Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Sio mechi I hii tu Mkuu rejea mechi ya Bradford city.
Ki ufupi bado sijaona timu itakayosepa na huu ubingwa msimu huu maana hata hao Manchester City nao sio ki vile japo wametoka kucheza mechi 2 hivi karibuni tafu sana...

Huu ubingwa upo wazi sana tofauti na ilivyoonekana wakati ligi inaanza.

YNWA
 
Kwa Pep hii draw ni kama point 3 kwake.
Tangu Ronado atue kwa Stretford End naona kama Salah imeongeza kiwango aisee yaaani wanasema kua bora lazima awashinde waliobora na Salah leo kaonyesha ubora wake...

Kwa kweli sielewi pamoja na nyomi ya nyumbani hawa jamaa tumewakosa aje na Fabinho pale ndio kafanya aje sasa....

YNWA
 
Ni sare nzuri kuipata na Man C
Klopp alikuja vyema kipindi cha pili
Tuzidi shikamana mambo mazuri yanakuja
 
Leo inahitajika nidhamu sana kwenye ulinzi, narudia tena nidhamu kwenye ulinzi, kosa lolote halitatuacha salama , mbele kule ninauhakika kuna goli 2+
nilitabiri goli mbili ila defence yetu sasa, kina salah wanafunga wao wako bize kuruhusu, Firmino nikiri kuwa amechoka kama sio kulala yoo, aliingia kutukaba, yani ameisha vibaya mno
 
keita, ox, origi nk hizo ni takataka zingine ambazo hazina msaada wowote kwa timu yani kifupi benchi lipo tupu
 
Leo huu ukuta umekua wa tope kabisa aisee...

Nwa anyday vs Pep pointi moja sio haba.

YNWA

Goli la pili mkuu ni deflection,sijaona goli tulilofungwa hapo la kulaumu beki mbovu.

Goli kama la mo salah alilowafunga man city hilo ndio ungesema beki mbovu .

Tuko vizuri na ubingwa msimu huu tunabeba .

16 Epl matches still unbeaten .
 
Goli la pili mkuu ni deflection,sijaona goli tulilofungwa hapo la kulaumu beki mbovu.

Goli kama la mo salah alilowafunga man city hilo ndio ungesema beki mbovu .

Tuko vizuri na ubingwa msimu huu tunabeba .

16 Epl matches still unbeaten .
beki mbovu hasa upande wa Milner na Matip karuhusu goli la kijinga kwa kumpa space Foden
 
Tangu Ronado atue kwa Stretford End naona kama Salah imeongeza kiwango aisee yaaani wanasema kua bora lazima awashinde waliobora na Salah leo kaonyesha ubora wake...

Kwa kweli sielewi pamoja na nyomi ya nyumbani hawa jamaa tumewakosa aje na Fabinho pale ndio kafanya aje sasa....

YNWA
Huyo Fabinho huyo nimemlaani vikali
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom