Hezekiah alipewa taarifa ya kufa kwake siku chache zijazo ila aliikataa hiyo taarifa na kuomba Mungu, Mungu alimpa miaka mingine 15 ya uhai.
2 Wafalme 20
1 Siku hizo Hezekia akaugua, akawa katika hatari ya kufa. Isaya, nabii, mwana wa Amozi, akamjia akamwambia, Bwana asema hivi, Tengeza mambo ya nyumba yako; maana utakufa, wala hutapona.
2 Basi Hezekia akajigeuza, akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba Bwana akasema,
3 Nakusihi, Bwana, ukumbuke sasa, jinsi nilivyokwenda mbele zako katika kweli na kwa moyo mkamilifu, na kutenda yaliyo mema machoni pako. Hezekia akalia sana sana.
4 Ikawa, kabla Isaya hajatoka katika mji wa kati, neno la Bwana likamjia, kusema,
5 Rudi, ukamwambie Hezekia, mkuu wa watu wangu, Bwana, Mungu wa Daudi baba yako asema hivi, Nimeyasikia maombi yako, na kuyaona machozi yako; tazama, nitakuponya; siku ya tatu utapanda nyumbani kwa Bwana.
6 Tena, nitazizidisha siku zako, kiasi cha miaka kumi na mitano, nami nitakuokoa wewe, na mji huu, na mkono wa mfalme wa Ashuru, nami nitaulinda mji huu kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Daudi, mtumishi wangu.
Madaktari hawana hatima ya maisha yako, nikimaanisha hawajabeba mwisho wako wa kuishi kwako, wao wamekupa tu majibu ya kitaalumu, unaweza kuyakataa kwa kuelekeza uso wako mbele za Mungu.
Mungu anaweza kufanya jambo jipya kwako, mwamini sasa.
Usiogope lipo tumaini la kuishi tena.