Makapuku Forum

Makapuku Forum

Ulipotelea wapi jamani? Dada anakutafuta🫣
...mimi wa kupotea unadhani!!! Nilisahau tu njia, nikajikuta nimepoteza simu na line ikauzwa na yule wakala anayetembea kabeba kispika kama cha adhana. Hapa nahangaika kurudisha namba yangu ile ile.
Dadaako hajanitafuta maana hadi SLP langu analijua, kabanwa tu na utawala binafsi
 
...mimi wa kupotea unadhani!!! Nilisahau tu njia, nikajikuta nimepoteza simu na line ikauzwa na yule wakala anayetembea kabeba kispika kama cha adhana. Hapa nahangaika kurudisha namba yangu ile ile.
Dadaako hajanitafuta maana hadi SLP langu analijua, kabanwa tu na utawala binafsi
Makiwendo Mungu anakuona.
 
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam, Jumanne Muliro ametangaza kuanza kwa operesheni maalumu dhidi ya Makundi ya matapeli wanaojihusisha na vitendo vya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu, akisema Jeshi la Polisi limetangaza “kiama cha kisheria” dhidi yao.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Agosti 4, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Central Police Jijini Dar es salaam, SACP Muliro amesema matapeli hao hutumia mbinu mbalimbali kuwalaghai Wananchi, ikiwemo kujifanya Wafanyabiashara wa madini, Wauzaji wa magari na viwanja, Wanunuzi wa mazao kama korosho na dengu, pamoja na watoa huduma za usafirishaji wa mizigo, kisha kutoweka baada ya kupokea fedha kutoka kwa waathirika.

Amesema Jeshi la Polisi limeendelea kupokea malalamiko kutoka maeneo mbalimbali Nchini, yakiwemo Newala, Kibondo, Kasulu na Mbinga kuhusu Wananchi waliopoteza fedha kupitia udanganyifu huo.

Kutokana na hali hiyo, Muliro amesema operesheni hiyo itaendelea hadi Watuhumiwa wote watakapobainika na kufikishwa kwenye Vyombo vya Sheria, akisisitiza kuwa Jeshi la Polisi halitavumilia vitendo vinavyowaumiza wananchi na kuhatarisha usalama wa uchumi.

Aidha, ametoa wito kwa Wananchi kuendelea kutoa taarifa kuhusu viashiria vya uhalifu ili kusaidia kuzuia na kudhibiti matukio ya kihalifu kabla hayajatokea.
Screenshot_20260804_155909_InstaPro%20.jpg
 
Mtu mmoja ambaye bado hajatambulika anayedaiwa kuwa Mkazi wa Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha, amefariki dunia asubuhi ya leo Agosti 4, 2026 baada ya kuanguka katika choo cha umma kilichopo Stendi Ndogo Jijini Arusha.

Kwa mujibu wa Mashuhuda, marehemu aliwasili stendi hiyo akitokea Dar es salaam na alikuwa akijiandaa kupanda daladala kuelekea Monduli ambapo inadaiwa aliacha mzigo wake ndani ya daladala kabla ya kuelekea chooni.

Mashuhuda wamesema Mwanaume huyo alionekana kuwa katika hali mbaya kiafya na alikuwa akitembea kwa shida, hivyo alisaidiwa kwa kupewa fimbo ili afike chooni na baada ya kuingia, alikaa kwa muda mrefu bila kutoka jambo lililowatia wasiwasi Watu waliokuwa eneo hilo.

Mhudumu wa choo hicho amesema alipofungua mlango alimkuta Mwanaume huyo akiwa ameinama ambapo alijaribu kumtoa nje ili apatiwe msaada, lakini muda mfupi baadaye alianguka na kufariki dunia.

