Muziki: Uji Sio Supu ya Ugali
Kama hujawahi kujua hili lijue leo maana hata mimi silijui, kumbe siku zina harufu na kiukweli harufu ya Ijumaa ni tofauti na siku nyingine kama Jumatatu. Ijumaa huwa inanukia kama uvumba na manemane na ina ladha ya emebe mawazo huku jumatatu huwa na harufu ya pilipili kichaa na ndo maana hakuna mtoko wa Jumatatu, sijui. ninakusalimia Kapuku muheshimika, u khali gani! niko poa sana na furahiday ndo hii, take it easy and don't work hard kesho. Kwa wale wenye zamu ya kutumika kimwili basi weekend ndo hii, kazaneni sana maana mwili usipotumika utakuwa bored.
Kwanza niseme tu, maneno spesho kwa
husna muba ambaye kiukweli sihitaji kukufikiria ili nijisikie vizuri. Kila wakati unanifanya, sema nifanye nini! Kuna mtu alisimamisha jua, ukitaka nisimamishe saa nitasimamisha, good to see you buddy. Msidhani nimesahau kumsalimia
Tumosa kisa tu nimesoma commeny ya
shululu aliyetuhabarisha kwa magazeti. Niseme nini juu yako
Shunie kwa kutupa sala na ukamuamsha mjomba wangu
lee empire akatuletea BBC, hadithi zilizomfanya
Jimena atukumbushe kutosahau historia. Nitakutaja tena Husna kwa simulizi za Che, mtaasisi mwenzangu
Nyagei ukatuspotisha na mtaalam mwenyewe
Bitoz kwa kubwa kumi, asanteni sana wadau.
Mkushi wa kusi ,
Clkey ,
Sakayo ,
BlessedHope ,
Transcend ,
eden kimario ,
dingimtoto ,
Mondray mahondaw ,
Madame S ,
mzeewakungoa koncho77 Bailly5 na wewe unayesoma hapa hata kama sijakutaja kwa jina, sijakusahau maana wewe ni tmu muhimu sana hapa jukwaani. Unalifanya Jukwaa hili lipendeze na unapozidi kuulamba basi nasi tunajua kabisa uji sio supu ya ugali.
Muziki sasa, kuna wakati unaweza kujiuliza mbona anayerudia kaharibu, well zipo baadhi ya nyimbo waliozirudia (cover) zimkuwa nzuri kuliko original. Unamjua Cindy Lauper na TAT (time after time), kama umemjua mwaka 2013 alipoalikwa kwenye kuapishwa kwa BO basi huyu alitamba miaka ya 80s na wimbo wake umerudiwa na Daynea Deacon mjamaika huyu katika mahadhi ya reggae.
Burudika
Chaguo la wadhamini na wapendanao litakujia baada ya dakika 15