Makapuku Forum

Makapuku Forum

Nimekukimbilia wewe Bwana nisiaibike milele kwa haki yako uniponye

Unitegee sikio lako, uniokoe hima uwe kwangu mwamba wa nguvu, nyumba yenye maboma ya kuniokoa

Ndiwe genge langu na ngome yangu, kwa ajili ya jina lako uniongoze, unichunguze

ZABURI:31:1:3

Muwe na usiku mwema mlindwe na damu ya Yesu kristo
Amen
 
3/Corazon Kqamboka
43a8f5f4e5d25ffa729f6c72daf33be6.jpg
496b53390c330cc0d0fb28e46a342d4a.jpg
fe6e9db8b1bec4d40719937359cb6a44.jpg
Amezaliwa mwaka 1993 hapo ukivuka border la Kilimanjaro kwa wale jamaa wanaodai Mlima Kilimanjaro ni wa kwao
Huyu ni binti wa Kikenya
Ni mwanasheria ila ikumbukwe kila Wakili ni mwanasheria ila siyo kila mwanasheria ni wakili
Pia kuna wanasheria ngazi ya cheti,Stashahada na sjahada
anayechuana na Vera Sidika

.................

Duh anayaweza aisee

Huyu wa kwetu abadilike
 
Muziki: Uji Sio Supu ya Ugali

Kama hujawahi kujua hili lijue leo maana hata mimi silijui, kumbe siku zina harufu na kiukweli harufu ya Ijumaa ni tofauti na siku nyingine kama Jumatatu. Ijumaa huwa inanukia kama uvumba na manemane na ina ladha ya emebe mawazo huku jumatatu huwa na harufu ya pilipili kichaa na ndo maana hakuna mtoko wa Jumatatu, sijui. ninakusalimia Kapuku muheshimika, u khali gani! niko poa sana na furahiday ndo hii, take it easy and don't work hard kesho. Kwa wale wenye zamu ya kutumika kimwili basi weekend ndo hii, kazaneni sana maana mwili usipotumika utakuwa bored.

Kwanza niseme tu, maneno spesho kwa husna muba ambaye kiukweli sihitaji kukufikiria ili nijisikie vizuri. Kila wakati unanifanya, sema nifanye nini! Kuna mtu alisimamisha jua, ukitaka nisimamishe saa nitasimamisha, good to see you buddy. Msidhani nimesahau kumsalimia Tumosa kisa tu nimesoma commeny ya shululu aliyetuhabarisha kwa magazeti. Niseme nini juu yako Shunie kwa kutupa sala na ukamuamsha mjomba wangu lee empire akatuletea BBC, hadithi zilizomfanya Jimena atukumbushe kutosahau historia. Nitakutaja tena Husna kwa simulizi za Che, mtaasisi mwenzangu Nyagei ukatuspotisha na mtaalam mwenyewe Bitoz kwa kubwa kumi, asanteni sana wadau.

Mkushi wa kusi , Clkey , Sakayo , BlessedHope , Transcend ,eden kimario , dingimtoto , Mondray mahondaw ,Madame S , mzeewakungoa koncho77 Bailly5 na wewe unayesoma hapa hata kama sijakutaja kwa jina, sijakusahau maana wewe ni tmu muhimu sana hapa jukwaani. Unalifanya Jukwaa hili lipendeze na unapozidi kuulamba basi nasi tunajua kabisa uji sio supu ya ugali.

Muziki sasa, kuna wakati unaweza kujiuliza mbona anayerudia kaharibu, well zipo baadhi ya nyimbo waliozirudia (cover) zimkuwa nzuri kuliko original. Unamjua Cindy Lauper na TAT (time after time), kama umemjua mwaka 2013 alipoalikwa kwenye kuapishwa kwa BO basi huyu alitamba miaka ya 80s na wimbo wake umerudiwa na Daynea Deacon mjamaika huyu katika mahadhi ya reggae.
Burudika

original




Chaguo la wadhamini na wapendanao litakujia baada ya dakika 15

Nilijua tu leo kitu kutokea huko
 
1/Noni Zondi
f6ad44fbe6eef8b6e1f02b0957c2082a.jpg
e5110ad36871fd1b0c06edf717836bfb.jpg
57296b48f9670abe6bdd4ef9a8880b32.jpg
Sijajua mwaka aliozaliwa huko kwa Rais mkware na taifa kinara kwa Virusi Vya Ukimwi duniani
Huyu ni celeb wa huko Afrika Kusini
Anaishi pia jijini London
Hujishughulisha na mambo mengi ya Sanaa ikiwepo muziki na vipindi vya luninga
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
Shukrani kwa mliosapoti mada
Niwatakie Usiku Mwema
Tukutane Jumatatu
Mwisho

..............

Shukrani Bitoz nyangema kwa supu za weekend
 
Muziki wa Wapendanao

Hakuna ubaya kufanya unachoamini katika moyo wako kuwa ni sahhi, kila mtu ana belong kwa mtu wake. Chaguo la wapendanao leo ni kwa hisani ya Shunie na lee empire

Tufurahike pamoja nao



Mnaosemaga mapenzi sio dawa njooni mbishe hapa, yaani nyimbo mbili kwa mtu mmoja, its like moving from dedication to deadication
Tufurahike nao zaidi na unapoagiza combo jua kabisa unapata a meal + a drink


Big up mtaasisi
 
Kwa mara nyengine Cj4 anaonekana akiwa kavaa mavazi ya kipolisi yenye cheo cha Inspector huku akiwa anaendeesha gari aina ya Land cruiser nyeupe ya kipolisi speed kali kwenye barabara ya vumbi na safari yake ilimpeleka hadi mbele ya kituo kikuu cha polisi Mkuyuni ambapo baada ya kushuka alipigiwa saloot na askali aliowazidi cheo mahala pale na moja kwa moja alienda kukutana na mkuu mpya wa kituo na baada ya kusalimiana alijitambulisha.
"Naitwa Inspector Sudy kama ulivyoipata taarifa ya ujio wangu nimekuja kwa nia ya kukutana na baba wa marehemu mkuu wa kituo aliyekutangulia kwa ajili ya kwenda nae makao makuu Dar."
aliongea kwa ukakamavu Cj4 japo ukweli hakuwa askali polisi bali ulikuwa ni mpango wa siri tu uliofanywa na viongozi wakubwa ili iwe rahisi kufanikisha zoezi la kwenda na mzee Cyplian kwa mahojiano maalum ya siri ili wapate kumvumbua huyo Mr.X
"Sawa Inspector basi utaongozana na vijana wachache wataokupeleka mahala anapoishi mzee Cyplian"
alijibu mkuu wa kituo na baada ya hapo amri ilitolewa na ndipo Difender moja iliyowabeba askali watatu iliongoza njia na kufuatiwa na gari ya Cj4 moaka kule ambako alikuwa anaishi baba wa marehemu Ocs John ambae ni mzee Cyplian

