Makapuku Forum

Makapuku Forum

TUKIO HALISI LA WIZI LILILO ISHANGAZA DUNIA


sehemu ya 02:

Basi baada ya bint kufanya mawasiliano na marubani ambao nao waliwasiliana na makao makuu ya uwanja wa ndege kule ndege ilikotakiwa kutua na ilikotoka.

Walikubaliana wamsikilize anachokitaka asije kuua watu bure.
Basi alidai ili asilipue ndege basi apewe fedha halali za kimarekani dola 200,000( msemo huu fedha halali utakuja kuona maana yake huko mbele ya stori)

Pia aliamuru apewe parashuti NNE na ndege itakapofika ktk uanja wa settle kue na gari ya kujaza mafuta ktk ndege ile na impeleke sehemu atakayoitaka.

Muhudumu alieahakikishia ni kweli bwana kopa anabom na kuwatajia vyote alivyoviona. Baada ya kupata orodha ya demand's za bwana Cooper basi mawasiliano na vyombo vya usalama yakafanyika haraka.

Wamiliki Wa ndege na vyombo vya ulinzi vilikubaliana jamaa apewe hizo pesa ili kunusuru maisha ya abilia 42 waliokuwemo ndani ya ndege. Kubwa zaidi ni injinia wa ndege na marubani wale wawili.

Basi walikubaliana kumpa hizo pesa ila walipanga kumfatilia kila hatua ikiwezekana wamdungue kabla hajafika chini. Kwakua aliagiza parashuti basi wakajua akiruka tuu wanae.

Hivyo basi wahudumu wote waliopo kwnye ndege waliamliwa wampe ushirikiano bwana cooper asishtuke na kuepusha hatari yoyote. Walimuomba awape mda kidogo ili wamkusanyie vitu alivyovitaka.

Basi muhudumu alimfata bwana kopa na kumkuta ameshavaa miwani myeusi na amerelax kabisa bila presha maana mbinu zote walizokua wakipanga yeye alishazisoma darasani.

Inaonekana kabla hajapanga kuiteka ndege alishasoma kwnz mazingira na kila kitakachopangwa na vyombo vya usalama. kifupi hakukurupuka na alipopewa jibu Kua asiwe na wasiwasi mikwanja yake anayoitaka inaandaliwa aliitikia kw kichwa na kisha akawasha sigara nyingine kw raha zake.

Aliagiza pia na maji ya kunywa na kwamshangao chenji iliyorudi alimpa yule muhudumu aliekua akimuhudumia.

Muda wote huo abilia wengine wote walikua hawajui nn kinaendelea na ili wasishtuke maana safari ya nusu SAA ilikua imezidi umbali ikabidi watangaziwe kuna tatizo la kiufundi kwnye kutua itabidi wakaekae angani tatizo litatuliwe kwnz.

Ndege ilikaa angani Massa 2 ikiwa inazunguka zunguka tuu ili kusubiria kule chini vitu vya cooper viandaliwe ndipo itue.

Ndani ya Masaa 2 FBI walifanikiwa kukusanya dola 200,000 kutoka bank, pesa zote walizipiga picha na kuchukua serio namba za kila pesa ili akifanikiwa kuzipata basi akamatwe atakapozitumia.

Hakua boya na yeye hayo yote aliyajua ndomana nakwambia alitumia akili nyingi nguvu kisoda watafurahi tuu. Basi bwana wakafanikiwa kupata na parashuti NNE km alivyoagiza bwana cooper.

Walizichukua kutoka ktk jeshi la nga na Tacoma kilichopo karibu na uwanja Wa ndege Wa settle. Baada ya kumaliza kufanya hayo yote mnamo majira ya 11:24 wakawasiliana na ndege hiyo iliyokua bàdo inawayawaya juu, walimwambia bwana cooper vitu vyake vipo tyr,

Walipompa orodha akadai hataki parashuti za jeshi anataka za kawaida za kiraia. FBI wakafanikiwa kuzipata kutoka katika kituo cha kujifunza watu kuruka cha skydiving.

