Majambazi Wakenya Walivyotikisa na Kuweka Historia Kanda ya Kaskazini Nchini Tanzania

Kipindi icho itv walilirusha tukio la vita ya awo jamaa Njiro, aisee ile ghorofa ya njiro ili tapakaa risasi, na miaka iyo Arusha na ujambazi damudamu, arusha haikuwa sehemu salama kuishi kama una mali, na kwa watu wasioishi Arusha pichani mwao hadi sa hivi fikra zao wanafikiri Arusha muda wowote ni vitavita tu, na wakisikia unaenda uko basi utapewa husia wa maanana ndo maana siku hizi kati ya mkoa unaoongoza nyumba nyingi kulindwa na kampuni za ulinzi kama SGA, Garda na nyingi ni Arusha , nenda Njiro utajionea kila jumba getini lazima ukute kibati cha this premises protected by SGA, KK security now days as GardaWorld na mi dogs juu aswa mi bulldogs, Germany shepherd na species nyingine , kwa utashi wangu ukizubaa tu kuishi bila ulinzi imekula kwako, sema wachagga ni noma kwenye kutafuta pesa , ukizubaa tu umekwendamfano ni tukio La billionaire wa Tanzanite , Msuya, ila naskia pia mahotels mengi, business nyingi na majengo ni ya majambazi wa zamani ambao walishafariki au kuokokasema wachagga wana akili kwenye matumizi ya pesa ata kama ni za ujambazi ila atafanya investment za maana,
Tulikuwa tunangoja muendelezo wa hi story afadhali imeiendeleza na kuimalizia kabisa mkuu. Thanks a lot
 
Kipindi icho itv walilirusha tukio la vita ya awo jamaa Njiro, aisee ile ghorofa ya njiro ili tapakaa risasi, na miaka iyo Arusha na ujambazi damudamu, arusha haikuwa sehemu salama kuishi kama una mali, na kwa watu wasioishi Arusha pichani mwao hadi sa hivi fikra zao wanafikiri Arusha muda wowote ni vitavita tu, na wakisikia unaenda uko basi utapewa husia wa maanana ndo maana siku hizi kati ya mkoa unaoongoza nyumba nyingi kulindwa na kampuni za ulinzi kama SGA, Garda na nyingi ni Arusha , nenda Njiro utajionea kila jumba getini lazima ukute kibati cha this premises protected by SGA, KK security now days as GardaWorld na mi dogs juu aswa mi bulldogs, Germany shepherd na species nyingine , kwa utashi wangu ukizubaa tu kuishi bila ulinzi imekula kwako, sema wachagga ni noma kwenye kutafuta pesa , ukizubaa tu umekwendamfano ni tukio La billionaire wa Tanzanite , Msuya, ila naskia pia mahotels mengi, business nyingi na majengo ni ya majambazi wa zamani ambao walishafariki au kuokokasema wachagga wana akili kwenye matumizi ya pesa ata kama ni za ujambazi ila atafanya investment za maana,
 
SEHEMU YA TATU

MOJA katika mchoro huo ni idadi ya watekelezaji wa ujambazi huo katika benki ya NMB MWANGA, kwa mujibu wa “mastermind” mwenyewe ambaye ni MACHO MBAYA aliona kunahitajika watekelezaji sita [6] tu ili mchoro utendewe haki na ujambazi wao kufanikiwa.

Hapo wao majambazi WAKENYA ni watatu basi kutaongezwa majambazi wengine watatu ambao watakuwa WATANZANIA na suala la washirika hao kupatikana na kutumika katika utekelezaji wa mchoro wao ilikuwa jambo rahisi wakisaidiana na washirika wao.

MACHO MBAYA alichofanya ni wao majambazi WAKENYA ndo watakuwa mstari wa mbele katika ujambazi huo kwa zaidi ya asilimia 90 wao ndo watahusika na alipanga hivi ili kuepusha makosa madogo kutendeka kwa kujiamini wao hawawezi kufanya makosa madogo ni wako makini kupitiliza na kwenye utekelezaji tutaona jinsi wao watakavyokuwa mstari wa mbele.

MBILI katika mchoro huo kunahitajika magari mawili ya kazi hiyo ya ujambazi na MACHO MBAYA alipendekeza gari ziwe za kazi zinazotembea haswa na aina ya magari ambayo MACHO MBAYA alitamani yawe ni LAND CRUISER na TOYOTA COROLLA 100.

