Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Mkuu lazima ukubali Liverpool wako vizuri,kwenye mechi 4 mlizokutana nao mmepata point 1 tu lakini mnakuwa wabishi eti Liverpool ya kawaida?

Mashindano yote mpaka Saizi Liverpool kapoteza mechi 3 tu, hiyo timu unayoisifia imepoteza mechi ngapi mashindano yote? Ni zaidi ya mechi tatu imepoteza lakini bado unaisifia kisa Liverpool kakufunga na hutaki kukubali.

Umefungwa na Liverpool Mechi 2 ukiwa nyumbani kwako bado unalazimisha Liverpool wakawaida kweli?
Wivu unamsumbua achana nae
 
mechi zetu zilizobaki ni dhidi ya timu kubwa tu, wakati wenzetu wamemaliza nao!

bado tuna
everton
spurs
manyu

Mkuu game ngumu kwangu ni kama timu nilitoka sare au nilifungwa.

Lakini hao Man U tumewapiga tano bila wakijitahidi watapunguza magoli lakini kushinda big no.

Timu zote zilizobaki tumeshazifunga round ya kwanza isipokuwa Spurs na man city tulitoa sare.

Sina wasiwasi na timu yoyote zaidi ya hizo.

Vipi wewe ugumu wa timu umeangalia nini?
 
Ngumu hapo ni wolves na city

Hao wolves hawafai aiseee
Wolves bila baunsa Traore kwetu ni wepesi sana.

Tunamalizia nao Ligi pale Anfield i guess.

Naona ubingwa utakua ushakua decided mpaka hio mechi.

Kipara anahitaji Fernandinho atumie uzoefu wake kupoza joto dressing room ya Ethad maana ni dhahiri sasa kwao sare itakua sawa na wamepigwa.

Fernandinho amekua credited na team talk matata sana especially under pressure.

Kimsingi wao washinde gemu zao na sisi tushinde zetu haya mengine yapo nje ya uwezo wetu. Hatuwezi kusema atafungwo na Aston Villa au Wolves nk lakini ikitokea hivyo tutasema cheers itakua powa pale tushinda gemu zetu.

YNWA
 
Ni kweli mmeshinda ila mpira mliocheza ni wa kawaida sana sidhani kama mna ubavu wa kushindana na city na mkikutana nao ndio mtajua hamjui
Aisee tunachojali sie ni pointi 3 ugenini Emirates hayo ya Manchester City kutufunga ama kumfunga sio wakati wake.

Tuelewane wenzio tunachukua mechi baada ya mechi haya mambo ya kuchukua mechi jumla jumla yaliisha wakati wa akina Fergie na Wenger kwa sasa ligi hii lolote linaweza tokea ndugu.

Tottenham kampige Manchester City lakini kapigwa na Manchester United ambae nae kapigwa na Manchester City yaaani hii ligi haina matokeo ya mfukoni kwa kuweka mambo sawa ni kua positive muda wote kwamba upo ushindi.

YNWA
 
Kwa hali ilivyo...ile jana arsenal alitakiwa kuifanya kazi kubwa kuliko uwezo wake na hatimaye wameshindwa...SASA SISI CITY HII SHUGHULI TUTAIFANYA WENYEWE tareh 10-April...HATUTAKI TIMU NYENGINE KUJINASIBU ETI ZINAWEZA KUMTULIZA LIVER!...Narudia tena shughuli za wanaume zitafanywa na wanaume wenyewe nasio wavulana.
Mkuu unashabikia Manchester City?

YNWA
 
Mimi kabla sijamsoma sana nilimchukulia hivyo,ila nilipokuja kumzoea nikagundua ni mtu mmoja wa mizaha sana
Na nikimsoma nacheeeka
Kuna muda nisipomuona namiss uwepo wake kwa kweli.

Kuna namna anachekesha jamaa.
Haxhekeshi

Mpuuzi tu yule
 
Ofcourse najua mechi za ubingwa hazina cha home or what...ndo maana nikasem itakuwa 50/50. But city wenyewe wanasem kitendo cha nyie kuja etihad haitakuwa rahisi kushinda pamoja na huo moto wenu, ngoja tuone...KIMSINGI HIYO GAME INAWEZA IKAWA KALI KULIKO ATA FAINALI YA UEFA MSIMU HUU!

View attachment 2153749
Hakuna uwanja mwepesi kwa Liverpool kama Ethad yaaani sijui wale mashabiki wa Ethad hua ni mabitozi ama namna gani yaaani kuna kipindi hata Pep mwenyewe aliwai kutoa maneno makali kwamba hawapati sapoti ya mashabiki Ethad match day kama timu zingine hapo najua alimaanisha Liverpool 🤣🤣...

Tunakwenda kusaka pointi 3.

Tupo tayari.

Hapa maombi kwa ma boys waki break mechi za ki mataifa werejee salama wote tuamshe upya tutakapoishia.

YNWA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom