Mbowe na tafakuri zake...

Mbowe na tafakuri zake...

Mzee Jasusi,

Heshima yako mkuuu, mimi sio Chinga samahani sana, hoja hujibiwa kwa hoja bila vitisho wala ukali,

Udhamini wa wazee wa Pwani kwa TANU, uliwapa wazee hao Waisilamu the upper hand over all the party's final decisions na muelekeo wa chama hicho, ambacho originally kilikuwa ni strickly cha watu wa pwani tu!

Mpaka ulipofikia wakati wazee hawa wadhamini wa pwani, na Waisilamu wakagundua kuwa hawana mtu wa front aliye strong politically, anayeweza kuwa-represent mbele ya Wazungu, the then watawala,

ndipo alipotokea "MAKAPUTULA" Mwalimu, na single handed ulikuwa ni uamuzi wa Doss Aziz aliyekuwa kiongozi mkuu na Muisilamu, kumpatia Makaputula uongozi wa chama hicho, uamuzi haukuwa collective as a chama, kwa hiyo ni clear kuwa wadhamini hawa walikuwa na monopoly au upper hand katika maamuzi ya mwisho ya chama hicho,

Makaputula au Mwalimu ndiye aliyekiletea chama hicho inclusiveness, kwa kuanza kuwa-recruit kina Kamwenye Muhogo Mchungu, Kambona, Bomani, na the likes, huku akikitanua na kukieneza mikoa yote nchini, na haikuchukua muda Dossi Aziz na wenzake wote yaani the originals Waisilamu wa Pwani na wadhamini wa chama hicho walitupwa pembeni na hatimaye Mzee Rupia, ndiye akwa the sole mdhaini wa chama hicho mpaka wakati wa kifo chake,

Kama kuuliza kwa nini wadhamini wote wa Chadema ni matajiri wa kutoka kabila moja, ni kuwa mkabila so be it lakini swali langu halijajibiwa Mzee Jasusi!
 
Mzee Tanzania njema,

I have an idea wewe ni nani, lakini HOJA HUJIBIWA KWA HOJA!

maneno yako mengine ndio mijadala ya pua ambayo imekataliwa na wazee wenzio Mwanasiasa, na Mnyika!

Next time andika kwa heshima kidogo huu uwanja ni mkubwa na wa kimataifa baba yako na wangu hawana nafasi hapa kwenye mjadala wa taifa!

Ahsante Mzee!
 
WAISILAMU = WAKIRISTO
WAISLAM =WAKRISTO

kumbe kiswahili nacho kina wenyewe
 
Turudi kwenye ishu, tafadhali!

nitarudi kesho ngoja nitoke kidogo, this is lovely yaani true politics ya Tanzania!
 
Haya kaka,

Kuhusu mimi ni nani wala usipate taabu ndugu. Kila anayenifahamu anajua kuhusu Tanzanianjema.

Tuje kwenye issue.

Nakubaliana na wale ambao wamejitokeza kuuliza maswali kuhusu Ndugu yangu Mbowe. Nadhani hata ndugu yangu Mnyika aache kuwa msemaji wake kwani Mbowe mwenyewe anaweza kuja kujibu yote hayo. Ni wazi kuwa hawa jamaa wa CHADEMA wanaenda vizuri na ndio maana hatuoni kina Mrema, Cheyo, Lipumba na wengineo wanaoelekea ukingoni wakiadiliwa ila wao ndio wamekuwa akilini mwa watanzania anayejaribu kuangalia kwa undani jinsi nchi yetu inavyokwenda.

Nijuavyo mimi na kutokana na ukaribu wangu na hawa ndugu zangu walioko CHADEMA ni wazi kitendo cha Mbowe ni cha kishujaa kwani uamuzi wa kujiunga Hull hajauchukua kwa papara tu bali aliulizia ushauri kwa muda mrefu na kuupima vilivyo. Ndio maana akaishia ile kozi anayochukua ambayo ni kozi maarufu sana kwa wanasiasa wa Uingereza. Naambiwa Gordon Brown, Mandelson na wengineo katika Labour na hata Conservative walisomea kozi hiyo. Mbowe alikuwa tayari hata kuingia mlimani na nakumbuka kuna wakati alikuwa haishi kuja mlimani kupata mawazo kutoka kwa wasomi wetu kuhusiana na suala hilo la kusoma na mengineyo.

Kama tunavyojua wapo wenzetu wengi ambao kwao wao siasa ni kuwa watu fulani mathalani RAISI ama MBUNGE ambao wamejitokeza kufakamia degree majina tu ambazo haziwasaidii kupanua ufahamu wao katika nyanja mbalimbali na hata huko kwenye siasa.

Nionavyo mimi huyu jamaa amegundua kuwa suala sio kuwa na makaratasi yanayoitwa degree ili uwe fulani bali kupanua ufahamu ili uweze kufanya mambo fulani (having compitence for not becoming someone but being able to something)

Suala la "mimi nitakuwa fulani" linatupeleka pabaya ndugu zangu. Tangia JK afanikiwe kuwa rais na Zitto kuwa mbunge basi vijana wengi tumefakamia ndoto za kuwa RAIS ama MBUNGE. Matokeo yake wengi wetu tunajiingiza katika mifumo ya maisha (kijamii na kisiasa) ambayo hata kama tukifanikiwa kuzipata hizo nafasi tunajikuta tukiendelea kubomoa badala ya kujenga.

Wengi wetu tunajikuta tukiuza utu wetu, kujitengenezea mitandao michafu, kufakamia degree feki na kadhalika ambavyo mwishowe ndio vinatumika kutuweka mateka mikononi mwa manyang'au.

Nadhani mfano hai upo mbele yetu. Mwenye macho aambiwi tafuta.

Kuhusu ufadhili nadhani ni kuwaonea CHADEMA. Hivi katika vyma vyote vya siasa ni chama kipi kimeweka mahesabu ya matumizi yao ya kampeni kwa uwazi zaidi yao? Kuna wengine ni hivi juzi tu wameanza kutanakilisha mali zao sembuse ufadhili.

Na uko wapi ubaya kama wafadhili wanatoka Moshi. Ni wazi kuwa hawa ndio wapo tayari kuwa wazi kutokana kujitoa bila ya kuogopa mfumo wa kisiasa tulio nao ambao kusaidida chama kisicho tawala ni dhambi.

Ndugu yangu Mzee ES, usichungue sana ukadhani kuwa ni kweli ati CHADEMA inategemea ufadhili wa wazungu tu. Ndugu yangu ukichimba sana unaweza ukajikuta unamwaga mpunga wa mtu wako wa karibu mno.

Ushauri kwa Mnyika na vijana wengie wa CHADEMA: Wakiendelea kuwasumbua sana waambieni kuwa hata nanihii ni mfadhili mzuri wa CHADEMA. Si unajua jamaa uchaguzi karibuni na tayari mmoja ameshatangaza kuwaripua wanaoitwa wasaliti. Ni hapo sasa....

Yangu ni hayo

Tanzanianjema
 
Mzee ES,

upo bado?

Lets keep going. Leo nina muda wa kutosha

Tanzanianjema
 
Mbowe pole kwa yaliyokukuta endelea kupigana kamanda. kufeli ni jambo la kawaida bora wewe unahangaika kupata cheti chako kina Mrema na Mathayo David WANANUNUA TU.

ila usimtumie Balile kukufanyia kazi zako kwani utakuwa huna tofauti na wanaonunua vyeti.

Tanzanianjema.

sio kweli chama kinachoogopewa ni Chadema. chama cha upinzani makini ni Cuf AMBAcho CCM na serikali vinakosa usingizi. hujaona uchaguzi wa Tunduru? Chadema wamewakilishwa na katibu mkuu wa taifa msaidizi kama mgombea Ubunge na hawakufua dafu kwa Cuf walioweka mtu wa kawaida tu wa Tunduru.

hata masuala la muafaka serikali na CCM inafanya na CUF ikijua ni chama chenye nguvu na kina wanachama wa kweli.hivyo bora papatikane muafaka.

Chadema uchaguzi wa 2005 kilikuwa kinatafuta nani atakuwa mgombea kwani kilikuwa hakina watu wanaoweza kugombea kinyume na CUF hata NCCR huko wagombea urais haikuwa issue hadi chadema ikaangukia kwa Dj. NA kuna wakati walimuomba JK atoke CCM ili wampe nafasi aende kugombea kwa tiketi ya chadema, hiyo ni dalili tosha hicho ni chama cha ubabaishaji tu.

jamani kama Mbowe kafeli ule mjadala wa kina Mwanakjj kudai kuwa watu wa Kilimanjaro wana sababu za kihistoria za kusoma umeishia wapi? kumbe vichwa vigumu namna hiyo? huyu Mbowe angeweza UDSM? ikiwa huko Hull KAPEWA SEEN EXAMINATIONS bado kafeli, nadhani amuulize Mnyika vipi dose ya udsm kwani mnyika kaulaza.

au Mwanasiasa alikushauri usiguse Udsm Utaumbuka hakuna seen exam? nenda Hull mheshimiwa.
 
Kaka Mswahili,

CUF inaelekea kaburini. Na endapo hawajaamka na kufanya political rejuvination, CUF itamalizika punde hoja ya Unguja na Pemba itakapoisha makali ama wazanzibari watakapoamka na kuamua kuwatosa wanasiasa maluuni kutoka vyama/makundi yote mawili kule ZNZ.

Tofauti na CHADEMA ambayo ina mpango wa muda mrefu, CUF inategema siasa za mazingira (political invironment of the said period) badala ya kujenga asasi (institutions) za kutanua chama.

Ni kweli kuwa hadi sasa ukitoa CCM, CUF ndio kundi la kisiasa lenye mass constituent lakini kadiri siku zinavyokwenda CUF inazidi kumong'onyoka na kupoteza umuhimu (zaidi kwa upande wa bara) na wakati CCM na CHADEMA zinapanda.

Kuhusu muafaka sidhani kama ndugu yangu nawe unashindwa kung'amua kitanzi cha kisiasa. Waulize PLO walipoamua kuacha kuwa chama cha ukombozi (kama ilivyo CUF) na kuwa chama tawala.

Wenzio kina Duni wanalijua hilo.

Wasalam kaka
 
Mswahili,

Katika Siasa kuna kitu kinaitwa MORAL AUTHORITY. Ingawa sijawa na uhakika kuhusu suala la Mbowe kufeli. Hivi ndugu yangu una moral authority ya kuhoji maendeleo ya Mbowe kielimu?


tanzanianjema
 
pamoja na kelele zote hapa ni mtu mmoja tu kanitumia maswali... yaliyowekwa hapa hadharani siyaulizi.....
 
Mzee Mwanakijiji

I quite don't understand why a member of JF should have to go through your radio to respond to his fellow members.

Chinga,

Umekosea kidogo detail. Anayemsaidia zaidi homework Mbowe in Ansbert Ngurumo sio Balile. Hata zile Tafakuri anaandika Ngurumo. I have always said kwamba sooner or later, it will emerge as to who the real Mbowe is.

Tanzania Njema,

Acha kuuhada umma kwamba CUF inaelekea kaburini. Hii habari kwamba CUF ni chama cha Zanzibar (na Waislam) pekee ni propaganda ambayo mtu sophisticated kama wewe hukupaswa kuinunua. But I can understand, as a member of CHADEMA, you are bitter kwamba kwenye uchaguzi mwaka jana mmepata kura nusu ya CUF (600,000 to 1.3 mil). Hata uchaguzi ukiitishwa leo, matokeo yatakuwa hayo hayo. CHADEMA is all about mbwembwe za Dar, mikutano ya ukumbi wa Maelezo, kuandika makala ndefu na kuhudhuria makongamano. CUF wanazidi kutengeneza washabiki nazi nchi nzima.
 
Mzee TZNjema,

Acha vitisho, eti nikuliza hoja against Chadema mtu wangu wa karibu atapata madhara, una maana gani? Halafu mimi nilifikiri mambo ya kujadili pua hayatakiwi sasa lakini I am sorry kuwa ndio hasa unachokifanya kwenye hoja zako, can we change the subject na ku-deal na hoja?

Isipokuwa I am taking serious vitisho vyako, in the next six hours nitajua unasema nini halafu nitakurudia on hilo la vitisho!

Mzee MMJ,

Heshima yako mkuuu, niwe mkweli na wewe ndugu yangu, wananchi zamani tulikuwa tunakuamini kuwa huna upande mmoja , ndio maana tulikuwa tunakutumia maswali, sasa recently tumeona mabadiliko kwenye msimamo wako ndio maana hiyo interview hatuiamini kuwa ni genuine na baadhi yetu hatujatuma maswali, na tunakutakia interview njema!

Ahsante mzee.
 
Mbowe mwenyewe au msaidizi wake au mwanachadema yeyote mwenye ufahamu wa maswali yaliyoulizwa/yanayoulizwa anapaswa kujibu hata kama wao wanayaona ni njama za kupunguza umaarufu wa Mbowe/ CHADEMA. Kwa mtizamo wangu naona kuyajibu hayo maswali ndiyo njia ya kuondoa utata na hata propaganda zozote zilizojitokeza na zitakazojitokeza.

Kuhusu kurudia mitihani kwa Mbowe (kama ni kweli) ni kitu cha kawaida vyuoni. Hao wanaosema kafeli ni vizuri wakasubiri akashindwa mitihani anayotakiwa kurudia ndipo kauli yao itakapokuwa na nguvu.

Lakini bado nakubaliana na wote wanaotaka kupata habari binafsi za watu kama Mbowe, Kikwete, Mrema, Lipumba, Mbatia n.k kwa sababu wao wanataka kutuongoza na sisi lazima tujue maisha yao binafsi wanafanya nini kwa sababu ule msemo wa fuateni maneno yangu msifuate matendo yangu umeshapitwa na wakati.
 
Members:

Pamoja na kwamba tuna haki na wajibu wa kuwajadili viongozi wetu hapa, lazima tujue kuwa hatuna haki ya kuzusha mambo. Ni wazi kwamba maneno ya Chinga yamejaa usushi na chuki dhihi ya Mbowe. Chinga na Mgongo mna haki ya kumchukia Mbowe, lakini hamna haki ya kumzushia na kumbambikizia mambo. Sikuona ajabu Chinga kuzusha haya mambo maana chuki zake kwa Mbowe angalau tumezizoea, lakini nimeshangaa zaidi baaada ya kuona Mgongo naye kaingia katika mkumbo huohuo. Kwa mfano:

i) Mambo ya matokeo ya mitihani ni siri ya mtahiniwa na mtahini-yeye Chinga kayapata wapi? Hata kama amefeli hizo course 2, so what? Sote tuliopita mashuleni tunajua kuwa supplementaries, kufeli, ni sehemu sana ya kusoma. Tunaweza kuweka hapa orodha ndefu ya maprofesa maarufu waliopata kufanya supplementaries wakisoma, but so what?
ii) Mnnaweza kuthibitisha vipi kwamba Mbowe anaandikiwa coursework na Balile au Ngurumo?
iii) Mbowe amekuwa akiandika makala katika magazeti kwa muda mrefu. Nakumbuka kusoma makala zake katika gazeti la Rai tangu 1995; ni uendawazimu kuwaambiwa kwamba leo etu anaandikiwa makala na Ngurumo.

Mgongo I believed you're above this cheap kind of politics, Don't force me to change my opinion about your capacity to argue rather than shout.

Ushauri kwa members na hasa wanaopenda/wanaotarajia kuwa wanasiasa: Nafasi ya siasa za character assassination katika karne hii ni ndogo sana. Bahati mbaya hizi Siasa bado zipo katika CCM. Huko tuendako utapata mafanikio kwa uwezo wako. Na wala hutaweza kumshinda mshindani wako kwa njia ya character assassination; ni kwa kuonesha kwamba wewe unaweza ku-deliver kuliko yeye.

