Lissu: Sheria na Tamaduni za kitanzania haziungi mkono mapenzi ya jinsia moja, mimi pia siungi mkono jambo hilo

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Jul 24, 2021
576
1,626
Lissu ameyasema hayo baada ya kuulizwa swali kwenye kipindi cha Clouds 360 ambapo mtangazaji alimuuliza Lissu yupo upande gani sababu mahasimu wake wa kisiasa wamekuwa wakimtuhumu kuwa supporter wa mapenzi ya jinsia moja kwakuwa anakaa ulaya.

Lissu amesema hizo ni siasa za maji taka na kwamba hajawahi kusema popote kuwa anaunga mkono mapenzi ya jinsia moja.

Anasema jambo hili liliibuliwa alipojibu swali kwenye kipindi cha Hard Talk BBC ambapo alisema mambo ya faragha serikali haitakiwi kuingilia na kwamba nchi ina katiba inayosema serikali hairuhusiwi chumbani.

Akielezea msimamo wake juu ya jambo hili Lissu amesema, "Watu wenye utamaduni huo waendelee na utamaduni wao, sisi wenye utamaduni tofauti tuendelee na utamaduni wetu, sheria na tamaduni zetu haziruhusu ushoga hivyo tuendelee na utamaduni wetu, siungi mkono ushoga."

 
Alipokua huko kwao alisema vile, na amerudi hapa kwetu amesema hivi.
Nikama anacheza na wakati na hii ndio maana halisi ya siasa...
Wewe ni mwongo. Lisu, hata siku moja hajawahi kutamka kuwa anaunga mkono ushoga. Yeye alifafanua juu ya katiba yetu, inasema nini juu ya mambo ya faragha.

Kama unaclip ambapo Lisu alusema anaunga mkono ushoga, uiweke hapa ili utuumbue tunasema wewe ni mwongo.

Tatizo la watanzania wengi wanaendeshwa na mihemko, Lisu wakati wote amekuwa makini sana, ndiyo maana kila mara atakuambia sheria au katiba inasemaje juu ya jambo analoongelea.
 
Wewe ni mwongo. Lisu, hata siku moja hajawahi kutamka kuwa anaunga mkono ushoga. Yeye alifafanua juu ya katiba yetu, inasema nini juu ya mambo ya faragha.

Kama unaclip ambapo Lisu alusema anaunga mkono ushoga, uiweke hapa ili utuumbue tunasema wewe ni mwongo.

Tatizo la watanzania wengi wanaendeshwa na mihemko, Lisu wakati wote amekuwa makini sana, ndiyo maana kila mara atakuambia sheria au katiba inasemaje juu ya jambo analoongelea.
Kwa hivyo Lissu anauga mkono Ushoga wa faragha. Jee sheria inasemaje kuhusu wale wanao tumia au kuuza Gongo, Mihadarati kwa faragha, wanaruhusiwa kuvamiwa na polisi na kupelekwa mbele ya sheria? Au katiba hai ruhusu kuwaingilia watu vyumbani?
 
Wazee wa upinde mpo imara kutetea
Wewe ni mwongo. Lisu, hata siku moja hajawahi kutamka kuwa anaunga mkono ushoga. Yeye alifafanua juu ya katiba yetu, inasema nini juu ya mambo ya faragha.

Kama unaclip ambapo Lisu alusema anaunga mkono ushoga, uiweke hapa ili utuumbue tunasema wewe ni mwongo.

Tatizo la watanzania wengi wanaendeshwa na mihemko, Lisu wakati wote amekuwa makini sana, ndiyo maana kila mara atakuambia sheria au katiba inasemaje juu ya jambo analoongelea.
 
Back
Top Bottom