Namshakende
JF-Expert Member
- Sep 23, 2021
- 844
- 2,184
Habari za jioni wana-JF,
Nimeona nije hapa jukwaani kuandika haya machache, huenda kuna wanaopitia hali kama yangu au waliowahi kuivuka wakashare nami namna ya kukabiliana nayo.
Mimi ni mtu ninayependa sana kuwa busy na majukumu yangu. Kipindi cha nyuma, nilikuwa na vitu vingi vilivyonipa burudani na kunichangamsha; nilikuwa mpenzi mkubwa wa kusikiliza Music [emoji444], kuangalia filamu, na hata kutoka mara moja moja. Upande wa pombe nilishaamua kuacha kabisa huko nyuma.
Hata hivyo, siku hizi mambo yamebadilika kabisa. Kila Ijumaa inapoingia , kwangu inakuwa ni mwanzo wa stress na boredom ya hali ya juu.
Yale mambo yote yaliyokuwa yananipa furaha mwanzo (muziki, muvi, mitoko) sasa hivi vimepoteza ladha kabisa, nikijaribu kuvifanya nahisi upweke na muda hauendi.
Hata upande wa mahusiano umekuwa na changamoto sana, kwani imekuwa ngumu kukutana na watu wenye uelewa na ukomavu wa akili unaoenda sawa na mimi.
Kimbilio langu pekee limebaki kwenye kazi. Hamu yangu kubwa kila weekend inakuwa ni kutamani Jumatatu ifike haraka ili nirudi kwenye majukumu yangu ya kila siku, kwa sababu huko ndiko akili yangu inapotulia.
Nimeona nije hapa jukwaani kuandika haya machache, huenda kuna wanaopitia hali kama yangu au waliowahi kuivuka wakashare nami namna ya kukabiliana nayo.
Mimi ni mtu ninayependa sana kuwa busy na majukumu yangu. Kipindi cha nyuma, nilikuwa na vitu vingi vilivyonipa burudani na kunichangamsha; nilikuwa mpenzi mkubwa wa kusikiliza Music [emoji444], kuangalia filamu, na hata kutoka mara moja moja. Upande wa pombe nilishaamua kuacha kabisa huko nyuma.
Hata hivyo, siku hizi mambo yamebadilika kabisa. Kila Ijumaa inapoingia , kwangu inakuwa ni mwanzo wa stress na boredom ya hali ya juu.
Yale mambo yote yaliyokuwa yananipa furaha mwanzo (muziki, muvi, mitoko) sasa hivi vimepoteza ladha kabisa, nikijaribu kuvifanya nahisi upweke na muda hauendi.
Hata upande wa mahusiano umekuwa na changamoto sana, kwani imekuwa ngumu kukutana na watu wenye uelewa na ukomavu wa akili unaoenda sawa na mimi.
Kimbilio langu pekee limebaki kwenye kazi. Hamu yangu kubwa kila weekend inakuwa ni kutamani Jumatatu ifike haraka ili nirudi kwenye majukumu yangu ya kila siku, kwa sababu huko ndiko akili yangu inapotulia.