujue tuna shida ya ujasiri katika ile nchi yangu na pia unafiki. CCM imesimama kwa sababu ya woga na unafiki wa wasomi na wanasiasa wasio majasiri, walioamua kuficha unafiki na woga wao katika kushambulia wale waliojitolea kuleta mabadiliko kupitia vyama makini vya upinzani. Hili ni tatizo kubwa la msingi sana ambalo sijui dawa yake nini.

Kama nilivyosema hili ni swali pana, linalohitaji jibu pana. Tuendelee na majadiliano.
 
Dah!!! Maneno mazito Mwanasiasa endele hivi hivi kutupa mashule haya .
 
mwanasiasa... finally watu wanaanza kuelewa ile mada ya "Je wapinzani ni wakombozi?".. take 10!
 
kuna kitu hapa wapinzani wameshindwa kukigundua au mimi ndio siju, ni kuwa ulipoanzishwa mfumo wa vyama vingi na ccm nayo ilibidi ife iliwaanze wote kwa pamoja.ccm wanatumia goodwill ambayo ilipatikana na kujengwa katika mfumo wa chama kimoja.
kwa hiyo umma wa watanzania huwa wanachagua chama cha ccm kwa kuwandio jina ambalo limewakaa katika akili zaotoka miaka ya 70 na hivyo sio raisi kusahaulika kwa watu ambao uwezo wao ni mdogo katika kujua ni nini maana ya mfumo wa vyama vingi.
kwa maana hiyo ccm bado wana mtaji wa kutosha katika kuongoza nchi.
kama vyama vyote vingeundwa upya sidhani kama leo ccm wangekuwepo hapo walipo.
 
Nimewasoma. Nitarejea kwa Ari mpya, NGUvu mpya na KAsi mpya....lakini sio ANGUKA
 
Mwanasiasa.

asante kwa maoni yako lakini kama unatizama vizuri kuna wanachama wengi tu humu wanataka kuhalalisha au kupiga debe kuwa Chadema ndio chama mbadala na hili litazame utaliona sehemu nyingi tu. ungeanza kuwaasa hao wanachadema wenzako kwa kuleta mgawanyiko. nilichouliza Tunduru ingawa Chadema waliweka katibu mkuu wa taifa kugombea ubunge na Cuf WAKAweka mwanachama wa kawaida sana tu mkazi wa Tunduru hata makao makuu ya chama hajafika na amekuwa wa pili. jee hizi nguvu za Chadema alisosema Tanzania njema ziko wapi? mie si mwanasiasa kama wewe kazi yangu kuuza nazi kariakoo sokoni sina chama ila Lipumba ni mashine ingine huwezi kumfananisha au kumlinganisha na Mbowe hata kwa robo. hata ngome ya Cuf iliyopo duniani sehemu mbalimbali including U.K huwezi kuishindanisha na chadema na hili nilimwambia Mnyika huko nyuma.

Kuhusu matokeo ya Mbowe kusema kuwa ni siri imejulikanaje hivyo ni uzushi hilo sio kweli Mwanasiasa umejikanyaga kwa kusema una orodha ndefu ya maprofessor ambao walifeli mitihani ya huko nyuma, jee hiyo orodha uliipata vipi? na WANABODI humu washindwe kuipata ya Mbowe?

nadhani njia ulizotumia wewe kuzipata za maprofessor ndio walizotumia wenzako kuzipata za mbowe.

Mwanakjj.

kweli sasa hivi umebadilika sana hadi napata shaka kuwa una mkono chadema au una mpango wa kuoa kilimanjaro uko bias sana na pia mdini. jirekebishe.
 
Mwanakijiji mdini? That will be a first. Unajua, ni rahisi sana kubandika watu majina bila hata kujiangalia mwenyewe nafsi yako kwanza.
 
Mzee Mwanasiasa,

Heshima mbele, nimezisoma kwa makini hoja zako na za Katibu tarafa,

(1). Nimeridhika na majibu kuhusu "HISIA ZA UKABILA", kwa mtu kama wewe ambaye sio kada wala mpenzi wa chama hicho, ni maneno mazito sana nafikiri mwenye macho ameyaona maswali yangu na majibu yako on ukabila, sasa ni uamuzi wa wananchi, lakini mimi nimeridhika nayo.