Gari aina ya LAND CRUISER haina mjadala inajulikana ni gari la kazi lenye nguvu na spidi ya kutembea iwe vumbi au lami na TOYOTA COROLLA 100 ni gari ambazo zimepata sana umaarufu kwenye suala la kukimbia na kupelekea matukio mengi ya kijambazi AFRIKA MASHARIKI kutumia sana gari aina hiyo ambayo hata bei yake ni ya kawaida tofauti na magari kama LAND CRUISER.

Upatikanaji wa magari hayo ni kazi ya mfadhili wa ujambazi huu na kwa magari mawili hayo itakuwa gharama sana kwake na MACHO MBAYA alijua hilo na kuja na mpango mbadala wa kuweza kupatikana magari hayo ambao ni uwizi kufanyika.

Wataalamu wa uwizi wa magari wapo na ikumbukwe MACHO MBAYA uwizi wa magari ndiko alikoanzia wakati anaanzisha utawala wake na pia katika matukio yake ya ujambazi mkubwa na genge lake magari waliyokuwa wanatumia ni ya uwizi ili wakishayatelekeza baada ya ujambazi wamiliki wa magari hayo watajijua wenyewe na polisi.

Mchoro mdogo wa uwizi wa magari ukachorwa na gari ya TOYOTA CORROLA 100 ni rahisi sababu zimejaa na ilipatikana haraka gari yenye namba za usajili T 979 AMY na mziki ukabaki LAND CRUISER ambayo ilisumbua kidogo kwa kupatikana tarehe 5 julai 2007.

LAND CRUISER ilikuwa na namba za usajili T 258 CD 11 ambayo ilikuwa mali ya UMOJA WA MATAIFA kwa kuibiwa katika ofisizi za UMOJA WA MATAIFA jijini ARUSHA, wakina MACHO MBAYA wanapotaka jambo lao hawajali cha UMOJA WA MATAIFA wala nini wao wanaagalia gari gani imewakalia pembe nzuri.

Upatikanaji wa magari haya ulienda vizuri na kuhifadhiwa kusubiri siku ya tukio na ilipangwa baada ya ujambazi yatatelekezwa kama walivyokuwa wanafanya nchini KENYA na upande wao hawana hasara ikizingatiwa mzigo mnene watakaoiba na wakisema waendelee kuyamiliki yataweza kuwatokea puani hata kama watayapitisha kwenye zile gereji za kubadilisha muonekano wa magari ya uwizi.

TATU katika mchoro huo pumziko la majambazi litakuwa SANYA JUU wilayani SIHA mkoani KILIMANJARO na baada ya kupumzika hapo kuangalia upepo wake ndo watarudi makao makuu yao NJIRO walipopanga jijini ARUSHA.

Jambazi MACHO MBAYA aliona ni hatari sana wakitoka wilayani MWANGA watakapofanya ujambazi wao mpaka NJIRO jijini ARUSHA ambako kuna kilomita takribani 134 na ikumbukwe wanavuka mkoa mwingine ila wakitoka wilayani MWANGA na kuchepukia SANYA JUU wilayani SIHA kupumzika hatari yake iko chini ikilinganishwa na kuelekea moja kwa moja jijini ARUSHA.

Pia hapo SANYA JUU wilayani SIHA ndiko mgawanyo wa fedha zilizoibiwa utafanyika nyumbani kwa mfadhili wao bwana KANJE, kwahiyo wakati fedha zinagawanya baina yao wanaangalia pia upepo unavumaje kutokana na tukio lao la ujambazi ili sasa warudi zao jijini ARUSHA.

NNE katika mchoro huo ni kufanyia mazoezi barabara watakazopita katika ujambazi wao maana ikumbukwe wakina MACHO MBAYA ni wageni kwahiyo wasije wakajikuta wanatoka wilayani MWANGA na kuelekea wilayani ROMBO wakijua wanaelekea wilayani SIHA.

Wilaya za SIHA na ROMBO zote ni wilaya ambazo zinachepuka ndani kwa kuacha barabara kuu ya mkoa na kama mtu mgeni anaweza kufanya makosa na ikawa faida kwa vyombo vya ulinzi na usalama vya TANZANIA kuwadhibiti sababu ya majambazi kupoteza muelekeo.

Mazoezi ya barabara yalifanyika siku chache kabla ya ujambazi wenyewe kwa watendaji wote wa ujambazi maana nini kitatokea siku hiyo hakuna jambazi anayejua kwa kuwezakana kupanga dereva kuwa mtu fulani halafu bahati mbaya kwenye purkushani akauliwa au kujeruhiwa nani ataendeleza kusongesha gari na ikumbukwe kutakuwa na magari mawili.

Mwisho wa siku mchoro unafeli sababu waliobakia kwenye gari hawajui muelekeo kwa barabara kuwachanganya na kupoteana kwenye mchoro wao, na hili “mastermind” MACHO MBAYA hakutaka litokee kwao kwa kuhakikisha kila mtendaji wa ujambazi anajua barabara watakazopita.

TANO katika mchoro huu kutatumika akili nyingi sana kuliko nguvu na MACHO MBAYA alichopanga ikiwezekana nguvu isitumike kabisa kwa kutomjeruhi wala kuua mtu katika ujambazi wao na hiyo ni nzuri upande wao kujipunguzia mzigo wa kesi na nguvu kubwa ya vyombo vya ulinzi na usalama kuwatafuta wao baada ya tukio.

Tukio la ujambazi likihusisha mauaji linakuwa na presha kubwa sana kwa vyombo vya ulinzi na usalama kuongeza nguvu zaidi katika kutafuta wahusika hasa waliouliwa wawe watu wao yani polisi, na pia ikitokea wahusika wamekamatwa hai wanakuwa na kesi mbili ya ujambazi na mauaji na kuchomoka kwake inakuwa ngumu sana.

Sasa kuepusha yote hayo ni akili nyingi itawalawe na hilo “mastermind” MACHO MBAYA alilisimamia huku changamoto kubwa ikiwa ni vipi akili kubwa itawazidi walinzi wa benki ya NMB ambao katika tafiti zake za kuandaa mchoro alijua wako wawili na wanatokea jeshi la polisi kitengo cha FFU.

Namna gani jambazi MACHO MBAYA alivyojipanga nao hao walinzi wawili wa benki ya NMB tutaona kwenye utekelezaji wa mchoro, na sababu nguvu itakuwepo katika ujambazi huu pale itakapolazimu ingawa “mastermind” alitamani na kujipanga nguvu isiwepo kabisa basi silaha lazima watazibeba.

Silaha hizo zitatumika kutishia na kutumika endapo italazimika kutokana na mazingira kubadilika maana walinzi wa benki ya NMB ambao ni polisi wana mafunzo ya kupambana na majambazi, sasa isije akili kubwa yao wakina MACHO MBAYA ikasawazishwa na walinzi hao na vita ikaanza baina yao halafu hawana silaha kwa kuamini akili kubwa yao tu, ni watakuwa wamekwisha.

Pia mtu akiona silaha anakuwa muoga na mtiifu kwa kila jambo analoambiwa akihofia kuuliwa kwahiyo MACHO MBAYA aliona vyema silaha ziwepo sababu zitakuwa na kazi ya kutishia pia ili kuwajengea hofu na kuwafanya kuwa watiifu kwa kila lisemwalo na wao majambazi.

SITA, mchoto huu ulianisha muda na siku ambayo ujambazi utatekelezwa katika benki ya NMB wilayani MWANGA mkoani KILIMANJARO na siku itakuwa tarehe 11 julai 2007 siku ya jumatano huku muda utakuwa jioni ya saa 1:30.

Jambazi MACHO MBAYA alipanga siku na muda huo kutokana na akili kubwa yake jinsi watakavyovamia benki hiyo ya NMB na muda huo benki inakuwa Imeshafungwa kwa kubaki walinzi tu eneo la benki na ndivyo “mastermind” alivyokuwa anataka kwa jambo lake kuamini litatiki muda huo.

Hayo mambo yote sita ndo yalikuwa mambo muhimu katika mchoro wa MACHO MBAYA kutekeleza ujambazi wake katika benki ya NMB tawi la MWANGA mkoani KILIMANJARO na hapo ilibaki utekelezaji tu kwa kusubiriwa hiyo tarehe 11 julai 2007.

UTEKELEZAJI WA MCHORO
Baada ya mchoro mzuri uliokwenda shule kukamilika na kila jambo la kutakiwa kukamilishwa kabla ya utekelezaji wa ujambazi kufanyika kuwa tayari mfano kufanyia mazoezi barabara watakazopita wao majambazi, kumezeshana mchoro wao majambazi n.k, sasa majambazi wakawa wanaangalia kalenda na saa yao wakisubiria siku na wakati ufike wakasimamishe mkoa wa KILIMANJARO.