Baada ya mwendo wa dakika ishirini waliingia mbele ya nyumba moja ya kifahari licha ya kuwa ilikuwa kijijini mbali na barabara kuu lakini ilitosha kumjuza mpita njia wa eneo lile kuwa mtu aliyejenga pale si mtu wa kipato cha chini.
Mara baada ya gari kusimama na walinzi ambao pia walikuwa ni askali wa jeshi la polisi walifungua geti na kuukaribisha ule ugeni ulioongozwa na inspector fake Cj4 mpaka ndani ya sebule kubwa baada ya kukaribishwa na kuruhusiwa na mzee Cyplian kwa njia ya simu ya upepo pindi askali alipomjuza juu ya ugeni ule na muda mfupi Cj4 alipokuwa ameketi sebuleni mzee Cyplian alianza kushusha ngazi taratibu huku akiwa amevalia suti nadhifu na mkononi mwake akiwa na bluefcase ndogo na kufika pale sebureni.
"Karibu sana kijana, nina taarifa zote za ujio wako na nilikuwa nakusubiri wewe hahahaa karibu sana mwanangu."
aliongea mzee Cyplian na kupeana mikono na Cj4.

Hakukuwa na muda wa Kupoteza zaidi ya Cj4 kuongozana na mzee Cyplian mara baada ya kuagana na familia nzima aliyoikuta pale akiwemo mama mzazi wa marehemu Ocs John na baada ya kutoa pole kwa mara nyengine aliaga na safari ilianza huku akiescotiwa na ile Difender mpaka morogoro mjini ambapo Difender ilirudi Mkuyuni nae kunyoosha tairi kuwahi Dar es Salaam huku kichwani mwake akipiga hesabu juu ya maswali ya kumuuliza yule mzee kabla hawajafika sehemu husika.

* * * * * *

Akiwa amekaa sebuleni akifatilia taarifa ya habari ikiwa ndio wiki yake ya mwisho kuendelea kuwapo nyumbani baada ya kupona vizuri, kamishna Shebby alistushwa na habari iliyokuwa inatangazwa muda huo juu ya wafungwa walioachiwa huru kwa msamaha wa rais huku kivutio kikubwa kikiwa kwa mfungwa mmoja ambae kesi yake ilitikisa miaka mingi naye si mwengine bali ni Hussein Bakari a.k.a babu bubu jina la utani alilopachikwa akiwa huko gerezani.
Macho yalimtoka Shebby baada ya kukumbuka kitu na kujikuta anaropoka kwa sauti ya juu na kumuita babaake aje pale sebureni aone.
"Baabaaa babaaa njoo , Nimekumbukaaa.. Aaagh!! nimekumbukaaa Nimekumbukaaa babaaa"
aliongea kwa furaha Shebby na kuwafanya wazazi wake warudi huku wakiwa na taharuki kwa shangwe na maneno ya mtoto wao.
"Vipi mwanangu?"
"Nimekumbuka baba, kumbukumbu zangu sasa zimerudi aaahhh!"
"Allahu akbaaru Allaaaah akbaaaaar"
alishukuru na kufurahi mzee Mwinchande huku wakikumbatiana na mkewe baada ya kijana wao kuthibitisha kuwa kumbukumbu zake zimerejea sawia.
"Kipi kimekukumbusha mwanangu?"
aliuliza kwa furaha na kutoamini mzee Mwinchande
"Taarifa ya habari, ngoja nimpigie Asha nimwambie nae Mungu amenisaidia nimekumbuka kila kitu sasa sina wasiwasi tena pindi nitapokutana na Kamanda kwa mahojiano aaaaah!!! masikiiini rafiki angu Kimarooo..."
aliongea Shebby lakini mwishoe alijikuta anaanza kulia mara baada ya kumbukumbu zake kumrudisha Mkuyuni na kuliona tukio zima lililojili miezi kadhaa nyuma na zaidi alimkumbuka rafiki ake kipenzi Kimaro na kuanza kulia kwa uchungu sana.
"pole babaa polee ndio uanaume na misukosuko ya kazi zetu hizo pole baba"
alimfariji mwanae mzee Mwinchande huku akimkumbatia wakati huo mamaake alibaki anawatazama huku machozi nae yakimtoka
"Babaa!! inatisha sanaaa, babaaa inaniumaa sanaa lazima nilipe KISASI"
aliongea kwa hisia zenye uchungu sana Shebby lakini babaake alimtuliza na kumsihi asije kuthubutu kufanya hivyo
"chonde chonde mwanangu mi mwenyewe ni askali mzoefu sana nakusihi na kukuomba sana kwa usalama wako futa kabisa hayo mawazo"
"kivipi baba?"
"Kwa sababu ni hatari ya maisha yako hebu fikiria unataka kulipa kisasi je unamjua huyo unaetaka kumlipizia?"
"Nitamtafuta mpaka nimjue sitokubali ni heri nife nikiwa namtafuta hata nitapokutana na wenzangu huko mbinguni watanipokea vizuri kuliko kukaa kimya na kufa bila kufanya kitu wakati mimi ndie niliyewaponza wengine"
alisisitiza Shebby huku akiwa amekasirika mno baada ya kumbukumbu zake kuendelea kumiminika kichwani mwake mithili ya bomba la maji lililokuwa limefungwa muda mrefu na sasa limefunguliwa koki.
"Hee! Shebby mwanangu kumbuka hata ufanyeje huwezi badilisha ukweli kuwa rafiki zako wamekufa na mtu uliyekuwa unamtetea kaachiwa huru sasa iweje bado unang'ang'ania kumtafuta mtu usiyemjua hata jina?"
"Namjua babaa.."
"Unamjua!!!"
"Hee, Nitatumia jina hilohilo analolitangaza mwenyewe na Kifo chake lazima nikishuhudie mbele ya macho yangu."
"Hee basi tulia baba unasema unamjua jina? ndio nani sasa?"
aliuliza mamaake wakati huo babaake alikuwa kataharuki na haamini jinsi mwanae alivyobadilika ghafra namna ile.
"Mama, Baba nawapenda na nawaheshimu sana naomba mnisamehe kwa kubishana nanyi ila niacheni nipambane na huyu mtu anayejiita Mr x."
"MR X!!!?"
"Ehh! Mshenzi mwenyewe anaitwa Mr X"
aliongea Shebby kwa hasira na kuelekea chumbani kwake moja kwa moja huku akijiapiza kulipa kisasi na kumlaani mr X akiwaacha wazazi wake wakiwa wanatazamana wasijue la kufanya au la kumwambia kijana wao.

* * * * * *

"Pole sana mzee wangu kwa kumpoteza shujaa akiwa bado na umli mdogo vile"
alivunja ukimya Cj4 mara tu walipoanza kukaribia mkoa wa Pwani na kuzifufua hasira za maumivu zilizokuwa kifuani mwa Kamanda mkuu wa Jeshi la polisi mstaafu mzee Cyplia.
"Aaagh! yaani mwanangu unavyosema hivyo unazidi kunitonesha kidonda cha mwanangu John! aaagh! mungu ampumzishe kwa amani."
"Daah! binafsi mzee wangu nimeamua kujikita katika upelelezi wa kujua kilichotokea kwani inasemekana chanzo kabisa ni mfungwa aliyekuwa gereza alilosimamia Kamishna wetu yule mtoto wa kamanda wako msaidizi enzi zenu "
"Aaagh! ndio mtoto wa Mwinchande!"
"eeh, sasa kumbe alikuwa katika mpango wa kumsaidia yule mfungwa baada ya kujua story yake na ukweli halisi wa kesi ulikuwa kule morogoro lakini alipoenda kufanya tafiti na kusaidiana na askali wa kule ndo yakatokea ya kutokea"
"Mh! sasaa kidooogo naanza kupata mwangaza"
aliongea mzee Cyplian na kumfanya Cj4 azidi kutuliza umakini kwani tayari moyoni mwake alishaanza kumuhisi huenda yule mzee akawa ndie Mr X lakini aliamua kuongea vile ili kumpoteza na kujifanya hajamstukia kitu ili iwe rahisi kumteka kimazungumzo
"Mwangaza gani tena mzee wangu"
"Kwa yaliyotokea ila naamini hadithi ya huyo mfungwa ndio funguo ya kumjua muhusika aliyewafanyia unyama wanangu.,,,,"
kauli ya mzee Cyplian ilibeep ubongo wa Cj4 wakati huo tayari walikuwa wanaingia Chalinze lakini mara ghafra kabla mzee Cyplian hajaendelea wala Cj4 hajauliza chochote ghafra walishangaa kuona basi lililokuwa linatokea njia ya Tanga likipitiliza na kuingia mkuku mkuku barabara kuu huku likiwa limewasha taa na kupiga honi mfurulizo kuashilia kuwa aidha dereva limemshinda au limekata breki na kutokana na speed aliyokuwa anakuja nayo Cj4 alijikuta anashindwa kusimama na kuhamia barabara ya pili ili apate kulikwepa lakini bahati haikuwa yake baada ya kukutana na kiuno cha tela la roli lililofunga breki za ghafra kwa kuogopa kulivaa basi lililokosa muelekeo na kusababisha tela kugeuka kuelekea usawa wa gari la kina Cj4 huku kikisikika kishindo kikubwa sambamba na milio ya breki iliyosababisha cheche kuwaka barabarani na kelele za hofu toka kwa wafanya biashara na watu mbalimbali zilizosikika Chalinze nzima.

Hakuna aliyeelewa jinsi gani ile gari ndogo Landcruiser nyeupe iliyokuwa inaendeeshwa na Cj4 ilivyofika fika kule kwenye tawa za umeme tena ikiwa imechakazwa mno sehemu za mbele, na baada ya watu kukimbilia hususani wale wahuni na vibaka mpaka pale ilipokwamia ile gari walimshuhudia mzee mmoja kwa ndani akiwa kabanwa ipasavyo kwenye kiti na bashboard huku ule upande wa dereva kukiwa patupu na ndipo vijana wale wa kihuni walipong'ang'a kuuchomoa mlango mmoja uliojikunja ili wapate kuingia na kuitoa blufkes waliyoiona kwa ndani wakiamini lazima kutakuwa na hela tu.
Lakini kabla hawajafanya hivyo walistushwa na sauti ya mtu akiwaamuru waondoke haraka ikitokea nyuma yao na walipogeuka kutazama walimshuhudia askali mmoja ambae mavazi yake ya juu yalichafuka kwa damu iliyokuwa inaendelea kuvuja kutokea kichwani na ndipo wale wahuni wote walipotimua mbio.
Hakuwa mwengine bali ni Cj4 dereva wa ile gari nyeupe iliyokwamia pale kwenye matawa ya umeme akiwa na jeraha lililokuwa linavujisha damu nyingi huku ikiwa haieleweki alitokajetokaje kutokana na kubondeka vibaya hasa ule upande aliokaa yeye.
Alimuangalia mzee Cyplian na moyo kumuuma zaidi mara baada ya kugundua kuwa alishafariki pale eneo la tukio na hapo hapo kwa speed bila kujali damu zilizokuwa zinamvuja Cj4 alianza kukimbia kuelekea barabara kuu ambapo jumla ya magari sita yalipata ajali iliyosababishwa na lile basi lililopoteza muelekeo ambalo lilianguka na kuseleleka upande wa pili hadi kwenye vibanda vya mama lishe na kusababisha maafa makubwa mara baada ya derva kulazimisha kukata kona licha ya mwendo kasi lililokuwa nao.
Kitu cha kwanza kufanya Cj4 akiwa kama mtu aliyechanganyikiwa alisimama na kulitazama eneo lile la ajali na kuanza kupiga hesabu alizozijua yeye wakati huo maaskali ndio walikuwa wanawasili eneo lile licha ya kwamba kituo hakikuwa mbali na mahala palipotokea ajali.
(''Hii ni ajali ya Kutengeneza kabisaaa,'')
aliwaza Cj4 na kukimbilia kwenye ile basi na kuvunja kioo cha mbele kwa kupiga teke kali na alibahatika kumchomoa dereva ambae licha ya kwamba hali yake ilikuwa sio nzuri lakini alijitahidi kuzungumza
"Jitahidi kuongea mimi ni askali nimekushika, nambie mara ya mwisho mlisimama wapi kwa ufasaha kabisa"
alionga Cj4 kumuuliza yule dereva ambae alitoa maelekezo kwa shida huku akimwambia kuwa gari iliferi breki baada ya kuhisi waya maalum uliopita kwenye propela ulioshikilia vipira vilivoenda kukamata ringi za taili za mbele kuwa ulikatika ghafra na hakujua chanzo.
maneno yale ya yule dereva yalizidi kumuaminisha Cj4 kuwa ile ajali ilitengenezwa tu sio bure lakini kama imetengenezwa wamefanyafanya vipi hao watu? hapo akakosa jibu ndipo alipotaka kumuuliza tena yule dereva mara askali wengine walifika eneo lile na kuanza kuwatoa majeruhi wa kwenye basi wakishilikiana na wananchi huku naye Cj4 akipigiwa saloot na askali aliowapita cheo na wakimsihi wampeleke nae akatibiwe kwani alikuwa kaumia sana kichwani licha ya kuwa yeye mwenye alijiona yuko sawa.
Na wakati akiwa kasimama akiangalia pilika pilika zilizokuwa zinaendelea za uokozi na wapiga picha eneo lile mara macho yake yaligongana mara mbili na macho ya binti mmoja aliyevalia kiislamu usoni mwake akifichwa na nikabu nyeusi akiyaacha macho tu huku akitembea kwa madaha bila wasi kuelekea sehemu aliyopaki gari yake ndogo lakini kila alivyokuwa anapita alipogeuka macho aliyaelekezea kule kwa Cj4 na kwa ile Landcruide iliyobondeka kwenye Tawa za umeme na hapo hapo aret ya hatari iligonga kichwani na Cj4 na kuhisi yule mwanamke ndie aliyesababisha ile ajali na kuanza kupata ufumbuzi basi huenda mzee Cyplian hakuwa mr.X kama alivyomuhisi awali ila alitia shaka kuwa huenda mzee Cyplian kuna vitu alivijua kuhusu mr X na ndio maana mr X amewatuma vijana wake kufanya ujanja wowote ili mradi wahakikishe mzee Cyplian hatoboi ukweli wala siri yoyote kuhusu mrX.
Lakini akiwa na maswali lukuki Cj4 kila alipomtazama yule bint moyo ulimtuma amzuie tu kwani macho ya yule binti yalionesha wazi kuna kitu anataka ahakikishe kule ilipodondokea ile gari na ndipo alipowaponyoka polisi wenzake na kukimbilia upande wa pili ilipokuwa ile gari ya yule bint ambayo ndio ilikuwa inaondoka taratibu eneo lile lakini kwa bahati mbaya zaidi Cj4 alianza kujisikia kizunguzungu kabla hajafika na kujikuta anadondoka katikati ya barabara ambayo ilikuwa inazungushiwa utepe wa kuzuia magari yasipite upande ule na macho yake yaliishia kuitazama kwa mbali ile gari pindi alipokuwa anadondoka na kupoteza fahamu.

* * * * * *

Akiwa amekaa huku mawazo na hasira juu ya yaliyopita hususani mr X na vifo vya rafiki zake huku akiwazia kukutana na Hussein bubu, ndipo Shebby alistushwa na sauti ya babaake pindi alipokuwa anaongea kwa njia ya simu kwa mshtuko mkubwa na kumfanya atoke na kukimbilia sebuleni aliposimama mzee Mwinchande akiendelea kuongea na simu.
"Vipi baba nini kimetokea?"
aliuliza kwa taharuki Shebby baada ya kuuona uso wa babaake ukionesha kushangazwa na kustushwa na alichokuwa anakisikia
"ajali mwanangu"
"Ajali? nani tena!"
"Mkuu mstaafu wa jeshi la polisi Kamanda Cyplian anasadikika amepata ajali mbaya wakati akiwa njiani kuja Dar"
"Kha!! ilikuwaje sasa, si yule babaake marehemu ocs wa Mkuyuni?"
"haswaaa, yaani aaagh! namkumbuka vizuri alikuwa mkubwa wangu na mtu wa karibu kipindi hiko daah!"
"Daah! shit, amepona?"
"Bado hatujapata hakika"
Baada ya Shebby kuzipata habari zile muda ule ule alichukua simu yake na kumpigia kamanda wa mawasiliano ya idala ya dharula na alipouliza walithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na tayari kuna timu ya vijana ilikuwa njiani kuelekea huko.

Aliingia ndani Shebby na kujiandaa kwa kuvaa gwanda zake hali iliyowashangaza wazazi wake na kumuuliza kulikoni lakini alichojibu kiliwashangaza wote.
"Baba najua ni ajali tu imetokea lakini kuonana na mzee Cyplian ni jambo la muhimu sana kwangu ktk njia za kumjua mr X"
alijibu Shebby na kutoka mkuku na kuchukua gari aina ya Jeep na moja kwa moja aliondoka kwa speed maeneo ya kwao mara baada ya mlinzi kufungua geti huku akiwa hataki kusikia chochote toka kwa babaake ala mamaake.

Mwendo aliokuwa anatembea Shebby nimeshindwa hata kuuelezea mara baada ya kupita maeneo ya Kibaha na kutembea upande ambao ulikuwa haumruhusu lakini alifosi hivyohivyo huku akipiga honi mfurulizo lakini ghfra alipokuwa anapandisha kilima cha kuingia Mlandizi almanusura nae apate ajali baada ya kukosana na gari ndogo aina ya toyota creaster uso kwa uso na kusababisha wote wayumbe na yule dereva mweney wa toyota bado kidogo atumbukie mtaroni lakini nae alikuwa mtaalam sana na alifanikiwa kuidhibiti gari na kutulia tena barabarani na kuangalia nyuma kwa kutumia site mirror ambapo aliishuhudia ile Jeep nayo ikiendelea kuambaambaa pembeni ya barabara na kukaa sawa huku speed ikiwa pale pale.
Chaajabu alitabasamu yule dereva badala ya kuchukia na kuendelea kupiga gea na hakuwa mwengine bali ni yule yule binti aliyejiziba uso kwa nikabu ambae Cj4 alimtilia shaka kule Chalinze.

Upande wa Shebby alikuwa nusu mzima nusu kichaa kwani alipoituliza tu gari mwendo ukawa uleule tena utadhani ndio kaambiwa aongeze vile huku akizipita gari kibao zilizokuwa zinaenda polepole kutokana na foreni nae kuweza kupita barabara ya pili akisaidiwa na sare alizovaa hakuweza kusimamishwa na askali yeyote mpaka alipoukaribia msafara uliokuwa unaelekea eneo lilelile la ajali na kufika nao pamoja.

"Wapi mzee Cyplian? wapi mzee Cyplian?!"
aliuliza Shebby mara tu ya kusimamisha gari ambalo wengi walilikwepa kwa jinsi lilivyokuwa linakuja kasi na polisi wa pale wote walishindwa cha kufanya mara baada ya kumuona dereva wake akiwa kawazidi cheo wote waliokuwapo pale.
"Wapi mzee Cyplian"
aliuliza tena Kamishna Shebby safari hii akimfata Seneor Inspector ambae ndie alikuwa mkubwa wa pale kipindi shughuli za uokoaji zikiendelea.
"mkuu ndio sasa ivi ambulance iliyobeba mwili wake imetoka."
"Whaat! ina maana amefariki?"
"Ndio mkuu ila ambulance ile ndio yupo inspector aliyekuwa anamuendeesha nae hali yake si mbaya sana ila amepoteza fahamu"
aliongezea yule s.inspector huku akiionesha kwa kidole ambulance iliyokuwa inatoka na palepale Kamishna Shebby aliingia kwenye gari na kuifatilia ile ambulance mpaka hospital ya Tumbi na pindi ilipopaki alishangaa kuona yule mgonjwa ambae ndie Inspector aliyekuwa anamuendeesha mzee Cyplian akishuka mwenyewe huku akiwa na bandeji kubwa kichwani akiwakataa polisi na madaktari waliomleta pale kuingia hospitali na kuichomoa ile sindano ya dripu aliyowekewa kwenye gari na kuanza kuondoka huku akiwa kama mtu aliyechanganyikiwa lakini anajiamini mno.
Hapo ndipo Shebby aliposhuka na kumfata yule inspector ambae ndie Cj4 huku akiwazuia askali wote waliokuwa wanajaribu kumzuia na kumuingiza hospital na kutokana na ukubwa wa Shebby wote walitii na hapo kwa mara ya kwanza Shebby alionana uso kwa uso na Cj4 huku akiwa hamjui ni nani hasa nae Cj4 alitabasam kuonana na Shebby huku akiwa anajua kila kitu ni nani hasa nyuma ya pazia.

"Nakufahamu wewe ni Kamishna Shebby nilisimama kwenye nafasi yako kuendeleza ulichokiacha, tuwahi haraka Dar kabla hajatoweka."
aliongea Cj4 na kuingia kwenye Jeep huku Shebby akiwa ametumbua macho akiwa haelewi nini anamaanisha yule inspector na imekuaje aongee kwa kujiamini vile ilihali yeye ni mkubwa kuliko yule inspector.
"Twende Kamishna tuiwahi crester iliyombeba muuaji."
Alipoongea maneno haya sasa Shebby alielewa kitu haraka na kuwahi kwenye gari na kuigeuza kwa fujo huku askali na madaktari wote wakishangaa kile kilichokuwa kinaendelea.

Ilikuwa ni ajabu na kweli ndani ya vichwa vya watu kwa kila aliyeiona ile gari jinsi ilivyogeuzwa na kuondoka eneo lile kwa speed ya hatari mithili ya gari ya mashindano huku Cj4 akiufurahia ule mwendo ambao kwake yeye Kamishna Shebby aliona kama vile gari ilikuwa haitembei kabisa.
"Inspector! Umesema ni Creaster nyeupe?"
aliuliza Shebby huku akiwa makini na barabara ambapo aliwasha taa zote full mbali na kuwa haukuwa usiku.
"Yap yap nyoosha mguu nyooshaa"
alijibu Cj4 kwa msititizo na kikatawala kimya baina yao zilibaki kusikika tairi za gari zikilalamika honi mfurulizo na muhemo wa injini tu.