(2). CCM tunao utaratibu wa kuuuliza maswali, lakini katiba yetu inatubana kuuliza kwenye vikao rasmi vya chama chetu kwa mujibu wa katiba zetu, ndio maana huwa hatusutani kwenye vyombo vya habari kama Mbunge Zitto alipoamua kupumzika, tunafahamu kuwa chama kilisoma kwenye media zetu, hakukuwa na kikao cha yeye kueleza uamuzi wake, na kutolewa to the public na msemaji wa chama au wa mwenyekiti, kama Mwingira, sijui huko upande wa pili msemaji wa chama ni nani?

(a). CCM tuna utaratibu mzuri wa kusema machungu yetu na kusikilizwa na viongozi wa juu na wa serikali yetu, na kufanyiwa kazi kwa mfano nitaaanza na ya awamu ya nne kwanza,

- Balozi wetu wa zamani huko Italy, alipatikana na tuhuma za kuhusika na ubadhirifu wa pesa za walipa kodi, yaani wananchi, wewe na mimi, katika kikao cha kwanza kamati kuu ya CCM kilichofanyika Ikulu Dar Mwenyekiti wa CCM alishambuliwa na wanakamti kuhusu kitendo hicho cha balozi, na wiki iliyofuatia mwenyekiti huyo ambaye pia ni rais wa jamhuri, alimfukuza kazi balozi huyo na aliporejea nyumbani balozi huyo alifunguliwa mashitaka rasmi na serikali ya jamhuri, na kesi hiyo bado inaendelea, hii ni pamoja na CCM kuheshimu "The Rule of Law" ishu ambayo hata wenzetu Zimabbwe majuzi wamekumbushwa na the Mighty South Africa's Government, kuheshimu hilo, sisi CCM hatuna tatizo na hilo!

-Wabunge wa CCM walipokuja juu sana kuhusu Richmond, serikali ya CCM ya awamu ya nne haikusita kuwaondoa mara moja wale wote waliohusika kutoka katika madaraka yanayohusika na masuala ya umeme na richmond, that is leadership yaani "rapid response" as opposed na maneno ya mnadani kwenye nyama, hiyo ni spinning at its best!

-Majuzi taifa letu limeshudia ishu ya Manji/Mengi ikitatuliwa bungeni bila ya woga, tumejionea spika wa bunge letu akitoa uamuzi wa haki kwa kufuata maoni ya wabunge wawili Anna Kilango/Sendeka (CCM) waliokuwa minority katika kamati ya bunge iliyokaa kama mahakama, na spika huyo hakuishia hapo tu ameikabidhi PCB tume ya kuzuia rushwa kulishughulikia suala hilo kwa mujibu wa sheria nchi yetu, Mengi ndiye aliyekuwa na haki katika kesi hiyo ambayo mbunge Malima alishindwa kuthibitisha madai yake kwamba Mengi hujipendela kwenye TV zake na kudharau viongozi, hujiweka dakika kumi na kuwapa viongozi wakuu wa nchi dakika moja au sekunde, baada ya tepu kuonyeshwa ndani ya bunge ikagundulika kuwa ni uongo, pamoja na mbinu zote zilizofanywa na kiongozi mmoja wa juu wa CCM ku-pre matokeo on Manji behalf, haikuwezekana, kwetu CCM sheria ni msumeno CCM,

nenda IIP uuulize siku ya hukumu kutolewa na spika jinsi Mengi na wafanya kazi wake walivyolia kama watoto, maana walikuwa na mawazo kama yako kuwa uamuzi utategemea njama zilizofanywa na kiongozi huyu mkuuu mmmoja wa CCM, CCM tunaheshimu haki za wananchi hata kama ni Mengi! na tunaheshimu mawazo ya wabunge wetu hata kama ni wawili against wenzao, muulize Mzee Ndesamburo, jinsi moto ulivyokuwa ukiwaka ndani ya vikao hivyo vya mahakama,

(3). Kuhusu swali langu la mwisho ninakubali kuwa ni tooo broad kujibiwa kwa mara moja, hivyo ninakupa the benefit of the doubt, lakini as we go on tutaendelea kuuulizana zaidi.

