Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Screenshot_20220317_104640_com.android.chrome_edit_101754344620930.jpg


Team talk = winning.

YNWA
 
Ni kweli mmeshinda ila mpira mliocheza ni wa kawaida sana sidhani kama mna ubavu wa kushindana na city na mkikutana nao ndio mtajua hamjui
Respct your opponents. Kama tulicheza mpira wa kawaida, mbona hamjapata hata point moja? Na hii ikiwa ni mfululizo tunakuja hapo na kubeba points zote. Na huyo unayemsema wewe mbona gape amepunguzwa imebakia moja? Alicheza mpira gani na Crystal palace akaishia kupata point moja? Gape mpaka linakuwa moja alikuwa anafanya nini?

Chill. Wewe shangilia chenga za Martinelli sisi tunayeya na Points 3. Ndo wakubwa wanavyocheza.
 
Mkuu lazima ukubali Liverpool wako vizuri,kwenye mechi 4 mlizokutana nao mmepata point 1 tu lakini mnakuwa wabishi eti Liverpool ya kawaida?

Mashindano yote mpaka Saizi Liverpool kapoteza mechi 3 tu, hiyo timu unayoisifia imepoteza mechi ngapi mashindano yote? Ni zaidi ya mechi tatu imepoteza lakini bado unaisifia kisa Liverpool kakufunga na hutaki kukubali.

Umefungwa na Liverpool Mechi 2 ukiwa nyumbani kwako bado unalazimisha Liverpool wakawaida kweli?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom