Mbowe na tafakuri zake...

Mbowe na tafakuri zake...

Ujumbe huu wa mpendwakwao umenichanganya kidogo najaribu kuuelewa lakini duh!!!.....................
 
TANZANIA NI YA KWETU SOTE, TUKUBALI KUTOKUBALIANA, TULIJENGE TAIFA LETU.
Maoni yangu kuhusu ujumbe huu ni kwamba uandishi wa habari sio talent bali inabidi ujifunze
pili hii ni wazi kabisa kwamba huyu mtu sio mwandishi wa habari ila ni mtu kajitungia tu kicha cha habari ili afikishe ujumbe wake
Tatu maana yake ni tata inaweza tokana na yeye mwenyewe alikuwa anafikiria nini wakati huo, yaweza kuwa tanzania ni ya watanzania wote wenye nia njema na tanzania, unaweza kuwa mtanzania na una nia nzuri na tanzania waweza kufanya makosa kinachotakiwa uwe tiyari kukosolewa lakini haitakiwi jazba kama za Mkapa, na mwisho anatwambia basi tushirikiane kujenga taifa letu.
 
Mzee Mugongo Mugongo,

Damn! nilikuwa sijaviona vitu vyako duh1 vizito sana bro halafu siku zote ninazokufahamu sikujua kuwa na wewe una mawe, safi sana tunahitaji angalau balance kidogo ingawa ndio imeshindikana lakini sauti nne zinatosha against zote,

Ila nitakupigia waya leo jioni bro, damn!
 
mugongox2

Vitu vyako ni vizito, kula tano mzee
 
Ndugu wana JF,

Nimeingia leo kwenye forum yenu. Mara chache nimekuwa nikifungua kusoma baadhi ya mijadala inayochapishwa hapa. Nimekuwa nikisoma na kuondoka. Pole pole, nimegundua kwamba baadhi ya mijadala ina umuhimu, ila inajadiliwa bila mpangilio, na kuna watu wanaingia kati kuvuruga wenzao kwa lugha ambazo hazishahabiani na usomi unaotajwa tajwa katika forum hii.

Nimegundua pia kuna mijadala ya kijiweni kabisa, ambayo inashusha hadi ya forum na wanaojadili. Kwa sababu hii, nimepata kuwaza kwamba inawezekana hili linapaliliwa sana na ukweli kwamba wanaoandika hapa wanadhani hawajulikani. Hivyo wanaandika lolote wanalojua hawawezi kuwa 'responsible' nalo.

Huko nyuma, niliwahi kusoma baadhi ya wachangiaji wakitaka watu wajiandikishe kwa majina yao ili kuufanya mjadala uwe wa maana. Baadhi yao walijibu kwamba wengine humu wasingependa kujulikana kwa sababu wanafanya kazi "usalama wa taifa"!

Katika kufuatilia hoja za wachangiaji hapa, sijaona kitu chochote kinachofanana na hoja zao na kazi yao, kitu ambacho mtu anaogopa kusema na kuhusishwa nacho. Nilifika mahali nikadhani kwamba kama baadhi ya kauli hizi zinatoka kwa watu wanaojiita watu wa "usalama wa taifa," basi ndiyo maana taifa letu haliko salama! Ni wazi kabisa kwamba tafsiri yangu ya dhana za "taifa" na "usalama" ni ile inayohusu usalama wa watanzania, si viongozi au watawala; ni ile inayolinda raslimali za taifa kwa ajili ya vizazi hivi na vijavyo; ni ile inayojali maslahi ya taifa, ya wanyonge... ambao mara nyingi maisha yao ya kila siku yapo hatarini! Huu ni mjadala mpana.

Kwa sababu hiyo, kabla ya kuingia hapa nimefanya jitihada binafsi kujua wanaoandika hapa. Nimefanikiwa kuwajua baadhi yenu kwa majina halisi. Nilifanya hivi kwa sababu kwa 'nature' ya kazi yangu, napaswa kuwa curious.

Sikutaka kujadiliana na watu waliovaa mask, wanaoficha utambulisho wao bila sababu ya msingi katika nia njema waliyo nayo. Naamini kwamba mtu msomi, mkakamavu na jasiri, mwenye kusema ukweli huusema ukweli huo na kukubali matokeo yake.

Hata hivyo, nimegundua kuwa katika forum hii kuna watu wana akili nzuri na uwezo mkubwa wa kujadili hoja na kuchambua za wenzao. Hawa, hata bila kutaja majina yao wazi, wanatetewa na kazi zao. 'Zinanukia' usomi na uelewa. Na nilipokuja kuwajua, nilikubali kwamba ni watu makini.

Yapo mengi niliyotazama kwa kina katika forum hii. Yapo niliyojifunza, na yapo niliyoyadharau!

Lakini kuna mambo mawili yamenisukuma niingie na kuandika leo.

Kwanza, ni kujitambulisha kwenu, na kuwahamasisha muendelee kuandika MAMBO YA MAANA, na kuyajadili KIUTU UZIMA. Katika hili napenda niwaeleze pia kwamba utambulisho wa mtu una nafasi kubwa katika kazi anayoifanya. Na kazi inayofanyiwa mafichoni inapokelewa kwa mashaka. Watanzania wengi wamezoea kuzungumza mambo ya maana kwenye vikao visivyo rasmi; wakipewa fursa ya kuyasema hayo hadharani au katika vikao rasmi, ama wananyamaza au wanayakana!

Hawa ndio wanaotushangaa sisi tunaoandika makala kali magazetini kuwakosoa na kuwashauri watawala wetu, na tukakubali kuweka majina yetu, 'kusimama na kuhesabiwa.' Wengine wanatulaumu, wanatushangaa. Wanadhani sisi tunaojitambulisha hatuna miili na damu kama wao; hatupumui kama wao...

Hapana! Hoja hapa ni mtu kuamini unachoandika kwamba ni kweli, na ukawa tayari kukisimamia na kukitetea. Vinginevyo, kama wewe hukiamini; kwa nini wengine wakiamini? Kama hujiamini, kwa nini wengine wakuamini? Tulitafakari hilo.

Pili, nimeona baadhi yenu (mnajitambua) hamfanyi utafiti wa kutosha. Yapo mengi ya kudhihirisha hili, lakini nitatoa mfano wa hoja za watu kuhusu Freeman Mbowe, hasa wale wanaombeza kwa sababu wanazozijua. Baadhi yao wamefika mahali pa kutunga uwongo na kuubandika hapa kama sehemu ya propaganda ya kisiasa. Na hii ilikuwa baada ya baadhi yenu kutilia shaka uamuzi wake wa kwenda chuo kikuu. Baada ya kuwa-proved wrong, wakaja na hoja kwamba amefeli mitihani. Baada ya kuwa-proved wrong, sasa wananiingiza na mimi katika kazi zake za chuo na nyingine za magazetini!

Nimeshangaa pia kasi ya baadhi yao kusoma na kuamini uzushi na kuanza kuujadili kama vile wamepata authoritative information! Nimejitokeza kuwasema hao na kuwaumbua hapa! Fanyeni utafiti, hasa mnapokuwa mnazungumzia mambo ambayo yanafahamika kwa wengine.

Huu pia ni ushahidi kwamba baadhi yenu hawawajui vema baadhi ya watu wanaowajadili. Laiti mngejua UWEZO HALISI wa Mbowe, msingethubutu kurusha 'vumbi' na kuliita 'mawe.' Laiti mngejua kwamba mimi mwenyewe nahitaji kujifunza mengi kwake, msingefika mahali pa kudhani mimi naweza kufanya kazi zake. Hata hivyo, mngepaswa kujua kuwa kama ni kuandika makala, Mbowe hajaanza na Tanzania Daima. Ameliandikia sana gazeti la RAI akiwa mbunge, na hoja zake zimekuwa kali kama hizi za leo.

Kitu ambacho mngefanya kikaeleweka, na mkaonekana makini, ni kuzichambua hoja zake moja baada ya nyingine; nasi wasomaji tukaona uwezo wenu.

Zaidi ya hayo, hotuba zake bungeni ni ushahidi mwingine. Nendeni kwenye hansard. Msisahau pia ametoa hotuba nyingi katika mikutano ya hadhara tangu akiwa mbunge na wakati wa kugombea urais 2005. Si mimi niliyekuwa nahutubia. Wala hakuwa anasoma hotuba zilizoandikwa.

Mimi sijawahi kumsindikiza katika mahojiano yake na vyombo vya habari vya ndani na nje alipokuwa akijibu maswali ya hapo kwa papo. Ni uwezo wake; ni karama yake aliyojaliwa na Mungu. Huhitaji kuwa msomi kuyatambua haya na kuyakubali, hata kama huyapendi. Wala huhitaji kufanya utafiti sana kuyajua. Yapo juu juu, lakini watu wanataka kuyapotosha.

Na kila ninaposoma baadhi ya maandishi ya wanaomtukana na kumbeza Mbowe na kumkosoa katika Forum hii, wakituingiza na sisi wengine kwenye mkumbo huo kwa sababu wanazozijua, huku wakijipiga vifua na kushangilia usomi wao, na nikilinganisha uwezo wao (katika maandishi yao) na wa Mbowe, nabaki mdomo wazi kwa viwango hivi wanavyovionyesha na kuvishangilia. Sioni 'quality' wanayoitetea, wanayoilinganisha na ya Mbowe! Naelewa kwa nini hatuendelei.

HITIMISHO: Tafadhari niondoeni kwenye mijadala ya Mbowe. Nina nafasi na nafsi yangu. Inanitosha. Kama mnamtaka Mbowe fanyeji jitihada mmjue kabla ya kumwandika. Kama ni hoja leteni, tutajadiliana. Upuuzi si kazi ya waungwana. Nadhani nimeeleweka. Asanteni.
 
Ngurumo,

Maneno mazito lakini mbona umeingia na jina Bandia au ndio lako hilo?
 
Hahahaha Mkandara!

I think anaitwa Ansbert Ngurumo. Hata hivyo hoja yake ina msingi; yote aliyoongea nadhani ni kama amerejea kauli za wengi. Katika hoja zote lazima itafikia sehemu watu tutofautiane, au watu waingize utani ili kupunguza stress.

Sawa mzee Ngurumo, umesomeka. Hope wengi wataweza kutoa hoja zao na natumaini kujifunza pia toka kwako as long as huwa nazimia michango yako yenye upeo mpana. Kumbuka; kutofautiana ni rahisi sana na yataka moyo kuvumilia yote. Si kila hoja lazima ijibiwe; hata kimya ni jibu lakini hupendeza pale mtu asipokimbia (kuingia mitini) pale hoja inapomlenga.

Anyway; jina langu ni Mnyoo (kwa kilugha chetu) na ndo maana waona najiita wOrM.

Karibu jamvini... Ni mwanzo tu naamini hoja zaidi zinakuja - am tuned!
 
wOrM,
Shukrani sana nimemsikia mzee Mgurumo...duuuh hilo jina lako mzee wangu (Mnyoo) kwa lugha za kanda ya ziwa ni - malka. hee heehee! samahani lakini.

Ngurumo,
Freeman Mbowe ni mkubwa (BIGGER) zaidi ya hizi tuhuma kisiasa. Haya ni mambo ya mjini ambayo sidhani kama yanamkosesha usingizi..kwani tukitazama viongozi wote wameshambuliwa kwa madongo na mawe!...yote hii ni mitihani.

Mitume wote walipitia mitihani tena mizito kuliko anayoikabir Mbowe lakini hawakuchoka hata siku moja kuwaongoa wale waliopotea na kuwaongoza ktk ufalme ulioongoka!..
Ikiwa Freeman ni mtume wa Uongo ktk mapinduzi ya kifikra kwa Watanzania itakuja julikana ktk utume wake!...Sii kwamba Ujumbe wake haufiki! Unafika tatizo challenges zote zinatokana na wale waliosikia Ujumbe wake ila bado wapo katikati wakiyumbishwa na imani iliyotangulia.

Ni bora hawa waliokwisha upata ujumbe kuliko wale waliokataa kabisa hata kuusikia!.
J.J Mnyika na wengineo msikate tamaaa kwani somo bila maswali haliwezi kukua, hata elimu zetu huzidi kupanuka kila siku kutokana na curiosity za binadamu. Sii Sayansi wala Hesabu!... kwa hiyo umizeni vichwa kutafuta ujumbe ufike mbali zaidi...
Unajua tena mila za Mdanganyika hata akitaka sabuni ya Kufua nguo huagiza niletee OMO!... yaani tunatazama kasha kwanza badala ya uzuri wa sabuni iliyomo!
 
karibu ANSBERT NGURUMO....ndiee hasa wala hajifishi..nasoma sana makala zako,zimetulia ..na pole kwa pilika za masomo hapo london..we need more people of your calibre..wellcome!!!
 
wOrM,
duuuh hilo jina lako mzee wangu (Mnyoo) kwa lugha za kanda ya ziwa ni - malka. hee heehee! samahani lakini.


Hata kwetu Lukunyu Mkandara ndio kama vile usikiavyo wanasema "Lufufu" yani ni ukoo wa weusi tiiii... (kweli lakini usijali mtani wangu)

Ngurumo,
Ikiwa Freeman ni mtume wa Uongo ktk mapinduzi ya kifikra kwa Watanzania itakuja julikana ktk utume wake!...Sii kwamba Ujumbe wake haufiki! Unafika tatizo challenges zote zinatokana na wale waliosikia Ujumbe wake ila bado wapo katikati wakiyumbishwa na imani iliyotangulia.


Mkandara, you're damn right! Kufikia kilele cha Kilimanjaro si rahisi kama kukwea kichuguu. Safari ya Freeman inaweza kuwa na vikwazo vya aina mbalimbali lakini yeye ndiye mwenye kila silaha za kusafisha njia yenyewe. YEYE na si mwingine... Anaweza kuwashirisha wadau kadhaa ambao yawezekana wakawa wanampa kamba ama maji ya kunywa njiani lakini YEYE ndiye mwenye jukumu zito la kuuthibitisha ukweli wa unabii wake. Katika hoja zote ukiwa kama kiongozi wa aina yoyote lazima uziangalie kwa fikra pana zaidi ya kilichoandikwa. YES, si kila hoja inayoweza kurushwa kwa kiongozi yeyote inaweza kuwa sahihi; lakini ukiona mmoja anakuja na hoja flani ambayo binafsi waweza kuipuuza na kusema it's nonsense basi kuna umma mkubwa wa wenye mawazo ya huyo uloona anaongea pumba.

Ndio maana nikasema SI KILA HOJA LAZIMA IJIBIWE. HATA KIMYA NI JIBU! Sishauri akae kimya kwa kila hoja, hapana. Pia safari hii aweza kudhani yu pekee nyikani. Hapana; wengine tunasoma tafakuri zake n.k na kujifunza mengi na kuna uwezekano tunampa credit kadiri anavyoandika. LAKINI... Si wote wenye mtizamo unaooana na wake. Raha ya siasa uwe na aliye na mtizamo tofauti na wako. Si siasa tu. Ndiyo challenge ya maisha ati...

J.J Mnyika na wengineo msikate tamaaa kwani somo bila maswali haliwezi kukua, hata elimu zetu huzidi kupanuka kila siku kutokana na curiosity za binadamu. Sii Sayansi wala Hesabu!... kwa hiyo umizeni vichwa kutafuta ujumbe ufike mbali zaidi...


I see! Na kama kuna mtu nakubali uvumilivu wake basi ni kijana Mnyika. Sijui how come nowadays haonekani JF. Huenda yuko kusiko mtandao. Jitihada za kujibu hoja zote zinazoilenga CHADEMA kwa ushirikiano na Eric Ongara (naye haonekani nowadays) zimewafanya watu kadha wa kadha kuijua CHADEMA kwa undani. Sijui vyama vingine vya upinzani kama vinajua matumizi ya teknolojia ya mtandao lakini tungekuwa na walau mitizamo tofauti wakti tukiujadili mustakbari wa taifa letu basi ingependeza zaidi.

Kutofautiana katika hoja ni changamoto ya maisha. Maisha bila challenges huonekana rahisi lakini yanadumaza akili!
 
Ngurumo,

Maneno mazito lakini mbona umeingia na jina Bandia au ndio lako hilo?

Bwana Mukandara,

Si kwamba natumia jina bandia. Ni mimi Ansbert Ngurumo mwandishi wa Tanzania Daima. Kama mnataka picha yangu nitawapa. Ingekuwa vema na baadhi yenu mtoke kwenye 'pazia,' mjitokeze tujuane, tupeane majukumu, tujenge nchi; kwa matendo badala ya maneno.
 
Karibu Ngurumo,
Ni utaratibu tu wa kutumia majina ya kimtandao Lakini Hakumaanishi uwoga kwa waliowengi.Wa kuogopwa ni Mwenyezi Mungu kwani ndiyo mtoa riziki!
 
Ngurumo,

Shukran naitwa Mkandara Aka. Jina kubwa - Babu Ubishi!...Hilo Mukandara linaleta tafsiri ya wOrM...unaharibu!

Mzee wangu sipo ktk kiza hata siku moja na ndio maana Babu ubishi limekuja kwani Mbishi ktk Tafsiri ya mtaani ni yule asiyehadaika kirahisi huwezi kumpandisha mkenge kirahisi!....

Karibu sana JF na tunategemea utamwaga vimbanga vyako hapa -
Utume haijakamilika bado!.... Asheee!
 
Karibu Ngurumo,
Ni utaratibu tu wa kutumia majina ya kimtandao Lakini Hakumaanishi uwoga kwa waliowengi.Wa kuogopwa ni Mwenyezi Mungu kwani ndiyo mtoa riziki!

Kazi,

Haya nimekupata. Lakini hoja yangu ni kwamba baadhi ya watu, kwa kutumia majina yasiyo yao, wanadhani hawafahamiki. Hivyo, wanaweza kuandika chochote, ambacho hata hawawezi kukizungumza mbele ya watu. Ndiyo maana nilianza kufanya utafiti kabla ya kuandika ili nijue walau sehemu kubwa ya watu wanaoandika hapa kwa majina na sifa zao halisi. Sikupenda kuzungumza na 'mizimu.'

Ni vigumu mtu (ambaye hana tatizo la akili) kutumia jina lake halisi akaandika upuuzi wa wazi makusudi. Ninachotetea hapa ni umakini kwa kuwa Forum hii imekuwa ikijitangaza kuwa ya watu makini. Basi, umakini huo uonekane katika fikra zinazochomoza kwenye maandishi.

Naelewa pia kwamba hata utani ni jambo la maana katika maisha. Lakini ipo tofauti kubwa (naamini mnajua) kati ya utani na uzushi au upuuzi. Kwa mfano, kitendo cha mimi kuhusishwa na kazi za Mbowe chuoni na magazetini, si utani. Wala si sifa kwa yeyote. Pale nilipoandika stori inayomhusu Mbowe niliifanya kama sehemu ya kazi yangu, na niliweka jina langu. Baadhi ya stori hizo mmekuwa mnazisoma hata hapa JF. Ninachozungumzia hapa ni suala la 'personal integrity;' wala si kukosa uvumilivu. Au sio?

Ndiyo hoja yangu.
 
Kazi,

Haya nimekupata. Lakini hoja yangu ni kwamba baadhi ya watu, kwa kutumia majina yasiyo yao, wanadhani hawafahamiki. Hivyo, wanaweza kuandika chochote, ambacho hata hawawezi kukizungumza mbele ya watu. Ndiyo maana nilianza kufanya utafiti kabla ya kuandika ili nijue walau sehemu kubwa ya watu wanaoandika hapa kwa majina na sifa zao halisi. Sikupenda kuzungumza na 'mizimu.'

Ni vigumu mtu (ambaye hana tatizo la akili) kutumia jina lake halisi akaandika upuuzi wa wazi makusudi. Ninachotetea hapa ni umakini kwa kuwa Forum hii imekuwa ikijitangaza kuwa ya watu makini. Basi, umakini huo uonekane katika fikra zinazochomoza kwenye maandishi.

Naelewa pia kwamba hata utani ni jambo la maana katika maisha. Lakini ipo tofauti kubwa (naamini mnajua) kati ya utani na uzushi au upuuzi. Kwa mfano, kitendo cha mimi kuhusishwa na kazi za Mbowe chuoni na magazetini, si utani. Wala si sifa kwa yeyote. Pale nilipoandika stori inayomhusu Mbowe niliifanya kama sehemu ya kazi yangu, na niliweka jina langu. Baadhi ya stori hizo mmekuwa mnazisoma hata hapa JF. Ninachozungumzia hapa ni suala la 'personal integrity;' wala si kukosa uvumilivu. Au sio?

Ndiyo hoja yangu.

Nimekupata na ninatumai na wanabodi wote wamekuelewa.Hilo la integrity tumelizungumzia hapa kwa nyakati tofauti na tumekuwa tukilisisitiza kwenye hii forum.Umefanya vizuri kuongelea kile kilichokukwaza na kukitolea ufafanuzi kile kilichopotoshwa.
 
Naamini Ngurumo umeuona ukweli ila pia elewa kwamba humu kuna watu ambao kazi yao ni kupotosha ili ukweli usiweze kuwafikia wengi.

N i kweli kuwa Mbowe ni kiongozi mwenye uwezo mkubwa sana na zaidi ni talented ndio maana kwa wale mnaosoma makala zake mtagundua ya kuwa Mbowe ni mwandishi wa aina yake kwani muda wote huw anaandika mawazo yake na huwa anafanya rejea mara chache sana na hilo linaonyesha jinsi alivyo na uwezo wa kueleza msimamo na mawazo yake binafsi.

Mbowe ni zaidi ya kiongozi ndio maana ukiangalia CHADEMA ya leo sio kwamba tuu ameibadilisha ila pia ameifanya ikawa na uwezo wa kipekee kujiendesha ndio maana pamoja na yeye kuwa nje ya nchi bado CHADEMA ndio chama cha upinzani hapa Tanzania ambacho huwa kinasikika zaidi kila kukicha ,hii ni kutokana na Mbowe kukifanya CHADEMA kuwa chama taasisi nba sio chama mwenyekiti, hilo pia linaonyesha uwezo wa Mbowe katika kuendesha taasisi ndio maana wengi wetu tunamkubali Mbowe kuwa anaweza kuwa rais wa taifa hilil

Ukisoma hotuba mbalimbali za Mbowe alizozitoa maeneo tofauti kuanzia zile za kiswahili na hata zile za kiingereza utagundua kwamba huyu bwana anao uwezo mkubwa sana tena ni wa kipekee kabisa kwani naamini kuwa huwa anafanya mwenyewe.

Nimejaribu mkutembelea website ya CHADEMA na nilipokwenda kwenye makala nimeikuta makala za Mbowe na kati ya nyingi za kusisimua jaribuni kuisoma ile inayosema ikishangaa ya musa basi utayaona ya Mudhihiri,ikumbukwe kuwa hiyo aliiandika kwenye gazeti la rai akiwa anamjibu mudhihiri na wakati huo Mbowe alikuwa ni mbunge na aliyoyaandika ni mazito.

Kwanini Mbowe awe ndio wa kwanza kilakukicha huwa anashambuliwa ni kuwa wanauona uwezo wake haswa wapinzani wake wa kisiasa kwani wanaona amewazidi sana kiuwezo na ndio maana amekuwa ndio targeti yao kila kukicha,mbona huoni yeyote akimshambulia kijana Mbatia pamoja na ukweli kwamba chama kimemfia mikononi?

Mbona hakuna wa kumshambula Lipumba pamoja na ukweli kwamba sera nyingi za utandawazi tunazozitekeleza leo alihusikA MOJA KWA MOJA WAKATI AKIWA MSHAURI WA RAIS mWINYI?Ukiangalia yote hayo utagundua kwamba Mbowe anashambuliwa na watu ambao wana malengo yao binafsi na wanamwona Mbowe kuwa ni kikwazo kwa wao kuweza kufikia malengo yao kama asipochafuliwa.

Humu utaona Mbowe na Conservative ,mbona hata siku moja hatujawahi kuona humu watu wakijadili Lipumba na uliberali wake tena kibaya zaidi ni kuwa Lipumba ni makamo mwenyekiti wa uliberali hapa Afrika ,na misimamo ya kiliberali ni mibaya kuliko ya conservatives,hilo linaonyesha kuwa kuna mkakati wa kummazliza Mbowe na Kosa wanalolifanya hao ambao wanapanga mikakati hiyo ni kukosa uwezo wa kupangua hoja za Mbowe kila ANAPOJITOKEZA NA KUANDIKA AMA KUZUNGUMZA.

Mbona hakuna anayejitokeza kuwapongeza wakina Mbowe kwa kuweka hadharani bajeti yao ya uchaguzi mkuu uliopita?mbona hilo limekuwa likionekana kama sio issue hap[a kwetu jamvini?

Mbowe kaza mwendo ,kaza buti kama wanavyosema vijana wa kijiweni ,
Ngurumo usiondoke kwenye forum kwa sababu nyepesi kiasi hicho,wewe jadili ukweli wa mambo sema upande wa pili wa shilingi kuna siku ukweli utaonekana,

Ipendeni kweli kwani itawaweka huru ,na mkiwa huru mtakuwa na amani maishani.
 
Ngurumo

Pole pole, nimegundua kwamba baadhi ya mijadala ina umuhimu, ila inajadiliwa bila mpangilio, na kuna watu wanaingia kati kuvuruga wenzao kwa lugha ambazo hazishahabiani na usomi unaotajwa tajwa katika forum hii...............Nimegundua pia kuna mijadala ya kijiweni kabisa, ambayo inashusha hadi ya forum na wanaojadili. Kwa sababu hii, nimepata kuwaza kwamba inawezekana hili linapaliliwa sana na ukweli kwamba wanaoandika hapa wanadhani hawajulikani. Hivyo wanaandika lolote wanalojua hawawezi kuwa 'responsible' nalo..............................Kwa sababu hiyo, kabla ya kuingia hapa nimefanya jitihada binafsi kujua wanaoandika hapa. Nimefanikiwa kuwajua baadhi yenu kwa majina halisi. Nilifanya hivi kwa sababu kwa 'nature' ya kazi yangu, napaswa kuwa curious...........................Hawa ndio wanaotushangaa sisi tunaoandika makala kali magazetini kuwakosoa na kuwashauri watawala wetu, na tukakubali kuweka majina yetu, 'kusimama na kuhesabiwa.' Wengine wanatulaumu, wanatushangaa. Wanadhani sisi tunaojitambulisha hatuna miili na damu kama wao; hatupumui kama wao...

Hapana! Hoja hapa ni mtu kuamini unachoandika kwamba ni kweli, na ukawa tayari kukisimamia na kukitetea. Vinginevyo, kama wewe hukiamini; kwa nini wengine wakiamini? Kama hujiamini, kwa nini wengine wakuamini? Tulitafakari hilo..........................................


Hivi hata kabla ya kuanza kujibu hoja humu ulianza kuwasaka wachangiaji wa hii JF ili uwafahamu maana yake ni nini hasa? Unaogopa kitu gani kusema bila kuwachunguza wachangiaji? Hii inaonyesha jinsi ulivyo filisika kimawazo i.e. unaangalia nani kasema nini badala ya hoja iliyotolewa. Inaonyesha jinsi ambavyo bado una safari ndefu katika masomo yako kama ni kweli na uelewa wako. Kutumia jina la bandia au kutumia jina halisi ni uchaguzi na hakuna sheria hapa JF ya kukutaka utumie jina lako halisi. Vile vile kuna sababu nyingi tu za kutumia jina bandia i.e. theft of identity, naona ndugu yangu bado umechelewa uko dunia ipi? Theft of identity ina-cost millions of dollars or pounds kwa taarifa yako siyo kitu cha kuchezea vile ambavyo unafikiri. Unaweza kutoka na one million pound in a day na kusafisha jina itakuchukua muda (credit rating).

Well endelea na another task force operation kama hii:http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=2456 ya kuwachunguza JF members.

Unaongelea elimu, tulikuwa na Mkwawa, Kinjekitile, Mirambo, Chaburuma etc. waliweza kuongoza makabila tofauti na kutufikisha katika fani tofauti tofauti. Mfano Mkwawa aliweza kuwapiga Wajerumani na kuweza kuwakomesha katika vita yao ya kwanza, na walilifahamu hili, bila shaka uliona jinsi walivyojizatiti mara ya pili. Kuna kitu kinaitwa elimu dunia, sio lazima ukae darasani tu kuwa na elimu.

Vile vile hakuna sheria ya whistle blowers Tanzania unataka wale wanaoleta nyeti za viongozi (mfano wakubwa wao wa kazi) wawafahamu, you must be joking! Where is the freedom of speech? Una maanisha kama mtu hakusoma kutokana na definition yako asichangie? Mbona hao waliosoma ndio wametufikisha hapa! (PANAPONUKA) Sasa hiyo elimu ina maana gani kama kila siku mnaimba kwa kutegemea kura kwa wasiosoma lakini kwenye mawazo hamuwataki.

Kinachotawala hapa ni hoja, hatishwi mtu hapa. Leta maneno au shutuma zilizoelekezwa kwako na tuelezee ukweli na si vinginevyo. Wewe weka ukweli hapa - PERIOD!

Tunafahamu waandishi wengi wanatumiwa na wale wanaowawekea kitoweo mezani, huwezi kukata mkono unaokulisha hivyo huandika yale ambayo hayako mioyoni mwao bali ya vikaragosi wao kwa hiyo hubadilika na kuwa vibaraka.

Ngurumo kukata mzizi wa fitna wapo ambao watafungua forum kwa wale wanaopenda kutumia majina halisi n.k. ni uchaguzi. Usije hapa na kutuletea longolongo ambalo halina maslahi kwa Taifa. Kama umekwazwa jibu hoja na weka ukweli, waswahili husema kwenye uongo ukweli hujitenga.
 
Mpaka kielewe,
misimamo ya kiliberali ni mibaya kuliko ya conservatives

Sii kweli kabisa kuwa mfumo wa Kileberali ni mbaya kuliko Conservatives hapa Afrika na sidhani kama unaweza kunipa chama hata kimoja chenye mfumo huo ambacho kinafanya vizuri kuliko chama cha Kileberali....

Navyoamini mimi Afrika tumekopa mifumo hii toka nchi za magharibi na haiwezi kutumika kwetu kwa malengo sawa na nchi hizo hata kidogo!...Hatuna mabepari wetu wenyewe wa kutosha, Mabepari ambao wanaweza kuwekesha ktk viwanda, Biashara na miradi mingine mikubwa zaidi ya kutegemea wageni!...Hapa tayari jumuiko la mambo haya utapoteza maana ya mrengo ktk utekelezaji wake.
Pinda pindua mifumo yote hii inategemea wageni na misingi ya mahuasiano ya kibiashara inayopangwa nje. Siasa zetu ni majina tu ambayo kwa mtazamo ni maandishi yasiyoweza kuwa na mrengo ktk utekelezaji wake hapa kwetu Afrika.

Kuhusu CUF, imekuwa vigumu kwa wengi wetu kuweza kuhoji Liipumba na Uliberali kwa sababu hakuna mwakilishi wake humu ndani na sidhani kama Freeman Mbowe na akina Ngurumo ndicho kinachowapa taabu...Maswali ndani ya mrengo na mfumo wa Chadema nadhani ndio mapenzi yao makubwa zaidi kuyatangaza ila kinachowashinda wao ni pale waswahili tunapoanza kuchimba maisha yao kutafuta makosa kama vile wao wametangaza Utume wa dini ama wao kuwa ni Saint!..
Binafsi nakubaliana sana na wOrM ya kwamba kuna maswali ambayo sii lazima yajibiwe jambo ambalo J.J Mnyika anafanya makosa kutaka kujibu maswali ambayo yanahusu maisha ya mtu. Maisha ambayo hawajawahi kumhoji ki ngozi hata mmoja nchini toka tumepata Uhuru, na wala hawawezi kuthubutu na hakuna siku tutaweza kuhoji maisha ya kiongozi wa kiafrika. After all hayo ndio maswala ya kijiweni...
 
Nilizungumzia mfumo huo kwenye moral persipective,kwani sisis waafrika ni watu ambao huwa tunajali zaidi maadili kuliko jambo lingine.

Nitakuwa mwakilishi wake ili walau tuanze kuwajadili kwani ndio wagombea wa urais hivyo hatuna budi kuwaqhjua ili kuwachambua na kujua ni nani tutamkabidhi nchi yetu.
 
Mabepari huwa wanajengwa huwa hawaibuki kama uyoga,hivyo tukiamua kutengeneza daraja la kati lenye maslahi kwetu tunaweza ila tatizo ni pale watawala wanapotaka kuwekeza kwa wageni kwani wanapewa 10%ambazo wenyeji wengi ndio kwanza wanamitaj midogo na hata benk zetu huwa zinawajali zaidi wageni katika kuwapa mikopo kuliko sisi wazawa.
 
Back
Top Bottom