Mzee Katibu Tarafa,

Heshima yako mkuuu, maneno yako mazito ingawa kuna sehemu flani ni misguided, kwa mfano CCM kutumia a goodwill ya the past chama kimoja, hapana si kweli maana kuna wabunge wa upinzani kama Mheshimiwa Dr. Slaa wameweza kuishinda CCM, tena kwa kura nyingi, pamoja na hiyo gooodwill kuwepo, Mheshimiwa Kabwe Zitto pia ameidhinsa CCM, kwa hiyo hoja ina walakini ndugu yangu, ingawa umeitoa kwa nia njema kabisa I can see that.

But, on the other hand una a valid point kwenye "wananchi wenye uwezo mdogo wa kujua nini maana ya mfumo wa vyama vingi", lakini again hiyo haiwezi kuwa the final authority on the ishu kwa sababu bado unahitaji kufafanua how wananchi waliweza kuichagua CUF kule Pemba yote under hiyo circumstances za uwezo mdogo wa kuelewa, na pia waliwezaje kuwachagua kina Dr. Slaa na Zittto, kwa sababu ni understatement kusema kuwa wananchi wa Kigoma, Mbulu, na Pemba ndio peke yao wenye uwezo mkubwa wa kuelewa mifumo ya vyama vingi, katika Tanzania, otherwise heshima zangu za dhati kwa uwezo wako mkubwa wa kujadili taifa letu.

Kwa wenzangu wengine samahani, muda wa kujibu hoja za pua hatuna tena, halafu forum ni forum, na redio ya mwanforum sio ya forum tusichanganye mambo, mpaka tutakap[oambiwa officially, kuwa hiyo redio ni part ya hii forum!

Mzee Lunyungu, kama kawaida heshima mbele bro, RESPECT, wengine tupunguze hasira life is too good!

Ahsanteni Ndugu Zangu! Tutaonana kesho majaliwa!
 
Mzee E, RESPECT. Umeanza kuingia kwenye rank ya mwanasiasa kwa kuwa mkata issue mahiri!! lakini hebu tufafanulie...we unadhani issue kama richmond ambayo mabilion yamepotea kweli CCM mlitutendea haki kwa "kuonyana wenyewe" kwenye vikao vya chama? wakati kodi zetu zimeteketea? Mi narudia accountability haikufanyika mkuu..tuwe honest na sincere. Unajua issue aliyoongea mwanasiasa alikuwa right..wabunge inabidi wapewe space waweze kueleza mawazo yao, swala sio wao kuongelea kwenye vikao wakati wamejifungia (au wamefungiwa?).. kwani tuliwatuma sisi na tulilipa kodi zetu kujenga ule ukumbi wa bunge kama platform yao ya kuongelea..na mambo ya kuongelewa ndo kama hayo, ambayo wawakilishi wetu wangehoji!!

Sasa kama kwenye Richmond au maskendo mengine CCM haina cha kuficha kwa nini isiweke mjadala huru?! Maana hata kama hukubali..CCM bado ina kitu kinaitwa "accumulated priveleges" na hili lipo hata US wazungu wana accumulated priveleges na advantages over wenzetu weusi..huwezi tegemea wakawa sawa just kwa sababu umetunga sheria leo zinazowapa hizo nafasi..Same kama CCM na hawa wanachadema au CUF...lazima CCM ifanye jitahada za maksudi kuwasaidia la sivyo itakuwa ni kuwadanganya wananchi for Public relations za wafadhili.

