geraldkowero1
JF-Expert Member
- Jul 5, 2014
- 1,838
- 647
hata kama ni mimi ndugu wa erasto nisingekubali mali za ndugu yangu ziliwe na mwanaume mwingine....Hizo mali za erasto zirudi kwa ndugu zake pamoja na watoto wake ...mama saimoni aende akatunzwe na huyo mume wake mpya
Kwa kweli Marry kaeleza vizuri sana kiasi cha kuwaongoza hata wapelelezi wakajua pakuanzia au kuendeleza.Mke wa Erasto na kama walivyo wengi hakutumia busara hata kidogo.Hii inaonyesha hata marehemu Erasto akiwa hai huyu mkewe alikuwa anachepuka sana.Kwa kipindi kifupi hivi asingeweza kutafuta wa kumwoa kwani wazazi na ndugu bado walikuwa na machungu ya kumpoteza kijana alietegemewa na wote.Kama hamu zilimzidi angekutana na bwanake kwenye vyumba vya hoteli zake.Kwa vyovyote vile hasira za mawifi na wakweze ziliamshwa kwa kuona mali za ndugu yao Erasto zinaenda kumnufaisha mwanamme mwingine asiyezitolea jasho.Hili kibinadamu halivumiliki na ndicho kilichosababisha hata baba mkwe wake kuacha nadhiri yake na kutafuta ukweli wa kifo cha mwanae kwa waganga na kwa vyovyote vile ingawa siko akilini mwake alikuwa anataka kujua kama mkwewe alihusika na kifo hicho kwa kuona hakikumgusa sana na kutafuta mme mwingine.Huyu mke wa marehemu Erasto inaonyesha hayuko karibu na watu vinginevyo wangemshauri aache mpango huo kwani bado mapema na anao watoto wa kulea.