Sasa members ni juu yetu kushabikia uzushi au kuupiga vita na kuwazomea wazushi kwa juhudu zetu zote. Hatuna njia ingine zaidi ya kuwazomea maana hatuwezi kuwashtaki!

Mzee ES: You have raised intriguing questions; I will try to provide responses later.
 
Mbowe is not untouchable man nami nasema kama kiongozi lazima tuhoji mambo ambayo yeye kama Kiongozi mkubwa na mkomavu wa Upinzani ana shiriki. Personal hapana ila kama atakamatwa ugoni akiwa na title hii ya sasa tutamvaa bila ya uoga .

Mbowe kaitwa kila aina ya majina machafu na ya kijinga na wajinga . Maana ni mjinga pekee anaweza kusema na kufanya ujinga lakini ukiwa kiongozi basi unakuwa kama jalala .Kuna watakao kuwa nawe na wengine watakataa na hii ndiyo uhuru wa mtu kuachagua na kuamua .Mimi hata kama kafeli sioni ajabu wako viongozi wangapi leo hii ndanui ya CCM na Serikali ambao wali feli lakini does it bring sense kuja hapa na kusema Mbowe kafeli masomo 2 na naandikiwa course work sijui na akina nani ? Kweli mjinga ni mjinga tu lakini sitaki kuamini kwamba huu ni ujinga ila najua kuna umakusudi kulinda na kuendeleza mambo binafsi .

Mtu kafikia mahala pa kusema hana imani na interview,what the hell ?Yaani mtu kuhojiwa maswali na kujibu kwa sauti bado huna imani kivipi ?Etu watu wengine maswali hatuleti.Wacha kupeleka maswali uone kama inteview haitakuwepo. Kwanza mko na nani mimi siko nawe na nitauliza maswali yangu bila kuogoa wala kumpendelea Mbowe.
Jamani siasa ziwe na manufaa ya Nchi na si matumbo na ndugu zetu pekee . Uzushi mwingine mara ukabila mara hivi ujinga huu .Zitto na Mnyika wamesha jibu upuuzi wa uzushi huu lakini mko kila siku mnaacha issues mnakimbilia vijimabo . Aibuuuuuuuuuu kata issue utaheshimika .Si kila mtu anaweza kukaa hapa na kukubali utumbo no .Watu wana akili sana .Kumwita Mbowe DJ ni kumkosea haki . Je maneno haya unaweza kuyasema uso kwa uso ama ni nguvu ya screen unatumia kwa kwa humuoni ? Kinana wetu ana duka la kufua nguo na akitoka pale yeye na wana CCM kibao wanaenda Bilicanas kuwachukue hao mnawatukana Malaya .Je kinana apimwe kwa kufua nguo na tumwite mfua nguo ? Hii mifano michache lakini mkitaka tutakuja ndani zaidi .
 
Tanzanianjema: Nimesoma post zako mara tatu; nakubali mwenzangu hilo ni somo zito. Endelea kuelimisha, wenye macho na masikio wataona na kusikia!

Mswahili: Ndugu yangu kujigamba kuwa CUF ni bora zaidi ya CHADEMA ni kujiingiza kwenye mtego wa CCM wa kuhakikisha vyama vya upinzani vya upinzani havinawiri. Kama kweli wewe ni mwanachama wa CUF au chama chochote cha upinzani au kama nin mojawapo ya watu wanaopenda demokrasia ya vyama vingi ikuwe katika nchi yetu, hupaswi kuwa na mawazo haya. Sisi sote ambao ni wananchama wa vyama vya upinzani tunapaswa kuendelea kujiuliza ni kwa nini viongozi wetu hawataki kuunganisha nguvu japokuwa wanajua kabisa kuwa wakienda kwenye uchaguzi moja moja tutashindwa? Sasa badala ya kujiuliza maswali magumu, nawe umeingia kwenye mtego wa CCM wa kuvishindanisha vyama vya upinzani!

Sio siri kuwa vyama vya CUF na CHADEMA ndio vyama vikubwa vya upinzani kwa Tanzania sasa hivi. Lakini ni kweli pia kwamba hivi vyama vina udhaifu wa asili ambao ni kikwazo kikubwa katika kukua kwao. CUF wana dhambi ya asili kwamba ni chama cha udini na cha upemba. Sasa inawezekana hii sio kweli, lakini ndio taswira walio nayo. Nasi CHADEMA tuna dhambi ya asili kwamba hiki ni chama cha wachaga na kwamba ni cha kifamilia. Inawezekana pia kwamba hili sio la kweli, lakini ni ukweli pia kwamba hii ndio taswira ya chama chetu. Kwenye siasa taswira ya nje wakati mwingi ni muhimu kuliko kilichopo ndani! Kwa maoni yangu dawa moja kubwa ya kuvunja hizi dhambi za asili zinazokabili hivi vyama viwili ni kuunganisha nguvu. Kwa CHADEMA na CUF kuja pamoja, madai ya uislamu na ukabila yatakakuwa ndio mwisho wake. Kuendelea kutunishana msuli kwa hivi vyama hakusaidii zaidi ya kuthibitisha taswira iliyopo kwa jamii.

Kuna watu wengi wamekuwa wakidai kuwa eti hivi vyama haviwezi kuungana kwa kuwa vina itikadi, falsafa na agenda tofauti. Hili sio kweli. Ukisoma katiba na sera zao, vyama vyote viwili hivi ni vyama vya mlengo wakati ambao ni liberalism. Kuna kipindi vyama vyote pia huegemea kidogo katika mlengo wa kati kushoto. Ukiangalia falsafa zao pia zinafanana kwa kiasi kikubwa ukiacha mbwembwe za slogans.

Kwa hiyo kikwazo cha kuungana sio sera wala itikadi, bali ni ubinafsi na ushabiki wa kijinga wa baadhi ya viongozi na wanachama kama wewe Mswahili unayeshabikia kuwa eti CUF ina nguvu kuliko CHADEMA. Nguvu gani hizo wakati chama hakina mbunge hata moja katika majimbo zaidi ya 200? Are you serious au unafurahisha baraza? Hatuwasaidii viongozi wa vyama vyetu kwa kushabikia ujinga. Inakuwa ni ujinga zaidi pale ambapo ushabiki wa namna hii unafanywa na wanachama wa vyama vya upinzani. Unless Mswahili uniambie unafanya kazi ya CCM, nitakuelewa; vinginevyo nakuomba urudi nyuma kidogo, shika tama, then angalia haya mambo kwa sura pana. Kushindanisha vyama hivi viwili ni sawa na kushindanisha wagonjwa badala ya kuwatafutia dawa wapone ili wakashindane na mpinzani wao CCM!
 
Mzee MMJ,

Heshima yako mkuuu, niwe mkweli na wewe ndugu yangu, wananchi zamani tulikuwa tunakuamini kuwa huna upande mmoja , ndio maana tulikuwa tunakutumia maswali, sasa recently tumeona mabadiliko kwenye msimamo wako ndio maana hiyo interview hatuiamini kuwa ni genuine na baadhi yetu hatujatuma maswali, na tunakutakia interview njema!

Ahsante mzee.

asante sana! Mbingu na nchi zitapita lakini maneno ya Bwana yatasimama milele!! nabakia kutokuwa na upande, sipendi mtu, sipendelei wala siogopi mtu.. yote mema, mkituma maswali msipotuma yote sawa.. wale waliotuma bado wanaonesha imani yao kwangu. Sichezi ngoma wanayopiga wengine.
 
Mwanasiasa.... Bravo!
Haya ndio mambo!

Nakuunga mguu 100%!

Mnyika.. you have alot of stuffs to learn from Mwanasiasa!
 
Back
Top Bottom