Lakini walipofika maeneo ya Kibamba pale njia panda ya kijiji cha Hakipo walishangaa kuuona moshi mzito umetanda pia waliuona umati wa watu kwa mbali na askali wa usalama barabarani sambamba na gari ya zima moto huku askali moto wakiwa bussy kuzima moto uliokuwa unawaka na kusababisha hali ya hewa pale kuwa na ukungu uliosababishwa na Moshi.
Walisimama na kushuka mkuku mkuku eneo lile na kuwahi kushuhudia kilichotokea wakiwa na wasiwasi isije kuwa ni yuleyule mtu aliyekisiwa na Cj4, na kweli baada ya kushuka na kusogea kuangalia kilichokuwa kinawaka walishangaa kukuta ni gari ndogo na walipoichunguza vizuri ilikuwa ni ileile Toyota Creaster aliyokosa kosa kugongana nayo Shebby na ndio ile aliyopanda yule mwanamke aliyemtilia mashaka Cj4
"Vipi afande ilikuwaje?"
aliuliza Kamishna Shebby kwa mmoja wa askali barabarani (trafic)aliyekuwapo maeneo yale baada ya kupokea heshima yake
"Ni ajabu kidogo mkuu, tulipigiwa simu na raia wema kwamba kuna moto umezuka kutoka kwenye hiyo gari na umekutwa mwili wa mwanamke mmoja ambae inasadikika alikuwa dereva wa hiyo gari akiwa kaungua vibaya mno."
alijibu yule afande na kumfanya Shebby akune kichwa na kushusha pumzi lakini Cj4 alicheka na kumvutia pembeni Kamishna Shebby.
Vitendo vya Cj4 kutomtetemekea wala kueka nidhamu ya uoga kwa Shebby ilizidi kumshangaza Shebby na kujiuliza huyu ni askali gani mwenye cheo kidogo kuliko yeye lakini haoneshi kuogopa wala kumnyenyekea mkubwa wake na kufikia hadi hatua ya kumshika mkono na kumvutia pembeni? lakini alijikuta anashindwa kumkatalia wala kumuuliza na kukubali kusogea nae pembeni.
"Vipi inspector?"
aliuliza Shebby kwa taharuki mara baada ya kuvutiwa pembeni na Cj4 wakati yeye alikuwa bado anahoji kilichotokea.
"Tushamkosa, kashatuzidi akili"
"Kivipi?"
"Huyu mwanamke muuaji"
"Muuaji, lakini mbona na yeye amekufa! hapa lazima kutakuwa na mtu aliyemuua"
aliongea Shebby kauli iliyopingwa na Cj4
"Hapana Kamishna, huyu mwanamke ni special Killer na anajua kupoteza ushahidi. nina imani yule aliyeungua si yeye"
aliongea Cj4 na kumfanya Shebby abaki na taharuki akishangaa maneno ya Cj4, na kuanza kuhisi huenda huyu si askali wa kawaida.
"Sikia Shebby, washa chombo twenzetu turudi taratibu eneo la tukio ukaniache hapa hakuna kitachoweza kutusaidia ila maswali yote unayojiuliza nitakujibu tukiwa njiani"
aliongea Cj4 na kumfanya Sheby awe mpole na kuingia kwenye Jeep na kuanza kuendeesha kuelekea walipotoka huku akiwa anajiuliza mara mbili mbili kuhusu inspector wake ambae licha ya kuwa ameumia sehemu za kichwa na hata ile bandage aliyofungwa kwenye ambulance ilianza tena kuvujisha damu lakini hakuonekana kujali.
"Enhee, kwanini Inspector unalazimisha turudi tena eneo la tukio?"
"Kule ndipo tutapata uelekeo wa sababu za ajali na alipotokea muuaji aliyetuzidi akili."
"Kivipi sasa katuzidi akili?"
"Si umeona katengeneza kifo fake!!"
"Kifo fake? kwa hiyo unataka kusema yule aliyeungua si muhusika?"
"Ndio maana yake ni kamchezo kadogo sana, nahisi kumbukumbu zako zimerudi unakumbuka nini kuhusu Mkuyuni?"
alijibu Cj4 na kumuunganishia swali Kamishna Shebby lililofanya amtazame na kuamua kumjibu kiunagaubaga
"Mkuyuni nakumbuka vifo tu"
"Nina mashaka na muuaji wa Mkuyuni anaweza kuwa yuleyule mwanamke aliyesababisha ajali"
aliongea Cj4 maneno yaliyomfanya Kamishna Shebby kufunga breki za ghafra za gari na kupaki pembeni huku akimuangalia kwa mshangao Inspector wake.
"Unasema??"
aliuliza Shebby mithili ya mtu aliekuwa na matatizo ya masikio mara baada ya kusimamisha gari.
"Nina wasiwasi na yule mwanamke aliyesababisha ajali ndie aliyewashambulia Mkuyuni."
"Khaaa! wewe ni Inspector kweliiiii ama umevaa sare tu?"
aliuliza Shebby akionesha kuanza kuwa na wasiwasi na Cj4 kutokana na maneno yake kugusa mulemule
"Hapana mimi ni Inspector kwa sasa... Naitwa Inspector Sudy kama ilivyoandikwa"
alijibu Cj4 na kumshangaza sana Shebby
"Sawa Inspetor hata mimi naanza kukubaliana na wewe kuwa ule mwanamke ndie aliyetushambulia Mkuyuni"
aliongea Shebby na kumfanya Cj4 amuangalie kwa umakini na ndipo Shebby alipozidi kufunguka
"Nilimshuhudia muuaji wa Mkuyuni kabla hajanipiga risasi ya mguu, alikuwa ni Ninja wa kike ila kwa bahati mbaya nilimjua kwa sauti tu na muonekano lakini sikubahatika kuona walau macho yake yalivyo kutokana na miwani aliyovaa"
"So, unadhani kwanini alikuacha? wakati wenzako wote aliwaua?"
aliuliza Cj4
"Mh! kwakweli hata mimi sikudhani kama angeniacha ila nakumbuka alichosema kuwa eti nina bahati na kunipa agizo toka kwa mr X kwamba nisije kuthubutu kumtafuta tena mr X kwa usalama wangu. Lakini pia kuna kauli alinambia ambayo ilinichanganya sana hadi sasa"
"Ipi hiyo?"
"Alinambia iwapo nataka kupambana na Mr X basi inatakiwa nianze kufanya mazoezi ya kusimama juani na kupambana na kivuli changu mpaka nikikamate"
"Aaaahaa sasa naanza kupata taswira"
aliongea Cj4 huku akifikiria kitu na kumshangaza zaidi Kamishna Shebby.
"Taswira gani tena Inspector!"
"Juu ya mr X"
"kivipi?"
"Nina wasiwasi mr X ni mtu aliye katika mzunguko wa maisha yako ya kila siku."
"Mhh! mbona sikuelewi unamaanisha nini?"
"Namaanisha mr X ni mtu anayekujua vizuri na inawezekana nawe ukawa unamjua pia, na anapatikana katika sehemu kuu tatu"
"Mbona sikuelewi wee Inspector? ni sehemu gani hizo?!"
"Usipanic Shebby, nina wasiwasi mkubwa kuwa mr X ni mtu anayepatikana katika mzunguko wa maisha yako ya kila siku yaani kazini, serikalini ama nyumbani."
"Nyumbani?"
"Yap, huenda akawa na ukaribu hata na babaako mzazi, au huenda akawa moja ya wakuu wako wa kazi ama kiongozi mkubwa serikalini aidha mstaafu ama bado yupo madarakani"
maneno ya Cj4 yalizidi kumchanganya kabisa Shebby na kabla hajauliza tena lolote ndipo Cj4 alianza kufungua vifungo vya shati ya sare ya kipolisi aliyovaa na kuisogeza pembeni vest yake na kumuonesha eneo la kifua Shebby ambae macho yalimtoka baada ya kuona mchoro wa bawa na alama za Komandoo wa Jeshi.

