huyo fred unaemponda Brazil piga ua anaanza na ni favourite wa world cup, mchezaji ambaye mechi 60 anacheza mbaya 5 unaongelea level za world class huwezi wapata 11 unless una hela kama za Man city na PSG wachezaji wanaolipwa na Taifa. Eriksen na uwezo wote aliouonesha toka asajiliwe tayari ameshatimiza mechi 5 alizocheza vibaya na ndo kwanza msimu hata kati bado.
na sijui kama umenielewa hoja yangu vs Rashford jamaa tayari ameshavunja record za Ma legend akiwa na miaka hio, kuna watu wamecheza Man u mamia ya mechi wanafunga kila siku ila vs timu kubwa output yao ni ndogo sana, Rashford ni vice versa yeye vs timu kubwa ndio anafunga zaidi.
na mashabiki wengi ni vigeu geu dakika kadhaa tu mnasahau timu imetoka wapi, imefanikiwa nini na inaelekea wapi, msimu uliopita tulicheza vibaya sana, tulikuwa na striker anafunga magoli alikaribia kuwa top scorer kabisa lakini as a team tulikuwa ovyo, ila kocha mpya amekuja na hili ni tatizo la kwanza kulifanyia kazi, tucheze kitimu zaidi, akaamua striker wake atakuwa ni hard worker zaidi kuliko mmaliziaji, unaweza ukaona sasa hivi timu haifungi ila ukamsajili huyo unayeona atafunga ikawa unaharibu timu zaidi.
kwa nilivyomuelewa ETH kuna uwezekano asije striker sio January tu hata dirisha kubwa anaweza asije na badala yake akaja Gakpo ambaye ni winger mould hizo hizo za kina Rashford. ipo benefit ya kucheza na wachezaji watatu ama wanne mbele ambao wote ni hard workers, just mechi iliopita ya spurs umeona mziki wake, na hata leo tulikuwa hatuna nguvu kama spurs ila tuliwadhibiti vizuri tu,