Siku yenyewe kufika ambayo ilikuwa tarehe 11 julai 2007 timu ya majambazi ikiongozwa na “mastermind” MACHO MBAYA ilisogea eneo la tukio ambalo ni wilayani MWANGA wakiwa kwenye gari zao za kazi mbili zile LAND CRUISER na COROLLA 100.

Eneo la tukio walifika mapema tu ili kuangalia usalama wa mchoro wao uko asilimia 100 isije vyombo vya ulinzi na usalama vya TANZANIA vikawa na taarifa tayari za ujio wa ujambazi hapo na kuwawekea mtego wawakamate eneo la tukio.

Kwa muda waliofika na kukaa mpaka jioni ya saa moja kuingia waliona ni shwari tu hakuna mabadiliko yoyote na kuamini wako salama kuendelea na kilichowaleta na wakawa wanasubiri ifike saa 1:30 jioni ili utekelezaji wa mchoro uanze mara moja huku wakitegemea kabla ya saa mbili usiku wawe wamepotea eneo la tukio wanaitafuta SIHA.

Kengele ya saa zao kulia tu ina maana muda umefika na kazi kuanza mara moja kwa mchoro wa ujambazi kuanzia nyumbani kwa meneja wa benki ya NMB tawi la MWANGA aitwaye ROBERT MARANDO umri miaka 56 [kwa mwaka 2007] ambaye hakuwa anakaa ndani ya benki na ikumbukwe ghorofa iliyoko benki ya NMB hapo hapo kuna makazi ya wafanyakazi wa benki ya NMB.

Meneja wa benki bwana MARANDO baada ya kutoka ofisini alielekea zake nyumbani bila kujua atavamiwa siku hiyo na akiwa ameshaoga zake ametulia hana hili wala lile majambazi wakina MACHO MBAYA wakavamia ndani kwake na kuwaweka chini ya ulinzi familia nzima.

Familia ya bwana MARANDO ikaanza kuhaha kwa kutoelewa nini kinafuata sababu vipande vya watu vimeshika mitutu na MACHO MBAYA ndo muongeaji kwa ukali na mikwara ili kumchanganya meneja MARANDO atii kila atakachosema.

Jambazi MACHO MBAYA alimwambia meneja MARANDO kuwa yeye na familia yake wameshawateka na akijaribu kujifanya yeye mwanaume basi ajue atapoteza familia yake ila akiwatii basi atabakishwa salama yeye na familia yake maana hawana shida nao.

Meneja MARANDO akawa tayari kuwatii wakina MACHO MBAYA wanataka nini, na akaambiwa wataelekea wote benki ya NMB kuchukua fedha kupitia gari yake ambayo haitaleta mashaka kwa walinzi wa benki sababu wanamjua meneja na gari yake.

Yeye meneja kama ataulizwa lolote kuhusu muda huo usiku kufungua benki au aliombatana nao wakina nani basi yeye meneja atajua cha kuwazuga kuwa ni ishu ya kikazi na dharura ambapo haiwezi kusubiri kesho ifike na kwa majibu hayo hakutategemewa swali lingine ikizingatiwa meneja ndo bosi wa tawi la benki husika.

Pia akili kubwa hii ya ujambazi ilikuwa mpya nchini TANZANIA kwa kutowahi kutokea majambazi kuvamia benki kidizaini hiyo na walinzi inakuwa ngumu kujua ni ujambazi unatendekea huku meneja naye akijifanya yuko sawa hakuna lolote sababu anahofia familia yake na yeye watadhuriwa.

Nchi za wenzetu huko ujambazi wa aina hii ushawahi kutokea wa kudili na meneja kazi imeisha, meneja MARANDO kukubali kuwatii kwa lolote wasemalo ili mradi wasiwadhuru yeye na familia yake alimwambia MACHO MBAYA kuwa funguo na kuweza kuingia ndani ya kuba lazima meneja operesheni awepo ambaye ndo bibi SALOME MATEMU.

Jambazi MACHO MBAYA akasema hamna shida yeye meneja na familia yake wanaelekea nyumbani kwa bibi SALOME MATEMU kumteka na familia yake kama walivyofanya kwa familia yake na safari ikawa kuelekea huko na jambazi MACHO MBAYA akapanda gari ya meneja aina ya CARINA yenye namba za usajili T 524 AED.

