Makapuku Forum

Makapuku Forum

ZABURI 68

19 Na ahimidiwe BWANA ,siku kwa siku hutuchukulia mzigo wetu;MUNGU ndiye wokovu wetu.

MUNGU ndiye kila kitu,ukitambua hili utatenda mema.

MUNGU wetu anatupenda,ni WOKOVU wetu,ni MWANGA wa maisha yetu
Tumtumikie,Tumfuate,Tumuombe,Tumshukuru yeye siku zote.

TUOMBE:

Mtakatifu,Mtakatifu,Mtakatifu BWANA MUNGU mwenye enzi,asante kwa kutufikisha siku ya alhamisi ya leo,wapo wengi waliotamani kuiona siku ya leo hawajaweza.

Tunajitakasa mbele yako Mungu wetu tukiomba usikumbuke uovu wetu wote,tusamehe Baba makosa yetu yote.

Asubuhi ya leo pamoja na nia zetu mbalimbali tunaombea

Mipango yetu yote.

Wagonjwa,wasafiri,wanafunzi wote hasa kidato cha sita waongoze katika mitihani yao.

Vijana wote walinde katika maisha ya ujanani ,wapate Elimu sahihi,kazi,mitaji,malezi,wake/waume,ushauri,Amani

Kusudi la maisha yetu.

Wafiwa wote wafariji.

Marehemu wote Raha ya milele uwape Ee BWANA,Mwanga wa milele uwaangazie ,wapumzike kwa Amani,Amen


Tunaomba haya yote katika jina la Yesu Kristo Amina.

MUWE NA SIKU NJEMA,MBARIKIWE
Amen mama mchungaji

Ubarikiwe sana
 
NUKUU YA LEO

Movies are a fad. Audiences really want to see live actors on a stage.

Sinema ni mtindo, Watazamaji wanataka kuwaona wahusika moja kwa moja kwenye jukwaani.

Haya maneno yalipatwa kusemwa na mchekeshaji na mcheza filamu wa kiingereza Charles Spencer Chaplin maarufu kama Charlie Chaplin. Charlie alizaliwa 16 April 1889 katika viunga vya walworth kusini kwa jiji la london.

Charlie alizaliwa katika familia maskini na waliishi katika maeneo duni, wazazi wake walikuwa wote ni waburudishaji kwenye kumbi za miziki, baadaye wazazi waliachana na hapo ndio ikawa chachu ya charlie kuanza kuigiza kwenye majukwaa ya watoto akiwa na umri wa miaka 5 tuu.

Baadaye mama yake alifariki na ikabidi charlie akaishi marekani na kuanza kutengeneza filamu silent filming. alitengeneza kazi nyingi na kufungua kampuni yake binafsi, wakati huo alishakuwa star wa dunia tayari.

Charlie aliwahiwa kufukuzwa marekani baada ya uchunguzi wa FBI kugundua alioa wanawake wadogo sana na mtazamo wake wakupenda siasa za kikomunisti. Baada ya hapo Charlie aliienda kuishi Switzerland hadi mauti yalipomfika kwa ugonjwa wa kupooza.

Charlie aliacha watoto 11 aliozaa na wanawake 4, Bado hadi leo filamu zake zinauza na amebaki kuwa mchekeshaji mkubwa ambae alikuwa haongei. kwanza yeye mwenyewe ukimuona tayari unacheka tuu.

Nukuu ya leo, jamaa alitaka watu wapige live, leo hii ndio tunaita stand up comedy ya kina Mc pilipili, annie kaasiime na eric omondi.


Hatari sana

Rest in peace my model
 
Tongotongo la Asubuhi
6020ad62cfb9c43fa61357978fec6d5b.jpg

Simba mpanda miti
Sina hii ya Simba wanapatikana Tanzania pekee
Sasa mtu unaenda mbugani ukijua simba ujifovha tu kwenye nyasi hivyo kutembea kwa mavhale kumbe mnyama yupo juu ya mti anakuchora tu
Asubuhi njema
.......
Na wanapatikana mbuga moja tu nchini
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom