Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Mkuu tuna wamiliki wachumi balaa. Amini usiamini huu ununuzi wa Diaz unamengi sana nyuma ya pazia aisee. Usije shangaa Salah, Mane wakanyimwa nyongeza ya mikataba yao ama ukaona Mane amepewa mkataba mpya na pengine wamlipe £180 au £200 kwa wiki na waongeze miaka miwili ina maana mpaka 2025.

Kwa Salah FSG wanatega hivi, Mbappe atasaini mkataba mpya PSG kama ndio FSG wanaweza kumuuza Salah Real Madrid, ama je Barcelona kuna pesa wanategemea je wanaweza kumshawishi Salah atue kwao.. FSG wanamtega Salah kwa kuangalia movement za wachezaji wengine ambao ni Mbappe na Haaland. Timu zenye uwezo wa madai ya Salah ni PSG, Real Madrid, Manchester City na Juventus labda kwa baadae akiona vipi Chelsea na Barcelona wakipata hela.

Hili sakata la Salah ndio kwanza asubuhi labda watonywe mapema movement za Mbappe na Halaand zipo hivi na hivi.

Firmino naona ni rahisi kupata kama akihitaji kwa vile dogo hua hana makuu hata ya dakika uwajani hanuni asipopangwa wala sub na pia hata mshahara wake sio ishu kubwa kwa £180k,wakimpa miaka 2 inamtosha.

YNWA
Jamaa wapo kibiashara sana, ila kumuachia Salah au mane haitopendeza.
 
Jamaa wapo kibiashara sana, ila kumuachia Salah au mane haitopendeza.
Ki ukweli FSG sio kwamba hawataki Salah, Mane, Firmino wabakie Anfield mbali ile policy yao ya sell to buy ndio inawabana. Ukumbuke Klopp katua 2015 na mpaka sasa ana EPL moja tu haswa kutokana na ufinyu wa kikosi alichokua nacho angalau sasa ana depth kiasi bila Mane, Salah tuna uwezo wa kushinda mechi, sasa Klopp hakuja Anfield kusidikiza Kipara Pep awe anachukua EPL kama anavyofanya. Hivyo lengo kuu ni kua na kundi la wachezaji watakaocheza kama ambavyo mwalimu anataka Salah na Mane ni mfano bora kabisa kwamba Klopp ni mwalimu haswa walikuja hapa wakiwa hawana majina na stat za kimataifa lakini ndani ya miaka mitano sasa almost wamewekwa kwenye ramani ya mpira katika levo za juu. Hivyo ni hasara kwa klabu pia kuwaachia wakiwa bado wana mengi sana ya kuleta Liverpool kuanzia magoli, ma assist nk

Tuna bahati sana corona ilizichapa sana Real Madrid na Barcelona vilivyo kipesa kiasi sasa akina Mane na Salah ndoto zao baada ya kukupiga Uingereza wakacheze na kule ni ngumu kwa sasa labda waodoke bure 2023 ama FSG waamue kupokea chochote ilimradi wasiodoke bure lakini bei kabla ya corona ya Salah ilikua £150m na Mane £100m na Real Madrid akiwepo Zizou alivutiwa sana na hawa jamaa.

Kwa sasa wanategeana tu hakuna nama FSG ni wachumi huku Salah na Mane wakijua fika umri umesogea hivyo huu mkataba unaokuja pengine ndio wa mwisho ambao wanauwezo wa madai hivi na vile kwa kua pia wapo kwenye ubora poa kabisa.


Ni ngumu kujua Liverpool hio Juni 2022 wanataka nini sokoni je watanunua right winger mmoja kum challenge Salah, maana Diaz anashindana namba na Mane, Jota yupo kwa Bobby sasa Salah nae analetewa mbadala na je hii ndio ujumbe kwa kambi za Salah na Mane kwamba tunasajili kwa ajili ya maisha bila wao 2023 haha ni ngumu kujua aisee.

Ki ufupi sie yetu macho.

Kwa sasa tuwafurahie Mane na Salah tunao msimu huu na msimu ujao. Na kama wakituachie zawadi za EPL zingine 2 na wakasepa zao kutokana na ubahiri wa FSG basi inatosha kwani naamini tunabaki katika mikono salama ya Jota, Diaz nk

YNWA
 
Dah! Ngoja na mimi niwe natumia pc maana nisipo jiunga kifurushi kikubwa DSTV huwa natumia sim.
Mkuu Laptop/PC haili sana bundle, utofauti wake na simu ni kidogo sana, kitu kinacho matter in quality ya streaming link ikiwa HD basi itakula bundle sana na ikiwa SD basi itakula kidogo. Mfano binafsi ikitokea nimetumia Laptop kuangalia game kwa link ya SD basi kwa 90 minutes zote sitotumia zaidi ya 500MB ila kwa link za HD huwa inafika hadi 800MB.

YNWA
 
Dah! Laptop siinakula Sana bundle?
Mkuu cheki settings za Pc yako mfano kama umeruhusu automatic updates baasi hapo bando huwa linaliwa sana maana drivers zinakuwa zinajirun na kutumua bando kuweka mambo yake sawa na System kiujumla .
 
Kwani Leo tulikubaliana tunaamka sangapi???
Ahahhhhhhh guys najua mko na furaha mob..
IPO hivi kama tukishinda mechi zetu zote zilizobaki tayari n mabingwa EPL hahhhahhh it sound good..
Tujiandae kusherekea ubingwa wa 20 wa EPL Na kurudi kwenye ufalme wetu tulioporwa na NyumBu kimiujiza..
Sherehe zitaanza jumapili hii tr 27 pale mjini Wembley ambapo Chelsea atalia kilio cha mbwa mwizi baada ya hapo tunampiga Norwich kwenye FA ili tuzidi kuikalibia faninali Go Milani chaali. Ahahahahahah.. Hawana hamu tena na majogoo ya jiji imebaki kukamilisha tu ratiba, bahati mbaya watakuja kumalizia ratiba yao Anflied teh teh teh teh....

Hiyo UEFA nazani tutacheza na Bayern au PSG final hahahhahahhh raha sana.. Mwaka wetu ni huu.
mpira wa maneno ndio unakujaga kuwaponza.
Subiri jumapili tuwafunge midomo nyie kuku.
Kwamba ninyi ni nani mubebe EFL,FA,EPL na UEFA hahahahahaha ..munaleta ushabiki maandazi kisa viushindi vyenu viwili vitatu😂😂😂

#CFC💙💙💙
 
Tupo na jamaa yangu wa Kaskazini OllaChuga Oc hahaha yaaani atajua hajui.

Itakua gemu powa sana kocha wao kashakua mtalaam wa fainali.

Bila Kovacic pale kati watapwaya maana dogo ni bonge la MF akisimama na Kante hua wanatuvuruga sana.

Itakua vita ya German vs German.

YNWA
nyie subiri jumapili ndio mutajua hamujui ..Unampiga leeds mchovu ndio unajiona una kikosi cha kubeba kombe mbele yetu.?!

#CFC💙💙💙
 
Wakuu jpili Game itakuwa kali sana binafsi sitaki kuzungumzia kiushabiki ila mimi naona ni 50/50 hapo hapo sisi tukifunga goli 2 bc tumewamaliza tunaweza kuwafunga na mengine ila Chelsea akishapata goli 1 tu wametumaliza wanajuaga kulinda sana ni muda muafaka sasa wa klop kuchagua kikosi kizito chenye nguvu siku ya jumapili

YNWA LFC❤️
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom