Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

  • Group L: Man Utd, Astana, Partizan, AZ Alkmaar

Kwa uzembe wa timu yetu unaweza kukuta tunacharazwa hapo na hizo timu maana wakina gomes watapata namba hapo sasa huyo astana na az alkmaar wapo vizur si wabovu
 
Mi mwenyewe naona kwa smalling kidogo tumekurupuka hii safar ilikuwa ya jones kwanza
Inabid ufurahi deadwoods zinapoondoka ,maana wanaokuja ni upgrade ,

Asipondolewa sasa unaweza shangaa akawekewa mkataba wa miaka 4
 
Hakuna kitu Rudiger anachomzidi Lindelof,,ukaachana na urefu na aggresiveness isiyokuwa na maana
Rudiger nachomkubali ni umakini wakati wa kulinda lango na uwezo wake kwenye kumalizana na Forward anaekokota mpira kwenda kufunga
 
Wote waliongezwa mkataba, Jones na Smalling Mkuu

Ila Jones alipaswa kuwa wa kwanza kutolewa kabla ya Smalling (Itakuwa wateja wamekosekana)

Nadhani Rojo haondoki sababu ya cover ya left back na kati sio mnajua Shaw ana miguu ya glass
Rojo alitaka kuondoka na Everton walikuwa interested United wakablock deal,kama angepata timu nje ya England wangemuachia
 
Rojo alitaka kuondoka na Everton walikuwa interested United wakablock deal,kama angepata timu nje ya England wangemuachia
Everton walikuwa wanamtaka kwa mkopo, na United walikuwa wanataka kumtemana naye moja kwa moja

Japo uturuki huko wanamtaka, kwa sasa ni ngumu kumuondoa kutokana na hali ya kikosi
 
Kwa uzembe wa timu yetu unaweza kukuta tunacharazwa hapo na hizo timu maana wakina gomes watapata namba hapo sasa huyo astana na az alkmaar wapo vizur si wabovu
Mkuu Radika umekata tamaa kabisa na timu yako dah.
 
-Uingereza lingard toka apate namba man u anaitwa, na sio tu kuitwa anacheza,
-van Gaal alikuwa anamkubali Sana
-mourinho alikuwa anamkubali sana
-ole pia anamkubali Sana

Kama walimu 4 tofauti kila mmoja anamuona Ni mchezaji mzuri kuanza Kuna Jambo pengine hujaliona


Nakubali Lingard sio top player Ila usi mu underestimate jamaa ana skills za kipekee, na attribute yake kubwa Ni off the ball, akiwa Hana mpira Ni hatari zaidi kuliko akiwa na mpira.
Hata Lingard unamtetea?

Tena kwa hoja dhaifu hivi?
 
Kwa watazamaji tu wa mpira hii ni ngumu sana kuielewa, lakini kwa wale wapenzi wa soka wanaoangalia soka kwa jicho la 3 wanaielewa vizuri hii

Ngoja nijaribu kukuelewesha

Miaka ya nyuma mchango wa mchezaji especially mchezaji wa mbele ulikuwa unaangaliwa zaidi pale mchezaji alipokuwa na mpira (hapa tunaongelea ku dribble, kutoa pasi, kufunga na kadhalika)

Miaka ya hivi karibuni Baada ya mpira kuwa na ufundi mwingi (hapa naongelea tactics na sio technics) movement za Wachezaji bila mpira zikaonekana ni muhimu kama zilivyo movement za mchezaji akiwa na mpira

Tunaposema mchango wa mchezaji bila mpira, hapa tunaongelea movement za mchezaji, sio kusimama sehemu moja kusubiri upewe pasi, kukimbia huku na kule ili umpe options nyingi mtoa pasi (Teamate wako mwenye mpira kwa wakati huo), kukimbia huku na kule ili uwachanganye mabeki wasijue wamkabe nani maana wakikufuata wewe pasi anapewa mchezaji mwingine na wakimkaba mwingine pasi unapewa wewe unafunga. Hapa ninaongelea timu kuwa DYNAMIC na sio PREDICTABLE.

Pia movement bila mpira inahusisha kukaba/pressing kuanzia juu/kwa wapinzani ambapo hii kazi sio kila mchezaji duniani anaiweza. Lakini movement bila mpira, kama umewahi kucheza mpira wa basketi utanielewa zaidi, unakuta mchezaji anakaa Njiani kimakusudi ili beki asipite kuzuia, na hii mbinu inatumiwa sana na Barca na City kwa sasa (mfano rahisi ni kama kona zinapopigwa halafu foward anakaa mbele ya kipa, sasa hii ipo hata mchezo unapoendelea katikati ya uwanjani) .

Tukirudi kwa Jesse, changamoto aliyonayo ni kutochangia sana timu yake ikiwa na mpira na kwenye hili anapaswa kurekebisha lakini kuna kazi kubwa sana anayoifanya bila mpira

Nicheke tena na mimi Mkuu
Hana impact yeyote.

Angekuwa na impact angeleta matokeo uwanjani.

Huko kukimbia hata mi naweza.
 
Kwa uzembe wa timu yetu unaweza kukuta tunacharazwa hapo na hizo timu maana wakina gomes watapata namba hapo sasa huyo astana na az alkmaar wapo vizur si wabovu
Timu yetu haina uhakika wa ushindi inapocheza na timu yoyote ile,hamna cha timu ndogo wala kubwa.

Tukikutana na timu inayozuia sana basi ni sare tunaambulia, hakuna mbinu ya kupata ushindi kwa kupenya ukuta.

Tukitangulia kufungwa basi hapo ni sare au kufungwa.
 
Hata Lingard unamtetea?

Tena kwa hoja dhaifu hivi?
Kucheza chini ya makocha wa 4 na wote wakakuchagua uwe kikosi Cha kwanza Ni hoja dhaifu?

maybe mtuambie nyie kwanini Hawa makocha wanapiga benchi wachezaji wengi tu kwa ajili yake? Tena world cup ndio kabisaa piga ua anacheza
 
Sikatai cheif,ila mchezaji wa kaliba yake lazima awe na mchango kwenye team kama sio ku score basi ku assisst,sasa yeye mara ya mwisho kufunga àu kuassist ilikua Dec 2018 akifunga goli 3 kwa style hiyo unadhani anafaa kuendelea kuanza au kucheza kisa tu amekubalika na walimu wote wa 4 ikiwemo UK?enzi za SAF haikua rahisi play maker kucheza miezi 8 bila kuscore wala kuassist ndo maana hata kina Ole walikua wanatokea sub na rating zao zilikua nzuri haipiti mechi 5 bila kuscore au kuassisst.Lingard ukitoa MU hakuna team nyingine kati ya big 6 anayoweza ruhusiwa kufanya hata mazoezi. Angalia Leicester kuna Maddison,City kuna Bruyne,etc..Lingard ni mchezaji wa hovyo kuwahi kucheza MU bora hata Obertain
Ukirudi misimu 10 nyuma tulikuwa na number 10 bora kuliko Lingard. Na mchango wao uwanjani unaonekana.

Sio huyo Lingard wa kumuangalia kwa jicho la 3.

Hovyo kabisa.
 
Kuna kipindi(miaka ya 2011 mpaka 2013) mimi na kaka yangu tulikuwa tunachukia kweli kweli tukiona jina la Michael Carrick miongoni mwa watakaocheza siku hiyo. Ajabu hata baada ya sir Alex kustaafu, bado alichezeshwa na makocha waliofuata. Nilikuja kuona umhimu wake alipoumia.
Ndio ndio.

Mimi Mwanzoni nilikuwa simpi umhimu sana Pamoja na Milonjo miguu ya kwale Fletcher.


Fletcher nilikuwa simkubali yeye mpaka anaoondoka sijawahi kupenda uchezaji wake.
 
Virgil Van Dijk was the most expensive defender last year and won the UEFA mens player of the year award!

Over to you Harry Maguire.
Mr. P & Mr.J----Awards.

Mr. P "Hawa Mabwana wamechukua Zawadi sana,Wametawala sana,kila siku wao tu,Tumewachoka sasa.Tunataka sura Mpya"

Mr.J "Lakini kwa sasa sioni Mtu wakuwavuta shati,Naona Mtu Mita kumi kurudi nyuma,kama wanauwezo wapewe hata Miaka 20"

Mr.P " Hawana jipya saizi,yote Marudio,Wakae pembeni,Hapa tunataka sura mpya..Over."

Mr.J "Basi na iwe hivyo..Over"




"I love Football"
 
Back
Top Bottom