"Usistuke nimeingia kwenye hii kazi kwa msaada wa kupoteza kwako fahamu, mimi si polisi ila kama unataka kazi hii ifanikiwe na tumgundue huyu mshenzi mdogo inatakiwa asijue mtu yeyote kama kumbukumbu zako zimerudi"
aliongea tena Cj4 huku akifunga vifungo vya shati yake na wakati huo wote Shebby bado alikuwa katumbua macho akiwa haamini kuwa kumbe yule aliyekuwa anazunguka na kuzungumza nae muda wote ni Komandoo wa heshi!!
"Zingatia Kamishna kwa usalama wako na urahisi wa kazi hii. take care twenzetu tukapate mchoro eneo la tukio lakini kumbuka hii tunajua mimi na wewe"
aliongea tena Cj4 na ndipo Kamishna Shebby alipoanza kuondoa gari huku akiitika kwa kichwa akiwa bado haamini kilichokuwa kinaendelea hadi serekali wampandikize Komandoo katika kazi ile.

* * *

Baada ya Kamishna Shebby na Cj4 kufika tena Chalinze eneo la tukio na kufanya utafiti wa siri walioujua wao kabla ya Cj4 kukubali kujishusha na kuingizwa tena kwenye ambulance ambayo ilitokea ikulu pasi na mtu yeyote kujua na madaktari waliokuwa mule karibu wote walikuwa ni wanajeshi lakini walifanya hayo kwa agizo la mkuu wa majeshi kuwa wao ndio waondoke na yule dereva wa marehemu mzee Cyplian kwa lengo la kuwazubaisha hadi polisi wengine wasijue nini kinaendelea kwani isingekuwa vyema Cj4 kutibiwa na raia ama polisi wa kawaida.

Baada ya Kamishna Shebby kuondoka eneo la tukio huku akiwasiliana na baadhi ya wakubwa zake akijifanya bado kumbukumbu zake hazijarudi kama alivyoagizwa na Cj4 alifika nyumbani huku kichwa kikiwa kinamuwaka moto akiyakumbuka maneno ya Cj4 na kuona kweli mr X anatumia akili nyingi sana na inawezekana kabisa yupo katika mzunguko wa maisha yake ya kila siku.
('Mh! sasa itakuwa nani? au mh Wazili? mhh sidhani.. au Kamanda mkuu anatuzunguka? Mh! !!')
aliwaza Shebby usiku pindi alipokuwa ndani lakini mara akiwa katika mawazo mazito alipokea ujumbe wa sms kutoka kwa Dk Asha ambae alikuwa mchumbaake akimlaumu kwa kupata riport kuwa alielekea eneo la ajali iliyotokea mchana huo mbali ya kuwa bado likizo yake ilikuwa haijaisha.
Alitabasamu na kuendelea kuchart na baby wake Asha japo ukweli moyoni alikuwa na mawazo mengine kabisa.

* * * * *

Siku kadhaa zilisonga huku ukweli wa chanzo cha ajali ya Chalinze ukibaki kuwa wa kubahatisha na hata kile kikao cha siri alichopanga mh Rais kifanyike kiliahilishwa kwanza na kuupisha msiba uliozuka ghafra wa Kamanda mkuu mstaafu wa jeshi la polisi mzee Cyplian na kuzidi kuwachanganya wakubwa wa serikali washindwe kuthibitisha moja kwa moja juu ya ajali ile ilikuwa imetengenezwa ama laah.
Hii hata mkuu wa Majeshi ilianza kumpa wasiwasi mara baada ya kupokea ripoti toka kwa Komandoo waliyemchomeka na kumwambia kuwa ajali ile ilisababishwa na watu wa mr X so, ni lazima kwenye kikao cha siri walichofanya kutakuwa na spy anayevujisha siri kwa mr X ama mr X mwenyewe anaweza kuwamo kwenye vikao vyao.
Na ripoti hii ilifikishwa kwa mh Rais tu na kukubaliana na ushauli wa mkuu wa majeshi kuwa haina haja ya kutangaza tena ile ripoti wala kueka tena kikao huku akimuahidi kuwa kijana wake shupavu ataifanya hiyo kazi na mr X atakuja kuletwa mbele ya macho yake siku moja.

Kamishna Shebby alirudi rasmi kazini huku akiigiza bado kumbukumbu zake hazijarudi na kuwashangaza tena wazazi wake ambao awali walikuwa na uhakika kuwa mtoto wao kumbukumbu zimerudi.
Hali hii ilimliza sana mamaake Shebby na kumuombea kila siku alipokuwa anasali akiwa haelewi inakuaje mtoto wao mara kumbukumbu zirudi mara zipotee tena?
Hata mzee Mwinchande hii ilimshangaza sana lakini ukweli ulibaki katika moyo wa Shebby na Cj4 huku wakiendeleza mission yao ya siri ya kumnasa mr.X pasi na mtu yeyote kujua.

* * * *

Ilikuwa ndio siku rasmi ya kutoka kwenye makazi ambayo hakutegemea kama angetoka tena mara baada ya msamaha wake kutangazwa na kupitishwa wiki chache zilizopita na Mh Rais wa Tanzania.
Geti kubwa lile la mwisho lilifunguliwa kwa mitambo ya umeme na oparator aliyekuwa kwenye moja ya jengo la usalama wa gereza lile na mwanga wa nje ukaanza kummulika Hussein babu bubu huku akiwa haamini kama kweli leo hii anakuwa huru kwa mara nyengine japo alikuwa hajui wapi aelekee kwani wenzake wote waliotangazwa kuachiwa walipokelewa na ndugu jamaa na marafiki kadha wa kadha waliokusanyana nje ya geti la gereza kuwasubiri isipokuwa yeye tu.
Akiwa kava nguo mpya alizonunuliwa na serikali huku mkononi kabeba kijibegi kidogo chenye nguo za kubadilisha na shuka ikiwa ndio vitu pekee alivyoambulia kama msaada kutoka serikalini juu ya maisha yake mapya anayoenda kuyaanza huko uraiani.
Alimshukuru mungu na kuanza kupiga hatua mdogo mdogo akiifata barabara ndogo ya lami iliyoenda kukutana na barabara kubwa katika njia panda ambapo kulikuwa na stendi ya daladala japo hakujua hata akifika hapo stendi atapanda gari ya wapi ama atafikia wapi na mfukoni alikuwa na kiasi cha shilingi elfu tano aliyorudishiwa ikiwa ni pesa aliyokutwa nayo kipindi anakamatwa miaka iliyopita ambayo kwa kipindi hiko ilikuwa haina thamani kabisa ya kumsaidia mtu walau siku tatu.
Lakini akiwa anaendelea kupiga hatua huku kichwa akiwa kakiinamisha chini akienda huku anatafakari mara alisikia muungurumo wa gari ikitokea nyuma yake upande ule wa gereza na kuchapukia pembeni kwa kuipisha lakini alishangaa ile gari ikisimama karibu yake na kushushwa kioo na mara sauti ya mtu ambae alikuwa dereva wa ile gari ilisikika akimwita na aliposogea kuchungulia hakuamini kuona ni Kamishna Shaaban na ndipo alipoingia garini akiwa haamini kama amekutana tena na kijana aliyetokea kumuhusudu kupita binaadam yeyote tangia aanze maisha ya jera.
"Kamishna baba!! aah, siamini mwanangu kumbe umerudi"
aliongea huku chozi la furaha likimdondoka Hussein babu kwa kutoamini kabisa hasa mara baada ya Shebby kuvua miwani meusi aliyovaa na kofia.
"Nimerudi baba nakaribia wiki sasa, hongera sana kwa kupata uhuru hatimae unarejea uraiani"
alijibu Shebby kwa furaha ya kukutana tena na Hussein
"Ahsante mwanangu leo hii nimekumbuka sana maneno yako pindi nilipokuwa natoka rasmi pale getini daah! mwanangu pole sana kwa matatizo.. Naomba unisamehe sana"
aliongea Hussein huku akiendelea kufuta machozi yaliyokuwa yanatililika mashavuni mwake ghafa kila alivyokuwa anamuangalia Kamishna Shebby
"Hapana baba, hupaswi kuniomba msamaha kwani ile ilikuwa ni moja ya kazi. Usijali babaangu kwakuwa leo hii upo huru hata moyo wangu umefurahi sana najua kazi niliyobakiza ni moja tu"
"Kazi gani tena baba"
"Nataka kumjua huyo mr X nilipe kisasi"
"Haa! sasa kisasi cha nini tena mwanangu wakati mi nishakuwa huru! isitoshe naomba swala hilo niachie kwani mi mwenyewe nataka nilipe kisasi kwa mr.X nishasali sana miaka yote nikiwa jera kumuomba Mungu anitendee muujiza siku moja nitoke jera na nikamuue mr X kwa mikono yangu na mpaka sasa naona Mungu kashaanza kunijibu dua zangu. Futa mawazo ya mr X mwanangu sitaki nikuponze tena hii ni kazi yangu sasa ni zamu yangu"
aliongea Hussein babu kwa hisia kali na safari hii machozi yaliacha kumtoka huku akimuangalia kwa umakini Shebby ambae sasa alianza kuiondoa gari taratibu na kuelekea kule alipokuwa anaelekea Hussein na alipoifikia ile barabara kuu alikunja upande unaoenda kutokea Kongowe.
"hahaha, hapana baba si rahisi kama unavyofikiria lakini pia sifanyi kwa sababu ya wewe tu bali nafanya kwa sababu ya rafiki zangu wote waliokufa"
alijibu Shebby huku akizidi kuongeza mwendo wa gari
"Mwanangu nakuomba chondechonde mi sina ubora wowote niliobakisha wala thamani hapa duniani hivyo hata kama kumuua kwa kumpiga nisipoweza, niko tayari hata nijilipue tufe wote lakini si wewe kurudi tena kwenye matatizo baba nakuomba"
alisisitiza Hussein lakini Shebby hakuonesha kujali sana zaidi ya kuongeza mwendo mpaka walipoipita Kongowe na kuanza kuufata muelekeo wa mbagara na walipofika Mbagala Zakiem aliingiza gari kwenye parking ya hoteli moja mpya ya kisasa iliyokuwa pale Zakiem na kumuomba Hussein waongozane kuingia kwenye ile hoteli na kumshangaza sana Hussein mara baada ya kushuhudia Kamishna Shebby akimlipia chumba na bili ya chakula cha wiki nzima pale hotelini.
"Usijali baba utakaa hapa kwa wiki moja kipindi nikikutafutia makazi rasmi ya kuishi usiwe na wasiwasi simu hii utatumia kwa mawasiliano endapo kutatokea tatizo, line yake imeunganishwa na kifurushi cha wiki na ina namba mbili tu zilizoseviwa na zote ni za kwangu.. Kuwa na amani baba"
Ni maneno ya Shebby pindi walipoingia kwenye chumba cha hoteli kilichokuwa ghorofa ya pili ambapo Hussein alibaki kataharuki tu akiwa haamini moyo wa yule kamishna na vile anavyojitolea kiasi kile kumsaidia ilihali hawana undugu wowote.
"Mi nahitajika kuwahi tena gerezani baba, ila hii Elfu hamsini itakusaidia kwa matumizi madogo madogo na ya dharula"
"Asante babaaa.. aaaah Asante sana mwanangu Mungu akuzidishieeee eeeh!! Akulinde na kila shari jamaniiii Asante babaaa"
alishukuru hadi akapiga magoti Hussein lakini Shebby alimuinua na kumsihi asijali kabisa kisha aliagana nae na kutoka hadi ilipopaki gari yake.
["Hallow, yah Cj4 kazi kwako sasa tayari nishafanikisha yupo chumba namba 90 ghorofa ya pili"]
yalikuwa ni maneno ya Shebby kwa njia ya simu akiongea na Cj4 mara baada ya kuingia ndani ya gari yake na kuanza kugeuza kuondoka maeneo yale.

Ulikuwa ni mchezo wa akili nyingi waliokuwa wanaufanya Kamishna Shebby na Cj4 na muungano wao hakukuwa na mtu mwengine yeyote aliyekuwa anaujua, na kumbe Cj4 alikuwa na jukumu la kuchunga usalama wa Hussein babu na kumfatilia pale kwenye ile hoteli ama ikitokea ametoka ama kama kuna mtu yeyote atayekuja kuufatilia uwepo wake pale basi atashughulika nae.
Naam na huo ulikuwa ni ulinzi na usalama mkubwa uliomzunguka Hussein pasi na yeye mwenyewe kujua hadi atapojulikana mr X ni nani.

* * * * * *
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom