MeinKempf
JF-Expert Member
- Jun 11, 2013
- 11,092
- 7,236
Mazungumzo ya kitenge na mkurugenzi wa EFM wakati wa kusaini huo mkataba .Taarifa zilizopo ni kuwa kiko Dodoma.
Hapa ndio yale yale ya 'simba na yanga', na mara nyingi mwisho wake ni fulfillment ya tamaa za muda mfupi lakini haya mambo ya kuhamia hamia vituo vya huko Dar es Salaa hakuchangii lolote fani ya habari. Anyway, yote maisha.
Mtangazaji mahiri wa habari za michezo,Maulidi Baraka Kitenge akisaini Mkataba wa kazi na kituo cha radio kiitwacho EFM 93.7 kilichopo Kawe jijini Dar Es salaam.
Kitenge:Haka ndo katakuwa "ka mshahara" kangu.??? Ohhh...waooo.
Mkurugenzi EFM:Ahahaa..kadogo sana bw. kitenge tafadhali hebu ongezea japo sifuri mbili mbele.
Kitenge: Mbona kubwa sana mkuu, mpaka inatoka kwenye kibox cha kujaza
Mkurugenzi EFM:Kawaida kitenge kwani ile barua yako nimeiona , ikanisikitisha sana kwani gharama za maisha ziko juu sana.
Kitenge:Asante sana mkuu, najuta sana kuchelewa kujiunga nanyi, kwani kule koo lilikuwa lishaanza kukauka na ngozi kunywea kama mtu aliyekula chumvi nyingi.
Mkurugenzi EFM:Ahahaahhhaa .... Usijali sana kitenge hesabu kuanzia sasa utaanza kung'aa kama zile enzi zako kwani umekuja kwenye maziwa na asali.
Kitenge :Lazima niende kwa mzee wa upako nikatoe ushuhuda juu ya
mambo haya makubwa.
Mkurugenzi:Haya piga sahihi yako kwanza hapo juu ya jina lako na usisahau kuhakiki tarehe ya kusaini mkataba kama iko sahihi.