Tanzanianjema: Nimesoma post zako mara tatu; nakubali mwenzangu hilo ni somo zito. Endelea kuelimisha, wenye macho na masikio wataona na kusikia!
Mswahili: Ndugu yangu kujigamba kuwa CUF ni bora zaidi ya CHADEMA ni kujiingiza kwenye mtego wa CCM wa kuhakikisha vyama vya upinzani vya upinzani havinawiri. Kama kweli wewe ni mwanachama wa CUF au chama chochote cha upinzani au kama nin mojawapo ya watu wanaopenda demokrasia ya vyama vingi ikuwe katika nchi yetu, hupaswi kuwa na mawazo haya. Sisi sote ambao ni wananchama wa vyama vya upinzani tunapaswa kuendelea kujiuliza ni kwa nini viongozi wetu hawataki kuunganisha nguvu japokuwa wanajua kabisa kuwa wakienda kwenye uchaguzi moja moja tutashindwa? Sasa badala ya kujiuliza maswali magumu, nawe umeingia kwenye mtego wa CCM wa kuvishindanisha vyama vya upinzani!
Sio siri kuwa vyama vya CUF na CHADEMA ndio vyama vikubwa vya upinzani kwa Tanzania sasa hivi. Lakini ni kweli pia kwamba hivi vyama vina udhaifu wa asili ambao ni kikwazo kikubwa katika kukua kwao. CUF wana dhambi ya asili kwamba ni chama cha udini na cha upemba. Sasa inawezekana hii sio kweli, lakini ndio taswira walio nayo. Nasi CHADEMA tuna dhambi ya asili kwamba hiki ni chama cha wachaga na kwamba ni cha kifamilia. Inawezekana pia kwamba hili sio la kweli, lakini ni ukweli pia kwamba hii ndio taswira ya chama chetu. Kwenye siasa taswira ya nje wakati mwingi ni muhimu kuliko kilichopo ndani! Kwa maoni yangu dawa moja kubwa ya kuvunja hizi dhambi za asili zinazokabili hivi vyama viwili ni kuunganisha nguvu. Kwa CHADEMA na CUF kuja pamoja, madai ya uislamu na ukabila yatakakuwa ndio mwisho wake. Kuendelea kutunishana msuli kwa hivi vyama hakusaidii zaidi ya kuthibitisha taswira iliyopo kwa jamii.
Kuna watu wengi wamekuwa wakidai kuwa eti hivi vyama haviwezi kuungana kwa kuwa vina itikadi, falsafa na agenda tofauti. Hili sio kweli. Ukisoma katiba na sera zao, vyama vyote viwili hivi ni vyama vya mlengo wakati ambao ni liberalism. Kuna kipindi vyama vyote pia huegemea kidogo katika mlengo wa kati kushoto. Ukiangalia falsafa zao pia zinafanana kwa kiasi kikubwa ukiacha mbwembwe za slogans.
Kwa hiyo kikwazo cha kuungana sio sera wala itikadi, bali ni ubinafsi na ushabiki wa kijinga wa baadhi ya viongozi na wanachama kama wewe Mswahili unayeshabikia kuwa eti CUF ina nguvu kuliko CHADEMA. Nguvu gani hizo wakati chama hakina mbunge hata moja katika majimbo zaidi ya 200? Are you serious au unafurahisha baraza? Hatuwasaidii viongozi wa vyama vyetu kwa kushabikia ujinga. Inakuwa ni ujinga zaidi pale ambapo ushabiki wa namna hii unafanywa na wanachama wa vyama vya upinzani. Unless Mswahili uniambie unafanya kazi ya CCM, nitakuelewa; vinginevyo nakuomba urudi nyuma kidogo, shika tama, then angalia haya mambo kwa sura pana. Kushindanisha vyama hivi viwili ni sawa na kushindanisha wagonjwa badala ya kuwatafutia dawa wapone ili wakashindane na mpinzani wao CCM!
Mwansiasa unajenga hoja vizuri na kwa ufasaha sana. Endelea na makamuzi mpaka kieleweke! Ila kwenye suala la muungano wa vyama natofutiana na wewe.
Wachambuzi mbalimbali wa masuala ya kisiasa wemekuwa na mtazamo kwamba vyama vya upinzani havifanyi vizuri katika chaguzi kwa sababu ya kutoungana! Kwa mtazamo wangu siamini kuwa muongano wa vyama vya upinzani ni suluhisho,bali ni kituko kingine kwenye medani za siasa Tanzania.
Muungano ni jambo lenye mantiki, lakini nikitafakari zaidi linaniumiza kichwa.Vikiungana kichwa kichwa bila malengo tutakua hatujafanya lolote, kuiondoa CCM ni jambo moja kuiletea Tanzania maendelo ni jambo jingine.
Lazima malengo yawe zaidi ya kuiondoa CCM. Chukulia CUF inajitambulisha kama chama cha Kileberali, CHADEMA social democrats(mlengo wa kati) NCCR naona wana mguso wa kijamaa sasa je wakiuangana hicho chama kitafuata sera zipi? Hatuoni kama tutakuwa tunadumaza uwanja mpana wa mawazo?Itapendeza tukiwa na vyama vinne au vitano imara, tuweze kufaidika na mawazo toka itikadi na falsafa mbalimbali.
Cha msingi ni jamiii ya kitanzania kuamka zaidi ya vyama kuungana. Hakuna haja kuilazimisha jamii kuchagua nyeusi na nyeupe tu, jamii itambue kuna nyekundu, bluu na kahawia pia.Tuondoe dhana ya uwili, CCM na upinzani, ndio na hapana, ukweli na uongo! huu ni utupu, ujinga, ukale na ujima! Jamii ya kisasa haitarajiwi kuwa na mtazamo chakavu kama huu.
Kunatakiwa kuwepo ushindani wa fikra, hoja nzito/sera mbadala.Tusitengeneze NARC nyingine Tanzania ambayo malengo yalikuwa kuondoa KANU pekee. Vyama viungane kama malengo, maono au itikadi zinauwiana na si kwa lengo la kuitoa CCM pekee. Hofu yangu ni kuwa, huu muungano wenyewe utakuwa ni ulafi, ya kwamba badala ya vyama vilivyoungana kujadali sera na mambo ya msingi ya kuliendeleza Taifa wakaishia kujadili majimbo mangapi wagawane, kila chama kitapata mawaziri wangapi badala ya kuanagalia sera za kuongoza hizo wizara, hii ni vurugu.
Ndio maana Mrema aliwahi kubeza muungano wa vyama akisema, vyama vya upinzani vikiungana vinaunganisha nini? Je kwa matokeo ya kura ya 2005,2000 na 1995 tukiunganisha kura za upinzani zingeweza kuiondoa CCM?
Tatizo la msingi liko kwa wapiga kura na mfumo mbaya wa uchaguzi(tume ya uchaguzi, katiba n,k).Haya ndio mambo ya kuyashambulia sasa. Vyama vya upinzani, jumuiya za kiraia na wananchi makini waunganishe nguvu zao kudai katiba na tume huru ya uchaguzi ili hatimae tuwe na uchaguzi wa kidemokrasia ifikapo 2010.