Makapuku Forum

Makapuku Forum

Baada ya siku ya bia duniani..

TBL washusha bei ya ndovu..

13250077c105d29b53703da83bc34e79.jpg
Bahati mbaya sana sio mpenzi
 
1/Jesus of Nazareth
d9d86d3ed6278d2a11070d1b0969b3a9.jpg
38a9dc4e18ee78686fd323669b3e09b1.jpg
c482c60eb9f0cfab52596f0fcb22b990.jpg

Aliishi kati ya mwaka 5BC hadi 28 AD Ila wafuasi wake bado wanaamini yupo hai mbinguni sasa sijui kama keshazeeka au lah
Alizaliwa na Bikira Maria kwa uwezo wa Roho Mtakatifu {kama wewe unahisi alizaliwa kama wewe ilivyotokea kwa wazazi wako mimi sijasema hivyo)
Pamoja na kuishi bila shari na mtu akasalitiwa na bwana Yuda Eskariote na wenzake wachache kisha Pilato akavuta mlungula na kutoa hukumu ya kidwanzi halafu akasulubiwa akafa kisha akapaa mbinguni
Hivyo ukisalitiwa na rafiki/ndugu/mpenzi wako usiwaze sana kumbuka hata Yesu yalimkuta pamoja na kufanya mazuri kwa 100%
Ameandikwa kwenye vitabu visivyo na idadi

Anatafutwa X 25,000,000 na ushee kwa mwezi

.
.
.
.
.

.
.
Samahani kwa niliowakwaza kwa mada ya leo najua nimekorofisha imani za wstu maana ilikuwa hakuna namna
.
.
.
Shukrani kwa mliosapoti mada
Tukutane kesho
Niwatakie Usiku Mwema
Mwisho
........
Tuko pamoja mkuu
 
Ee Mungu wa sifa zangu usinyamaze
Kwa maana wamenifumbulia kinywa, kinywa cha mtu asiye haki, cha hila wamesema nami kwa ulimi wa uongo

Naam kwa maneno ya chuki wamenizunguka, wamepigana nami bure

ZABURI 109:1-3

Muwe na usiku mwema mlindwe na damu ya Yesu
 
Kiumbe pekee ambaye tunaelezwa hakuzaliwa kupitia mbegu za mwanaume

Hakika Mungu ni muweza wa yote

Baadhi ya maandiko husema

Alifanya miujiza mingi sana na ya kushangaza ambayo haijapata kufanywa na yeyote toka dunia iumbwe
Hakika
 
Muziki: Usiku wa Manane

Sijui kama ni sahihi kuanza kusalimia muda huu, maana utaianzaje salamu sasa wakati hata mwenyewe baada ya nukta tu nitalala. Well, nikutakie usiku mwema. Unajua nafasi yako hapa jukwaani haiwezi kulinganishwa na chochote. KF ni sehemu nzuri kwa kuwa wewe ni sehemu yake.

Utakuwa umenote kitu, mahudhurio yangu wiki jana na hii yamekuwa down sana, ni kwa sababu , kama ni mpira basi timu yangu inashambuliwa na refa kapoteza kipyenga linesmen virungu vimeloa kwa hiyo inabidi hadi kipa akabe.

Kifupi nimetingwa na nikamuomba shululu aweke muziki au member yeyote ambaye ataweka kwenye mida segment ya muziki inapoanza baada ya 10 kubwa. Shululu umekuwa kimya hebu mawasiliano yako. Niwashukuru lee empire mjomba wangu huyu, Jimena kwa historia, Nyagei kwa sports, Shunie kwa neno na sala, husna muba kwa hadithi na maarifa kwa ufupi bila kumsahau Bitoz

Ninyi watu Tumosa ninakuangalia tu, maana kutokuwemo humu sio kwamba sisome fitna zote, ha ahahhaah, dumejeuri asante kwa kulichangamsha jukwaa, mzeewakungoa asante mdau, makaveli10 , Madame S , BlessedHope , Transcend , Mondray , dingimtoto , demi , Curious gal na wewe ambaye sijakutaja maana usiku umeenda, ni jambo zuri kuwa hapa

 
Muziki: Usiku wa Manane

Sijui kama ni sahihi kuanza kusalimia muda huu, maana utaianzaje salamu sasa wakati hata mwenyewe baada ya nukta tu nitalala. Well, nikutakie usiku mwema. Unajua nafasi yako hapa jukwaani haiwezi kulinganishwa na chochote. KF ni sehemu nzuri kwa kuwa wewe ni sehemu yake.

