Sikupingi, najua ni umbali gani tulitoka pamoja na liverpool hii ndani ya jukwaa hili tangu enzi za kina Lambert. Lakini umekuw ukitumia nguvu kubwa sana kupinga maoni ya wengine kiasi ya kwamba hadi unawagawa kwa mafungu. Kama ilivyo kwako ukitaka maoni yako yaheshimiwe, kwanini usifanye hivyo kwa maoni ya wengine? Wewe unamuelewa Klopp akimchezesha Henderson na wengine hawamuelewi kwanini usikubaliane nao?
Lakini kurudia rudia kauli zilizopita ili tu kujionyesha uko sahihi hapo ndipo naposema gubu lenyewe. Hivi Klopp hakosei? Hatakiwi kukosolewa? Ifikie mahali kila mmoja aheshimu maamuzi ya mwengine hata kama hukubaliani nayo, hapo ndio tunapata mjadala. Sasa tukikubaliana kwa kila kitu huo utakuwa mjadala kweli?