Jeshi la Polisi limefika eneo la tukio na kuuchukua mwili kwa ajili ya kuhifadhi katika chumba cha kuhifadhia maiti, huku uchunguzi ukiendelea kubaini chanzo cha kifo hicho.
Screenshot_20260804_160148_InstaPro%20.jpg
 
Klabu ya Simba imetangaza kusimamisha kwa muda masuala yote yaliyokuwa yakiendelea kuhusu Baraza la Wadhamini, kufuatia uamuzi uliofikiwa katika kikao cha Bodi ya Wakurugenzi kilichofanyika Agosti 3, 2026.

Kupitia taarifa iliyotolewa leo Agosti 4, 2026 Bodi imeeleza kuwa imeamua kusimamisha matukio yote yaliyotokea awali kuhusiana na Baraza la Wadhamini hadi itakapotolewa taarifa nyingine.

Katika kipindi hicho, Bodi imesema itaelekeza nguvu zake katika masuala muhimu yanayohusu klabu, ikiwemo mchakato wa usajili wa Wachezaji, maandalizi ya Simba Day, mchezo wa Ngao ya Jamii pamoja na maandalizi ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwa msimu ujao.

Aidha, Bodi imewasihi Wanachama na wapenzi wa Simba kuendelea kuiunga mkono klabu hiyo ili kuhakikisha inapata mafanikio makubwa katika msimu unaotarajiwa kuanza hivi karibuni.

Taarifa hiyo imesainiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Simba, Crescentius Magori pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Bodi, Murtaza Mangungu.
Screenshot_20260804_160335_InstaPro%20.jpg
Screenshot_20260804_160403_InstaPro%20.jpg
 
Baadhi ya abiria wanaotumia mabasi ya umeme Zanzibar wameiomba Mamlaka inayosimamia huduma hiyo kupitia upya kiwango cha kiyoyozi (AC), wakidai kuwa baridi yake ni kali kupita kiasi.

Malalamiko hayo yamekuja sambamba na kero nyingine ya kusubiri mabasi kwa muda mrefu, ikiwa ni siku chache tangu Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ianze rasmi kutoa huduma ya usafiri huo wa mabasi ya umeme.

Ayo TV imetembelea Kituo cha Mabasi cha Kijangwani na kuzungumza na watumiaji wa huduma hiyo. Baadhi ya abiria wamesema AC ni kali mno, huku wengine wakieleza kuwa hali hiyo ni ya kawaida na ni sehemu ya ubora wa mabasi hayo mapya. Aidha, wengi wameeleza kuwa changamoto kubwa kwa sasa ni uchelewaji wa mabasi na upatikanaji wa kadi za usafiri.

Akizungumzia malalamiko hayo, Mkurugenzi wa ZSSF, Nassor Shaaban, amekiri kuwepo kwa uchelewaji wa mabasi katika baadhi ya vituo, akieleza kuwa huduma inaendeshwa kwa ratiba maalum ya muda. Pia amesema uhaba wa kadi umetokana na baadhi ya mawakala kuuza kadi nje ya maeneo yanayohudumiwa kwa sasa, jambo lililosababisha upungufu wa kadi katika vituo vinavyotumika na mabasi hayo.
Screenshot_20260804_160517_InstaPro%20.jpg
 
Mkazi wa Sinza, Dar es Salaam, Janeth Ndimbo (30), amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashtaka nane ya usafirishaji haramu wa binadamu.

Mshitakiwa huyo anadaiwa kuwaajiri wanawake kwa ahadi ya kuwapatia kazi nje ya nchi kisha kuwasafirisha kwenda China kwa lengo la kunyanyaswa kingono.
Screenshot_20260804_160848_InstaPro%20.jpg
 
Hali ya kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye (70) ni dhaifu na hawezi kuzungumza, mkewe Winnie Byanyima ameeleza.

Besigye, ambaye amewekwa chini ya uangalizi maalum tangu Julai 30 mwaka huu alipoanguka mahakamani wakati wa kesi yake, amekuwa kizuizini tangu mwishoni mwa mwaka 2024.
Screenshot_20260804_161057_InstaPro%20.jpg
 
Back
Top Bottom