Utakuwa umenote kitu, mahudhurio yangu wiki jana na hii yamekuwa down sana, ni kwa sababu , kama ni mpira basi timu yangu inashambuliwa na refa kapoteza kipyenga linesmen virungu vimeloa kwa hiyo inabidi hadi kipa akabe.

Kifupi nimetingwa na nikamuomba shululu aweke muziki au member yeyote ambaye ataweka kwenye mida segment ya muziki inapoanza baada ya 10 kubwa. Shululu umekuwa kimya hebu mawasiliano yako. Niwashukuru lee empire mjomba wangu huyu, Jimena kwa historia, Nyagei kwa sports, Shunie kwa neno na sala, husna muba kwa hadithi na maarifa kwa ufupi bila kumsahau Bitoz

Ninyi watu Tumosa ninakuangalia tu, maana kutokuwemo humu sio kwamba sisome fitna zote, ha ahahhaah, dumejeuri asante kwa kulichangamsha jukwaa, mzeewakungoa asante mdau, makaveli10 , Madame S , BlessedHope , Transcend , Mondray , dingimtoto , demi , Curious gal na wewe ambaye sijakutaja maana usiku umeenda, ni jambo zuri kuwa hapa


Ahsante kwa muziki mzuri mtaasisi
 
Wale wa simulizi ...chini ya udhamini wa my sweetheart kipenda roho mpendwa wa lee ...twende sawa

Alitamani kumuuliza kitu palepale lakini ulimi wake ulikuwa mzito na kubaki kimya lakini akilini tayari ilikuja picha ya mwanamke aliyewahi kumpenda miaka mingi.
Picha ya mwanamke aliyemuamini kupita kiasi.
Picha ya mwanamke aliyeweka doa katika historia ya maisha yake mpaka kufikia pale alipo.
Picha ya mwanamke huyo iliyomjia akilini haikuwa picha ya mwanamke yeyote mwengine bali ni picha ya Zainabu.
Mwanamke aliyeuteka moyo wa Hussein na kumuonesha mapenzi ya dhati yaliyomfanya awali Hussein ajione yeye ndie mwanaume bora kuliko wote lakini mwisho wa siku mwanamke huyo ndie aliyekuja kutoa kauli iliyomfanya Hussein miaka yote abaki na imani kuwa wanawake ni wauaji.
Alimtazama mama Shebby mke wa mzee Mwinchande na kwenye macho yake aliweza kuiona taswiera ya Zai wake aliyesingiziwa alimuua mwenyewe sambamba na mtoto wao wa kiume ambae aliushuhudia mwili wake ukiwa umekatwa kichwa na viganja ambavyo vilikutwa mifukoni mwake.
Lakini hata hivyo aliamua kulipotezea lile wazo kichwani na kumuomba Mungu kimoyo moyo amuondolee akili ya kumuwaza sana Zai kwani kuna muda aliamini kabisa Zai amekufa lakini kuna muda pia hakuamini na alihisi kuwa Zai hajafa ila waliyemuulia pale ni mtoto wake kipenzi aliyekuwa na miezi mmne tu.
Lakini japo alijitahidi kupotezea bado kuna vitu akiviona kwa yule mama ambae yeye hakuonesha kumjua Hussein hapo kabla hata kidogo, vilimfanya amkumbuke sana Zai mke wake na kitu kikubwa kwanza ni uvaaji wa Kiremba.
Jinsi ambavyo alikuwa akimtazama mama Shebby ule ufungaji wake kiremba cha kitenge ulimfanya pia amkumbuke sana Zai ambae nae alipenda sana kufunga kiremba tena kwa mtindo wa kipekee ambao wengi walikuwa hawafungi vile na ajabu mtindo ule wa mkewe Zai kwa mara nyengine aliukuta kwa mama Shaaban.
Kitu cha pili kusoma (kuimba) qaswida hasa nyakati za asubuhi.
Hili nalo aliligundua kwa mama Shebby siku hiyo asubuhi alipoonana nae tena na kumshangaa kupita kiasi alikuwa anatembea huku akiimba qaswida jambo ambalo hata mkewe Zai ndio alikuwa analipenda sana.
Lakini mbali na sababu hizo pia kulikuwa na sababu nyengine akizifikiria zinamkatalia kuwa mama Shebby si Zai na moja ya sababu hizo ni umri wa Shebby ambae uliandikwa kwenye daftari maalum siku wanafungishwa ndoa kuwa Asha alikuwa na miaka 29 anakaribia 30 jambo ambalo lilikuwa sahihi kabisa kwani alipokuwa anapelekwa jera baada ya kuhukumiwa barua ya mchumbaake wa zamani Mariam ilionesha kuwa tayari Asha ana miaka mitatu na yeye amekaa miaka 26 gerezani.
Lakini kwa upande wa Kamishna Shebby yeye umri wake ulionesha ni miaka 28 jambo ambalo lilikuwa tofauti kabisa kwani miaka hiyo 28 ndio kwanza alionana na Zai Arusha na hakuwa na mtoto wala hata alivyokutana nae mwaka uliofuata baada ya kushinda mitihani aliyopewa na Zai alimkuta ni bikra yaani yeye ndie alikuwa mwanaume wake wa kwanza kwa hiyo aliamini wazi kuwa Zai hakuwahi kuwa na mtoto mwenye umri mkubwa kama Shebby kwani mtoto wao kipenzi wa pekee aliyezaa na Zai alichojua aliuawa miaka 26 iliyopita.
Kwa kigezo cha umri wa Shebby kilimuondoa kabisa kwenye mashaka ya kumfananisha mamaake Shebby na aliyewahi kuwa mkewe ambae bado hakuwa na uhakika kama alikufa au mzima bi Zainab.

* * * * *

Usiku baada ya sherehe zile kuisha na watu wote kutawanyika alionekana Cj4 ambae alikuja na pikipiki moja iliyomtambulisha kama mpiga picha kutoka ofisi ya wazili wa mambo ya ndani na hata kitambulisho alichokuwa amevaa kilionesha hivyo na kila aliyemuona aliamini hivyo kutokana na kumtambua muhusika wa kile kitambulisho na muonekano wa Cj4 hakuna aliyemtilia hofu hadi wakati anaondoka pale ukumbini.

Safari yake ilimpeleka hadi sehemu moja pembeni ya barabara kulipokuwa na daraja na kusimamisha pikipiki ile nyuma ya gari moja ndogo iliyokuwa imeegeshwa pembeni na kushuka lakini aliachana na ile gari yeye alienda moja kwa moja hadi chini ya barabara uvunguni mwa lile daraja ambalo lilikuwa limekauka maji, na alipotoa simu yake ya mkononi kumulika mule uvunguni alionekana mtu mmoja ambae alifanana nae sana jinsi alivyojiweka, akiwa kafungwa kamba mikono na miguu huku mdomoni kazibwa na plasta kubwa.
"Good mr, kazi imeisha kama nilivyokuahidi siwezi kukudhuru kwa kuwa mimi si mtu m baya ila ukitaka kuujua ubaya wa mtu upoje uende ukatoe siri kuwa aliyekwenda kwenye ile sherehe ya harusi hukuwa wewe."
aliongea Cj4 na kumtoa plasta ile iliyokuwa mdomoni mwa yule jamaa aliyekuwa na kitambi kiasi sambamba na mustachi mkubwa.
Alibakia anahema tu yule bwanakipindi Cj4 akimfungua zile kamba na alipomaliza alimrudishia kitambulisho chake sambamba na funguo ya pikipiki kisha akatoa memory iliyokuwa ndani ya ile kamera na kumkabidhi kamera tupu.
"Zingatia ndugu niliyokwambia"
aliongea Cj4 na kutoka mule darajani huku yule bwana akiwa amesimama haamini hadi pale aliposikia gari ikiwashwa na kuondoka ndipo nae alipotoka mbio kule na kuwasha pikipiki yake na kuondoka.