MTU mmoja huyo anaijambisha serikali, robo saa baadae saa 11:39 ndege ilitua ktk uanja wa settle na cooper akaamuru rubani asimamishe ndege sehemu pweke na yenye mwanga wa kutosha. Hakua mbumbumbu akijua wanaweza kutumwa sniper wamtungue ndomana alitaka ndege isimame eneo lenye uazi mpana na kue na mwanga Wa kutosha.

Pia aliamuru rubani azime taa zote ndani ya ndege lengo kuepusha wadunguaji wasifanye ujanjaujanja maana snepeee Wa FBI wangeweza kufanya yao.

Baada ya ndege kusimama mtumishi mmoja wa kampuni ya Northwest Orient Airline's aliejulikana kama AL LEE akiwa amevalia kiraia kuepuka kumchanganya bwana cooper asidhani ni askari akiwa amevalia sare za uwanja wa ndege alikabidhiwa mabegi yenye ule mkwanja alioutaka bwana cooper pamoja na zile parashuti.

Al Lee aliisogelea ndege na bwana cooper aliamuru muhudumu mwingine ndani ya ndege alieitwa Bi mucklow afungue mlango Mdogo wa dharula na kupokea mabegi hayo.

Na mucklow akatii, Baada ya bwana cooper kuhakikisha Kua fedha na kila kitu alichohitaji viko sawa akaruhusu abilia wote washuke akabaki na marubani wote wawili, yule bint macklow na pamoja na fundi Wa ndege yule injinia.

Baada ya hapo aliamuru gari la kujaza mafuta lije lijaze ndege mpaka atakaposema inatosha, ikawa hivyo na akawapa mwongozo Wa safari anapotaka kwenda na speedi anayotaka ndege ikipaa iende na umbali kutoka aridhini kwenda juu anaotaka ndege ipae ili hata ikidunguliwa sirasi zisifike.

Kwanza akawataka ndege ielekee Mexico city na ndege iende speed ya km 190/hour na ndege iruke umbali wa futi 10, 000 kutoka ardhini. Pia aliwambia waondoe mgandamizo ndani ya ndege (cabin pressure) na wakiruka waache matairi bila kuyakunja kana kwamba ndege inataka kutua.

Pia mlango Wa nyuma Wa ndege uwe wazi km mizigo inapakiwa na mabawa ya ndege ya pembeni yawekwe kwnye nyuzi 15. Hiyo ilionesha bwana cooper sio mwizi mwizi Wa uswahilini. Msomi Wa hali ya juu na anajua anachokifanya.

Ilionesha kabla ya tukio alishafanya risechi na kuijua ndege nzima hadi uvunguni. Hapo akaamuru sasa ndege iruke.....

Je FBI watakubali mikwanja isepe?.
kwakua bwana cooper anajua Kua pesa alizopewa tyr serious namba polisi wanazo atawachezea gemu gani kutumia pesa zile andapo atafika salama?. ......tulia uone alivyokua na akili za ajabu na anakumbukwa mpaka kesho.

ITAENDELEA .
 
TUKIO HALISI LA WIZI LILILOISHANGAZA DUNIA:

sehemu ya 03:

Baada ya majadiliano ya kina kampuni ya ndege ya Northwest orient wakakataa ombi la bwana cooper eti ndege iruke ikiwa imefunguliwa mlango wa nyuma mkiani au pembeni kw madai Kua itahatarisha maisha.

Lkn cooper kw kujiamini kabisaa akawambia ni salama kabisaa na sitaki kubishana na MTU najua ninachokifanya.

Walipogoma alifungua mlango kw mikono yake mwenyewe. Ndege sasa iliruka kutoka ktk uanja Wa settler mnamo majira ya 11:40. Ikiwa imebeba watu 5 tuu waliobaki ndani ya ndege. Yaani cooper, macklow, fundi wa ndege yule injinia na marubani wale wawili.

Marubani na yule fundi walikua mbele kabisa katika chumba cha kuendeshea ndege (cockpit) na Cooper pekee na yule muhudumu macklow ndiwo waliobaki sehemu ya abilia.

Mara baada ya ndege hiyo kupaa kabisaaa zilifata ndege mbili za kivita aina ya F-106 kutoka kituo cha kijeshi MC chard air force Base. Ziliruka kuifukuzia ndege iliyotekwa na bwana cooper.

Ndege hizo ziliruka ktk namna ambayo zisingeweza kuonekana kw mtu yeyote aliekua ktk ndege waliyokuwemo wakina cooper. Moja iliruka juu zaidi na nyingine chini ya ile ndege iliyotekwa na bwana cooper. Yaani wakaiweka MTU kati, waliifatilia bega kw bega huku wakiwa na masneper hatari kabisaa kuhakikisha wanamnasa bwana cooper.

Takribani saa 2:00 usiku, alam ya mlango wa nyuma ikalia mbele kwnye chumba cha marubani kuashilia mlango wa nyuma kabisaa umefunguliwa.

Kabla ya kufanya hivyo bwana cooper alikwisha mfungia yule muhudumu aliekua nae siti ya nyuma.
Alimfungia chumba walichokua marubani na yule injinia. Hivyo akabaki peke yake kwenye siti za abilia.

Baadae walisikia km kishindo km kunakitu kimetupwa. basi ikiwa km SAA 4:15 wakaamua kutua kwenye uanja wa RENO VADA. lkn bwana cooper hakuwemo. Licha ya setilaity zote za inchi kufatilia kw karibu sana ndege ile pamoja na ndege mbili kufata nyuma zikiwa na FBI wenye uzoefu wa vita lkn hawakuona MTU akiruka wala begi.

Yaani kusema kweli rada yenyewe haikuonesha km kunakitu kimetoka ndani ya ile ndege ya akina cooper. Kabisaa hakuna kilichoonekana na hata km angeruka asingefika chini bila kuonekana na ndege iliyokua inafatilia chini ya ndege ya akina cooper.

Watu waliohusika na kuchezea setilaiti walikua macho kodo na ndege waliiona mwanzo mwisho ila hakuna kitu kilichoonekana kikiruka mpaka ndege inatua.

Hapo sasa kitendawili huyu jamaa alifanyaje mbona ndani ya ndege hakuwemo?. Pia makomandoo walidai hata uruke na parashuti ya kijeshi huwezi kufika chini salama maana ndege ilikuwa mbali mno na pressure ya juu hakuna aneweza kupumua vzr kutoka kule inakosadikika ndege aliyokuwemo bwana cooper ilikua inapita.

Je jamaa alirukaje?....
Usikose hapo kesho kumjua huyu bwana DAN COOPER. watafurahi tuu nilishakwambia akili nyingi nguvu kisoda.

usiku mwema......
 
TUKIO HALISI LA WIZI LILILOISHANGAZA DUNIA:

sehemu ya 04:

Baada ya maafisa wa FBI kuizunguka ndege na kuikagua hadi kwenye vioo na kumkosa bwana cooper, ikabidi kutafuta tena mpaka kudeki ndege ila holaa.

MSAKO WA KIHISTORIA UKAANZA:

baada ya FBI kujiridhisha huyu kiumbe hakuwemo kabisa ndani ya ndege wakaona hizi sasa dharau, Nadharia pekee iliyobakia ilikua bwana cooper aliruka tuu hakuna namna.

Watu na mafunzo yao na vifaa vya kisasa kabisa wakakubali kuzidiwa akili na abilia tuu. Ktk upekuzi wao wakagundua parashuti mbili tuu ndizo zilizobaki ndani ya ndege tena zile imara.

.hapo sasa ikawa mazingaombwe, jamaa aliruka na parashuti za kawaida na kuacha zile imara, tena alitumia zile za kujifunzia, swali je aliwezaje kuruka na parashuti tatu na mabegi mawili ya pesa aliyabebaje na uzito wa maparashuti haukua Mdogo?.

Kabla ya kufungua parashuti lazima uruke kwnz kutoka ndani ya ndege na ukiwa ktk balance ya anga (free space) ndipo unaruhusiwa kufungua parashuti kw taratibu zote za urukaji.

Sasa kwakua kulikua na ndege mbili zinafatilia mpaka muda wa flat areas ambao ndio ruhusa pekee ya kufungua parashuti kwnn vyombo vyote vya usalama havikumuona?.

Darubini zote na ndege za kivita mbili zote zikiwa na watu makini ktk vita lkn holaa tatu bila. Jambo jingine lililowaacha wamezubaa ni marubani wa ndege za kivita zilizokua zinafatilia ndege aliyokua amepanda bwana cooper hawakuona hata kivuli na hata kuhisi kitu.

Hapo ikabidi kamati ikae na kutafakari kw kina, pesa zote hizo haziwezi kupotea kijinga jinga namna ile na serikali IPO na watu waliosomea vita wapo.

Basi watu wenye akili na vyeti vyao wakaa na kutafakari na kukubaliana FBI watengeneze safari km ile, ndege itumike ileile na muda km ule na rubani au marubani wale wale ili kuona km watahisi ni eneo gani yule kiumbe aliweza kutoweka.

Basi bwana ndege ile ile na kutoka uwanja ule ule na muda ule, ikapaa huku sasa vyombo vyote vya usalama wakiwa makini kupita Mara ya kwanza yaani utafikiri ndio alikuwemo ndani ya ndege.

KITENDAWILI kikaja .......
Ni wapi ambapo bwana cooper anaweza Kua aliruka?. mbili kutokana na hali ya eneo ambalo labda angeruka kulikua na mvua kubwa angani na upepo hivyo mpaka kufika uanja wa ndege ambapo ndege iliamua kutua asingeweza kuruka angefia njiani.

Mtihani mwingine nikwamba eneo ambalo alam ilisikika ikilia ya mlango wa nyuma ambapo inahisiwa labda aliruka kuna msitu mkubwa na mgandamizo mkali wa hewa hakuna free spece kw hata mwanajeshi kufungua parashuti angekufa mapema mno.

Je huyu kiumbe alitowekaje?.

Wanajeshi wakaingia kazini

ktk msitu mzima kuanzia mwanzo wa safari mpaka mwisho wakiwa na mbwa na watalam wa misitu kuhakikisha km alifika chini basi ajatoka msituni. Ndege za kijeshi zikaanza msako msitu mzima hatua kw hatua . vyombo vyote vya usalama vikafunga mkanda sasa huyu binadam mpaka apatikane awe hai au kafa...

Je walimpata?.....

Nakama wakimkosa watawambia nini wananchi juu ya huyo MTU?.

. nilishakudokeza Kua hili ndilo TUKIO lililovunja rekodi ya DUNIA ..... jamaa anaakili mpaka anajiogopa.
 
TUKIO HALISI LA WIZI LILILOISHANGAZA DUNIA:

Sehemu ya 05:

Baada ya kurusha ndege na kulianza TUKIO km ilivyokua ikabidi FBI waende hatua kw hatua.

....Ilipofika saa 2:13 km ilivyokua siku ya tukio wakaliza alam na wakafungua mlango wa nyuma ya ndege kwenye mkia km ilivyokua siku ya tukio.

Muda huo ndio muafaka waliokua wamekisia bwana cooper aliruka maana ndio muda halisi alam ililia kuashilia mlango wa nyuma unafunguliwa. Basi wakapitisha moja kwa moja ndio muda alioruka.

Kwkua mwendo na umbali kutoka aridhini walitumia ule ule hivyo wakawa na majibu eneo hilo ni dhahili aliruka hapo. Basi FBI nao wakashusha ule mlango wa nyuma aliopitia bwana cooper wakarusha maafisa kadhaa wa FBI.

Wengine walibaki ktk free fall tofautitofauti kabla ya kufungua parashuti na baadae wakafungua na wakatua chini.

Baada ya kutua chini walibaini mvua ilionekana kunyesha siku ya tukio.inaonekana kulinyesha mvua siku ya tukio, licha ya mvua hali ya pale ilionesha kulikua na kimbunga maana miti ilikua hovyo hovyo.

Ukizingatia cooper aliruka ndege ikiwa umbali wa futi 10,000 kutoka aridhini changanya na mvua na kimbunga pia ikabainika kulikua na Giza totoroo aliponaje?.

