Tatizo kocha amejipa presha za kipumbavu kabisa, una pogba una Matic una Bruno unawezaje kucheza mpira wa kukaba mbele ya Southampton?
Ile mechi waliotukaba walikuwa Pogba na Mason Greenwood hawakuwa mchezoni pamoja na matukio wachache aliyoyafanya pogba.
Martial na Rashford walitupotezea nafasi tatu za kufunga magoli kwa uchoyo wao tu wa kutaka kufunga achilia mbali nafasi ile aliyokosa Rashford akacheza keeper.
Soton walitupigia pindi sana kabla ya kuja kwenye game walichokifanya ni kumtarget Pogba kama weaklink yetu kwa kumkaba na kumnyima space ya kufanya maamuzi.
Walimkaba Bruno asifanye maamuzi kwa haraka lakini wakablock passing lanes zote kwenda kwa Martial na Greenwood.
Kingine waliamua kukabia juu na kuwapress sana centerbacks wetu kiasi cha kutufanya tushindwe kufanya build up kuanzia chini badala yake tukajikuta tunapiga Highballs kwenda mbele hii iliwafanya midfield wetu wawe tortured kutafuta mipira ya juu.
Soton walituwin kwenye kucheza second balls na speed wao ndiyo walikuwa wanaamua matukio mengi uwanjani yaende vipi hii ilikuwa ni hatari sana kwetu hasa wanapofanya transition kuelekea golini kwetu.
Jana Maguire alikuwa kama Amateure mara nyingi kila alichokifanya kilipelekea second balls kwa Soton na kuendelea kutupa pressure kubwa sana wakati wote.
Nani alipaswa kutoka na dakika ya ngapi ? Mimi niliona Greenwood hakufanya kazi yake sawa sawa jana na alipaswa kutoka mapema kabla hata ya Pogba pengine ingesaidia kumfanya Ryan Betrand asionekane shujaa.
By the way Pongezi zangu zangu ziende law Ralph Hassenhuttl huenda aliangalia mara mbili mbili ile mechi yetu na Norwich na akajua madhaifu yetu yako wapi.
Mechi ya jana ilinirudisha nyuma mpaka kwenye finali ya UEFA champions League mwaka 2011 kati ya Bayern Munichen na Chelsea kazi alioufanya Romeu jana ilikuwa haitofautiani na ile aliyoifanya katika mechi ile ya finali.
NB
Nilisema toka mwanzo katika mechi tulizokuwa tumebakiza nilikuwa nawahofia Southampton kuliko timu nyingine yoyote kwa sababu ya historia yao dhidi yetu.