Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Nina uhakika Lingard kwa sasa anakula bakora nyingi kwa kuwa timu haipati matokeo mazuri

Nina uhakika timu ikijakupata matokea Lingard ataonekana kama Iniesta wa Man Utd

Na kupata matokeo mazuri yanasababishwa na timu nzima kucheza vizuri

Nina uhakika Man City ingekuwa haipati matokeo kuna wachezaji tungewaona wa kawaida sana (akina Zichenko, akina Otamendi, akina Rodri labda abadilike mbele ya safari)

Kwa sasa kuna vitu naona Lingard inabidi aongeze ili a improve game yake, lakini haimaanishi ni mbovu kama watu wanavyomsemasema

Nina uhakika matokeo ya mechi zilizopita yametu dis appoint sana, lakini pia nina uhakika kuna mambo madogo madogo ambayo yangetokea/yasingetokea kwenye mechi zilizopita hasa ya Cristal Palace leo hii tungekuwa tunaongea mengine

Martial kuangushwa na Garry Cahil kwenye penalt box, ingetolewa penati na Garry Cahil angepewa kadi ya pili ya njano sidhani kama matokeo yangekuwa yale tuliyopata

Rashford kukosa penalt. Ni jambo linalotokea kwenye soka mchezaji kukosa penalt lakini ni nafasi rahisi ya kufunga kuliko nafasi nyingine yoyote uwanjani hivyo Rashford angetumia nafasi ile leo tungeongea mambo mengine

Martial kuumia dakika za mwishoni na kufanya United inayohitaji goli la kuongeza kubaki na watu 9 uwanjani

Kuna watu watasema ndio mpira ulivyo, nakubaliana nao. Lakini kwa mechi iliyopita ni kwamba hatukuwa na bahati na si kuzidiwa kiwango
Bila kusahau Kuna Var ambayo wanatuaminisha ingesolve haya mambo, Mfano Kama hii Cahil Ni last man yupo yeye na martial tu, martial anaenda kufunga akamchezea foul, hii Ni clear red card Sheria IPO wazi na vidic ashakula red za aina hii nyingi against Torres Ila refa sijui katoa maamuzi yake wapi na kutoa yellow.

 
Europa League sucks,,bigtime

Sijui ni lini tutarudi level zetu..
 
Kwa Namna ambavyo Lukaku, Snchezi, Smallling, Darmian, Herreira Fellaini ambavyo wamefanikiwa kuondoka na kuingia kwa Bissaka, Maguire, Chong Tunzebe and Mensah plus other academy Players tunahitaji two years ili kuja kuwa na team ya ushindani.
Alichofanya Ole ni sahihi as long as Club na Management hawatakuwa na haraka ya matokeo, Ameanza kuitengeneza team Upya kwa aina ya Mchezo na Falsafa ya Manchester United.
Kwa kikosi kilichobakia United the highest paid player ni Pogba so tusitegemee tena kuona mchezaj atakaesajiliwa kuzid hapo kwa sasa.
Tukubaliane na matokeo ya msimu huu ila hiki kizaz cha kina Bissaka Maguire Pogba James Chong and Rashford in the next three seasons kitakuwa Bora na cha ushindani sana.
 
Huyo Roma
smalling.jpg
 
Nilichogundua solskjaer kamtoa sanchez kinguvu jezi namba 7 iwe wazi ipate mtu sahihi hii inaitwa safishasafisha kwa sababu tunaupungufu wa ushambuliz lakin bado kakomaa jamaa asepe
Hajamtoa kinguvu Sanchez hastahili kubaki epl his time is over
 
Nilichogundua solskjaer kamtoa sanchez kinguvu jezi namba 7 iwe wazi ipate mtu sahihi hii inaitwa safishasafisha kwa sababu tunaupungufu wa ushambuliz lakin bado kakomaa jamaa asepe
Kwahiyo huyo No saba anakuja lini??
 
So Smalling is a deadwood but Phil Jones is not right?
Ninaamini kwa mabeki waliokuwepo, Smalling ni beki namba 4 kwa ubora baada ya Maquire, Lindelof na Axel. Baily majeruhi yanam cost na hana consistence, huwezi kumtegemea.

Nadhani anaondoka yeye kwa kuwa hao wengine wamekosa wanunuaji
 
So Smalling is a deadwood but Phil Jones is not right?
Huyo Jones umeshamuona hata benchi? Tuanzebe Ni wa tatu, ikiwa lindelof ama Maguire ameumia Dogo ndio atachukua nafasi. Na ole ameshasema Rojo hauzwi, inamaana pengine Jones akawa hata Ni wa 5 kwenye chaguzi.
 
Kwakuwa Shaw ameumia ili kuondokana na Young,hakuna haja ya kubadili mfumo timu ikacheza na walinzi watatu nyuma?

Nawaza tu wakuu.
 
Ninaamini kwa mabeki waliokuwepo, Smalling ni beki namba 4 kwa ubora baada ya Maquire, Lindelof na Axel. Baily majeruhi yanam cost na hana consistence, huwezi kumtegemea.

Nadhani anaondoka yeye kwa kuwa hao wengine wamekosa wanunuaji
Walimuongeza mkataba Jones wakaacha kumuongeza Smalling ambaye hana injury record lakini pia ni experienced kuliko huyo Axel na Baily
 
Back
Top Bottom