Lastly, kwa nini CCM inaogopa mgombea binafsi kama kweli mna nia ya kukuza demokrasia na mnaamini kwamba chama kinakubalika Tanzania yote? labda hata mimi na mwanakijiji siku moja tungekwenda kwetu huko Usukumani au Kigoma tukagombea (kunradhi MKKJ). Kwa sababu rafiki yenu mkubwa Mseveni aliruhusu wagombea binafsi ila hawajamzuia kubadilisha katiba na hata akiamua kuendelea, sidhani kama watamfanya kitu! Kwa nini Chama Chetu cha Mapinduzi hakitaki???? Kumbuka Mahakama imelitoleta maamuzi kibao hili swala....
 
Unajua MWANSIASA nimekupa heshima ya juu zaidi ya MNYIKA katika suala hili

japo bado ninatafuta mwanza wa ku counter majibu yako lakini umefanya kitu ambacho JJ MNYIKA kilimshinda kabisa


nashangaa bado kuna watu wanaendelea kubishana na MNYIKA ili hali mtu wa kujadiliana naye ni MWANASIASA regarless kama unakubaliana na siasa zake au la

Unajua hata mimi DUA kuna baadhi ya threads nakubaliana naye lakini inaonekana katika ile thread ya ZIMBABWE tunamitazamo tofauti lakini still tunaendelea kujadiliana based on the issues raised

Hakuna matusi wala nini kule ni ISSUE after ISSUE na naweka kukubali kuwa kuna baadhi ya hoja zake nimezikubali ili hali zingine sijazikubali

Nashangaa kwa nini MYIKA hajaja at least kuwatetea MDC wakati wao ni wapinzani kama CHADEMA
 
Mikuki bwana . Unaongea very slow lakini bongo tupu .Wacha mimi nisome tu kwa sasa .
 
Haya aliyo yasema Es si kwamba kakata issue bali yapo yanajulikana na yote ni uongo huhitaji PhD kuona spinning hapa . Uhuru ndani ya CCM mara kadaki Chadema na Zitto .Hivi jamani wewe Es vipi mzee .Uwezo wa Es na MKJJ ni tofauti sana . Mzee MKJJ yeye ni issues na si watu tofauti na wewe mzee wa character assessination .Lakini tupo hapa tutakueleza kila uki spin .Mwanasiasa bravo Mikuku irushe tu .DrWho mmmmmmmmmmmmmmmmm
 
Naomba nikaribishwe kwenye kijiwe.

Napenda ujue ndugu yangu Chinga ya kuwa kufaulu na kufeli ndiyo elimu yenyewe; kwa mwanafunzi yeyote mambo ya supplimentary ni ya kawaida kabisa, suala liwe ni kuhitimu na si kufeli baadhi ya masomo. Katika elimu ya juu kufeli ni kukosa sifa za kuendelea na masomo na si kurudia mitihani na ndiyo maana vyuo vyote duniani wanatoa nafasi kwa mwanafunzi kurudia somo alilofeli.

Kumuandma M<bowe kuwa amefeli masomo mawili ni chuki binafsi na ndiyo maana Chinga unasema kuwa Mbowe ajibu ni dada zetu wangapi waliambukizwa UKIMWI pale Bilicanas. Sijui ni nani atajibu swali hili si Mbowe wala hao unaodai kuwa waliambukizwa UKIMWI!

Chinga, unataka kutuambia kuwa Mbowe ndiye aliyewambukiza akina dada hao UKIMWI? Mbona huzungumzii mfumo mbovu wa uchumi wa nchi hii ambayo umeletwa, kulelewa, kukomazwa na kuendekezwa na watawala wa nchi hii ambao wewe unawajua na wametutawala miaka na mikaka? Akina dada wanaojiuza pale Mtaa wa Ohio ni matunda ya Mbowe au utawala mbovu ambao umedumu na utaendelea kudumu hadi wewe Chinga na wengineo wenye mawazo ya namna yako watakpofumbuka macho? Mwenye macho haambiwi tazama!

Suala la kufanyiwa coursework na Balile ni chuki zako binafsi tu ndugu yangu Chinga, acha hizo, maana hata wewe huwezi kuthibitisha poleka hiyo hoja kwenye nyepesinyepesei.
 
Back
Top Bottom