Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Mkuu me sikupenda kuwekwa huyo dogo golini nilikuwa nawasiwasi sana nilikasilika sana.

Nilikuwa nataka allison ndio akae golini.ila dogo kafanya vizuri tu.
Huyo dogo alijituma sana, ni zao bora la Liverpool kwenye ugoli kipa. Mimi sikuwa na wasiwasi nae kabisa sijui kwanini tu.
 
Tumeshinda ila honestly sikuridhishwa na ukabaji wetu hasa kipindi cha pili, tulikabia macho sana, tuliwaruhusu sana chelsea kutengeneza nafasi nyingi za watu VAR ikafanya yake, Klopp aifanye timu iwe compat ili hata mpinzani kupiga on target iwe tabu, mchezo wetu ni kama wa bayern munich wapinzani wanatufikia sana.

ila still bado KEITA ni failed project, keheller, pale tunahazina ya golikipa, DIAZ, msimu ujao watu wajipange
 
Juzi katoka sub tu na Chelsea wakaanza kushambulia kwa kasi. Aliwa pin sana mpaka anatoka walishukuru.

Dogo kivulege anasumbua balaa hakuna mpira uliopigwa kwake akakosa kuufuata aisee mentality yake sio ya kawaida.

Anakimbiza mpaka kivuli cha mpira Hahaha yaaani huyu nadhani tuseme ameletwa kuchukua kazi ya Bobby na sio Mane kama inavyoonekana. Kushambulia yupo vizuri lakini pia tukiwa hatuna mpira ana press moja matata sana.

Huyu bei yake sasa Real Madrid wakimtaka ni £100m hahaha.

YNWA
 
IMG_20220301_103810.jpg
 
Our VVD


Nilijifunza kuwa kumbe bao mabeki wanapaswa kujua kufunga
Na makipa pia wanapaswa kujua kufunga

Yaani kuwa mchezaji ni lazima ujue kucheza angle zote .
Kabisa inapobidi kama vile lazima wote wawajibike na Klopp iliwaadaa kabisa kwa yatakoyanayo siku ile.

😂😂😂😂Kepa walimwadaa kudaka wakasahau kuna kupigaaa hahaha yakamkuta.

Ni muda wetu wa Liverpool tumechekwa sana, tumeteswa sana, tumesemwa sana mara ooh 1 man team (Salah) sasa unajiuliza zile penati zote alipiga Salah peke yake 😂😂😂😂.

Klopp ni levo zingine wakati anajenga kikosi wapo waliomuona kama mpita njia lakini sasa nimeona mpaka Rio Ferdinand akiwashauri Manchester United wafuate mbinu za Liverpool kurudi kileleni hivyo wajipe kama miaka miwili kurudi kwenye kushindana na kuwania EPl au UCL yaaani ukiona sworn enemy akina Rio, Neville wanasema jambo njema kuhusu Liverpool ujue jamaa zangu tupo kwenye laiti traki.


YNWA
 
Tumeshinda ila honestly sikuridhishwa na ukabaji wetu hasa kipindi cha pili, tulikabia macho sana, tuliwaruhusu sana chelsea kutengeneza nafasi nyingi za watu VAR ikafanya yake, Klopp aifanye timu iwe compat ili hata mpinzani kupiga on target iwe tabu, mchezo wetu ni kama wa bayern munich wapinzani wanatufikia sana.

ila still bado KEITA ni failed project, keheller, pale tunahazina ya golikipa, DIAZ, msimu ujao watu wajipange
Klopp hili kashalitolea maamuzi alisema "the gains are more than the risk".. Kwamba ukikaba almost uwanja katikati ni rahisi ku regain mpira pindi unavyokua under pressure lakini pia alisema unavyoweka high line inawapa wachezaji wetu muda mwingi kuweka kibanda upande wa upinzani hivyo kua rahisi kuanzisha mashambulizi kwa haraka zaidi. Ukumbuke Klopp anatumia 4 3 3 attacking hivyo yeye anachojua na kua half ya upinzani lakini hilo unalosema sio tu Jumapili mbali gemu nyingi tu MF ikisinzia kiasi basi ujue tunateseka mno..

Kwa kawaida mabeki wa Liverpool hua wanakua almost mita 42+ kutoka kwa Alisson au Kelleher. Siri ya pale MF inavyopitwa ku maintain high line na discipline ili mpinzani acheze offisde na kwa msimu huu VAR kwenye offside hawajaharibu kabisa na VVD na crew yake wana rekodi highest kuwatega pinzani Off side...

Kingine unavyokua na MF design ya Keita, Henderson ni ngumu kuwategemea kukamilisha show bila msaada wa karibu wa backline.

So ili MF iwe compact, imara na progressive unahitaji wachezaji sahihi kwa sasa hatuna serial MF zaidi ya Fabinho hawa wengine hawana continuity kumpa Klopp anachohitaji.

Thiago man. Huyu majeruhi ndio mchawi. Lakini akicheza hua mipira haipotea kizembe kwa vile ana control tempo kupunguza presha kwa mabeki na pia kuwapa overlapping RB na LB muda wa kuregain position na pia front line kutazama upya penye mpenyo wa kuwaumiza opponent.

Keita sina cha kuongeza zaidi Liverpool wakipata ofa June 2022 wachukue ela mapema. Ana rekodi nzuri sana Liverpool overral katika alizocheza ana win percentage ya over 90% kama sikosei amepoteza mechi 4 au 5 tu lakini sasa shinda kwake ni aidha anakua played out of position ama majeruhi yalimtia uoga au yote kwa pamoja au anajua mwenyewe. Ajabu tangu atue sina hakika hata kama amecheza mechi 100 huyu dogo. Au alidanganya umri 🤠🤠 haha. I had high hopes lakini kwa sasa i have given up kabisaaaa

Ukumbuke pia MF yenyewe haitengezi magoli wala ma assist ya kutosha lakini pia ukitazama msimu huu tumepoteza mechi 2 mbili nadhani ya Westham na Leicester katika Mashindano yote ina maana mfumo huu sio tatizo mbali siku hio ya mechi mchezaji nani yupo kutetea badge. Akiwepo Thiago na Fabinho wewe agiza popcorn ushindi upo hahaha

YNWA
 
O-0 HT. Hii tumecheza vizuri. Japo kuna uzembe, chelsea wanavizia counter watupige.
Diaz ni shoka isee.
Counter attack gani hata nyie mlikuwa mnavizia, defense yetu sie zile za akina leeds mnaenda tu kama mnaingia public toilet za stendi. Honestly game ilikuwa kubwa na hakuna upande wenye kujidai walicheza vizuri zaidi ya mwenzake. Period
 
Counter attack gani hata nyie mlikuwa mnavizia, defense yetu sie zile za akina leeds mnaenda tu kama mnaingia public toilet za stendi. Honestly game ilikuwa kubwa na hakuna upande wenye kujidai walicheza vizuri zaidi ya mwenzake. Period
Ila Leeds wameporomoka kwa kasi ya 5G. Wamegawa pointi kama njugu bora yule babu katimuliwa wacheze mfumo unaoedana na wachezaji walionao wazima.

Otherwise gemu ili balance ndio maana tukafika matuta tukafanye jambo moja its coming home la 9.

YNWA
 
Kabisa inapobidi kama vile lazima wote wawajibike na Klopp iliwaadaa kabisa kwa yatakoyanayo siku ile.

Kepa walimwadaa kudaka wakasahau kuna kupigaaa hahaha yakamkuta.

Ni muda wetu wa Liverpool tumechekwa sana, tumeteswa sana, tumesemwa sana mara ooh 1 man team (Salah) sasa unajiuliza zile penati zote alipiga Salah peke yake .

Klopp ni levo zingine wakati anajenga kikosi wapo waliomuona kama mpita njia lakini sasa nimeona mpaka Rio Ferdinand akiwashauri Manchester United wafuate mbinu za Liverpool kurudi kileleni hivyo wajipe kama miaka miwili kurudi kwenye kushindana na kuwania EPl au UCL yaaani ukiona sworn enemy akina Rio, Neville wanasema jambo njema kuhusu Liverpool ujue jamaa zangu tupo kwenye laiti traki.


YNWA
hako kakepa walivyokasalia Sala zote,wamekazunguka nako kanaviringisha Mpira kwenye jezi Huku kanasali nikawaza tu kuwa Leo moto utawaka
,,
Kalivyopaisha sikuamini.


...
Ile mechi imenifundisha kumbe mchezaji anatakiwa kuwa flexible.
Muda wowote atatakiwa kupiga penalty,,kipa akipewa redcard itabidi afanye kazi ya kukeep goli aisee
Ilinishangaza kidogo kuona wachezaji wooote wamepiga penalty..na wakapata.




Klopp sasahivi ni levo zingine.
Man u sijui hata wafanyeje na timu lao like aisee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom