Mbowe na tafakuri zake...

Mbowe na tafakuri zake...

nitumieni maswali yenu yote... na yote nitamuuliza.. kazi itakuwa kwake kujibu

Mimi sitakuwa na swali kwake kwanza ninampa nafasi ya kujieleza na kuulizwa na wengine sasa baada ya kumsikiliza hoja zake ndiyo nitakuwa na maswali,Naomba kama tutaona kuna Umuhimu wa kuitwa tena utusaidie Lakini kwanza wenye maswali kwasasa pamoja na yale ya Family NGO........NK Nafasi hiyo!
 
Maswali

1.Ndugu Chama chako kimejaa shutuma za ukabila kuanzia juu hadi chini , wewe unasemaje juu ya hili ?

2.Kuna shutuma kwamba mligaa viti vya Ubunge Viti maalum kwa ukabila na urafiki , je unasemaje ?

3.Kwa nini Chadema haikuweza kuwaachia CUF kule Tunduru ili Upinzani uoate nyongeza ya Mbunge ?

4.Kuna haja gani ya kuendelea kushiriki chaguzi kwa Chadema kama misingi na sheria za Tume hazitoi haki sawa kwa Vyama ?

5.Kuna mkakati wowote wa kudai Tume huru ya Uchaguzi ambayo itawajumuisha Wapinzani kwenye kufanya maamuzi ya namna Uchaguzi utakavyo enda ?

Mswali yangu hi haya na mengine yatakuja nikiwa nayo .
 
Katika hii thread, Mwanasiasa is the best! Mimi sio mwanachama wa chama chochote ile ni mpiga kura makini! Mwanasiasa, I salute you! Kuhusu kufanya PhD bila masters Its very possible! Infact kwa sasa hata UD you can do it subject to the senate approval! Na masters bila first degree inawezekana kabisa na watu wanafanya (subject to some conditions but mainly experience ya hiyo field unayotaka kusoma). Personally I have a colleague who is doing it from one of the reputable university! Ila at the end of the day kama unaaspire kuwa politician nadhani you should go Muungwana Mbowe`s way (kuamua kufanya first degree) kuepuka watu kuwa na walakini na elimu yako!
 
Maswali yangu kwa DJ Mbowe.

alichangia kwa kiasi gani dada zetu kupata ukimwi pale billicanas? jee alikuwa anawapa nasaha? na wakiuguwa aliwasaidia kwa madawa ya kurefusha maisha?

katika matokeo ya mitihani yake ya kwanza aliyofanya januari matokeo yametoka mwezi machi mwanzoni na amefeli masomo mawili kati ya manne. amefaulu kozi work mbili tu na mitihani miwili amefeli. jee kwanini amefeli? na ataacha lini kuandikiwa course work na balile?

na akanunishe kuwa Balile hajampeleka pale chuoni ili kumsaidia yeye course work.
seminar amekuwa hachangii chochote anasinzia tu. kwanini hivyo?
Mnyika msimshirikishe kwenye mijadala inayohusu Elimu kwani yeye si mpenzi wa elimu na si msomaji. anataka kuongoza chama cha wajinga.

mwanakjj naomba nami nimpigie maswali Mbowe jee nitumie ile simu yake inayoanza na +4478......?
 
Duh! Hii kali hadi anavyofeli? kweli wabongo ni hatari? Kazi kwenu CHADEMA.
 
Alikumbwa Na Tatizo La Cheating,plagiarism And Collusion.
Alifikiri Kusoma Ni Udj? Any Way Amepewa Nafasi Arudie Mitihani Yake Kwenye Summer. Tumuombee Mungu Kama Tunavyoiombea Timu Yetu Ya Taifa Jumamosi Dhidi Ya Senegal.
 
Mzee wangu Mwanasiasa!

Hongera zangu za dhati kwa hoja zako na za kielimu, hata kama zina mapungufu flani, lakini RESPECT bro na ni mfano wa kuigwa!

Mzee Wangu Lunyungu!,

Heshima yako ndugu yangu, maswali safi ila punguza munhari kidogo lakini respect kwa maswali yako!

Mzee Admin,

Hatimaye sasa you have my respect, na ni worthy kurudi tena kwenye forum!

Mnyika,

I am very disappointed kwa mara ya kwanza na majibu yako, lakini ni demokrasia at work, maana umeshindwa kuelewa aliyeuliza maswali ni nani, halafu ninaona kuwa ni fun maswali ya Dr. WHO, kwako ni kuongelea watu, kwa Mwanasiasa ni hoja kwa hoja,

Nasema tena Mwanasiasa you have my vote ukigombea anything!
 
Maswali yangu kwa DJ Mbowe.

alichangia kwa kiasi gani dada zetu kupata ukimwi pale billicanas? jee alikuwa anawapa nasaha? na wakiuguwa aliwasaidia kwa madawa ya kurefusha maisha?

katika matokeo ya mitihani yake ya kwanza aliyofanya januari matokeo yametoka mwezi machi mwanzoni na amefeli masomo mawili kati ya manne. amefaulu kozi work mbili tu na mitihani miwili amefeli. jee kwanini amefeli? na ataacha lini kuandikiwa course work na balile?

na akanunishe kuwa Balile hajampeleka pale chuoni ili kumsaidia yeye course work.
seminar amekuwa hachangii chochote anasinzia tu. kwanini hivyo?
Mnyika msimshirikishe kwenye mijadala inayohusu Elimu kwani yeye si mpenzi wa elimu na si msomaji. anataka kuongoza chama cha wajinga.

mwanakjj naomba nami nimpigie maswali Mbowe jee nitumie ile simu yake inayoanza na +4478......?



tutaamini vipi kama unasema ukweli?
 
Nadhani kuna majungua hapa sasa. This is too much. Balile anafanya course work ya Mbowe and why is that? Kama Mbowe kafeli 2 kapita 2 ndiyo maana ya kusoma badala ya kufeli kabisa unakuwa huna cheti na bado ni Mbunge wa CCM .

Kama kafeli means atarudia na ndiyo kusoma huko .
 
Mzee Mwanasiasa,

Majibu yako ni murua sana, isipokuwa binafsi nina maswali ya nyongeza,

(1). umekubali kuwa wafadhili wa Chadema ni pamoja na FREEMAN MBOWE, NDESAMBURO, na Mzee EDWIN MTEI, kipesa hawa tunafahamu kuwa ni wananchi wenye uwezo, sasa the fact kwamba wote ni kutoka kabila moja la eneo la Kaskazini, yaani Wachagga, huoni kwamba inaweza kuleta hisia mbele ya jamii kwamba huenda kuna cheche za ukabila ndani ya chama hicho cha taifa cha siasa, ambacho kikatiba ya taifa letu kinapaswa kuwa ni kioo chenye sura zote za taifa letu kuanzia kwenye level ya udhamini, mpaka viongozi na wanachama wake?

(2). Pia uamuzi wa kutumia helikopta wakati wa uchaguzi, nitashukuru kama utanifafanulia kama ni kweli ulikuwa ni wa kamati kuu ya chama hicho kama katiba ya chama hicho inavyosema, ninauliza hivyo kwa sababu kuna wagombea ubunge wa chama hicho ambao ilibidi wajitoe kwenye uchaguzi wa ubunge uliopita kutokana na kutokuwa na pesa za kuendesha kampeni kutoka kwenye mfuko wa chama hicho, huku mapesa mengi yakitumika katika kutumia chombo hicho ambacho ni cha kisasa, na ambacho sisi wananchi tunafahamu kuwa kinahitaji mapesa mengi kukitumia kwa ajili ya kampeni za uchaguzi kama kilivyotumika na chama hicho?

(3). Katika uchaguzi uliopita ni mafundisho gani Chadema imejifunza, kuanzia na positives na pia negatives as far as siasa na wananchi wa Tanzania yaani wapiga kura kwa ujumla is concerned?

Ahsante ndugu yangu na pia nitashukuru kama kuna na wengine wanaweza kuongezea majibu ya hayo maduku duku yangu!

Halafu nina mengine zaidi ya nyongeza tutaulizana as we go, Ahsante!
 
Jamani,
Acheni umbeya na character assassination. Matokeo ya mitihani ya watu huwa si public information. Sasa hawa kina chinga aka mr es ambao hujitokeza kwenye forum hii kunapozuka suala la Freeman mnapataje hizo info? Kama si wivu tu na roho mbaya what else can it be?
 
Mr ES
Wakati TANU inaanzishwa wafadhili wa chama walikuwa watu wa pwani. Kwa hiyo isikukoseshe usingizi. Kuna historical precedence. Hata ikafikia watu kudai kuwa walioanzisha harakati wa uhuru walikuwa waislamu. Lakini akina Sykes, Azziz, hawakuweka uislamu wao kwanza. Kwa hiyo hata akina Ndesamburo sidhani wanatanguliza Uchaga wao kama unavyotaka tuamini. Kama ni ukabila basi wewe ndiyo mkabila.
 
Mzee Es,

Hivi kweli unataka kujua nani mfadhili wa CHADEMA? Ukifanikiwa kurudi nyumbani muulize Mzee wako. Akikwepa swali chungulia bank statement zake. Ukishindwa nyamaza kimya hadi utakapo mrithi nafasi yake kama mipango itaenda vizuri.

Tanzanianjema
 
Back
Top Bottom