
ZABURI 68
19 Na ahimidiwe BWANA ,siku kwa siku hutuchukulia mzigo wetu;MUNGU ndiye wokovu wetu.

MUNGU ndiye kila kitu,ukitambua hili utatenda mema.

MUNGU wetu anatupenda,ni WOKOVU wetu,ni MWANGA wa maisha yetu

Tumtumikie,Tumfuate,Tumuombe,Tumshukuru yeye siku zote.
TUOMBE:
Mtakatifu,Mtakatifu,Mtakatifu BWANA MUNGU mwenye enzi,asante kwa kutufikisha siku ya alhamisi ya leo,wapo wengi waliotamani kuiona siku ya leo hawajaweza.
Tunajitakasa mbele yako Mungu wetu tukiomba usikumbuke uovu wetu wote,tusamehe Baba makosa yetu yote.
Asubuhi ya leo pamoja na nia zetu mbalimbali tunaombea

Mipango yetu yote.

Wagonjwa,wasafiri,wanafunzi wote hasa kidato cha sita waongoze katika mitihani yao.

Vijana wote walinde katika maisha ya ujanani ,wapate Elimu sahihi,kazi,mitaji,malezi,wake/waume,ushauri,Amani

Kusudi la maisha yetu.

Wafiwa wote wafariji.

Marehemu wote Raha ya milele uwape Ee BWANA,Mwanga wa milele uwaangazie ,wapumzike kwa Amani,Amen
Tunaomba haya yote katika jina la Yesu Kristo Amina.
MUWE NA SIKU NJEMA,MBARIKIWE