Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kuna mashabiki wenzetu wanadai aangaliwe kwa vile tu ametoa adhabu kwa Ronaldo akiwa kwenye harakati za kujenga nidhamu.
Wanasahau kwamba hapa Duniani msingi wa kila aina ya mafanikio ni NIDHAMU.

Timu yetu inacheza vizuri sana chini ya EtH, unaona kabisa ari na, muunganiko na hamasa waliyonayo wachezaji. Wote wanajuana na kuelewana, leo nimeona kitu ambacho sijawahi kikiona tangu Sir AF astaafu.

Timu kwa sasa inamhitaji mtu mwenye uchu wa kufunga magoli, kimsingi tunahitaji 'Haaland' wetu.
Rafaela Pimenta tells Sky Sport: “Release clause for Haaland? I can’t comment about that. He’s really top, top guy. His father is the secret”

…but yes, release clause is there — valid from 2024 for €200m.
 
TenHag akipewa muda kama aliopewa Ole natumai ataleta mafanikio makubwa coz naona timu inacheza kitimu na hana kulea wachezaji wakizungua ,kapiga benchi Maguire , Ronaldo ,Elanga alikuwa anampa nafasi ya kuanza naye alipozidisha utoto sasa yuko benchi.

Akifanya marekebisho katika kikosi akapata players anaowataka na kuwa na kikosi kipana huyu kocha ataifikisha timu mbali.
 
Hii Hali ilitukuta Arsenal kipind Arteta ameamua kuwafurumusha Auba na Ozil, alipokea maneno mengi ,Lakini alisamama na msimamo wake

Tena Ten hag naona ana kahuruma kiasi, nimeona sehemu eti aombe msamaha ,huyu alitakiwa asicheze Tena Hadi akimbie mwenyewe ,huyu kwa kosa lile la kwanza ,na Lile la preseason ilitakiwa hata mech za Europa asiguse ,apigishwe warm up halafu anarudisha bench

Auba na Ozil wanaelewa kilichowakuta , hata carabao walikuwa hawachezi, na kila week wanawekewa £350k , had Auba akaenda kupiga magoti kwa Rais was Barca asajiriwe ,

Ronaldo amshukuru Ten hag hata Europa anacheza,kwa matukio yake yakujifanya mkubwa kuliko klabu ,alitakiwa aminywe iwe fundisho .
Ningekuwa Tenhag ronaldo asingecheza milele chini yangu. Yani milele asingeingia uwanjani milele.

Hao wanaopiga kelele waanzishe timu zao wamuweke ronaldo awape makombe.
 
Chief sikuiona hii comment yako ila ukweli unafahamu vizuri kwamba yule dogo sio mchezaji wa kumtegea asilimia 100.

Wewe Chief mimi nakuonaga ni kama mzazi anayemtetea mtoto wake mvuta bangi mbele za watu ila ndani ya nafsi yako unajua kabisa hili toto chenga tu.
Rashford ana miaka sijui 24 tayari ana goli nyingi kushinda malegend kibao vs traditional top 6. mseme unavyomsema hii ni record yake huwezi kumyima, Jamaa ni deadly kwenye counter, sisemi ndio awe main striker wetu ana weakness zake kama mipira ya juu yupo ovyo ukicompare na urefu wake, ila ameprove tayari kwamba you can depend on him kwenye hizi mechi.
 
  1. Newcastle united
  2. Tottenham hostpurs
  3. Chelsea
Sikhofii tena kufungwa kwa manchester united bali nakhofia kutokufanga magoli kwa manchester united.

Hiyo ndio tathmini yangu ya mechi 3 zilizopita.

Nimesikia familia ya glazer hawatokuwa na hela kwa dirisha la january.

Si haki kabisa.
Hapa hawana option, nina uhakika Ronaldo anaondolewa kikosini mwezi wa kwanza. Hili ni jambo ambalo familia ya Glazer hawakuli-anticipate.

Timu ni lazima iingie sokoni la si hivyo presssure itakuwa kubwa sana ya wao kuuza timu. Jim Ratcliffe kawaambia muda wowote wakiwa tayari kuuza timu Pound 6B ipo mezani.

Kuna interview yake moja juzi Jim Ratcliffe alisema aliongea na Joel pamoja Avram Glazer kama wapo tayari kumuuzia ila walimwambia hawauzi na hawakutaka mazungumzo yoyote yale yaendelee. Chini ya maji wanajua wakifanya ujinga Jim Ratcliffe atatumia hii fursa kuwa-force wamuuzie.

 
Rashford ana miaka sijui 24 tayari ana goli nyingi kushinda malegend kibao vs traditional top 6. mseme unavyomsema hii ni record yake huwezi kumyima, Jamaa ni deadly kwenye counter, sisemi ndio awe main striker wetu ana weakness zake kama mipira ya juu yupo ovyo ukicompare na urefu wake, ila ameprove tayari kwamba you can depend on him kwenye hizi mechi.
Miaka 24 sio kinda ktk mpira huu ni umri wa kubeba timu. United sisi sio timu ya kukubali mediocrity tunafaa kuwa na wachezaji wanaojua kumaliza kazi.

Ndio maana ninapowananga wachezaji kama Fred, Shaw, Degea n.k sio kwamba ni wabovu ila kwa standard za United sisi tunacheza kushinda makombe.

Tunahitaji kuona mchezaji ktk mechi 50 mpaka 60 ndani ya msimu basi unakua na siku mbaya labda gemu 5 ila sio zaidi ya 10.
 
Ningekuwa Tenhag ronaldo asingecheza milele chini yangu. Yani milele asingeingia uwanjani milele.

Hao wanaopiga kelele waanzishe timu zao wamuweke ronaldo awape makombe.
Nafikiri kucheza Ten Hag anaweza kumpa nafasi out of respect as a gentleman. Yule mholanzi hanaga nongwa na mtu ila anaonekana hana masikhara. Mfumo wa Ten Hag Ronaldo ni mzigo hana energy ya kufanya pressing.

Ronaldo ni legend as a player ila inaonekana ktk maisha yake ya kawaida ni mtu mwenye personality ya hovyo sana. Huwa nakereka sana ninapoona mwanaume anapenda attention pamoja na kuongozwa na hisia kama mtt wa kike.

Kuna muda mambo ktk maisha yanaweza yasiwe yanaaenda upande wako ila kama mwanaume unapaswa kudhibiti akili yako ili hisia zisianze kutawala uwezo wako wa kufanya maamuzi. Ronaldo karuhusu hisia kufanya maamuzi. Hajazoea kutokuwa key player. Pia hataki kukubaliana na nyakati.
 
Miaka 24 sio kinda ktk mpira huu ni umri wa kubeba timu. United sisi sio timu ya kukubali mediocrity tunafaa kuwa na wachezaji wanaojua kumaliza kazi.

Ndio maana ninapowananga wachezaji kama Fred, Shaw, Degea n.k sio kwamba ni wabovu ila kwa standard za United sisi tunacheza kushinda makombe.

Tunahitaji kuona mchezaji ktk mechi 50 mpaka 60 ndani ya msimu basi unakua na siku mbaya labda gemu 5 ila sio zaidi ya 10.
huyo fred unaemponda Brazil piga ua anaanza na ni favourite wa world cup, mchezaji ambaye mechi 60 anacheza mbaya 5 unaongelea level za world class huwezi wapata 11 unless una hela kama za Man city na PSG wachezaji wanaolipwa na Taifa. Eriksen na uwezo wote aliouonesha toka asajiliwe tayari ameshatimiza mechi 5 alizocheza vibaya na ndo kwanza msimu hata kati bado.

na sijui kama umenielewa hoja yangu vs Rashford jamaa tayari ameshavunja record za Ma legend akiwa na miaka hio, kuna watu wamecheza Man u mamia ya mechi wanafunga kila siku ila vs timu kubwa output yao ni ndogo sana, Rashford ni vice versa yeye vs timu kubwa ndio anafunga zaidi.

na mashabiki wengi ni vigeu geu dakika kadhaa tu mnasahau timu imetoka wapi, imefanikiwa nini na inaelekea wapi, msimu uliopita tulicheza vibaya sana, tulikuwa na striker anafunga magoli alikaribia kuwa top scorer kabisa lakini as a team tulikuwa ovyo, ila kocha mpya amekuja na hili ni tatizo la kwanza kulifanyia kazi, tucheze kitimu zaidi, akaamua striker wake atakuwa ni hard worker zaidi kuliko mmaliziaji, unaweza ukaona sasa hivi timu haifungi ila ukamsajili huyo unayeona atafunga ikawa unaharibu timu zaidi.

kwa nilivyomuelewa ETH kuna uwezekano asije striker sio January tu hata dirisha kubwa anaweza asije na badala yake akaja Gakpo ambaye ni winger mould hizo hizo za kina Rashford. ipo benefit ya kucheza na wachezaji watatu ama wanne mbele ambao wote ni hard workers, just mechi iliopita ya spurs umeona mziki wake, na hata leo tulikuwa hatuna nguvu kama spurs ila tuliwadhibiti vizuri tu,
 
kwa nilivyomuelewa ETH kuna uwezekano asije striker sio January tu hata dirisha kubwa anaweza asije na badala yake akaja Gakpo ambaye ni winger mould hizo hizo za kina Rashford. ipo benefit ya kucheza na wachezaji watatu ama wanne mbele ambao wote ni hard workers, just mechi iliopita ya spurs umeona mziki wake, na hata leo tulikuwa hatuna nguvu kama spurs ila tuliwadhibiti vizuri tu,
Hapa nakubaliana na wewe 100%. Binafsi huwa siupendelei sana mpira wa kuwa na mshambuliaji wa kuganda mbele kama barafu.
 
We ni boya kama hao kina Rio.

Ronaldo ameshaisha. Akiwa uwanjani hakuna anachofanya. Amewekwa benchi anaambiwa aingie sub anakataa.e

Yeye ni nani kama si mpumbavu? Unaambiwaje na kocha uingie unakataa?

Kama ni star sana mbona ametaka kuondoka na hakuna wa kumchukua?

Acheni ujinga nyie fans wa Ronaldo.
Cr7 ni muchezaji mukubwa mwenye profile kubwa hakuna wa kumuambia chochote huyu ameshashinda kila kitu yule kipara wenu 10hag atamwambia nini?
 
Back
Top Bottom