Wakakubaliana huenda bwana Dan cooper hakutua akiwa hai. Vilevile parashuti alizoziacha ndizo kidogo zingeweza kusaidia kuhimili upepo japo kutua salama ilikua ndoto. sasa yeye kw kujiamini alitumia zile za kujifunzia .

....Sasa km alikufa maiti yake iko wapi?.
Pia hata kipande cha nguo au parachuti hakuna, FBI wakasema haiwezekani tutaita hata wazee, wanajimu , wanasiasa hadi wanasaikirojia mpaka huyu binadam apatikane.

Yaani (mfano) km ingekua bongo tungesema watu watamuendea Bagamoyo, ikishindikana wataenda Tanga, ikibuma wataenda Sumba wanga na asipopatikana waende KIGOMA hapo akikosekana tutainua mikono.....

Basi bwana, jeshi likaongeza nguvu na vikao vya kumjadili huyo binadamu vikapamba moto, jeshi la anga, usalama wa mataifa zaidi ya moja, polisi migambo, sungusungu, jeshi na FBI wakaingia kazini.

UTAMU KOLEA......

Kwanza wakasambaza serial namba za zile pesa baa zote, kasino zote au popote atakapooatikana binadamu mwenyepesa yenye namba zilizosambazwa na vyombo vya usalama lkn holaa.(hoi kabisa)

Wakaita wanasayansi na watabiri wakachukua mpaka udongo ktk eneo walilodhani aliporuka alitua pale, wakaenda maabala kupima DNA holaaaaa...

HATIMAE......

.wakaomba msaada USA, CHINA na URUSI nao wakaingia kazini.

Hapo sasa mpaka baharini wakapeleka meli kubwa na nyambizi za kuzamia chini kabisa katika miamba holaaaa, mitaa yote C.I.A wakatapakaa, miji na vijiji vyote, kona zote na juu helicopter holaaaa.

Ikaundwa sasa kamati ya UNDER COVERS URGENT. hapo sasa km ni mzimu utafahamika tuu maana mafunzo ya hawa sio ya mchezomchezo.

Bwana Dan cooper ni huyu hapa chini. ukimaliza kusoma muangalie maana mpaka naingia mitamboni bado anatafutwa.

stori inaendelea subiri huku mbele ndo utajua huyu jamaa alikua wa namna gani. ( nikumegee tu kidogo pesa zilipatikana baadhi ktk mazingira ya maajabu)

Usikose......ITAENDELEA.....
 
TUKIO HALISI LA WIZI LILILOISHANGAZA
DUNIA:

.......sehemu ya 06:

Baada ya kuandaa kundi maalum la undercover urgent msako ukaanza upaya hatua kw hatua, nukta kwa nukta,

Marekani nayo ikaongeza wanajeshi wenye mafunzo ya hali ya juu wapatao 200, EEC inayohusika na ufukuaji wa vitu vilivyozama ndani ya maji au aridhini nayo ikaingia mzigoni.

Wakapata pia msaada kutoka jeshi la anga (air force) kuongeza nguvu na wanajeshi kutoka jeshi la ulinzi wa nchi( National guard troops).
Kwapamoja wakafanya msako nyayo kw unyayo. mate kw mate, angani ndege zikatapakaa km senene chini mabaka matupu full magwanda door to door mpaka apatikane.

...EEC wakatoa marine kuanza upya kufukua hadi vitu vilivyozama majini (marine survege farm). Msako ktk ziwa MERVINI, kujalibu kuona labda bwana cooper au vitu alivyoruka navyo labda vilizama. lkn hata nyuzi hawakupa, hata unywele holaaaa.

WAKAAMUAJE SASA?.............

Maafisa wa FBI wakaongezwa pamoja na kualika makampuni binafsi pamoja na wanachi kuombwa ushirikiano maana mambo sasa yalianza kutia aibu inchi.

Kw siku 18, miezi mitatu holaa, duu!!!!.
Mwezi wa 3, 1972, ukafanyika msako sasa mpaka MTO WASHONGUL nusura waukaushe maji kuona labda jamaa atakua kazamia kwnye matope holaa.

Sasa wakaitwa wanasayansi upya, safari hii walirudi ktk eneo walilohisi mwanzo labda alitua hapo. Wakachukua udogo na kujichimbia maabala wakipima tena DNA holaaa.

.......Wakaona sio bure, wakachapisha magazeti na habari zake kutangazwa kila siku Kua anatafutwa lkn holaaa,.

.....Sasa wakakaa tena kamati ya ufundi kujaribu wanajimu na wanafilosophia lkn tatu bila, wakaona sio kesi wakapanga mkakati Mpya ambao waliamini wakimkosa basi hakua MTU wa kawaida kulikua jini.

Je wajua ulikua mkakati gani?.

hivi alijificha wapi ashindikane na mataifa makubwa?.

...tukutane jioni ila kw kukuthibitishia angalia picha hapa chini Baada ya stori uone magazeti yalivyokesha yakiandikwa.

ITAENDELEA......
895b717d4aebeffb1a5732c6c66f715c.jpg
 
TOP TEN
Wakati Jf kuna pipo zinajiona ni maarufu wakati umaarufu wao ni wa humu humu ukienda Google huwezi kuwapata hata Facebook.....Humu maarufu wa kweli ni Maxence Melo na kubwa jinga Le Mutuz halafu kuna mtu kama Ontario ambaye now walau hata sura yake tunaifahamu....wengine wote umaarufu wao labda upo kwenye kuta za vyumba vyao tu ila Umaarufu bila pesa ni kazi bure lengo langu leo siyo kuwaponda watu bali kuwazungumzia watu kumi maarufu zaidi ever duniani

Yaani watu ambao wanafuatiliwa zaidi huko kwenye mtandao mkubwa wa Google ili waru asome habari zao

NB
Niyaandikayo hayahusiani na udini hivyo wafia dini mnisamehe nikiwataja watu wenu maana lengp limeshaelezwa hapo juu
Karibuni
......
Sawa
 
9/Leonardo Di Ser Piero Da Vinci
494cb6b7723353dbea44cf1d82befb56.jpg
6c8ce92b946a33003b4eb72bc60ce0af.jpg

Alizaliwa mwaka 1452 na kufariki dunia mwaka 1519
Huyu jamaa hapendwi kabisa na wakristo kutokana na baadhi ya Code Pictures kuhusu kanisa na mambo mbalimbali ambazo zinajikita kwenye kutoboa siri ya mambo yaliyojificha
Japo hapendwi ila yeye ndo aliyetuchorea sura ya bwana Yesu tunayoiabudu makanisani kwani baada ya kuichora ndio wakatafutwa watu wanaofanana nayo na kuigiza filamu za Yesu na hata picha za vitabuni
4c82f3445c7eaec3085a24ac68d01ad7.jpg
Jamaa pia ana mchoro wa The Last Super ambao una code zinazoonesha Yesu alikuwa na demu
7fc6f431811245f9bf704a0c0774aa84.jpg

Vipi juhusu Monalisa ?...kuna asiye hujua?
Ila jamaa anadaiwa alikuwa shoga
Kaandikwa kwenye vitabu zaidi ya 6,000,000

Kwa mwezi anatafutwa zaidi ya X 4,000,000
......
Wafia dini no

Sawa mkuu
 
3/Abraham
38fdaa931e99e4fe0e7434d7a083f0e6.jpg
865e5bd53f930501f9a65b79427bf03e.jpg
64a737397668c10337d818c89a702d24.jpg
Aliishi kati ya mwaka 1812C hadi 1537 BC
Achana na Abraham Lincoln hapa namzungumzia Abraham orijino
kuna tofauti kati ya Abraham na Ibrahim? Nafikiri ni sawa tu na Hasheem na Hashim au Hashimu
Abraham anajulikana zaidi kama Nabii Ibrahimu na Wakristo kwa Waislamu wanamfahamu
Anaaminika ndiye mtu wa kwanza wa Masharuki ya kati kuamini katika uwepo wa Mungu mmoja
Ameandikwa kwenye vitabu takribani 2,000,000

Anatafutwa zaidi ya X 10,000,000 kwa mwezi
.....
Mtoto wa tera alipofikisha miaka 12 tu alipewa mke sarah aliekuwa na miaka 8

Walihama kutoka nchi ya ukaldayo kwa sasa yasemekana kuwa ni eneo ilipo iraq

Kwa maono aliyoonyeshwa kwenda katika nchi asiyoijua

Huyu ndiye baba wa imani duniani
 
2/Abu Al--Qasim Mu Ammad Ibn Abd Allah
bddf0112af04c408b42b2c7d3374853e.jpg
78999669f3d1af55f73cffcac79987f7.jpg
65cba458e3cfc6b06f3154c78e9bc912.jpg

Aliishi kati ya mwaka 570 hadi 673 na sijui kaburi lake mahali lilipo
Kwawasio waislamu Mtume Muhammad ndio mwanzilishi wa Uislamu ila kwa wenye dini yao wanaamini/wanasema hakuanzisha chochote ....mimi simo wanadai Uislamu ulikuwepo kabla yake
Sasa nafiki ushaelewa maana ya Allah Akbar
Ameabdikwa kwenye vitabu kibao idadi haijulikani

Anatafutwa kwa mwezi X 14,000,000 ila hata kapicha hakuna!!
.......
Alianzisha uislam mwaka 640
Pia alikuwa mfanyabiashara mkubwa so kupitia biashara zake aliisambaza pia imani yake kwa kuwa alizitembelea nchi mbalimbali
 
Hiki ni chakula ambacho kinaupa mwili wako nguvu na kina virutubisho vingi sana ambavyo hutopenda kuvikosa!
Ina protein nyingi kuliko mayai
Calcium kwa wingi
Iron kuliko spinach
Manganese
Potassium
Vitamin C
Vitamin B1,B2,B3
Omega 3 kwa wingi
Fiber

Faida zake mwilini ni pamoja na
Vegan,
Regulate blood sugar
Anti oxidants
Anti Cancer
Inasaidia kucontrol weight
Matatizo ya moyo
Lower cholesterol
Usagaji wa chakula tumboni
Acts as sleep Aid
Inaboost Libido
Inaupa mwili wako nguvu
Increase Stamina
Inasaidia kukontrol mzunguko wa hedhi
Inasaidia kubalance hormones
Naomba niishie hapa kwa leo mengine unaweza kugoogle vinginevyo tutakesha
Ahsante kwa muhtasari huu Ankali
 
1/Jesus of Nazareth
d9d86d3ed6278d2a11070d1b0969b3a9.jpg
38a9dc4e18ee78686fd323669b3e09b1.jpg
c482c60eb9f0cfab52596f0fcb22b990.jpg

Aliishi kati ya mwaka 5BC hadi 28 AD Ila wafuasi wake bado wanaamini yupo hai mbinguni sasa sijui kama keshazeeka au lah
Alizaliwa na Bikira Maria kwa uwezo wa Roho Mtakatifu {kama wewe unahisi alizaliwa kama wewe ilivyotokea kwa wazazi wako mimi sijasema hivyo)
Pamoja na kuishi bila shari na mtu akasalitiwa na bwana Yuda Eskariote na wenzake wachache kisha Pilato akavuta mlungula na kutoa hukumu ya kidwanzi halafu akasulubiwa akafa kisha akapaa mbinguni
Hivyo ukisalitiwa na rafiki/ndugu/mpenzi wako usiwaze sana kumbuka hata Yesu yalimkuta pamoja na kufanya mazuri kwa 100%
Ameandikwa kwenye vitabu visivyo na idadi

Anatafutwa X 25,000,000 na ushee kwa mwezi

.
.
.
.
.

.
.
Samahani kwa niliowakwaza kwa mada ya leo najua nimekorofisha imani za wstu maana ilikuwa hakuna namna
.
.
.
Shukrani kwa mliosapoti mada
Tukutane kesho
Niwatakie Usiku Mwema
Mwisho
........
Kiumbe pekee ambaye tunaelezwa hakuzaliwa kupitia mbegu za mwanaume

Hakika Mungu ni muweza wa yote

Baadhi ya maandiko husema

Alifanya miujiza mingi sana na ya kushangaza ambayo haijapata kufanywa na yeyote toka dunia iumbwe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom