Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 5,226
- 17,975
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi amesema serikali itaendelea kuwakamata na kuwachukulia hatua wote wanaotengeneza akaunti kwenye mitandao ya kijamii kisha kuzitumia kutukana na kudhalilisha watu na hasa viongozi.
Aidha, amesema kuna utumiaji wa Akili Unde kutengeneza video, sauti na picha zenye lengo la uchochezi na kwamba wananchi wanatakiwa kuwa makini wasisambaze, huku serikali ikiwasaka wanaoziunda kwa kuwa wana lengo la kuivuruga nchi.
"Nawataka wananchi tuandike taarifa za maoni na majina ya watu wanaoandika na kusambaza taarifa za uchochezi kwenye mitandao ya kijamii, ili tuchukue hatua kwa kuwa kuna watu wamezamia nchi nyingine wanafanyakazi ya uchochezi, "amesema Katambi ambaye pia ni Mbunge wa Shinyanga Mjini.
Aidha, amesema lazima Watanzania watambue kuwa kuna haki na wajibu, ila wengi wanazungunzia haki bila kuzungumzia wajibu wao kwenye nchi.
Aidha, aliwaomba wananchi kuwa wataulivu wakati serikali inachukua hatua dhidi ya watu wanaoleta uchochezi kwa lengo la kuchafua nchi, na kwamba nchi inaendeshwa kwa kuzingatia utawala wa sheria.
"Ushahid wa kwamba taifa liko salama ni miradi ya maendeleo inayotekelezwa, na tutahakikisha tunaendelea kuwa salama, "amesema.
Waziri Katambj ameyasema hayo leo Jijini Mwanza wakati wa Uzinduzi wa Meli ya MV Mwanza, uliofanywa na Waziri Mkuu, Dk. Lameck Nchemba.
Aidha, amesema kuna utumiaji wa Akili Unde kutengeneza video, sauti na picha zenye lengo la uchochezi na kwamba wananchi wanatakiwa kuwa makini wasisambaze, huku serikali ikiwasaka wanaoziunda kwa kuwa wana lengo la kuivuruga nchi.
"Nawataka wananchi tuandike taarifa za maoni na majina ya watu wanaoandika na kusambaza taarifa za uchochezi kwenye mitandao ya kijamii, ili tuchukue hatua kwa kuwa kuna watu wamezamia nchi nyingine wanafanyakazi ya uchochezi, "amesema Katambi ambaye pia ni Mbunge wa Shinyanga Mjini.
Aidha, amesema lazima Watanzania watambue kuwa kuna haki na wajibu, ila wengi wanazungunzia haki bila kuzungumzia wajibu wao kwenye nchi.
Aidha, aliwaomba wananchi kuwa wataulivu wakati serikali inachukua hatua dhidi ya watu wanaoleta uchochezi kwa lengo la kuchafua nchi, na kwamba nchi inaendeshwa kwa kuzingatia utawala wa sheria.
"Ushahid wa kwamba taifa liko salama ni miradi ya maendeleo inayotekelezwa, na tutahakikisha tunaendelea kuwa salama, "amesema.
Waziri Katambj ameyasema hayo leo Jijini Mwanza wakati wa Uzinduzi wa Meli ya MV Mwanza, uliofanywa na Waziri Mkuu, Dk. Lameck Nchemba.