Niliposikia tu Jairo kawekwa likizo ya malipo nikajua mchezo umeanza kusukwa. Hakukuwa na uchunguzi makini. Kilichofanyika ni kile wazungu wanaita "white wash," kuwanusuru Jairo na Kikwete.
Jairo ni msiri mkubwa sana wa mkweree kwahiyo hata huo mchango inawezekana kabisa ulipata blessings za Ikulu. Siamini hata siku moja kuwa wanyama pori wanaweza kutoroshwa toka mbugani kwa ndege ya kijeshi na kupelekwa mpaka Qatar bila vyombo vya dola kufahamu, na kama hivyo ndivyo basi IKULU yetu ilikuwa na taarifa kamili juu ya wizi wa wanyama hawa. Kama hivyo ni sahihi basi kusimamishwa kwa mkurugenzi wa wanyama pori ni dongo lingine la macho tunalaopigwa wadanganyika lakini siku ya siku jamaa atarudishwa kazini kuwa hakuwa na hatia!! Hiyo ndio serikali ya kishikaji, lakini iko siku mtakuja juta kwa haya mnayofanya.