Gari walizokuja nazo majambazi hazitaingia eneo la benki zitasubiri kusikilizia kiendeleacho na kama MACHO MBAYA alivyotaka ndivyo ilivyofanyika kwa majambazi WAKENYA kuwa mbele kila sehemu ili kuhakikisha mchoro unaenda vizuri kwa kujiona wao ni bora zaidi.

Ikumbukwe huyu meneja operesheni bibi SALOME MATEMU ndo yule anatajwa moja ya sababu iliyowafanya wakina MACHO MBAYA kuchagua benki ya NMB tawi la MWANGA mkoani KILIMANJARO ila ndo hivyo mahakama ilimuona hana hatia na ushirika wa ujambazi huu.

Wakina MACHO MBAYA kufika nyumbani kwa bibi SALOME MATEMU naye wakamteka na familia yake kwa kuelekea sasa benki wakachukue hela na mkwara ni ulizidishwa wakijifanya wajanja tu basi wamekwisha wao na familia zao.

Walinzi wa benki siku hiyo walikuwa ni KONSTEBO MICHAEL MILANZI na KONSTEBO NAFTALI ASHERY ambao jioni ya siku hiyo ndo walikuwa wameingia kazini lindo kwa kutegemea asubuhi kumaliza kazi ya lindo kwa kuingia walinzi wengine kutoka jeshi la polisi.

Walinzi hawa ilikuwa bahati mbaya siku hiyo ya zamu yao ndo majambazi wakina MACHO MBAYA nao siku yao ya kutekeleza mchoro wao wa ujambazi, walinzi wawili hawa waliona gari aina ya CARINA ndani ya eneo la benki ambayo wanaitambua kuwa gari ya meneja wa NMB hapo wilayani MWANGA.

Gari ikaegeshwa na wakashuka wakina MACHO MBAYA pamoja mameneja wawili wale waliotekwa huku nyuma majambazi wenzao wakina MACHO MBAYA wako wanasikilizia upepo wakiwa wamejikoki vizuri kwa kusubiri amri za mkuu wao MACHO MBAYA wafanye nini na ndo yuko eneo la tukio na majambazi wenzie WAKENYA.

Walinzi wa benki mzunguko wote wa gari la meneja wanauona ila hawakuhisi baya lolote sababu eneo hilo la benki ni makazi ya wafanyakazi wa benki kwahiyo ndugu na majamaa kuingia na kutoka ni kawaida na pia wageni hao ambao ndo wakina MACHO MBAYA walinzi walidhani ni ndugu zake mameneja hao sababu ya kuambatana nao.

Hii ndo shida katika benki ya NMB wilayani MWANGA kuwapa wakati mgumu sana walinzi kujua nani ni nani sababu ya jengo moja kushea benki na makazi ya wafanyakazi na kuwa faida upande wa majambazi tofauti na benki ambazo hazina makazi hapo hapo walinzi wakishaona mtu amezama eneo la benki wanajihadhari naye mapema kupitia mafunzo waliyonayo katika kupambana na majambazi.

Tukio hili la ujambazi benki ya NMB tawi la MWANGA KILIMANJARO lilikuwa fundisho kubwa kwa jeshi la polisi na mabenki kuwa eneo la benki wafanyakazi wasikae hapo inawapa mwanya majambazi kufanikisha ujambazi wao na mwishoe lawama zote zinakwenda kwa jeshi la polisi.

Kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi kitengo cha operesheni maalumu kipindi hicho bwana VENANCE TOSSI alivalia njuga suala hili la makazi ya wafanyakazi wa benki kukaa eneo moja na benki baada ya kutokea kwa tukio hili la ujambazi ili isijirudie na aibu kuangukia kwa jeshi la polisi ambao tukio lolote la ujambazi likitokea kwa kushindwa kuzuilika lawama zote wanabebeshwa wao bila kuangaliwa wazembe wengine.

Mameneja na wakina MACHO MBAYA wakiwa wanasogea mlangoni walinzi wakawa wanawaangalia jinsi wanavyokuja muda huo ambao benki imeshafungwa na polisi kwenye mafunzo yao wanasomea saikolojia kusaidia kutambua jambo kupitia muonekano yani macho, mikono, miguu,sura, mwendo n.k bila mhusika kuongea.

Mameneja walikuwa kwenye hofu ambayo mtu mwenye uwezo kuwasoma anajua hali si shwari na ikizingatiwa pia muonekano wakina MACHO MBAYA ambao walikuwa wamevalia makoti wakizuga baridi kali jioni hiyo kumbe wameficha silaha zao.

Walinzi walikuwa wakiwaangalia kiwasiwasi sana wakina MACHO MBAYA na kupelekea kujishtukia wameshahisiwa na wakiwaangalia walinzi hao silaha zao ziko mkononi tayari na kama kweli wamewashtukia basi wameisha maana watawawahi wao ambao watahitaji sekunde kadhaa kufungua makoti yao watoe mitutu yao.

Nguvu isitumike ikashindikana kwa kujishtukia na wakachomoa mitutu kwa kuanza kuwashambulia walinzi ambao walijibu kidogo sababu ya kuwahiwa na wakina MACHO MBAYA ambao waliwazidi kwa KONSTEBO MICHAEL MILANZI kufariki sababu ya majeraha ya risasi huku mwenzie KONSTEBO NAFTALI ASHERY akiwa hoi chini anavuja damu na amesalimu amri akiomba wakina MACHO MBAYA wasimmalize.

KONSTEBO NAFTALI ASHERY ashukuru sana MACHO MBAYA aliamka vizuri sana siku hiyo kwa kutommalizia ila ingekuwa siku zingine asingecheka naye lazima angemmaliza, na wakati walinzi wakiwa chini wanavuja damu wakina MACHO MBAYA waliwaharakisha mameneja kuzama ndani ya benki wakachukue chao waondoke.

Wenzao kusikia mirindimo ya risasi wakajua kumekucha na haraka walisogea eneo la tukio baada ya kuwasiliana na MACHO MBAYA ili waje kuweka fedha kwenye magari yao na sio gari la meneja tena sababu tayari nguvu ishatumika hakuna tena kurefusha mambo kama mwanzoni mchoro ulivyosema kwa nia ya kuficha ujambazi umetendeka machoni mwa walinzi.

Mabadiliko kama haya ya mchoro ndo yaliyomfanya MACHO MBAYA atake wao majambazi WAKENYA ndo wawe mstari wa mbele ili kukitokea mabadiliko yoyote wanajua nini wanafanya wasiharibu ujambazi wao tofauti na kuwapa kipaumbele majambazi ambao hawaamini uwezo na uzoefu wao pale kunapotokea mabadiliko ya gafla na isije wakapaniki na kuharibu kila kitu.

Meneja operesheni bibi SALOME MATEMU kufungua kuba wakina MACHO MBAYA wakasomba mzigo wao na kuupandisha kwenye gari la LANDCRUISER tayari kuanza safari kupotea eneo la tukio kabla polisi hawajawasili maana ile milio ya risasi ilishtua wakazi wa MWANGA MJINI ambao hawakuelewa nini kinaendelea.

Wakina MACHO MBAYA kabla hawajaondoka eneo la tukio wakachukua zile familia mbili walizoteka na kuzifungia ndani ya kuba huku lengo likiwa washindwe kutoa taarifa polisi maana wao ndo mashuhuda wenye uhakika kumetokea tukio la ujambazi tofauti na majirani waliosikia mirindimo ya risasi watachelewa kutoa taarifa polisi sababu hawajashuhudia tukio hilo na hawana uhakika mirindimo ya risasi waliyosikia inahusu nini kama ni polisi wanatuliza ghasia au vinginevyo.

Familia za mameneja na mameneja wenyewe kufungiwa ndani ya kuba utelekezaji wa mchoro wa uwizi ulikuwa ukiendelea vizuri na hapo ilikuwa imebakia kipade cha mwisho cha utorokaji eneo la tukio salama ili mchoro sasa uhesabikee umekamilika kwa asilimia 100 bila kuharibiwa kokote.

Jambazi MACHO MBAYA kwenye kuondoka alivutiwa na ile silaha ya KONSTEBO MICHAEL MILANZI ambayo ilikuwa ni SMG yenye risasi 30 na kuona acha aichukue ili kuongeza idadi ya silaha katika stoo yao maana ndo wameanza tukio la kwanza la ujambazi na wanategemea matukio mengi ya ujambazi kufuata mpaka TANZANIA iwakome.

Kiasi cha fedha walichofanikiwa kuiba kilikuwa shilingi milioni 234 [234,000,000] na fedha nyingi hizo ilizidisha mchoro kwenda vizuri maana lengo la ujambazi huo ni kuiba fedha nyingi kadri iwezekanavyo na kwa kiasi hicho wako vizuri.

Gari mbili za CARINA na LAND CRUISER zikakanyagwa mafuta kuelekea MOSHI mjini ili sasa waelekee SANYA JUU wilayani SIHA nyumbani kwa mfadhili wao ambako huko ndo watagawana fedha walizoiba na wanapotea benki hapo ilikuwa mida ya saa mbili usiku na dakika zake.

Wakina MACHO MBAYA tayari wameshaondoka eneo la tukio ndo taarifa zinawafikia polisi wa wilayani MWANGA na kuwahi eneo la tukio kwa kukuta polisi mwenzao mmoja anavuja damu chini huku mwingine tayari ameshakufa na kuingia ndani ya benki kusaidia familia zilizofungiwa ndani ya kuba baada ya KONSTEBO NAFTALI ASHERY kuwaelekeza kuna wahanga huko ndani ya benki na watawasaidia kuwaeleza zaidi tukio lilivyokuwa.

Wapelelezi wa kipolisi wanakusanya taarifa hapo eneo la tukio pamoja na kuanza uchunguzi wa tukio hilo la ujambazi taarifa za awali kuhusu ujambazi huo zikasambazwa kwa vituo vya polisi na doria zote zilizokuwa zinaendelea usiku huo mkoani KILIMANJARO na ARUSHA sababu mashuhuda waliwaambia wapelelezi kuwa gari mbili zinazoaminika kubeba majambazi hao zilielekea njia ya MOSHI-ARUSHA.

Wilaya ya MWANGA kama unaelekea MOSHI au ARUSHA iko mbele kwa wilaya ya SAME ambayo nayo iko mkoani KILIMANJARO na ukimaliza wilaya ya SAME unaingia mkoani TANGA, kwa maelekezo ya mashuhuda haikuwa na haja kutoa taarifa mkoani TANGA sababu majambazi muelekeo wao ni mbele kutafuta MOSHI au wilaya zingine za mkoa wa KILIMANJARO isipokuwa SAME ambayo yenyewe inarudi nyuma kukutana na mkoa wa TANGA.

Taarifa ya ujambazi kutoka MWANGA ikawafanya polisi wa muelekeo gari za majambazi zilipoelekea kuingia barabarani kuona kama wataweza kuwaona na kuwadhibiti usiku huo, huku wakina MACHO MBAYA wenyewe wanakanyaga mafuta kwa LAND CRUISER kuwa mbele na CARINA kufuata nyuma.

Wakina MACHO MBAYA kufika mjini HIMO wilayani MOSHI VIJIJINI ambapo walikuwa wameshatembea kilomita 35.4 gari aina ya DEFENDER za jeshi la polisi ambazo zilikuwa doria ziliona gari mbili za LAND CRUISER na CARINA zikifukuzana kwa kasi zikielekea MOSHI MJINI na kuzitilia mashaka zinaweza kuwa ndo zile za ujambazi MWANGA sababu ripoti ya awali kutoka kwa wapelelezi wilayani MWANGA walitaja gari mbili za LAND CRUISER na CARINA kuaminika ndo zimebeba majambazi na fedha za uwizi milioni 234.

DEFENDER za jeshi la polisi zikaunga nyuma kuzifuatilia gari hizo walizozishuku na kama sio watu wema lazima watajishtukia tu na kweli kwa majambazi wakina MACHO MBAYA kutembea dakika chache mbele toka kuachana na njia ya panda ya HIMO kuanza kuwasiliana baada ya kuona DEFENDER za jeshi la polisi nyuma yao.

Jambazi PETER MBUGUA ambaye alikuwa kwenye gari aina ya CARINA kumpigia simu jambazi MACHO MBAYA aliyekuwa kwenye gari aina ya LAND CRUISER na kumwambia kuna DEFENDER za polisi zinawafuata nyuma kwa kuanzia pale mjini HIMO sasa wanafanyaje..?, na hapo inaelekea usiku wa tatu.

Jambazi MACHO MBAYA akatoa amri vita ianze dhidi ya hao polisi wanaowafuata na mashambulizi yataanzia kwa wao wakina PETER MBUGUA sababu gari yao ndo iko nyuma halafu wao wakina MACHO MBAYA watatanua kidogo kushoto ili wapate shabaha ya kuweza kushambulia DEFENDER za jeshi la polisi huku gari ya kina PETER MBUGUA itabaki kwenye mstari wake.

Huu ulikuwa mfumo mzuri sana kuhakikisha gari zao zote mbili zinashambulia polisi na hawatashambuliana bahati mbaya wenyewe kwa wenyewe, na baada ya mfumo kutekelezwa wakina PETER MBUGUA wakavunja kidogo kioo cha nyuma ili kupata shabaha ya maadui zao na kuanza mashambulizi huku wakina MACHO MBAYA wenyewe wakashusha vioo vya milango na kuanza mashambulizi pia.

Mapigano haya kati ya majambazi wakina MACHO MBAYA na jeshi la polisi ilikuwa kama vile filamu ya “FAST & FURIOUS” maana yalikuwa mapigano ya barabarani wote wakiwa kwenye magari yao na kudumu kwa takribani masaa matano toka mida ya saa 03 usiku mpaka saa 08 usiku na wakina MACHO MBAYA walitoboa kuonesha wao ni zaidi ya majambazi, MOSHI ilisimama.

Shambulizi la kwanza la majambazi lilikuwa la kushtukiza kwa polisi ambao hawakutegemea na kubidi wapunguze kasi huku wakiambaa ambaa na kuanza nao kurudisha majibu na mapigano makali ya risasi kuanza baina yao.

Mapambano yalikuwa makali sana kwa kuzungushana mitaa ya MOSHI huku wakirushiana risasi na wakina MACHO MBAYA dhumuni lao lilikuwa kuwazidi jeshi la polisi kwa kuwapoteza dira na kuwakimbia ili waendelee na mchoro wao kama walivyopanga wafike wilayani SIHA.

Baada ya mapambano ya masaa 5 wakati jambazi PETER MBUGUA akiwa amepokea usukani kwa kuendesha yeye gari alishambuliwa risasi na polisi sehemu za kichwani na mgongoni na kupelekea kupoteza muelekeo ikizingatiwa yeye ndo dereva na kwenda kugonga gari la LAND CRUISER la majambazi wenzie na gari lao wakina PETER MBUGUA kupinduka.

Eneo la YMCA pale MOSHI MJINI ndo kulitokea ajali hiyo kwa CARINA kupinduka ila LAND CRUISER haikupinduka na sababu wenzao katika gari ya CARINA walipinduka ikabidi wasiendelee na safari ili kuwasaidia wenzao wahamie katika gari yao ndo waendelee kukanyaga mafuta.

majambazi waliokuwa kwenye LAND CRUISER waliendelea na mapambano dhidi ya jeshi la polisi ili wasisogee hapo kwenye ajali wakati wanasaidia wenzao kuwahamisha kwenye LAND CRUISER na baada ya ajali pamoja na mashambulizi kuendelea gari za jeshi la polisi zilisimama umbali kidogo na ajali ilipotokea na kuanza kurudisha majibu.

Majambazi waliokuwa wanatolewa kwenye gari ya CARINA walimwambia MACHO MBAYA kuwa jambazi mwenzao PETER MBUGUA ameshafariki na jambazi MACHO MBAYA kusikitika sana ila hakuna namna ndo mambo ya ajali kazini.

Majambazi wote wakapanda LAND CRUISER na kuendelea na safari huku polisi wakiwarushia risasi ambao hawakuwakimbiza tena kwa kuelekea kwenye ajali na kukuta jambazi mmoja ameshafariki, wakina MACHO MBAYA waliendelea na mchoro wao huku wakiwa makini kama wanafuatiliwa nyuma mpaka kufika SANYA JUU nyumbani kwa mfadhili wao mzee KANJE.

Wakina MACHO MBAYA kufika salama kwa mzee KANJE ndo ilikuwa mwisho wa mchoro wao na ujambazi wao kuwa umefanikiwa ingawa walipoteza jambazi mwenzao, na mgao wa fedha ukaanza usiku huo kwa kila mshiriki anayejua ujambazi huo na kwa msaada wake kufanikisha ujambazi huo asilimia 100 hata kama hakuwepo nyumbani kwa KANJE usiku huo ni lazima mgao wake utamfikia siku zijazo kuanzia kesho yake.

Usiku huo doria kali mkoani KILIMANJARO na ARUSHA ziliendeshwa kuwatafuta majambazi wakina MACHO MBAYA ambao walikuwa wamepozi zao nyumbani kwa mzee KANJE wakisikilizia upepo mbaya huo kupita ili warudi zao ARUSHA makao makuu yao NJIRO.

ITAENDELEA.....!!!!!
Kali sana
 
Back
Top Bottom