Baada ya kufika ndani ya chumba chake alichokodi kwenye ile guest Cj4 alianza kubadilisha muonekano wake kwa kuondoa ule mustach wa bandia na kuanza kubambua mfuko wa plastik maalum uliobanwa tumboni mwake na kumuonesha kama aliyekuwa na kitambi cha wastani pindi alipovaa shati ile kubwa sambamba na kikoi.

Mara baada ya kumaliza kupambua vitu vya bandia mwilini mwake ndipo alipotumbukiza ile memory kwenye compyuta yake na kufungua mafaili ya video alizoshoot kwenye ile sherehe ya harusi ya Shebby ndipo kwa umakini mkubwa Cj4 alianza kufatilia matukio na nyuso za watu aliokuwa anawachukua ili kuhakikisha na kubaini kwa mbinu zake za kikomando kati ya wale wageni waliohudhulia pale nani alikuwa Mr X.


Alitulia kwa umakini mkubwa Cj4 kutazama yale matukio yaliyokuwa yanaendelea kipindi cha shughuli ile lakini kadri alivyokuwa anaangalia bado hakuona tofauti kwa mtu yeyote wala kupata taswira nani kati ya wale watu waliokuwepo kwenye ile shughuli ni Mr X?
Aliangalia hadi mwisho bila kumuhisi mtu yeyote aliyeoneka kuwa na utofauti furani ambao ungemsaidia kumtambua mr X na ndipo alipoamua kuianzisha upya safari hii akipunguza speed ya utembeaji wa picha na kueka ule wa taratibu na kiminato (slow motion)
Aliangalia tena kwa umakini mno wakati huo kila hatua aliyoichukua na mwishoe aliimaliza tena hadi mwisho bila kupata picha wala taswira ya kumjua huyo mgeni aliyeamini kuwa lazima atakuwepo kwa kuwa kauli za mr.X zenye mafumbo mazito kwake Cj4 aliweza kuyatatua kiasi yale mafumbo na kujua lazima Mr X atakuwa kwenye mzunguko wa maisha ya Kamishna Shebby iwe katika ngazi ya jeshi la polisi ama kwa marafiki wakuu wa babaake mzazi mzee Mwinchande kutokana nae alikuwa ni moja ya askali wakubwa enzi hizo hivyo alikuwa na mtandao wa karibu na watu wengi ambamo Cj4 aliamini lazima miongoni mwao atakuwa ndie Mr X.

Lakini safari hii alipofika mwisho kuna kitu kimoja alikiona akagundua hakipo sawa.
Hapo ndipo alipoanza kurudisha nyuma na kueka slow motion zaidi vile vipande vya Hussein bubu na kuna kitu akaanza kukibaini na kukitilia shaka.
Ni vile Hussein muda mwingi alionekana alikuwa anamuangalia sana mamaake Kamishna Shebby tena kwa kumuiba iba.
Alikaa vizuri Cj4 na kumzoom Hussein sehemu za macho yake na kugundua kuwa kuna kitu alikuwa anakifikiria ama anakifananisha kwa jinsi alivyokuwa anamtazama mamaake Kamishna Shebby.
("Mh! hapa hapa ndipo pa kuanzia.")
alijiambia akilini Cj4 na kumsogeza kwa karibu mamaake Kamishna Shebby sehemu za uso na kumplay katika slow motion kumchunguza vile alivyokuwa anamuangalia Hussein na hapo napo kuna kitu alikisoma kuwa mama Shebby hakuweza kabisa kumuangalia Hussein hata kwa sekunde kumi, na mara alipogonganisha macho na Hussein aliyakwepesha kiujanja na kugundua sehemu alipoyaelekeza ni upande aliokaa mumewe ambae ni babaake Kamishna Shebby.
"Mh!"
Aliguna Cj4 na sasa alianza kumzoom babaake kamishna Shebby ambae ni mzee Mwinchande lakini kila alivyoitafuta tofauti yoyote kutoka kwa mzee Mwinchande kwa kile alichokiona kwa Hussein na mama Shebby hakuweza kuona chochote kutoka kwa Mwinchande.
Alimueka katika slow motion ile ya chini kabisa lakini muda wote aligundua kuwa mzee Mwinchande alikuwa na furaha na muda mwingi alionekana yuko bussy na kile kilichokuwa kinaendelea ukumbini hususani kuwatzama bibi na bwana harusi.

Alirudia tena Cj4 kwa upande wa Hussein na mama Shebby walivyokuwa wanapelekeana macho na hapo aliikumbuka vizuri story ya Hussein juu ya maisha yake yaliyopita mpaka anaingia jera na kuanza kupata hisia inawezekana Hussein akawa anamfananisha mama Shebby na mkewe ambae ilisemekana alimuua.
"Hapa hapa kuna alama ya Mr X."
alijisemea mwenyewe Cj4 lakini kila alipotaka kumshuku babaake Shebby alijikuta moyo unakuwa mzito kukubali japo akili ilianza kumpeleka huko.
("Inawezekanaje huyu akawa ndie mke wa Hussein? Mh! ila pia inawezekana na kama ndio nina mashaka na babaake Shebby akawa ndie Mr X. ilaaaaa.... Agh! Nina wasiwasi na hapa hapa")
aliwaza na kujisemea moyoni Cj4 na kujilaza kitandani wakati huo tayari ilikuwa alfajiri.
"Mzee Mwinchande upo katika mstari wangu wa mashaka. Hii sasa itakuwa mission yangu peke yangu."
alitamka maneno haya Cj4 na kueka nia sasa mtu atayedili nae katika kumchunguza ni baba wa Kamishna Shebby ambae ni mzee Mwinchande, na hili alipanga kulifanya bila kumwambia hata Kamishna Shebby ambae ndie aliyekuwa anashirikiana nae katika mission zao za siri juu ya kumtafuta na kumnasa Mr X.

* * * * *

"Ibada ni jambo jema sana mzee mwenzangu."
"Kweli kabisa."
"Mwenye kufanya ibada hujieka jilani na Mungu na kujilinda na Sheitwaan"
"Naam."
"Mimi na mke wangu kama unavyotuona, sisi ni waislam safi kabisa na kila siku tunafanya ibada na ndio sababu nyumbani kwetu kuna amani na ndoa yetu imedumu miaka mingi."
"Daah! kweli kaka hongereni sana."
"Ahsante lakini hata wewe si mzee kama unaamua."
"Kuamua kivipi kaka."
"Amua uoe ili upate utulivu si unajua ng'ombe hazeeki maini?"
"KUOA!? hahahaa hapana kaka mimi maisha yangu nitayamalizia hivi tu."
alijibu Hussein bubu huku kipindi akizungumza na Mzee Mwinchande pale sebuleni majira ya mchana.

Mzee Mwinchande alikuwa anamuelezea Hussein habari nyingi nzuri na jambo kubwa alikuwa anamsisitiza juu ya imani yake kwa Mungu.
Maneno ya mzee Mwinchande yalizidi kumfanya Hussein amsome kuwa ni mtu mmoja mzuri sana na moyo wake ulifanana na wa Kamishna Shebby kwa vile alivyoonekana mwenye kujali na kuthamini wengine.
"Hivi unajua vizuri kusali?"
aliuliza mzee Mwinchande
"Mh! hapana kiukweli nimesahau dua nyingi sana za kusoma wakati unasali"
alijibu Hussein bubu.
"Basi mi nataka kuanzia leo uwe unajiunga nami tusali pamoja hususani alifajiri na usiku ndio mida mizuri sana kusali na kuomba"
aliongea mzee Mwinchande huku akipekua chini ya screen kubwa iliyokuwa ukutani pale sebuleni ambapo kwa chini kulijengewa kama kikabali maalum cha kuhifadhia vitabu na hapo alitoa kitabu kimoja kilichoandikwa SALA NA MAFUNZO YAKE, kisha alimkabidhi Hussein.
"Hiki kitabu kitakusaidia sana katika kujua kusali sala zote za kiislam."
"Asante sana kaka, daah! Nashukuru kwa kweli kwa kuonesha kunijali."
alijibu kiunyenyekevu Hussein wakati huo mke wa mzee Mwinchande alikuwa anashuka ngazi akitokea sehemu za juu ya nyumba yao na kama kawaida yake Hussein alipokutanisha tena macho na mama Shebby moyo ulimripuka tena na safari hii kuna kitu chengine alikiona ambacho kiliustua zaidi mtima wake.

ITAENDELEA. ...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom