Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Ndio tunacheza na Chelsea eeh?
Tupo na jamaa yangu wa Kaskazini OllaChuga Oc hahaha yaaani atajua hajui.

Itakua gemu powa sana kocha wao kashakua mtalaam wa fainali.

Bila Kovacic pale kati watapwaya maana dogo ni bonge la MF akisimama na Kante hua wanatuvuruga sana.

Itakua vita ya German vs German.

YNWA
 
Tupo na jamaa yangu wa Kaskazini OllaChuga Oc hahaha yaaani atajua hajui.

Itakua gemu powa sana kocha wao kashakua mtalaam wa fainali.

Bila Kovacic pale kati watapwaya maana dogo ni bonge la MF akisimama na Kante hua wanatuvuruga sana.

Itakua vita ya German vs German.

YNWA
Mimi naamini katika klopp
Wacha tuone..

Am sure tutawavuruga tu hivyohivyo hata kwa mbinde
 
Screenshot_20220224_103243_com.android.chrome_edit_21493685794635.jpg


Wakuu huyu ndio nani vile??

YNWA
 
Umeona. Yaaani ukiwa na kikosi kipana hakuna mchezaji anaetaka asugue benchi ile false 9 kaicheza vizuri sana.

Jana Mane alicheza vizuri sana. Yeye na Diaz walikua wanazunguka uwanja kusaidia timu. Ki ukweli Mane tangu atoke Afcon na kombe lake naona limempa push fulani kuongeza bidiii.

Kwa uchezaji huu wa Mane, Salah, Diaz hata pengo la Jota magoli au Firmino halipo tena,tupo vizuri.

Jana Diaz na Mane walifanya recovery ya mpira mara nyingi sana. Hii ndio team yako tunayohitaji.

YNWA
FSG wanasubir nini

Mpe Mane mkataba mpya
Mpe Salah mkataba mpya
Mpe Bobby kamakataba ka muda mfupi.
 
FSG wanasubir nini

Mpe Mane mkataba mpya
Mpe Salah mkataba mpya
Mpe Bobby kamakataba ka muda mfupi.
Mkuu tuna wamiliki wachumi balaa. Amini usiamini huu ununuzi wa Diaz unamengi sana nyuma ya pazia aisee. Usije shangaa Salah, Mane wakanyimwa nyongeza ya mikataba yao ama ukaona Mane amepewa mkataba mpya na pengine wamlipe £180 au £200 kwa wiki na waongeze miaka miwili ina maana mpaka 2025.

Kwa Salah FSG wanatega hivi, Mbappe atasaini mkataba mpya PSG kama ndio FSG wanaweza kumuuza Salah Real Madrid, ama je Barcelona kuna pesa wanategemea je wanaweza kumshawishi Salah atue kwao.. FSG wanamtega Salah kwa kuangalia movement za wachezaji wengine ambao ni Mbappe na Haaland. Timu zenye uwezo wa madai ya Salah ni PSG, Real Madrid, Manchester City na Juventus labda kwa baadae akiona vipi Chelsea na Barcelona wakipata hela.

Hili sakata la Salah ndio kwanza asubuhi labda watonywe mapema movement za Mbappe na Halaand zipo hivi na hivi.

Firmino naona ni rahisi kupata kama akihitaji kwa vile dogo hua hana makuu hata ya dakika uwajani hanuni asipopangwa wala sub na pia hata mshahara wake sio ishu kubwa kwa £180k,wakimpa miaka 2 inamtosha.

YNWA
 
Naomba kujuzwa naamin nitajuzwa

Kipi kilisababisha Liverpool yetu kupotea ghafla miaka ya 90 ilhali ilitamba Sana miaka ya 80? Sababu KUBWA hasa ilikuwa Nini?
Kutosajili?
Ukata?
Kocha alikuwa mbovu?

Sielewi kwakweli...

Hakuna kitu kiliniuma Kama mateso ya nyumbu miaka HIYO..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom